Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 7 May 2012

Jikoni Leo;Mswahili,da'Miriam Rose Kinunda,Pishi-Green Bananas na Mengine meengi ya kujifunza!!!


Da'Miriam Rose
imi huwa navutiwa mnoo na kazi zake dada huyu.Huwa sisiti kumuuliza pale nitakapo kujua zaidi.Sijapata nafasi ya k
HayaWaungwana leo nimewaletea da'Mriam Rose wa Kinunda.


Mukutana nae,Lakini kwa mawasiliano tuu kwangu ni mtu asiye na Majivuno,dharau,Umimi/Ubinafsi.Ni dada Mcheshi na mwenye Upendo, na meeengi.


Hongera sana na Ahsante sana da'Miriam Rose kwa yooote,Mungu azidi kukubariki.


Kufahamu zaidi kazi zake na yeye ni nani ingia "Taste of Tanzania"   http://www.tasteoftanzania.com

Sunday 6 May 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani- Pote Atawala,Unibariki,Umechoka!!!!!!

9:Nami nawaambia,Ombeni nanyi mtapewa;Tafuteni,nanyi mtaona;Bisheni,nanyi Matafunguliwa.

13:Basi,ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema,Je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao Wambombao?


Neno la Leo:Luka Mtakatifu;11:1-13.
Mbarikiwe sana na muwe na wakati mwema.

Saturday 5 May 2012

SHIME TUSHIRIKIANE KUMSAIDIA MWENZETU;WIMBO,TANZANIA ALL STAR- MBONI YANGU.


Wimbo huu ni maalum kwa ndugu yetu msanii Sajuki ambae anahitaji mchango wako wako wa hali na mali kuokoa maisha yake. Sajuki anasumbuliwa na uvimbe tumboni na mwezi huu anahitajika kusafiri kwenda nchini India kwa matibabu.
Wimbo huu unatoka katika filamu aliyowahi kuifanya na mkwewe ya MBONI YANGU.Na wimbo huu upo ndani ya filamu hiyo aliuimba Wastara.Wimbo huu umerekodiwa kuhamasisha na kumchangia Sajuki. Kutoa ni moyo bado hujachelewa. Unaweza kutuma mchango wako kupitia AKIBA BANK A/C # 050000003047 A/C ni ya mke wake Sajuki, Wastara Juma au unaweza kutuma kupitia M PESA 0762189592.

Mimi na wewe tunahitajika katika hili.

Habari zaidi na Picha,utazipata. http://www.jestina-george.com

Sajuki na Mke wake Wastara.
Sajuki alivyokuwa na Alivyo sasa.


Pole sana utapona tuu.

Pamoja waungwana.

Thursday 3 May 2012

Siku ya "Uhuru wa Habari" Duniani


        Ngoma Africa band yatoa salam za hongera kwa wanahabari


Bendi ya maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa band" aka FFU
yenye maskani yake nchini Ujerumani ,inatoa salam za hongera na pongezi nyingi
kwa wanahabari na vyombo vya habari vyote duniani,katika sherehe ya siku ya 
"uhuru wa vyombo vya habari" 3 Mai 2012,bendi hiyo inawapongeza wanahabari
na vyombo vyao,kwa kazi muhimu wanazofanya za kuwapasha habari walimwengu,
kwani mchango wa wanahabari katika kila jamii duniani,ni sawa na mbolea katka maisha 
ya kila siku,kwani maisha bila ya habari ,ni sawa miti bila mizizi,
Hongereni sana wanahabari na Wanalibeneke wote duniani.
FFU wa Ngoma Africa band sasa wanatamba song lao jipya
"Uhuru wa habari" wimbo ambao unasikika at www.ngoma-africa.com
au http://www.ngoma-Africa.com






Monday 30 April 2012

Wimbo Mpya "Uhuru wa Habari" kutoka Ngoma Africa band aka FFU





                  FFU wa Ngoma Africa Band wameachia Jipya "Uhuru wa Habari"
                  Unasikika at www.ngoma-africa.com


Kwa kawaida wanahabari na vyombo vyao ndio wanarusha hewani habari za
matukio mbali mbali pamoja wasanii na burudani zao kwa jamii,
Lakini bendi maarufu Ngoma Africa aka FFU imewageuzia kibao !!
Kuliweka hewani song jipya "Uhuru wa habari" wimbo huo mpya
utunzi wake kamanda Ras Makunja akiimba kwa kushirikiana na
kijana Christian Bakotessa aka Chris-B,ambaye pia ni mpiga
gitaa la solo(mtutu) wa kikosi kazi iko.
Bendi hiyo maarufu Ngoma Africa yenye makao yake kule ujerumani,
miezi michache tu iliachia hewani CD ya "Miaka 50 ya Uhuru" na sasa
wanarusha hewani "Uhuru wa habari" ,
Taarifa za kuhaminika zinaeleza kuwa Remix ya wimbo huo pia itakua
hewani siku za usoni,katika Remix hiyo kutakua na majina mengi ya wa
dau wa habari ambao wanachangia kuijulisha jamii habari mbali mbali.
Sikiliza na pata burudani ya bure katika ffu camp at www.ngoma-africa.com
au http://www.ngoma-africa.com


















Sunday 29 April 2012

Nawatakia J'Pili Njema;Burudani-liko lango moja wazi,Bwana Usehemu Yangu,Si Mbali



Nawatakia J'Pili Yenye Furaha,Upendo,Uvumilivu,Fadhili,Busara,Kiasi na Shukrani.
Utamlinda yeye ambaye moyo wake  Umekutegemea katika Amani Kamilifu,Kwa kuwa Anakutumaini
Neno la Leo;Isaya 26:3-4.
Mbarikiwe Woooote.