Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 30 November 2013

[AUDIO]: Kuzagaa kwa silaha za moto na kuongezeka kwa mauaji Tanzania‏


Picha kwa hisani ya thehabari.com
Si jambo geni tena hivi sasa nchini Tanzania kusikia fulani kashambuliwa au kauawa kwa risasi.
Silaha za moto hapa nchini hasa zile zinazomilikiwa kiholela zimekuwa zikimilikiwa na kila anayetaka... kama vocha za simu.

Hata mtu mwenye uwezo kidogo, na asiye na sababu ya kuwa na silaha anaweza kumiliki silaha nyumbani kwake .

Bastola kwa sasa zimekuwa kama bidhaa ya utashi na watu wanazimiliki kama wanavyomiliki simu za mkononi.


Ungana
na Sophia Kessy (L) na Mubelwa Bandio (R) katika sehemu hii ya kwanza kuangalia
tatizo hili linaloonekana kuzidi kuathiri na kutishia maisha ya
waTanzania wengi.



--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Wednesday 27 November 2013

Jikoni Leo;[Street food]Chipsi Vumbi Na Hapa kwetu!!!!!!!


Hapa tunapokumbukia Chipsi za Nyumbani, Ma binti zangu hupenda sana Chipsi Mayai[ZEGE]Na sasa wanapika wenyewe kama unavyoona hapo juu,Nyama Choma Baba anawasaidia...

Waungwana;Jikoni Leo Mtaani na Kwa Da'Rachel..
Vipi Chipsi Vumbi/za Mitaani Zina Raha gani? Na Karaha Gani?

Kuna mtu hajawahi kula Chipsi hizi?

Jee wewe uliyekula/Unayekula Wapi KIJIWE bomba Cha Chipsi upendacho?

Pale Dar,Ilala  Kulikuwa kwa Ndago,Barafaa....
Pale Iringa,Kulikuwa kwa Baba Nusa...


Hizi ni Chache tuu nawe Waweza Kuongezea....





"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Monday 25 November 2013

Sunday 24 November 2013

Nawatakia J'Pili Njema;Burudani-Here I am to Worship[Playlist]!!!!

Wapendwa;Muwe Na J'Pili yenye Baraka,Amani,Upendo na Furaha...
Lakini nafsini mwangu nalikusudia hivi,nisije kwenu tena kwa huzuni...
.Maana mimi nikiwatia huzuni,basi ni nani anifurahishaye mimi ila yeye ahuzunishwaye nami?
Neno La Leo;2Wakorintho:2:1-11.


"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 23 November 2013

Wa-Africa Na Mitindo Mchanganyiko!!!!!





Mhhhh..Mengi sina..ni Wa-Afrika na Mitindo...mimi naiita Mitindo TATA..
Vipi Inavalika? Si wanasema Wanawake tunavaa mavazi yanayo fanana na Yao..nawao jee?......haya na Nywele za dada kama hivyo.

Kuona Zaidi nifuate;http://www.mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Miaka 50 tangu kuuawa kwa Rais John F Kennedy‏



 

Ijumaa wiki hii,
Marekani imeadhimisha nusu karne tangu kuuawa kwa Rais wa 35 wa taifa
hilo, John F Kennedy aliyeuawa Novemba 22, 1963 alipokuwa akisafiri kwenye gari la wazi jijini Dallas

Rais John F Kennedy akiwa katika gari la wazi muda mchache kabla hajauawa kwa risasi. Pembeni yake ni mkewe na mbele yake ni aliyekuwa Gavana wa Texas John Bowden Connally, Jr.ambaye pia alijeruhiwa katika shambulio hilo
Kwa wiki nzima, kumekuwa na shughuli mbalimbali kukumbuka tukio hili lililoshitua wengi nchini humo. Mambo mengi yametendeka. Vitabu vipya vimeandikwa na watu wamezungumzia kuuawa kwa Rais huyo pamoja na ufuasi alioacha kwenye uongozi mpaka sasa. Na kama ilivyotegemewa, Kengele ziligongwa, maua yaliwekwa kwenye kaburi, bendera zilipepea nusu mlingoti na nyimbo mbalimbali ziliimbwa

Rais Barak Obama, aliadhimisha kumbukumbu
hizo Jumatano wiki hii kwa kuweka shada la maua kwenye kaburi la Rais
Kennedy na pia kutoa tuzo za heshima kwa watu mbalimbali akiwemo Rais
mstaafu Bill Clinton, mwanahabari maarufu Oprah Winfrey na wengine 14.

Rais Barack Obama (wa pili kulia) akiwa na mkewe Michelle, Rais mstaafu Bill Clinton (wa tatu kulia) na mkewe Hillary Clinton wakitoa heshima mbele ya kaburi la JFK jumatano wiki hii.


Hii
ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA
DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Novemba 23, 2013




--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Friday 22 November 2013

Jikoni Leo;African Market-Nima Market in Accra, Ghana!!!!




Waungwana;Jikoni Leo, Tupo sokoni  Ghana..haya tuangalie mahitahi...
Kuna vingine wewe huviwezi kula lakini wengine wanaweza.

Nini kimekuvutia?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.