Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 8 December 2011

Chaguo la Mswahili Leo ;Les Wanyika : Paulina!!!!

Siku kama ya leo kaka Henry Mwana wa Kapinga Alizaliwa!!!!!!



MPIGANAJI SASA ATIMIZA MIAKA KADHAA!!!

Mpiganaji wenu Henry Kapinga wa Blog yenu ya KAPINGAZ Blog leo Tarehe 8/12 ndio siku aliyozaliwa.
Nawashukuru wale wote walionipa Hongera kwa kuukaribia uzee, sasa sijui kama ni wote mnaupenda uzee, manake fainali yake ni shughuli.
ASANTENI SANA!
Nasi Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililojema katika maisha yako.

Monday 5 December 2011

Comment ya kaka Manyanya kwenye post ya Peter Kapinga!!!!!!

Delete
Blogger Goodman Manyanya Phiri said...
Asante Rachel Mdogo wangu kwa habari hizo.

Kwa wengine wasiejuwa jeshi, taarifa yangu ni kwamba wastani wapo aina tatu wa askari popote pale duniani.


1. WAPIGANAJI (THE MEN/TROOPS---"seamen" kama ni wa baharini, "airmen", wenye kutumia ndege). Ngazi ya chini kuliko zote. Hao ndio waliezagaa katika mambo ya filamu pale panomwagika damu. Kama anajina lake kama "fulani", Wazungu watamtambua kama "PRIVATE FULANI". Nchi nyingi watamchukua kijana yoyote yule mwenye nia kupata mafunzo katika ngazi hii.


2. WARRANT OFFICERS (au "sergeant majors"). Shughuli zao hao ni kuchunga nidhamu ya jeshi. Wapiganaji (MEN/TROOPS) hua wanawaogopa sana hawa warrant officers na ukiwa mwanajeshi na umemridhisha WARRANT OFFICER wako basi wewe unayo nidhamu ya hali ya juu. Hua wanapewa mamlaka wao na Waziri wa ulinzi katika mataifa mengi duniani, na kibali wanachopewa na Waziri kinaitwa "A WARRANT" na ndio maana wanaitwa WARRANT OFFICERS. (Kufika wa WARRANT OFFICER utakuwa wastani umepitia uKoporali, Sajenti, Staff Sajenti na kadhalika na unahitaji sana elimu kabla ya kuchaguliwa!)


3. MAAFISA WA KAMISHENI, COMMISSIONED OFFICERS (kama mhusika hapa) nao wanapewa wadhifa na Raisi wa nchi pekee! Kazi zao za msingi jeshini sio kupigana lakini NIKUIMARISHA JESHI KIMAWAZO NA KUTOA MBINU ZA KUPIGANA KWA MAFANIKIO. WANATAKIWA WAWE MFANO WA KUIGWA NA JESHI LOTE PIA NA WANANCHI WOTE! (Kwa kuwa unahitaji elimu ya juu kuwa afisa wa aina hii, nchi nyingi hutachaguliwa kama hujamaliza angalau kidato cha mwisho/Fomu 6 ya Tanzania. Baadhi ya ngazi za kupitia hapo ni CANDIDATE OFFICER, LUTENI, KAPTENI, MEJA, LUTENI KANALI, KANALI, BRIGADIER NA KADHALIKA KATIKA NYADHIFA SASA ZA UJENERALI au "u-admirali" ukiwa jeshini la maji au baharini)



Sasa tuje kwa Bw. Kapinga:


Huyu bwana usimuonee wivu KWANI ANAKAZI KWELI SASA.

Mifano:

1. Popote asipokuwepo Raisi, YEYE ANACHUKUA MAJUKUMU YA RAISI IKISTAHILI. Kwa mfano: mwiko kuumia kwa mwananchi ikiwa afisa yupo karibu na angemuokoa lakini eti afisa hakujisumbua hata kidogo!


2. Awe amevaa sare ya kijeshi au hakuvaa anatakiwa awe muungwana (GENTLEMAN) kuliko Mtanzania yoyote yule mwingine nchini !

(Hii inamaana akiwa D'salaam huyu bwana daima atakuwa amesimama kwa miguu katika usafiri wa daladala kwani si uungwana kuketi wakati mwanamama amesimama!)


3. Asije akaonekana amelewa pombe hata akiwa nyumbani kwake na ANAWEZA KUTIWA MBARONI kwani hastahili AFISA kuwa mlevi! Pia hamna ugomvi au makelele alipokuwepo yeye!


4. Hata katika mifarakano au hatari ya aina gani ya umma yeye asionekane muoga wa kijingajinga , wala asikimbie na kama anataka kujiepusha na hatari hiyo ASIJE AKAONEKANA ANAKIMBIA....huenda anaweza akatia pupa (PANIC) kwa wengine!

5. Yeye ndie wa mwisho kula jeshini na kama chakula ni kidogo watakula wanajeshi wote (TROOPS AND WARRANT OFFICERS) YEYE NDIE MWENYE KUKAA KWA NJAA!

...YOTE HAYA KUTOKANA NA KWAMBA YEYE NI AFISA , AJITOE MHANGA DAIMA!!!!! Na ukitaka kuona mfano mzuri wa afisa tena wa kuigwa: ni Kanali Gaddafi wa huko Libya yeye aliekataa katakata kukimbia mpaka kufa!




Luteni Peter Kapinga, mimi kama luteni kanali wa jeshi la hapa Afrika nakukaribisha sana katika wadhifa wa uafisa. Ninayo ndoto moja tu kwamba kabla sijaenda kaburini jeshi laTanzania, Msumbiji, Malawi, Uganda, Congo, Angola, Namibia, Swaziland, Botswana, Afrika Kusini, Lesotho na nchi zingine LITAKUWA JESHI MOJA TU LA NCHI MOJA LABDA NAWE UTAKUWA JEMEDALI AU FIELD MARSHAL WAKE!

Kazi ipo, Ndugu yangu; lakini siri kukupa mimi ziko mbili

1. Chunga afya yako
2. Chunga dhamira yako)
4 December 2011 14:57

Sunday 4 December 2011

Nawatakia j'pili Njema!!Pata kibao hiki-wakati wakuomba!!!

PETER KAPINGA SIKU ALIPOTUNUKIWA KAMISHENI NA RAIS DR JAKAYA KIKWETE.


Luteni Peter Kapinga

Tarehe 26/11/2011 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kama Amiri Jeshi Mkuu aliwatunuku Kamisheni wanachuo wa Chuo cha kijeshi cha Monduli Mkoani Arusha.

Peter akiwa mmoja wa wahitimu hao anapenda kuwashukuru wote ambao walioshiriki katika kumsaidia kwa namna moja na nyingine mpaka amefikia hapo alipofikia, zaidi anapenda kumshukuru Dada ake Esther Mbapila pamoja na Mr Mbapila kwa kushiriki katika mchakato wote mpaka akafanikisha kupata alichokihitaji.
ASANTENI
Nasi Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililojema katika Yote.

Friday 2 December 2011

OMARY MJENGA NA SHEREHE YA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI NCHINI SIERA LEONE.



Mwakilishi Mkazi wa UNOPS nchini Sierra Leone Bw Omary Mjenga akiwa na Mwakilishi Mkazi wa UNAIDS Bi. Mulunesh, raia wa Ethiopia, kwenye sherehe hizo, ambazo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Sierra Leone Mh Ernest Koroma. Bi Mulunesh aliwahi kuwa Mwakilishi Mkazi wa UNAIDS nchini Tanzania mwaka 1996 hadi 2000.


Thursday 1 December 2011

Jikoni Leo ni Dagaa!!pata na Burudani; Usiniseme-Ali kiba!!!!!!!

           Kitu Dagaa kipo Jikoni
Mimi Napenda zaidi na Ugali,Dagaa kila mtu anaupikaji wake, Mimi wa Chukuchuku,Mafuta Poa tuu,Lakini wa kuungwa/kuwekwa Nazi au Mawese wamenishinda!!Je wewe Mpendwa unapenda Dagaa? Unapikaje na Unapenda Kula na nini na kushushia na kinywaji gani?Karibuni sana Waungwana!!!USINISEME KAMA NAPENDA KULA!!!