Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 14 May 2015

Balozi mpya wa Malawi nchini Marekani atembelea Ubalozi wa Tanzania Washington DC


 Mhe balozi mpya wa Malawi Nector Mhura akipokelewa na Afisa ubalozi Swahiba Mndeme alipotembelea ubalozi.
 Mhe, balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja na mgeni wake balozi wa Malawi Nector Mhura.
 Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani akiweka saini kwenye kitabu maalum cha wageni.
 Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani Nector Mhura akimsikiliza kwa makini mwenyeji wake balozi Liberata Mulamula alipokua akijitambulisha.
  Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani Nector Mhura akiwa ameambata na mkuu wa utawala wa ubalozi wa Malawi bi, Jane Nankwenya.
 Mhe, balozi wa Malawi nchini Marekani Nector Mhura akiwa ameambata na mkuu wa utawala wa ubalozi wa Malawi bi, Jane Nankwenya, kulia ni balozi wa Tanzania nchini Marekani Liberata Mulamula na Afisa wa ubalozi Swahiba Mndeme.

                   PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI.

Monday 11 May 2015

Mahojiano na Mhe. Alhaj Ali Hassan Mwinyi kuhusu KISWAHILI‏


Kiswahili inaaminika kuwa lugha asili ya Afrika inayozungumzwa na watu wengi zaidi kusini mwa jangwa la Sahara.

Ni lugha ya taifa kwa nchi za Kenya na Tanzania na pia yazungumzwa kwenye nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Burundi, Rwanda, Uganda, Visiwa vya Comoro na nchi nyingine

Ikizungumzwa na watu wanaokadiriwa kufikia milioni 100 hivi sasa, Kiswahili ndio lugha pekee ya kiAfrika iliyo miongoni mwa lugha rasmi za Umoja wa Afrika.

Ni lugha muhimu katika habari, shule, kazi za kiofisi, kidiplomasia na hata usalama miongoni mwa mataifa. Lakini , licha ya ukubwa wake, lugha hii inakabiliwa na changamoto mbalimbali.

Hivi karibuni, Chama cha Ukuzaji Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) kilifanya mkutano wake wa nne, ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi. Na amekuwa mkarimu sana kujiunga nasi kuzungumzia juu ya lugha ya Kiswahili na changamoto zake.

KARIBU


Sunday 10 May 2015

TIMU TANZANIA YASHIRIKI MATEMBEZI YA SUSAN G. KOMEN WASHINGTON, DC




Timu Tanzania ikipata picha ya pamoja kabla ya kuanza matembezi ya saratani ya matiti ya Susan G. Komen yaliyofanyika Washington, DC siku ya Jumamosi May 9, 2015.


Wanusurika wa saratani ya matiti wakipata picha ya pamoja.


Matembezi yakianza.


Kushoto ni msaniii toka uingereza Matt Goss aliyeimba wimbo maalum wa Strong kwa ajili ya matembezi haya ya Susan G. Komen ambaye mwaka jana mama yake mzazi alifariki kutokana na maradhi ya saratani ya matiti akipeana mkono na watembeaji wa saratatani ya titi. Kati ni Nancy G. Brinker mdogo wake Susan G. Komen akipeana mkono na watembeaji siku ya maadhimisho ya matembezi ya saratani ya matiti kwa kumuenzi dada yake kwa kuanzisha oganaizesheni ya kupigana na gonjwa hili hatari mwaka 1982 kama ahadi aliyomwekea dada yake.


Mmoja ya watembeaji na mnusurika wa saratani ya titi akipatiwa huduma ya kwanza na watembeaji wenzake baada ya kuanguka na kupata majeraha kwenye paji la uso huku wakisubili gari la wagonjwa.


Timu Tanzania ikichanja mbuga kwenye matembezi hayo.


Mwanahabari wa Kwanza Production na Vijimambo Media Mubelwa Bandio(kulia) akiwa sambamba na mwimbaji Matt Goss na Nancy G. Brinker CEO wa Susan G. Komen


Timu Tanzania ikiwa imemaliza matembezi yao ya maili 3 takribani na kilomita 5


Watoto wa wazazi Watanzania wakipata picha ya pamoja baada ya kumaliza matembezi hayo na wazazi wao.


Picha ya pamoja ya kumaliza matembezi hayo pamoja na mmoja wa kikosi cha zima moto wa TDF aliyejumuika kupiga picha na timu Tanzania.

Picha zote na Kwanza Production na Vijimambo Media & Entertainment.
Kwa picha zaidi bofya HAPA

Friday 8 May 2015

Miaka 90 ya Rais Ali Hassan Mwinyi


Leo, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi anatimiza miaka 90.
Tulipata fursa ya pekee kuketi naye akatueleza mambo machache kuhusu maisha yake
UNGANA NASI


Sunday 3 May 2015

Natumai Jumapili Inaendele Vyema;Burudani-Freedom-Eddie James,Worshiping You - Deluge,Phil Wickham - At Your Name...


Wapendwa;Natumaini Jumapili inaendelea vyema,Iwe yenye Imani,Tumaini,Uponyaji,Faraja,
Shukrani na Utukufu tumrudishie MUNGU....

At Your name, the mountains shake and crumble At Your name, the oceans roar and tumble At Your name, angels will bow, the earth will rejoice Your people cry out Lord of all the earth We shout Your name, shout Your name Filling up the skies With endless praise, endless praise Yahweh, Yahweh We love to shout Your name, oh Lord
1 Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima enyi viumbe vya mbinguni,
semeni Mwenyezi-Mungu ni mtukufu na mwenye nguvu.
2Semeni jina la Mwenyezi-Mungu ni tukufu.
Mwabuduni katika mahali pake patakatifu.

Neno La Leo Zaburi 29;1-11
Sauti ya Mungu katika dhoruba
(Zaburi ya Daudi)

3Sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya maji;
Mungu mtukufu angurumisha radi,
sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya bahari!
4Sauti ya Mwenyezi-Mungu ina nguvu,
sauti ya Mwenyezi-Mungu imejaa fahari.
5Sauti ya Mwenyezi-Mungu huvunja mierezi;
Mwenyezi-Mungu avunja mierezi ya Lebanoni.
6Huirusha milima ya Lebanoni kama ndama,
milima ya Sirioni kama mwananyati.
7Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutoa miali ya moto.
8Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa,
Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9Sauti ya Mwenyezi-Mungu huitikisa mivule,
hukwanyua majani ya miti msituni,
na hekaluni mwake wote wasema:
“Utukufu kwa Mungu!”

10Mwenyezi-Mungu ameketi juu ya gharika;
Mwenyezi-Mungu ni mfalme atawalaye milele.
11Mwenyezi-Mungu na awape watu wake nguvu!
Mwenyezi-Mungu na awabariki watu wake kwa amani!
            Bible Society of Tanzania








"Swahili Na Waswahili"Muwe na Wakati Mwema.