Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Watoto na Malezi. Show all posts
Showing posts with label Watoto na Malezi. Show all posts

Tuesday 27 June 2017

Harakati za Wenye Ulemavu Afrika;WAAFRIKA TUACHE KUWANYANYAPAA WENYE ULEMAVU







 Mwezi Juni 2017, tumeshuhudia mshindi wa tuzo ya kimataifa ya upigaji picha kutoka Tanzania.
Samwel  Mwanyika , mwenye Mtindio Ubongo (Down Syndrome) alipokuwa London kupokea tuzo, alikaribishwa na Ubalozi wetu jijini.
Baadaye alizungumza na "Kwa Simu Toka London"
Kilio cha wazazi wake kuhusu namna tunavyowanyanyapaa wenye ulemavu chahitaji kusikilizwa!

Tuesday 3 December 2013

Kipindi cha familia kutoka Jamii Productuion...Majukumu ya Baba katika Familia‏


Karibu katika kipindi hiki cha FAMILIA kutoka Jamii Production.

Katika kipindi cha wiki hii, mjadala wa WAJIBU WA BABA KATIKA FAMILIA umefungua mfululizo wetu wa mijadala kuhusu wajibu wa mzazi kwa familia yake

Mbali na washiriki waliokuwemo studio, pia tumeshirikisha maoni toka kwa wasikilizaji wetu wapendwa waliyotoa kwenye ukurasa wa Facebook
Msimamizi wa kipindi Abou Shatry akifuatilia mjadala

Karibu uungane nasi



Mjadala ukiendelea
Mgeni wetu katika mjadala huu Isidory Lyamuya


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Saturday 10 August 2013

Watoto Na Malezi; Watoto wa zamani,Mnakumbuka Kipindi cha MAMA na MWANA?



Watoto wa Zamani Mpo? Mnakumbuka  MAMA na MWANA/WATOTO WETU/CHEI CHEIIII..Mhh mimi ni mmoja wa waliokuwa wapenzi  wa Kipindi cha Watoto RTD...
Enzi ya Shangazi/Mama, Debora Mwenda,Sango Kipozi,Eda Sanga na Wengine....

Mhhh Chei Chei Shangaziii..Uje tena Shangazii...


Sehemu ya Kwanza ya Hadithi ya Binti Mfalme;



Sehemu ya Pili



Kujua Mengi Kuhusiana na Watoto Nifuate Huku;http://Watotonajamii.blogspot.com Huku Utakutana na Mambo ya Watoto,Wazazi/Walezi.Hapa tutaendeleza Watoto Na Malezi kwani Swahili Na Waswahili ni Mama Leo..Lakini nimetenganisha Mambo Kidoogo..huko ndiyo Penyewe kwa Mambo ya Watoto na Jamii.

Pia kwa Mambo ya Mitindo Nifuate Huku;http://www.mitindoafrica-abroad.blogspot... Kwa Undani Zaidi..
Panapo Majaaliwa/Kwa Mapenzi ya MUNGU ipo siku yote yatakuwa kwenye Nyumba moja.
Yote Haya yapo Ndani ya SWAHILI NA WASWAHILI NA WAPENDAO YA WASWAHILI NA YASIYO YA WASWAHILI YANAYO FAA KUJUZWA WASWAHILI. 

Pamoja Daima.

Wednesday 16 January 2013

Watoto Na Malezi;Child Prostitution - South Africa!!!!







Waungwana;Watoto wetu ni Wapendwa wetu!!!!..Janga la Dunia...Nani wa kulaumiwa?

Mtoto wa mwenzio ni Wako au Mtoto wa mwenzio mkubwa Mwenzio?

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.


Friday 31 August 2012

Watoto na Malezi;Mtoto na Commando na Mtoto na Wachezaji!!!


Waunngwana Wazazi/Walezi;"Watoto na Malezi" Huyu anacheza na wachezaji,huyu anatupatia Picha la Commando!!!.

Duhh Huyu wa Commando kiboko...........Wewe unasemaje kuhusu mtoto mdogo na Wachezaji? na wa Commando jee? Kipaji,Ufuatiliaji mzuri au..
Vipi wewe ulikuwa wapenda nini Utotoni?

Tunasubiri Mtazamo wako.Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Thursday 12 July 2012

Watoto na Vipaji;Aliyah Kolf -Finale Holland's Got Talent na Natalie Okri-Britain's Got Talent!!!!!!

Waungwana, Wazazi/Walezi; Leo tuangalie Vipaji vya Watoto.
Nafikiri kila mtoto anakipaji chake, Jee unajua kipaji cha mtoto wako?Jee unawezaje kujua mtoto wako anakipaji gani?

 Wewe unakipaji Gani na Nani aligundua Kipaji chako?

Pia Watoto/Watu wengi wanapokuwa/Walipokuwa wadogo wana/Walikuwa na Ndoto ya kuwa/kufanya kitu Ukubwani jee NDoto hizi niza kitoto tuu au Wapo Waliofanisha/Wanaweza kumefanikisha NDOTO zao?

 Jee ulipokuwa Mdogo Ulitamani kuwa Nani/Kufanya Kazi Gani ukiwa mkubwa?Mwalimu,Polisi,Nesi,Mama Ntilie,Muimbaji au........!!
 "Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.

Wednesday 27 June 2012

Watoto na Malezi-Tatizo la Ndoa za Watoto;Pata Video!!!!!!!

Waungwana "WATOTO NA MALEZI".
Wazazi/Walezi leo Tuangalie NDOA ZA UTOTONI.


Kwanza nikuulize swali;Jee wewe ulilazimishwa kuolewa/Kuoa?jee Mume/Mke uliyenaye ni chaguo lako? .Jee wewe Umekeketwa?.


Sasa turudi kwa Watoto wetu ndugu zetu,wadogo zetu,Jee unafikiri kukeketwa kunawafaa?
Jee Unaushauri,Maoni,Ujumbe gani kwa Wazazi/Walezi na Jamii kwa ujumla kuhusina na Ndoa hizi za Watoto?.


Karibuni sana Tuelimishane kwa Upendo.
"SWAHILI na WASWAHILI" Pamoja sana.

Thursday 21 June 2012

Watoto na Malezi;Violence Against Children [Ukatili Kwa Watoto]!!!!!!!


Makala hii inaonyesha ukatili dhidi ya watoto na jitihada zinazofanywa na serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakishirikiana na wadau mbalimbali kutokomeza ukatili dhidi ya watoto.

Makala hii imetengenezwa ikiwa ni mwitikio wa hali ya unyanyasaji na ukatili ambayo watoto wanakabiliana nayo. Makala hii imeandaliwa sambamba na uzinduzi wa ripoti ya ukatili kwa watoto ambalo ni agizo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kutokomeza ukatili kwa watoto. Ripoti hii ilizinduliwa na Dr. Asha Rose Migiro, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Waungwana;Wazazi/Walezi Mnamaoni,Ushaurigani katika haya?


Shime Wazazi/Walezi;"Tutokomeze Ukatili  kwa watoto" Tuungane Pamoja katika kuwapenda,kuwatunza,kuwapa Malezi bora,kuwapatia Elimu na Kuwasikiliza.
"Mtoto wa mwenzio ni wako".
"SWAHILI na WASWAHILI" Pamoja sana!!!!

Saturday 16 June 2012

Watoto na Kujifunza Lugha-Pata video ya Mtoto wetu Wa Burundi!!!!

Wazazi/Walezi hapo vipi?Leo sina Mengi nasubiri kutoka kwenu,Mjumbe Hauawiii!!!!"
SWAHILI na WASWAHILI "Pamoja sana!!!!!!!!!!

Thursday 17 May 2012

Watoto na Vituko;Pata na Burudani!!!!!!

Waungwana Mambo hayo, sina la kusema,Zaidi unayo wewe!!!!!!
Pamoja sana sana.Swahili na Waswahili!!!!!!!!

Tuesday 3 April 2012

Shilingi ya ua tena Maua!!!!!!!


Waungwana sina la kuongezea hapo!!Jee Pesa ni kila kitu?Karibuni sana kwa Maoni na Kuelimishana kwa Upendo.

Wednesday 14 March 2012

Watoto na Urembo,Wanapaka Shedoooooo!!!!!!

Wazazi/Walezi hapo vipi?Kuna msemo sikuhizi; Aku babu najiremba mie napishana na Uzee!Nao Watoto sasa;Aku bibi nakufuata hukohuko!!Mambo ya kileo hayo, Zamani ulikuwa huruhusiwi kupaka,Wanja,Poda na vipodozi vingine, mpaka siku ya KUOLEWA!!Eti ukipaka  kabla,Siku ya Arusi hautapendeza!!Na walikuwa Wakisuka Nywele Ufunge kilemba mpaka MUMEO kwanza Aone!!''Hizi hadithi mie nazisikia''.Hahahahahha Ohiiii Leo hii nani umfungishe Kilemba?Tena ukienda salon ndiyo unafunga kilemba kama nywele zimeharibika, ukimaliza tuu kilemba kuleeee,Wataanza kuona kina baba/mama John,Juma,Neema,Pili na mnaopishana Njiani, hee dada wewe Umependeza, Umetoka Chicha na..Nani kakusuka dada mmoja anaitwa YASINTA NGONYANI!!!Muwe na Wakati Mwema Waungwa, Karibu Sana sana.

Thursday 9 February 2012

Friday 27 January 2012

Watoto wa Kiume na Wakike Wanamajukumu Sawa?


Nimatumaini yangu woote Muwazima!!!na Kama kunamgonjwa Pole sana na Mungu akuponye.
Waungwana Eti watoto wa kijijini wa Kiume na Wakike wanamajukumu sawa?Yaani si lazima wote waende kuchota maji pamoja,basi kama huyu anafagia mwingine aoshe vyombo,na ikifika saa ya kujisomea wote wanasoma,ikifika saa ya kucheza wote wanacheza.Najua kila familia inamalezi yake,Jee vipi kwa malezi ya kileo huko kijijini yameweza kubadili muonekano/Majukumu ya watoto? kama si kijiji kizima basi kuna nafuu?na kama hakuna jee tunaweza kuwasaidiaje?Sawa Mwanamke ni mwanamke, Mwanaume ni Mwanaume hilo naliheshimu pia.Jee Vipi na Watoto hawa wa Mjini?

Karibuni sana Wapendwa, kwa Mawazo,Ushauri,Kuelimishana  kwa Upendo.

Tuesday 10 January 2012

Wazazi /Walezi wa sasa na Malezi!!!!!!




                        watoto kutusaidia jikoni.

kusafisha vyumba vyao.

kusaidia kusafisha na sehemu nyinngine
Wabaki na Furaha/Amani.
Ni matumaini yangu wote wazima,
Haya wapendwa,Wazazi/walezi wenzangu,vipi watoto kufanya/kusaidia kazi za nyumbani,
Hii imekaaje/wewe unaonaje?kazi kama kusafisha vyumba,kuosha vyombo,kuaanda vyakula na kazi nyingine nyingi,Jee wewe unafikiri ni Umri gani uliosahihi kwa mtoto kuanza  kumfundisha kazi ndogondogo?naje huu ni Unyanyasaji au ni malezi ya kawaida? naje Kuna kazi za watoto wa kiume na wakike?kama ndiyo jee sisi wenye watoto wa jinsia moja je?Unafikiri watoto wote wanapenda kazi? je kama hataki?.
Mimi binafsi kazi nyingine sikuwa nazipenda kufanya nilipokuwa mtoto,lakini mama alikuwa ananilazimisha, jee alikuwa ananikosea au ndiyo malezi?Jee wewe unapenda/ulipenda kazi zote ufanyazo/ulizokuwa unafanya?.
Mwana Umleavyo ndivyo akuavyo au.......

Karibuni sana Waungwana katika kusaidiana Kimawazo,Kujadili na Kuelekezana kwa Upendo!!












Wednesday 7 September 2011

Watoto wa Shule na Tamaa!!!!!

                       Hawa wanandika kwenye ubao na chaki.
                                  Hawa wanamsikiliza mwalimu kwa tabasamu.
                                Hawa wamenyoosha mkono ili wapewe nafasi ya kujibu/kuuliza.
Baadhi ya Shule  zimeshafunguliwa hapa U.k.
watoto wa shule kila kona sasa, lakini baadhi yao walivyo jiremba mmhh,
mpaka  kugundua kama ni mwanafunzi ipo kazi.

Hili pia lipo kwa baadhi ya shule Afrika/Tanzania, hasa hizi shule za kulipia.
Sijui ndiyo kwenda na wakati auu....... Ninawaza tuu!!!!!


Mpendwa unafikiri kwa nini  baadhi ya watoto wa Shule wanakuwa na Tamaa?[1].Ni utoto tuu wakikuwa wataacha,Kutoridhika na maisha yao au...?[2.] Nivyema kwa watoto wa Shule kuvaa sare za shule au kutovaa sare kila mmoja aje na nguo zake?
[3.]Kupata chakula cha aina moja Shule au kila mtu ajitegemee.

Karibuni sana kwa Maoni,Kuelimishana katika malezi ya watoto wetu!!!!!!