Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 9 November 2013

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Athari za vita baada ya kumalizika mapigano‏


Wakati vita ya Congo
ikionekana kuelekea ukingoni, bado tunakumbushwa kuwa athari za vita
katika nchi mbalimbali huendelea kuwaathiri wahusika na hasa wananchi wa
nchi hizo kwa miaka mingi baada ya kumalizika kwa vita hivyo.

Baadhi
ya athari huwa wazi sana. Mfano ni majengo yaliyoharibika wakati wa
mapigano, watu wanaouawa wakati wa mapigano na hata uchumi unaozorota
kutokana na watu kutofanya kazi wakati wa mapigano hayo.

Lakini pia kuna athari ambazo hazionekani ama kutopewa kipaumbele machoni mwa watu wengi baada ya vita hivyo.

Hivi karibuni, waMarekani wamekumbushwa kuhusu hili

Hii
ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA
DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).



Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Novemba 9, 2013



*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

"MISUKOSUKO" KUTOKA KWA NDEGE 3


Jina la Nyimbo ni MISUKOSUKO.
Jina la kundi  ni NDEGE 3
Waimbaji ni Khadija Mnoga (Kimobitel) , Paulyne Zongo na Joan Matovolwa tumefanya featuring na Grayson Semsekwa.

  Audio imeshatoka na sasa VIDEO.




Kutoka kushoto ni Paulyne Zongo, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Joana Matovolwa.Wanamuziki hao watatu na wakongwe nchini ndio wanaounda kundi hilo linalojulikana kwa jina la NDEGE 3

Friday 8 November 2013

Mapenzi Na Wapenzi; [Love Story]Jee Ulimpata wapi huyo Mwenza wako?


Waungwana;Safari ya maisha huanzia mbali sana mpaka watu Kuchumbiana na  wakaamua Kufunga Ndoa/kuishi Pamoja kama Mke na Mume..Pia kila mtu/watu wanapo walipoanzia.
 Jee wewe ulianzia wapi?
 Hahahah..huyo Mchumba wako,Mkeo/Mumeo ulimtoa/Muona/kutana naye wapi?...
Ulitafutiwa,Mlikutana Njiani,kwenye basi,kazini,Chuoni au....?
Jee Unaushauri gani kwa wanaotafuta Wenza/Wachumba/Mke-Mume?






"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Tuesday 5 November 2013

Mahojiano ya Jamii Production na Dj Luke Joe‏


Dj Luke akiwa studio na Mubelwa Bandio wa Jamii Production
Karibu katika mahojiano na Dj mkongwe kutoka Tanzania na
mmiliki wa blog ya Vijimambo Lucas Mkami a.k.a Dj Luke Joe


Dj Luke ambaye makazi yake kwa sasa ni Maryland nchini Marekani ameeleza mengi kuhusu kazi zake hizi.

Katika mahojiano haya, ameeleza historia yake katika kuchezesha muziki, aliyemvutia kuingia katika kazi ya uDj, mafanikio ya Dj, changamoto zake, ku-blogu na mengine mengi.


Karibu Uuungane nasi



--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Monday 4 November 2013

Kipindi cha FAMILIA kutoka Jamii Production......FAMILIA ZA KAMBO (sehemu ya mwisho)‏





Mtayarishaji na mtangazaji wa kipindi cha FAMILIA, Georgina Lema
Moja ya sababu zilizotusukuma kujadili masuala kuhusu FAMILIA ZA KAMBO ni takwimu zilizopo hivi sasa kuhusu familia hizi.
Kwa mujibu wa mtandao wa www.blendedandbonded.com, hapa Marekani
• 41% ya ndoa za kwanza huishia kwenye talaka
• 60% ya ndoa za pili huishia kwenye talaka
• 73% ya ndoa za tatu huishia kwenye talaka
• 45% ya wanawake na 50% ya wanaume wataoa tena ndani ya miaka mitano ijayo
• 50% ya ndoa za marudio huhusisha watoto wa mahusiano yaliyopita walio chini ya miaka 18
•Ndoa 2100 huanzishwa kila siku nchini Marekani
• 42% ya watu wazima wana uhusiano wa kambo. Hii inajumuisha mzazi wa kambo / mtoto wa kambo ama ndugu wa kambo
Kwa idadi ya Marekani, takwimu hizi zinamaanisha kuwa familia za kufikia zinahusisha watu wazima wapatao milioni 95.5
•Kuna baba wa kambo milioni 16.5
•Kuna Mama wa kambo milioni 14.
•Wataalamu
wa mahusiano wanasema kuwa ndoa za kufikia ndio zitakuwa ndoa zenye
umaarufu na nyingi zaidi nchini Marekani na kuwa, kutokana na kukosekana
kwa taarifa sahihi kuhusu familia za kufikia, familia hizi mara nyingi
zimejikuta kwenye migogoro na mafarakano.
Nasi tuko hapa kujaribu kuepusha hilo kwa kushirikiana nanyi katika kile tunachoweza kuelimisha kudumisha ndoa hizo.
Ungana nasi katika sehemu hii ya mwisho ya MADA hii.




--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 3 November 2013

Nawatakia J'Pili Njema yenye Amani;Burudani-bado tupo ,Kijitonyama Choir,Ee Baba,Jehova Baba wa Upendo na...!!!!

Wapendwa Nawatakia J'Pili hii iwe njema..Na usikate tamaa MUNGU yupo na Anatenda/Ametenda/Atatendaaa.. Jehova Baba wa Upendo..Eeee Baba kama si wewe Ningekuwa/Tungekuwa/Ungekuwa Wapi?...Mhhh Acheni MUNGU aitwe MUNGU Bwaana!!!!!

Watulizeni mioyo,Watulizeni mioyo,Watu wangu asema MUNGU wetu....
Neno La Leo;Isaya:40:1-31;

Bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai;watapiga mbio,wala hawata choka;watakwenda kwa miguu,wala hawatazimia.






"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Saaana.

Saturday 2 November 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Oliver N'goma-Bane na Nyimgine..!!!






Waungwana "Chaguo La Mswahili Leo" Ni Oliver N'goma...
Mhh..wewe unakumbuka wapi na ilikuwaje/ulikuwa wapi wakati huo?
Maneno Meengi sina nasikiliza kutoka kwako..

Twende Sote sasaaa......





Swahili Na Waswahili Pamoja Sana.