Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 30 October 2013

Tanzania: Tunaweza kujitoa A. Mashariki

Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete

Serikali ya Tanzania imesema inatafakari ushiriki wake ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na inaweza kujitoa ndani ya Jumuiya hiyo iwapo itaendelea kutengwa katika baadhi ya vikao.
Aidha imesema Tanzania haitambui vikao vinavyofanywa na nchi tatu zilizopo ndani ya Jumuiya hiyo ambazo zimekuwa zikizitenga Tanzania na Burundi.
Taarifa zinazohusiana
Tanzania, Afrika Mashariki, Afrika
Waziri anayehusika na masuala ya Afrika Mashariki wa Tanzania Samwel Sitta ameliambia Bunge la Tanzania kuwa makubaliano ya vikao hivyo vinavyofanywa na nchi za Kenya, Rwanda na Uganda yatatekelezwa na nchi hizo zinazofanya vikao hivyo kwa sababu vinafanyika nje ya utaratibu wa mkataba wa jumuiya hiyo.
Katika mikutano iliyofanyika hivi karibuni Tanzania na Burundi hazikualikwa kwenye vikao hivyo.
Kwa mujibu wa Waziri Sitta mikutano ya wakuu wa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambayo ilianza kwa kuitenga Tanzania ilifanyika Entebbe nchini Uganda mwezi Juni mwaka huu na kufuatiwa na mkutano wa pili uliofanyika Agosti mwaka huu huko Mombasa nchini Kenya ambapo nchi hizo tatu bila kuishirikisha Tanzania walizungumzia uanzishaji wa himaya moja ya forodha.
Mambo mengine waliyozungumza wakuu hao ilikuwa uanzishaji wa visa moja ya utalii kwa nchi zao na matumizi ya vitambulisho vya uraia ambavyo vitatumika kama hati za kusafiria miongoni mwa nchi hizo.
Aidha Waziri Sitta amesema ndani ya mikutano hiyo pia walizungumzia kuanzisha mchakato wa kuanzisha shirikisho la nchi hizo.
Tayari Tanzania imeanza mazungumzo na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kuangalia ni kwa namna gani zitaanzisha ushirikiano nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama zinavyofanya nchi za Rwanda, Uganda na Kenya.
Habari kutoka;http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

Tuesday 29 October 2013

JAMII PRODUCTION YAZINDULIWA RASMI‏ !!




Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara alipokuwa akisisitiza jambo wakati wa mahojiano mafupi aliyofanya na Jamii Production kabla ya KUZINDUA RASMI shughuli za kutayarisha na kusambaza matangazo ya Radio na Video.



Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara akiwa na waanzilishi wa Jamii Production, Mubelwa Bandio (kulia) na Abou Shatry (kushoto)

Naam....
Kwa baraka za Mhe. Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt
Fenella Mukangara, JAMII RASMI IMEZINDULIWA RASMI Oktoba 26, 2013,
alipotutembelea kuangalia utendaji wetu na kuizindua rasmi hapa ofisini
kwetu Washington DC.
Hii ilikuwa ni ZAIDI YA TUKIO.
Ilikuwa ni BARAKA KWETU na tunamshukuru kila aliyewezesha hili.
NA SASA.....
Kazi ya kutekeleza yale yaliyousiwa na Mhe Waziri, yaliyo yaliyo msingi
wa kituo chetu, yale yaliyo MAHITAJI ya walaji (hadhira yetu) NA WAJIBU
WA FANI YETU ndio imeanza.
Na......
Hakuna litajalokuwa na maana kama hatutajua namna ambavyo utendaji wetu unaathiri maisha yako kwa namna CHANYA na HASI
Wewe (msikilizaji, mtazamaji na msomaji wetu) ni mdau mkubwa wa kufanikisha hili.
Tuzidi kushirikiana
TWAWAPENDA



Msimamizi wa vipindi na mpigapicha mkuu wa Jamii Production Abou Shatry akisisitiza jambo kabla ya kuwasili kwa mgeni rasmi


Mtayarishaji na Mtangazaji wa kipindi cha FAMILIA Georgina Lema akiwa "kitini"


Mmoja wa wawezeshaji wakuu wa Jamii Production Bwn Isidory Lyamuya wa Prestige Health Services akijaribu vitendea kazi vya kituo


Mhe. Waziri Mukangara akipokea maelezo ya utendaji wa kituo. Kushoto ni Afisa Ubalozi Mindi Kasiga

 
Mhe. Waziri akisikiliza RISALA ya Jamii Production 



 Mhe. Waziri Mukangara akijibu risala ya Jamii Production


Bwn Isidory Lyamuya akipata akipata picha ya pamoja na Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production



Bwn Isidory Lyamuya akipata mkono wa pongezi toka kwa Mhe. Waziri kwa msaada anaotoa kufanikisha kazi za Jamii Production

Abou Shatry akipongezwa na Mhe Waziri Mukangara


"Mwanamama" Georgina Lema wa kipindi cha FAMILIA akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri


 Mkurugenzi wa Mambo Jambo Radio Bwn Julius Makiri ambaye aliungana nasi katika uzinduzi huu rasmi akipata kumbukumbu na Mhe. Waziri



 Mhe. Waziri Dkt Fenella Mukangara na Afisa Habari katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Mindi Kasiga pamoja na wanaJAMII

 


Hakuna ZAWADI kubwa sawa na kilichofanyika. Na zawadi pekee tuliyonayo ni UPENDO. Ambao hauonyesheki wala haupimiki.

Lakini....tunapenda POPOTE UWAPO, UKUMBUKE SIKU YA LEO.
Na hivyo..twaomba KIKOMBE hiki kiwe kumbukumbu ya tukio hili kubwa kwetu

Abou Shatry akiwa mahala anapopatawala zaidi...


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 27 October 2013

Nawatakia J'Pili yenye Baraka;Burudani-Kijitonyama Choir,Ndani Ya Safina,Hakuna Kama Wewe!!!

Nimatumaini yangu J'Pili hii inaendelea vyema.. Iwe Yenye Neema,Baraka,Upendo na Amani....

BWANA akamwambia Nuhu,Ingia wewe na Jamaa yako yote katika Safina; kwa maana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki... 
Neno La Leo;Mwanzo:7:1-24


Ndani Ya Safina aahhh....ndani ya Safiiina aa humo ndani ya Safina oooohh kuna upendo mwingiiii..........Mhhhh..Wanyakyusa kwa Waheheeee..Wasambaa kwa wadigoooo..Njoni wote Tuingieee...






"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana

Saturday 26 October 2013

chaguo La Mswahili Leo;Mrisho Mpoto!!!!

Waungwana ni wakati mwingine tena wa "Chaguo La Mswahili"Leo chaguo limeangukia kwa kaka Mrisho Mpoto[HOME BOY]Mpoto kama ukimsikiliza juu juu..huwezi kumuelewa kabisa na ukashangaa huyu naye anaimba nini?Lakini ukitulia na kumsikiliza maneno anayotumia utakubaliana nami..Maneno yake ni Vichocheo,Mafunzo,Maisha Na Jamii inayotuzunguka...
Mhhh..mimi Mpoto ananikosha/nibamba/Kupenda kazi zake,,,Vipi wewe mwenzangu?


Iyeeehhh Mjomba Iyeehh...!!..Bora kujenga darajaaaa...!!
Mjomba hapa Nyumbani Tuna hadithi  na misemo mingi kujihakiki,Maana lake mtu halimtapishi Lakini kukumbatia maji kama jiwe ni ujingaaa...
Twende Sote sasa....








"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Msiba wa Martha Shani DC


Katika kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA wiki hii... Kutoka nchini Marekani, tuanze na habari za msiba ulioikumba jamii ya waTanzania waishio maeneo ya Washington DC.

Marehemu Martha Shani

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).a


Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 26, 2013 





*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Wednesday 23 October 2013

Tuesday 22 October 2013

MAENDELEO YA MSIBA WA BI MARTHA SHANI WASHINGTON DMV


                                          Marehemu Martha Shani[1976-2013]
Marehemu Bi Martha akiwa na mumewe Alex Pamoja na watoto wao Jose naChris 
                                         
                                   
NDUGU YETU ALEX KASSUWI BADO ANAHITAJI MSAADA WETU WA HALI NA MALI ILI KUWEZESHA KUSAFIRISHA MWILI WA MPENDWA MKE WAKE ALIYEFARIKI GHAFLA SIKU YA JUMAMOSI OCT 19, 2013.

KUTOA NI MOYO NA CHOCHOTE UTAKACHOWEZA KITASAIDIA NA HATIMAE KUWEZESHA SAFARI HII NDEFU YA KUMPELEKA MAREHEMU KATIKA MAPUMZIKO KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE TANZANIA

GHARAMA ZA MSIBA KUSAFIRISHA MAREHEMU NA FAMILIA YAKE NI $19,500

FEDHA ZILIZOPATIKANA HADI SASA NI $4,300
ZILIZOBAKI $ 15,200

TAFADHALI TUMA RAMBI RAMBI ZAKO KUPITIA ACCOUNT IFUATAYO :-
# 446030759150 BANK OF AMERICA,MD
ROUTING # 052001633
MAJINA KWENYE ACCOUNT NI ALEX KASSUWI & FAITH ISINGO

CHEKI ZINAWEZWA ANDIKWA KWA ALEX KASSUWI AU FAITH ISINGO.

PIA UNAWEZA KUTOA RAMBIRAMBI ZAKO KWA KUFIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU AMBAKO NDIKO MSIBA UPO
ADDRESS NI

482 ARWELL CT
FREDERICK, MD,21703

AU WAWEZA WASILIANA NA MMOJA YA WANAKAMATI HAPO CHINI NA KUMUELEKEZA UPO WAPI ILI AWEZE KUKUSANYA MCHANGO WAKO

Tino Malinda -240-565-7133
Dickson Mkama - 301-661-6207
Mariam Mtunguja - 240-422-1852
Quizella Ntagazwa - 240-602-5011
MV Mtunguja- 240-593-0575
Victor Marwa - 240-515-6436
Faith Isingo - 240-705-1055
Julius Manase-240-393-8445

UKISOMA UJUMBE HUU TAFADHALI MTAARIFU NA MWENZIO, MZIGO HUU NI WETU SOTE NA KWA PAMOJA TUNAWEZA

HAKUNA KIDOGO PALIPO NA NIA. NA HAKUNA KIKUBWA PALIPO NA UMOJA.