Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Wanawake na Urembo. Show all posts
Showing posts with label Wanawake na Urembo. Show all posts

Wednesday 12 February 2014

Wanawake Na Urembo-Nywele,Makeup!!!!



Waungwana;Wanawake na Urembo, jee wewe kwako UREMBO ni nini?
Kila Mwanamke  anacho anachokipenda kukifanya,kuboresha UREMBO wake,Wapo wanaopenda kunyoa Nyusi,Kupaka Wanja,Rangi za mdomo,Kusuka,Kuweka Nywele Bandia,Kucha na Mengine meengi.Jee wewe Wapenda nini?

kwapicha zaidi ingia;http://www.mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/


"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Thursday 27 September 2012

Wanawake na Urembo;Burudani-P-Square - Beautiful Onyinye ft. Rick Ross!!!!







 Waungwana;"Wanawake na Urembo" Urembo ni nini na Jee wewe kwamtazamo wako Mwanamke Mrembo  yukoje?Au wewe nini kinakuvutia kwa Mwanamke?
Sina Meengi ngoja Tusikie Wengine Mnasemaje.

Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.......

Monday 17 September 2012

Wanawake na Urembo;Ya Kale ni Dhahabu,Burudani-LES WANYIKA BARUA YAKO!!!!!!


 Waungwana; "Ya Kale ni Dhahabu" Alikuwa kabin'ti Enzi hiizo, sasa ni mama .
 Kuna kitu chochote unakumbuka katika picha hizi? Hizi nguo sijui zilikuwa zinaitwa Bahama au.......?

Karibuni sana Waungwana katika Yoote.kama Unapicha  za  Zamani unataka tuzirushe hapa, Usikonde Tuma;rasca@hotmail.co.uk. 

"Swahili  Na Waswahili" Pamoja Daima.

Wednesday 22 August 2012

Miss East Africa Belgium 2012Juliana Pierre!!!!!!!



Miss East Africa Belgium 2012
Mwakilishi wa Tanzania kwenye fainali Miss East Africa Belgium yatakayofanyika tarehe 1 September 2012, Miss Juliana Pierre

Muunge mkono mwakilishi wetu huyu kwenye Fainali husika kwa kuongeza  idadi ya kufahamika kwake.
Juliana anaomba uingie kwenye ukurasa wake wa (Face book) na kubonyeza kitufe cha “like” kwa anuani hii: https://www.facebook.com/JulianaPierreFinalisteMissEastAfricaBelgium2012

Tuesday 31 July 2012

Wanawake na Mitindo;Leo Mashungi/Kujitanda!!!!!!


Waungwana Leo Tuangalie Uvaaji huu Sijui kama ni Mwezi huu wa Ramadhani au Msibani/Hitimani au.....


Ukienda Rumi Fanya kama Wafanyavyo Warumi, Ukikuta Wenyeji Wanakunja Miguu nawe Kunja yako!!!!!


Kwenye Picha hizi si Woote waavaaji hivyo kila siku Waliheshimu Sehemu Husika.


Wewe unamawazo,Maoni,Ushauri Gani katika hili?


Jee nawe unapicha yako Umevaa hivi?Ruksa kushiriki Nasi, Unaweza kututumia rasca@hotmail.co.uk


Jimwage mwanakwetu!!!!" "
RAMADHANI NJEMA KWA WOOOTE"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Wednesday 4 July 2012

Wanawake na Urembo-Kunyoa Nyusi -Burudani Kipepeo!!!!!!



Waungwana Leo tuangalie Unyoaji Nyusi, Sikuhizi hata Waume wananyoa Nyusi.
Jee wewe  Unapenda kunyoa nyusi?
 Ungependa Mkeo/Mumeo,Mpenzi wako Anyoe Nyusi?


Jee unatumia njia gani?Jee unapenda kutoa zote au unapunguza tuu?


Hivi Watu wa Zamani nao walinyoa Nyusi?
Kunyoa Nyusi kunaweza kusababisha madhara yoyote kiafya?


Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.


"Swahili NA Waswahili" Pamoja sana!!!

Monday 14 May 2012

Wanawake na Urembo;Ya kale ni Dhahabu!!!Burudani-Rangi ya Chungwa,Pamelah!!

Mrembo wa enzi hizooooo
Nipe siri ya urembo huu


Waungwa Leo nimewaletea Mrembo wa zamani kidogo,lakini mimi kwangu bado wananibamba sana.
Angalia hajajichubua,Hana makoroooombwezo meengi,Shedo za kuwaaakaa,Jee Hajapendeza?

Na sasa naona kama vimitindo tindo vya zamani  vinarudi, Sijui kukosa ubunifu, Ya metushinda au kukumbukia Enzi?

Huyu yeye hakuweka dawa Nywele wala kusuka,Lakini wapo pia wazamani waliokuwa wakisuka,Nywele za Uzi,Rafya,Jicho la mke wenza,Kilimanjaro, walibana Mchicha, waliweka Zazuuu, wali roli , Waliweka Kan'ta, Walifunga Vilemba  na..... duuuh nimengi nao Walikuwemo sana tuu.

Jee kunachochote cha Mitindo ya Zamani wewe bado Unapenda au Kukumbuka? na nini Kimekugusa/Kuvuti,  kwa huyu Mrembo?
Unapicha za BABA/MAMA za Wakati huo wakiwa Vijana na Unapenda Tujifunze Mitindi yao?

Usiwe na Tabu Unaweza kututumia Kupitia email.rasca@hotmail.co.uk

Karibuni sana Waungwa!!!!!

Tuesday 13 March 2012

Wanawake na Mitindo ya Nywele,Pata na kideo Jinsi ya kuweka Nywele Bandia!!!!!!

Haya Waungwana Mitindo ya Nywele kwa Wanawake, Mmmh lakini kwa sasa hakuna cha Wanaume wala cha Wanawake, kila mmoja  anajaribu kuingilia Mitindo ya Jinsia nyingine,Au labda mimi ndiyo sielewi, kwamba hakuna Mitindo ya Wanawake na Wanaume Wote ni Sawa!!!!Wewe uliyepita hapa unaonaje?
Swali ;Wanaume wengi Wanaofanya Kazi  SALON zA Wanawake Wengi wao/Baadhi yao ni MASHOGA?

Saturday 10 March 2012

Wanawake na Mitindo-da'Levina na Rafiki zake!! Chaguo la Mswahili-Yvonne Chaka - Mamaland na Umgombothi


                                         Da'Levina[Aliye shika kiuno] na Rafiki katika poziii
                                         Dadazzz mmependeza mnoo,Asanteni sana  kwa kutuwakilisha.Siku ya Wanawake ,Wao walijumuika na wenzao kwa Shamim.Duuhh kivazi cha kanga kikitengenezwa, kinapendeza haswaaa.Wanawatakia Wanawake Woote Duniani ,Baraka, Amani,Upendo na Umoja.WANAWAKE JUU!!!

Wednesday 22 February 2012

Wanawake na Mitindo,Leo Uvaaji wa Miwani!!!!



Nimatumaini yangu woote wazima,Haya Waungwa vipi kuhusu Wanawake wavaapo Miwani,Nikuongeza Urembo,Kuvutia,Haiba,Kujikinga na jua au Wanaficha kitu,Wanaaibu,Wanajishaua? Na jee Wanaona vizuri kweli ?Wewe /Mkeo unapenda kuvaa/Avae Miwani na kwasababu ipi?


Karibu sana Waungwana.

Wednesday 25 January 2012

Wanawake na Urembo,Unapenda Shanga?

                                Wengine wanavaa Kiunoni.
                                     Wengine wanavaa Shingoni
                            Wengine Kichwani,Mikononi...........
Nimatumaini yangu wote muwazima!!!
Haya wapendwa leo tuangalie Urembo huu wa Shanga,Jee wewe Mama,Dada wapenda Shanga?
Nawe Baba,kaka Unapenda Mkeo,Mchumba wako ajipambe kwa Shanga?
Kuna wanaopenda kuvaa Miguuni,kuna Mikanda, Bangili,Hereni naa........,Jee wewe Unapenda/Ungependa Uvae/Avae wapi?Wengine wanapenda za Bendera ya Taifa na......Vyovyote vile ilimradi SHANGAAA!.
Kitamaduni zaidi au Vipi?

Karibuni sana Waungwa!!!!!

Friday 13 January 2012

Wanawake na Urembo!!!!!!!!






Nimatumaini yangu woote wazima,
Haya Waungwana Wanawake na Urembo! Kuna mengi kwenye hizi picha na kwa Wanawake kwa Ujumla,
Mimi leo si msemaji saana,Kazi kwenu nyie na Mitazamo yenu,kipi wewe umependa hapo/Kukuvutia na kipi hujapenda hapo,yaani kama ingekuwa wewe hapo ungeongezea nini au ungepunguza nini,Pia wewe Mwanaume kama ni Mkeo,dada,shangazi na...Ungependa nini aongeze au  apunguze nini?Na jee labda unapenda lakini hujui ufanyeje uwe/awe kama hivyo,au kunakingine unapenda hapo hakipo,Basi usisite kusema/Kutoa Mawazo,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Karibuni sana.


Monday 28 November 2011

Wanawake na Urembo!!!!!!!!

                        Huyu kapaka sijui manjano.......
                        Huyu kawa wa pinki
                        Huyu na manyonyo
                                               Huyu kakaba shingo
                                                Huyu kachora .
Haya Wapendwa Wanawake na Urembo,kila siku yanazuka mapya,Pia ya Zamani yanarudi kama si kukumbukwa.Nao zamani kulikuwa na yao mengi tuu,Zazuu,Kuchoma nywele,Kusukia Rafya[sijui kama nimepatia]na Mengine Meeeeeeengi.

Wasasa kuna wanaopenda Maziwa makubwa mpaka kuyaongeza,Kujichubua/Mkorogo,Kujichora kwa sasa si hina tuu kuna Tattoo tena mpaka kwenye Nyusi, Wananyoa na kuweka tattoo ili wasipate shida ya kupaka Wanja.Kuna wanaoongeza Kope,Kunakuweka Vidubwasha ndani ya macho  na kubadili Lenzi kuwa kama ya Wadhungu. Na Mengine meeengi labda sikuweza kuyaandika au Siyajui Yote hayo kwa SABABU YA UREMBO!
Haya sasa  Mwanamke wewe;Katika hayo yote wewe unapenda nini ili uwe Mrembo au unaweza kuongezea ambayo hayapo hapo nasi Tufunguke,Pia unachukia kipi?

Wewe Mwanaume jee unapenda Mkeo,Mchumba,Rafiki yako wa Kike atoke vipi katika hayo na Unaweza kutujuza ambayo hayapo ili awe Mrembo na Unachukia kipi?

Duuhh Lakini Urembo mwingine unataka Moyo!!
Karibuni sana Wapendwa  kwa Mawazo/Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo!!!!!