Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 8 December 2015

ASYA IDAROUS KHAMSINI ANOGESHA SIKU YA MTANZANIA SEATTLE, WASHINGTON


Walimbwende wakiwa tayari kufanya vitu vyao wakiwa na vivazi vya mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Mlimbwende akiwa kwenye kivazi kutoka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Kivazi chekundu kikiwa na riboni ya punda milia kikimfanya mlimbwende atabasamu jinsi gani alivyopendeza kivazi toka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Kivazi toka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.

Sunday 6 December 2015

BALOZI WILSON MASILINGI AANZA ZIARA YA KUTEMBELEA VYAMA VYA SIASA DMV AHUDHURIA MKUTANO WA HALMASHAURI YA CCM DMV

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi leo Jumamosi Desemba 5, 2015 alihudhuria mkutano wa Halmashauri ya CCM tawi la DMV ikiwa ni moja ya ziara zake anazotarajiwa kuzifanya kutembelea matawi ya vyama vya siasa nchiMarekani yenye lengo la kudumisha mshikamano na ushirikiano wa Watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao.



Akiongea kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV Mhe. Wilson Masilingi amesema lengo kuu ni kuwa karibu na vyama vya siasa kwa lengo la kuleta umoja na mshikamano ndani ya Jumuiya za Watanzania nchini Marekani na pia kuvitambua kama sehemu na sura ya Diaspora na kutoa wito kwa Watanzania waishio Marekani kuelekeza nguvu katika kuwekeza nyumbani bila kujali ufuasi wa chama unachoamini au kushabikia, wote ni Watanzania.



Mhe. Balozi Wilson Masilingi aliiomba Halmashauri hiyo ya CCM DMV kusaidia katika maendeleo ya Tanzania kwa kupanua wigo wao pamoja na kwamba lengo lao ni siasa na siasa ni sehemu ya maisha ya jamii na maendeleo ya jamii yanategemea siasa, kwa hiyo basi mnaposikia kuna muwekezaji yupo tayari kuwekeza Tanzania msisite Ubalozi upo wazi na utafanya kila liwezekanalo kuhakikisha muwekezaji huyo hapati vikwazo vyovyote.



Mwisho Balozi Wilson Masilingi aliwashukuru Watanzania kwa kuwa mabalozi wazuri nchini Marekani na kuwaasa kuishi kwa kufuata misingi na sheria za nchi ya Marekani.



 Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea jambo na mwenyekiti wa tawi CCM DMV Bwn. George Sebo kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 mkutano uliofanyika Hampton Inn, College Park, Maryland. Picha na Kwanza Production/Vijimambo Blog
Mkutano ulianza kwa sala na kuwakumbuka wote waliotangulia mbele ya haki.


Mwenyekiti tawi la CCM DMV Bwn. George Sebo akifungua kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.


Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea machache kwenye kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.


Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea machache kwenye kikao cha Halmashauri ya CCM DMV


Picha ya pamoja.
Bwn. John Mbatta katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Given  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Catherine  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Tino Malinda  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Aunty Grace Sebo  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Grace Mlingi  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Mzee Joel  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Dr. Secelela Malecela  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Katibu wa CCM DMV Bi.Jesca Mushala  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Mwenyekiti wa CCM DMV Bwn. George Sebo  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.

Tuesday 1 December 2015

Kipindi cha JUKWAA LANGU Nov 30 2015 (Full Show)‏





Kipindi hiki hukujia kila jumatatu kuanzia saa 11 jioni kwa saa za
Marekani ya Mashariki kuijadili Tanzania ya sasa na ile tuitakayo
Katika kipindi hiki tumejadili (mbali na mambo mengine) muelekeo wa serikali yatano ya Tanzania
Yanayofanyika yanaleta taswira gani kwa Tanzania? Na Je!

Yataendelea ama?

MISS TANZANIA USA 2015-2016 AEESHA KAMARA ASHINDA KUWA COVER GIRL KWENYE CALENDA YA MISS AFRICA USA 2015-2016‏



 Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara (kushoto) akiibuka mshindi na kuwa Cover Girl kwenye Kalenda ya Miss Africa USA 2015-2016 shindano ililofanyika New York siku ya Jumamosi Novemba 28, 2015.
 Mamiss wengine walioshiriki shindano hilo wakipita mbele ya majaji.
 Wadau wakipata picha na mamiss wakati mratibu wa mashindano ya miss Africa Lady Kate alipokua akitangaza shindi.
Ma Winny Casey (gauni jeusi) pamoja na Lady Kate (mwenye miwani) wakiwa na mamiss.