Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 16 March 2015

NesiWangu Show...Albinism


Karibu katika kipindi cha NesiWangu.

Katika kipindi hiki, Harriet Shangarai amezungumza na wanaharakati wa masuala ya Albinism. Sehemu ya kwanza ni mazungumzo na Daisy Makwaia wa Albino Charity Organization na sehemu ya pili ni mazungumzo yao na mwanaharakati mwenye Albinism Babu Sikare wa Afrobino Ltd

Karibu


Sunday 15 March 2015

Tumalizie Jumapili hii vyema;"Happy Mother's Day"Burudani-Upendo NkoneUpendo wa Yesu..!!!!

Wapendwa;Tumalizie Jumapili hii vyema.
"Happy Mother's Day" mama Rachel-siwa[mama'k]
 na Wamama wote wanao jua majukumu yao kama MAMA.
Mungu awape Busara,Hemakima,Maarifa,Upendo,Furaha,Amani na Maisha marefu.
Pole kwa wenzetu waliopoteza/kufiwa na MAMA ..MUNGU awape uvumilivu ,msiache kufuata  yale yote mema MAMA aliyo waachia.
Wale wanaotafuta Watoto MUNGU akaonekane na awabariki nanyi mpate watoto.
MUNGU azidi kutubariki katika malezi.


1Je, maisha yenu katika Kristo yanawapeni nguvu? Je, upendo wake unawafarijini? Je, mnao umoja na Roho Mtakatifu na kuoneana huruma na kusikitikiana nyinyi kwa nyinyi? 2Basi, ikamilisheni furaha yangu kwa kuwa na fikira moja, upendo mmoja, moyo mmoja na nia moja.

Neno La Leo;Wafilipi 2:1-30

Unyenyekevu na ukuu wa Kristo

1Je, maisha yenu katika Kristo yanawapeni nguvu? Je, upendo wake unawafarijini? Je, mnao umoja na Roho Mtakatifu na kuoneana huruma na kusikitikiana nyinyi kwa nyinyi? 2Basi, ikamilisheni furaha yangu kwa kuwa na fikira moja, upendo mmoja, moyo mmoja na nia moja. 3Msifanye chochote kwa moyo wa fitina au kwa majivuno ya bure; muwe na unyenyekevu nyinyi kwa nyinyi, na kila mmoja amwone mwenzake kuwa bora kuliko yeye mwenyewe.4Pasiwe na mtu anayetafuta faida yake mwenyewe tu bali faida ya mwenzake. 5Muwe na msimamo uleule aliokuwa nao Kristo Yesu:  6Yeye, kwa asili alikuwa daima Mungu;lakini hakufikiri kwamba kule kuwa sawa na Munguni kitu cha kungangania kwa nguvu.7Bali, kwa hiari yake mwenyewe,aliachilia hayo yote, akajitwalia hali ya mtumishi,akawa sawa na wanadamu,akaonekana kama wanadamu.8Alijinyenyekesha na kutii mpaka kufa,hata kufa msalabani.9Kwa sababu hiyo Mungu alimkweza juu kabisa,akampa jina lililo kuu kuliko majina yote.10Ili kwa heshima ya jina la Yesu,viumbe vyote mbinguni, duniani na kuzimu,vipige magoti mbele yake,11na kila mtu akiri kwamba Yesu Kristo ni Bwana,kwa utukufu wa Mungu Baba.




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 14 March 2015

PAZI REUNION HOUSTON, TEXAS LEO KUWAKA MOTO WACHEZAJI WENGI NDANI YA NYUMBA‏



 Timu ya Pazi wanaume wakipata picha ya pamoja na mashabiki wao walipokua nyumbani kwa madikodiko ambaye pia ni mmoja wa waratimu wa tamasha hili la kumbukumbu ya timu hiyo iliyowika miaka mingi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Tamasha hili lililobeba jina la Pazi Reunion litafikia tamati leo Jumamosi March 14, 2015 kwa mechi kadhaa na kuakumbuka na kuaenzi viongozi na wachezaji wa timu hiyo waliotangulia mbele ya haki.
 Pazi Queens wakiwa katika picha ya pamoja leo patakua hapatoshi.
Patrick Mwigula kutoka South Carolina na Atiki Matata kutoka Uingereza wachezaji wa Pazi waliowika miaka ya nyuma wakijadili mchezo wa leo kama walivyokutwa na kamera ya Vijimambo.
 Atiki Matata na Richard Kasesela wakipata picha ya pamoja.
Kulia ni Masawe shabiki wa Pazi wa miaka mingi si mazoezi si mechi alikua hakosekani uwanjani hapa akisalimiana na Richard Kasesela mara tu walipoonana baada ya kupoteana kwa miaka mingi.
Kutoka kushoto ni Emmanuel, Patrick na Kasesela wakikumbushana enzi zao za Pazi.
Wachezaji wa Pazi toka shoto ni Vitalis Gunda toka Maryland, Richard Kasesela toka Tanzania na Willy Crrusa toka Houston, Texas wakikumbushana enzi zao.
Kwa picha zaidi Bofya HAPA

Friday 13 March 2015

Pazi ReUnion USA. Mambo yazidi kupamba moto Houston Texas








 Watatu toka kushoto ni Richard Kasesela alipokua akiwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa George  Bush Intercontinental uliopo Houston, Texas nchini Marekani kwa ajili ya Pazi Reunion itakayofanyika siku ya Jumamosi March 14, 2015 katika uwanja wa mpira wa kikapu wa Pilgrim uliopo katika kanisa la Lutheran lililopo Houston. Wengine katika picha ni wenyeji wake waliompokea,  kutoka kushoto ni Willy Crrusa, Aika na Flora Mochiwa maarufu kama Madikodiko. Mchezaji mwingine anayekuja kwenye maadhimisho hayo ya Pazi toka nje ya Marekani ni Atiki Matata anayekuja siku ya Ijumaa March 13, 2015 akitokea Uingereza. Picha na VIJIMAMBO
 Richard Kasesela akitest uwanja wa mpira wa kikapu mara tu alipowasili uwanjani hapo mara tu baada ya kutoka uwanja wa ndege kushoto ni Davis mchezaji mwingine wa mchezo huo, Flora Mochiwa na Willy Crrusa wakiangalia kama bado wamo. Richard Kasesela richa ya kuwa mchezaji wa Pazi pia aliwahi kuwa Rais wa chama cha mpira wa kikapu Tanzania.
 Wachezaji wa mpira wa kikapu wakipata picha ya pamoja na Richard Kasesela.
 Mdau toka Columbus, Ohio akiwa tayari kushuhudia Pazi Reunion itayaofanyika siku ya Jumamosi March 14, 2015 ndani ya jiji la H-Town.
 Willy Crrusa katika picha ya pamoja na Andrew wakati wakiwa ndani ya madikodiko.
 Wageni wakipata chakula huku maongezi yakiendelea.
Andrew akipata picha ya pamoja na Richard Kasesela.

WaTanzania wa Houston Texas kurekodi kipindi kuhusu mauaji ya Albino Tanzania‏





Wadau kutoka New York katika moja ya vipindi vilivyorekodiwa.



Wadau wa North Carolina wakiwa kwenye kipindi kilichopata kurekodiwa.


Timu ya Vijimambo ikishiriana na Kwanza Production inapenda kwanza kutoa pongezi kwa Watanzania Houston kwa jitihada zao za kupambana na mauaji ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi
Pia inaandaa kipindi cha video kuongelea hili swala kwa mapana zaidi na kuangalia jinsi gani ya kukomesha mauaji haya ambayo yanaleta fedheha na aibu  ikiwemo ukiukaji wa haki za binadamu.

Kipindi kitarekodiwa siku ya Jumampili saa 8 mchana (2pm) mahali ni Extended Stay America chumba namba 224 anuani ni 2424 West Sam Houston Prkway, Houston, TX 77042. 

Kwa maelezo zaidi wasiana na 301 335 6383 asante


Ujumbe kutoka kwa ndugu zetu hapo chini.

Monday 9 March 2015

Mazungumzo na Mhe Samuel Sitta......Wizara na Kugombea Urais


Karibu katika sehemu hii ya pili ya mazungumzo na Mhe. Samuel Sitta (Mb)

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania mwaka 2014.

Aliketi nasi kuzungumzia kuhusu kazi zake kama Waziri wa Uchukuzi na pia nia yake ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu (2015)

Karibu