Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 10 June 2015

Niambie Live Show EP 4‏


Omby Nyongole, Henry Kente na Salma Moshi
Karibu kwenye kipindi hiki cha NIAMBIE LIVE
Kipindi kinachozungumzia mambo mbalimbali yaliyochukua nafasi za juu kwenye mitandao ya kijamii. Pia kupata Tip ya siku / wiki kusaidia kuboresha maisha yako.
Ni Niambie Live....
KARIBU

Sunday 7 June 2015

Natumai JumaPili Inaendelea/Ilikuwa Njema;Burudani-Yahweh - New Life Worship,Here I am to Worship,Days of Elijah ,My God is Awesome ...

Wapendwa Nimatumaini yangu Jumapili hii ilikuwa/Inaendelea Vyema
Nawataki kila lililojema,Amani,Furaha,Baraka na Fanaka.
Utukufu tumarudishie MUNGU.
.
5 Mwenyezi-Mungu ni mwema;
fadhili zake zadumu milele,
na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Neno La Leo;Zaburi 100

Wimbo wa sifa
(Zaburi ya shukrani)
1Mshangilieni Mwenyezi-Mungu, enyi nchi zote!
2Mwabuduni Mwenyezi-Mungu kwa furaha,
nendeni kwake mkiimba kwa shangwe!
3Jueni kwamba Mwenyezi-Mungu ni Mungu.
Yeye ndiye aliyetuumba, nasi ni mali yake;
sisi ni watu wake, ni kondoo wa malisho yake.
4Pitieni milango ya hekalu lake kwa shukrani,
ingieni katika nyua zake kwa sifa.
Mshukuruni na kulisifu jina lake.
5 Mwenyezi-Mungu ni mwema;
fadhili zake zadumu milele,
na uaminifu wake katika vizazi vyote.
Bible Society of Tanzania














"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Thursday 4 June 2015

Maisha;Hadithi Ya Kufundisha...


👌Hadithi ya kufundisha 👌
Siku moja jioni katika mji wa Washindao, kulikuwa na basi 🚍likisafiri kutoka mji huo kuelekea mji wa Wamtumainio.
Lilikuwa ni basi kubwa na limejaa abiria👫👪👬👭👫👪.
Wakati wakiendelea na safari, ghafla, mvua kubwa ☔iliyoambatana na radi⚡⚡⚡ ikaanza kunyesha.
Dereva hauogopa, wala abiria, wakaendelea na safari. Mara wakati wanaenda, radi ⚡ikaanza kufuatilia gari🚎. Kila wakienda, radi inapiga karibu na ⚡🚎⚡basi kana kwamba inalifuata basi. Likisimama, radi⚡ inapiga pembezoni mwa basi🚍⚡.
Dereva kuona hivyo, akasimamisha gari mita 5 kutoka kwenye mti 🚎............🌴. Akawaambia abiria👫👪👬👭👫👪, "Humu ndani ya basi, kuna mtu ambaye leo ni siku yake ya kufa🚷, tena kufa kwa radi⚡.
Ili tusife wote, nataka kila abiria🚶🚍💃 ashuke akaguse mti 🌴🚶💃🌴ili anayepigwa na radi, apigwe wengine wasife kwa ajili yake. "
Abiria wakitetemeka🙌🙇🙌, wakaanza kushuka🚶🚍💃 mmoja mmoja. Unaenda🌴🏃 unagusa mti , kisha unarudi 💃🚍kwenye basi. Abiria wote pamoja na dereva mmoja mmoja, wakaenda, wakagusa mti 🌴🏃na kurudi 💃🚍bila dhara lolote!
Akawa kabaki abiria mmoja tu🙇, ambaye alikuwa hajagusa mti.
Abiria wote kwa macho👀👀👀 ya hasira 😡😡😡wakamwambia akaguse mti. Akawa anaogopa 🙇🙌kufa. Akagoma. Wakamlazimisha kwa nguvu 💪sana na kumtoa nje
.🌴...... .......🚶👈🚍. Yule abiria akiwa amefumba macho😎, akaenda akagusa mti🌴🏃.
🙆Hamadi bin Vuu!
Radi kali sana⚡⚡⚡⚡⚡ ikalipiga basi🚍, abiria na wote waliokuwamo, wakafa palepale😪😔😪.
Kumbe uwepo wake ndio ulikuwa unazuia abiria wengine wasidhurike na radi.
📝MAFUNZO 📝
1. Unapofanikiwa, huwezi jua uwepo wa nani umefanikisha mafanikio hayo, usichukue sifa zote peke yako. Wapatie na wengine bila kumsahau MUNGU.
2. Unaweza kujiona huna thamani sehemu ulipo, iwe kwenye kundi la WhatsApp, darasani, kazini, kwenye basi, barabarani bila kujua kama uwepo wako ni wa muhimu sana kwa ustawi wa wengine.
3. Usimtenge wala kumnyanyasa mtu au jirani yako, huwezi jua uwepo wake unakusaidia kiasi gani.
4. Jali sana watu wako wa karibu, mchumba, mzazi, ndugu, mke, rafiki, jirani nk kwani uwepo wao ndio tunakuona unang'aa siku hadi siku.


Nimetumiwa Na Mpendwa


"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Wednesday 3 June 2015

Niambie Live Show


Omby Nyongole, Dotto Maongo na Salma Moshi
Karibu kwenye kipindi hiki cha NIAMBIE LIVE

Kipindi kinachozungumzia mambo mbalimbali yaliyochukua nafasi za juu
kwenye mitandao ya kijamii. Pia kupata Tip ya siku / wiki kusaidia
kuboresha maisha yako.

Ni Niambie Live....

KARIBU

Monday 1 June 2015

MISA YA KUMUAGA MZEE SAMUEL LUANGISA NEW YORK


Naibu balozi bi Maura Mwingira akitoa pole kwa watoto wa Mzee Luangisa, Bi Maura Mwingira kwa niaba ya balozi alipata nafasi ya kuongea machache mbele ya Watanzania waliojitokeza kwenye misa hiyo ya kumuombea marehemu mzee Luangisa pamoja na kuaga mwili wake tayari kwa safari ya kwenda nyumbani Bukoba Tanzania kwa mazishi.
Mtoto wa marehem Kwame akitoa wasifu wa mzee Luangisa wasifu huo uliwatoa machozi watu kutokana jinsi mzee Luagisa alivyokuwa mtu mwenye moyo wa kutoa kwakile alichonacho bila kuchagua wala kuhoji.
Mchungaji akiongoza misa mbele ya Watanzania wa New York na miji ya karibu na New York.
Watoto wa marehem wakiwa na sura za udhuni ya kuondokiwa na baba yao mpendwa ambae alikuwa nguzo ya familia hii pendwa.
Watu wakiaaga mwili wa mzee Luangisa pamoja na misa iliyofanyika jumamosi ya tarehe 30 mwezi wa 5. Kwa picha zaidi nenda soma Hapa.

Friday 29 May 2015

ZIARA YA MHESHIMIWA ALI HASSAN MWINYI JIJINI TEHRAN TAREHE 24 - 27 MEI 2015











Maadhimisho ya SIKU YA AFRIKA yafanyika Washington DC


Balozi wa Misri nchini Marekani Mhe. Mohamed Tawfik akiongea kufungua sherehe ya African Union iliyofanyika siku ya Alhamisi May 28, 2015 katika hotel ya JW Marriott, Washington DC
Balozi wa Morocco nchini Marekani Mhe. Rashad Bouhlal akiongea machahce.
Msemaji mkuu wa sherehe ya siku ya Afrika Mhe. Donald Tetelbaum.
Mchungaji Jesse Jackson akiongea kwenye sherehe ya siku ya Afrika.


Maureen Umeh mfanyakazi wa kituo cha luninga cha Fox News DC akisherehesha sherehe ya siku ya Afrika.



Mambalozi wa Afrika nchini Marekani wakiwa katika picha ya pamoja
Wageni waalikwa wakifuatilia hotuba.
Mkuu wa Utawala na Fedha mama Lily Munanka akisalimiana na Balozi wa Kenya nchini Marekani Mhe. Robinson Githae.