Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 9 April 2012

MAMA KANUMBA KAFIKA DAR NA RATIBA YA MAZISHI KAMA IFUATAVYO!!

 


WAKATI MAOMBOLEZO YA MSIBA YAKIENDELEA VIONGOZI MBALIMBALI WAKIFIKA KUTOA MKONO WAPOLE  AMBAPO LEO MHESHIMIWA PREZIDAR J.K ALIFIKA NYUMBANI KWA KANUMBA KUTOA MKONO WA POLE, NA KESHO ASUBUHU WAZIRI MKUU MHESHIMIWA PINDA ANATARAJIWA KUFIKA  KUTOA MKONO WA POLE KABLA YA KUELEKEA MKOANI DODOMA KWA AJILI YA BUNGE LINALOANZA JUMANNE
 RATIBA YA MAZISHI IMETOLEWA RASMI AMBAPO MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA SIKU YA JUMANNE KAMA ILIVYOKUWA IMEPANGWA, MAREHEMU ATAAGWA KATIKA VIWANJA VYA LEADERS CLUB AMBAPO KUANZIA SAA 4 SHUGHULI ZA MISA NA KUAGA MWILI ZITAANZA NA KISHA MAREHEMU ATAZIKWA KATIKA MAKABURI YA KINONDONI JIJINI.
R.I.P KANUMBA
Habari hii kutoka http://8020fashions.blogspot.co.uk.

Ahsanteni sana.

Saturday 7 April 2012

MAMA KANUMBA AONGEA;Mmmmmhh Pole sana Mama!!!!!!

Mama Mzazi wa Kanumba.
Mmmmhh,Pole sana Mama,Mungu akutie nguvu.
Picha na Video,kutoka ;http://bukobawadau.blogspot.co.uk   Ingia hapo kujua zaidi.Ahsanteni sana.

Ulale kwa Amani Kaka Steven Kanumba!!!!!

Steven Kanumba Enzi za Uhai Wake.
Poleni sana Ndugu,Jamaa,Marafiki,Majirani,WaTanzani na Wapenzi Woote Wa KANUMBA!!
Sisi tulimpenda sana Lakini Mungu amempenda zaidi,Tulie na Kumshukuru Mungu kwa Kila jambo,Sote ni Wapitaji katika hii Dunia,Mwenzetu Ametangulia,Inauma sana lakini hatuna Jinsi,Tukumbuke na Kuenzi Mema yote aliyoyatenda.Tuwe tayari wakati wote kwani hatujui Siku wala Muda,Tupendane na Tusameheane.Mungu awatie Nguvu Wafiwa katika Wakati huu Mgumu.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE NA LIHIMIDIWE MILELE;
AMINA.

Thursday 5 April 2012

Watoto na Mitindo,Kutoboa/Kutoga Masikio!!!!

Haya Waungwana;Wazazi/Walezi Unaonaje watoto kutoboa/kutoga masikio wakiwa Wadogo?jee Tunawafurahisha au Tunajifurahisha?ni vyema atoboe/kutoga yeye mwenyewe akikua au bora tuwafanyie labda wakikua watatulaum?
Karibuni Sana kwa Maoni na Ushauri.Pamoja!!!!!!

Tuesday 3 April 2012

Shilingi ya ua tena Maua!!!!!!!


Waungwana sina la kuongezea hapo!!Jee Pesa ni kila kitu?Karibuni sana kwa Maoni na Kuelimishana kwa Upendo.

NDG. OMARY MJENGA MWAKILISHI WA UNOPS NCHINI SIERA LEONE AMALIZA ZIARA YAKE NCHINI.


Ndg. Omary Mjenga akipiga picha ya kumbukumbu wakati alipokwenda kumtembelea na kumuaga Rais Jakaya Kikwete jana Ikulu.
Hapa ndugu Mjenga akipiga picha na Naibu Waziri wa Jinsia, Watoto na maendeleo ya jamii, wakati alipokwenda kumtembelea.

Baada ya kutoka kuonana na Viongozi hao alishiriki Dinner Party na Wanafunzi wenzake aliosoma nao Shule ya Sekondari Songea Boys ndani ya viunga vya Rose Garden akiwemo na Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Mh. Philipo Mulugo.
Picha zaidi mtazipata baadae za tukio hili la kihistoria, ambalo kwa mara ya kwanza lilifanyika katika Pub ya KAPINGAZ Pub wakati huo tukimpongeza Naibu Waziri Mh. Mulugo kwa kuteuliwa.
Wana BOX 2 (Wana Luhila) walimpendekeza Ndg. Henry O. Kapinga kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mpaka pale tutakapo itisha uchaguzi Rasmi.

Omary Mjenga anaondoka leo kurudi Siera Leone tayari kwa kuendelea na kazi zake za UNOPS.

Habari kutoka http://kapingaz.blogspot.co.uk/
Ahsante sana.

Sunday 1 April 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani-AIC Chang'ombe na Bahati Bukuku,Sikiliza mwenyewe!!


Wapendwa muwe na J'Pili yenye Amani na Baraka Tele!!!!!!Neno la Leo;zaburi:12;1-8.Bwana UokoeMaana Mcha Mungu amekoma,Maana Waaminifu wametoweka katika Wanadamu.....Endelea.