Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 10 May 2012

Mchague Joseph Lukaza !!!!!!!


Mchague JOSEPH LUKAZA ili aweze kuibuka mshindi katika shindano la EXCEL WITH GRAND MALT katika chuo kikuu cha Dodoma katika  Category ya Innovation Nominee
Jinsi ya kushiriki kwa njia ya kutuma ujumbe mfupi wa simu unaandika
"INV UDOM JOSEPH LUKAZA 3rd year" alafu unatuma kwenda namba 0653202000.
Na unaweza kupiga kura kwa kutumia tovuti
 
                             

Wednesday 9 May 2012

Jikoni Leo;Kitabu cha Mapishi cha da'Miriam Rose.Mapishi ya vitumbua kutoka kwa da'Cecy!!!

Cookbook Sneak Peek – Kitabu cha mapishi

Muonekano wa kitabu cha mapishi cha"A Taste of Tanzania".

Cover ame-Design Mwenyewe na Picha amepiga mwenye.Kitabu kitatoka hivi karibuni.

Utakipataje;Ataweka wazi jinsi gani unaweza kupata Kitabu.Ukiingia pale kwake kunasehemu ya mawasiliano,Unaweza kuwasiliana nae Zaidi kupitia http://www.tasteoftanzania.com

Jee da'Miriam anajua KISWAHILI?JIBU;Ndiyo,anakichapa haswa, kama ulivyoona kwenye ile post iliyopita niliandika ni Mswahili.

Nafikiri nimewajibu nijuavyo Waungwana mlionitumia Email na mlionitumia Messages kwenye sim.Na nimeweka hapa kama kuna wengine waliokuwa na maswali kama haya nao Wamepata Jibu.

Haya Waungwana pata mapishi ya UJI na FUTARI kutoka kwa da'Miriam Rose.Hapo juu.

Hapo chini;Mapishi ya "VITUMBUA"Kutoka kwa da'Cecy anapatikana http://mapishinacecy.blogspot.co.uk.

Mswahili mimi kupika vikorombwezo saaaana siweziiiiii,Najua kupika kiasi cha Kula  MUBENA yangu na Watoto yangu na Wageni kidogo tuu,Si kila mtu anaweza kila kitu jamani, Watu na VIPAJI Vyao.MIMI nitakuwa nakurushia Matukio tuu hapa.Na nikipata Muda nitaweza Kuwatembelea Wapishi Nyumbani kwao na Kuwawekea MAZUNGUMZO na MAPISHI HAPA!!AU VIPI WAUNGWANA.SWAHILI NA WASWAHILI!!!PAMOJA SANA TUU.

Monday 7 May 2012

Jikoni Leo;Mswahili,da'Miriam Rose Kinunda,Pishi-Green Bananas na Mengine meengi ya kujifunza!!!


Da'Miriam Rose
imi huwa navutiwa mnoo na kazi zake dada huyu.Huwa sisiti kumuuliza pale nitakapo kujua zaidi.Sijapata nafasi ya k
HayaWaungwana leo nimewaletea da'Mriam Rose wa Kinunda.


Mukutana nae,Lakini kwa mawasiliano tuu kwangu ni mtu asiye na Majivuno,dharau,Umimi/Ubinafsi.Ni dada Mcheshi na mwenye Upendo, na meeengi.


Hongera sana na Ahsante sana da'Miriam Rose kwa yooote,Mungu azidi kukubariki.


Kufahamu zaidi kazi zake na yeye ni nani ingia "Taste of Tanzania"   http://www.tasteoftanzania.com

Sunday 6 May 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani- Pote Atawala,Unibariki,Umechoka!!!!!!

9:Nami nawaambia,Ombeni nanyi mtapewa;Tafuteni,nanyi mtaona;Bisheni,nanyi Matafunguliwa.

13:Basi,ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema,Je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao Wambombao?


Neno la Leo:Luka Mtakatifu;11:1-13.
Mbarikiwe sana na muwe na wakati mwema.

Saturday 5 May 2012

SHIME TUSHIRIKIANE KUMSAIDIA MWENZETU;WIMBO,TANZANIA ALL STAR- MBONI YANGU.


Wimbo huu ni maalum kwa ndugu yetu msanii Sajuki ambae anahitaji mchango wako wako wa hali na mali kuokoa maisha yake. Sajuki anasumbuliwa na uvimbe tumboni na mwezi huu anahitajika kusafiri kwenda nchini India kwa matibabu.
Wimbo huu unatoka katika filamu aliyowahi kuifanya na mkwewe ya MBONI YANGU.Na wimbo huu upo ndani ya filamu hiyo aliuimba Wastara.Wimbo huu umerekodiwa kuhamasisha na kumchangia Sajuki. Kutoa ni moyo bado hujachelewa. Unaweza kutuma mchango wako kupitia AKIBA BANK A/C # 050000003047 A/C ni ya mke wake Sajuki, Wastara Juma au unaweza kutuma kupitia M PESA 0762189592.

Mimi na wewe tunahitajika katika hili.

Habari zaidi na Picha,utazipata. http://www.jestina-george.com

Sajuki na Mke wake Wastara.
Sajuki alivyokuwa na Alivyo sasa.


Pole sana utapona tuu.

Pamoja waungwana.

Thursday 3 May 2012

Siku ya "Uhuru wa Habari" Duniani


        Ngoma Africa band yatoa salam za hongera kwa wanahabari


Bendi ya maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa band" aka FFU
yenye maskani yake nchini Ujerumani ,inatoa salam za hongera na pongezi nyingi
kwa wanahabari na vyombo vya habari vyote duniani,katika sherehe ya siku ya 
"uhuru wa vyombo vya habari" 3 Mai 2012,bendi hiyo inawapongeza wanahabari
na vyombo vyao,kwa kazi muhimu wanazofanya za kuwapasha habari walimwengu,
kwani mchango wa wanahabari katika kila jamii duniani,ni sawa na mbolea katka maisha 
ya kila siku,kwani maisha bila ya habari ,ni sawa miti bila mizizi,
Hongereni sana wanahabari na Wanalibeneke wote duniani.
FFU wa Ngoma Africa band sasa wanatamba song lao jipya
"Uhuru wa habari" wimbo ambao unasikika at www.ngoma-africa.com
au http://www.ngoma-Africa.com