Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Msiba. Show all posts
Showing posts with label Msiba. Show all posts

Monday 30 May 2016

TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI


TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI

MAREHEMU JACKLINE OSWALD KAPINGA

Familia ya Marehemu Mzee Oswald Kapinga ya Sinza - Dar e salaam (karibu na  white inn) inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Jacqueline kilichotokea jana tarehe 29/05/2016 katika hospitali ya muhimbili jijini Dar es salaam. 

Familia inapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki ya kuwa, msiba utakuwa nyumbani kwa wazazi wake hapo sinza. 

Taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika, taarifa ya awali kutoka kwa familia, Marehemu wanategemea kumuhifadhi kwenye nyumba yake ya milele siku ya kesho (Jumanne) ya Tarehe 31/05/2016 katika makaburi ya sinza karibu na Ukumbi wa mwika kuanzia saa 8.00 Mchana. 

Kwa taarifa zaidi na maelekezo mbali mbali unaweza kuwasiliana na makaka wa marehemu hapo chini: 

JOSEPH O. KAPINGA (Mwananchi communication)  - 0788617654

GOSBERT O. KAPINGA - 0754286301

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, 
JINA LAKE LIHIMIDIWE
AMEN.



Thursday 1 October 2015

Msiba MAREKANI na TANZANIA


Bettisheba Pole Ketang'enyi enzi ya uhai wake

Tunasikitika kutangaza kifo cha mama Betisheba Ketangenyi, mama yake Yvonne Matinyi, Felicia Simms, Fredderek Ketangenyi pia ni Dada yake na Rossie Musika, Neema Musika, Daudi Musika, Sijaona Musika kilichotekea 9/30/15 katika hospitali ya NIH Maryland mipango ya kusafiri mwili wa marehemu inaendelea kwa mdogo wa marehemu Daudi Musika
3819 Gateway terrace Burtonsville MD 20866
Unaweza kuwasiliana
Frederick Ketangenyi 267 809 5124
Felicia Simms 240 608 8686
Rossie Musika 240 408 2693
Neema Musika 571 991 9819
Specioser Musika 571332 2215
Sijaona Musika 202 487 8412

Tuesday 22 October 2013

MAENDELEO YA MSIBA WA BI MARTHA SHANI WASHINGTON DMV


                                          Marehemu Martha Shani[1976-2013]
Marehemu Bi Martha akiwa na mumewe Alex Pamoja na watoto wao Jose naChris 
                                         
                                   
NDUGU YETU ALEX KASSUWI BADO ANAHITAJI MSAADA WETU WA HALI NA MALI ILI KUWEZESHA KUSAFIRISHA MWILI WA MPENDWA MKE WAKE ALIYEFARIKI GHAFLA SIKU YA JUMAMOSI OCT 19, 2013.

KUTOA NI MOYO NA CHOCHOTE UTAKACHOWEZA KITASAIDIA NA HATIMAE KUWEZESHA SAFARI HII NDEFU YA KUMPELEKA MAREHEMU KATIKA MAPUMZIKO KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE TANZANIA

GHARAMA ZA MSIBA KUSAFIRISHA MAREHEMU NA FAMILIA YAKE NI $19,500

FEDHA ZILIZOPATIKANA HADI SASA NI $4,300
ZILIZOBAKI $ 15,200

TAFADHALI TUMA RAMBI RAMBI ZAKO KUPITIA ACCOUNT IFUATAYO :-
# 446030759150 BANK OF AMERICA,MD
ROUTING # 052001633
MAJINA KWENYE ACCOUNT NI ALEX KASSUWI & FAITH ISINGO

CHEKI ZINAWEZWA ANDIKWA KWA ALEX KASSUWI AU FAITH ISINGO.

PIA UNAWEZA KUTOA RAMBIRAMBI ZAKO KWA KUFIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU AMBAKO NDIKO MSIBA UPO
ADDRESS NI

482 ARWELL CT
FREDERICK, MD,21703

AU WAWEZA WASILIANA NA MMOJA YA WANAKAMATI HAPO CHINI NA KUMUELEKEZA UPO WAPI ILI AWEZE KUKUSANYA MCHANGO WAKO

Tino Malinda -240-565-7133
Dickson Mkama - 301-661-6207
Mariam Mtunguja - 240-422-1852
Quizella Ntagazwa - 240-602-5011
MV Mtunguja- 240-593-0575
Victor Marwa - 240-515-6436
Faith Isingo - 240-705-1055
Julius Manase-240-393-8445

UKISOMA UJUMBE HUU TAFADHALI MTAARIFU NA MWENZIO, MZIGO HUU NI WETU SOTE NA KWA PAMOJA TUNAWEZA

HAKUNA KIDOGO PALIPO NA NIA. NA HAKUNA KIKUBWA PALIPO NA UMOJA.

Saturday 21 September 2013

TAARIFA YA MSIBA WA MAREHEMU LILIAN NABURI - TANGA

R.I.P LILIAN NABURI Bwana Ametoa na bwana ametwaa jinalake libarikiwe     Tuungane jumatatu kumsindikiza mpendwa wetu


Marehemu Lilian Naburi
Familia ya Mzee Geofrey Naburi wa Nguvumali Tanga inatangaza kifo cha Binti yao Mpendwa Lilian Naburi kilichotokea Arusha Jumatano ya tarehe 18/09/2013. Mazishi yanategemewa kufanyika Jijini Tanga siku ya Jumatatu ya tarehe 23/09/2013 katika makaburi ya Bombo.
Kwa mawasiliano zaidi unaweza ukawasiliana na kaka wa marehemu
Ndugu Ben Naburi kwa namba ya simu +255 713 563003
Blog hii inaungana na familia katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.
Bwana alitoa na bwana ametwaa jina la bwana lihimidiwe

Sunday 25 November 2012

TAARIFA RASMI YA MSIBA WA MTOTO MARY SHABANI KACHUA KUTOKA CANADA.


Marehemu Mary Shabani Kachua (3 Yrs) enzi za uhai wake.
Familia ya Dr Shabani Kachua kutoka Canada inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Mary Kachua kilichotokea tarehe 19/11/2012 nchini Canada.
Mwili wake uliagwa jana York Funeral Home, Fredericton, NB. Canada na leo kutakuwa na misa maalum Symthe Cathedral Church, Fredericton, NB, Canada.
Familia ya Dr S. Kachua wataondoka leo Canada kuelekea Jijini Dar es salaam Tanzania kwa ajili ya kuupokea mwili na wanatarajiwa kufika kesho jumapili saa 7:30 Mchana kwa ndege ya Ethiopia Airlines.
Mwili wa marehemu Mary Kachua unatarajiwa kufika siku ya Jumatano tarehe 28/11/2012 kwa ndege ya KLM. Shughuli na taratibu za mazishi zinatarajiwa kufanyika nyumbani Tanga mjini.
Kwa mawasiliano zaidi ya taratibu zote za mazishi unaweza ukapiga namba:
+255 784 670866
+255 713 254553
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi.
Amen

Tuesday 20 November 2012

DR SHABANI KACHUA APATA MSIBA: AFIWA NA MTOTO WAKE KIPENZI.!!!!!!!


Mke wa Dr Shabani Kachua, Jemima akiwa na mtoto wao kipenzi Mary wakati wa uhai wake.
Dr Shabani Kachua
Mama Shabani Kachua akiwa amembeba mtoto wake kipenzi marehemu Mary wakati wa uhai wake.
Mtandao wako unaungana pamoja na familia ya Dr Shaban Kachua katika kipindi hiki kigumu cha majonzi, kwa heshima kubwa tunampa pole sana kwa msiba huu mkubwa ambao wameupata.
Mtoto Mary amefariki Dunia Nchini Canada jana alipokuwa anaishi na wazazi wake, mazishi yatafanyika huko huko.
"BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

Thursday 25 October 2012

TANZIA!!!!!



FAMILIA YA  MAREHEMU MCHUNGAJI MWAKIPUNDA WA NGAMANGA IPINDA KYELA WANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MZEE NSUBISI SAMUEL MWAKIPUNDA (MKURUGENZI WA ZAMANI WA IDARA YA MAELEZO)  KILICHOTOKEA SIKU YA JUMATANO TAREHE 24/10/2012.

MIPANGO YA MAZISHI INAFANYIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU PUGU KINYEMWEZI DAR ES SALAAM.
HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.

KWA MAWASILIANO ZAIDI
+255655994499
BWANA AMETOA BWANA, AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

AMEN

Tuesday 24 July 2012

ENGINEER WA VODACOM JOSEPH MWAPINGA APATA PIGO: AFIWA NA MKEWE.




Marehemu Belinda J. Mwapinga enzi za uhai wake.

Mwili wa Belinda ukiwa katika kanisa la roman katoliki extenal.

Baba Padre akitoa heshima yake ya mwisho kwa mwili wa Belinda. J. Mwapinga jana katika Kanisa la Katoliki Extenal Dar es salaam

Joseph Mwapinga mwenye suti nyeusi akiwa na watoto wake alio achiwa na mke wake kipenzi Belinda.


Wafanyakazi wa VODACOM Tanzania wakiwa wamebeba mwili wa Marehemu Belinda wakiufikisha katika makaburi ya Kinondoni.

Hawa ni baadhi ya waombolezaji waliohudhuria kwenye safari ya mwisho ya Belinda.


Mwili wa Marehemu Belinda ukiwa umewekwa juu ya nyumba yake ya milele katika makaburi ya Kinondoni Dar es salaam.

Mhandisi Joseph Mwapinga akiweka shada la mauwa kwenye kaburi la Mke wake.



Baba Padre akisali sala ya mwisho kwa ajili ya kumuombea Marehemu Belinda J. Mwapinga katika makaburi ya Kinondoni.
kulia kwa Padre ni Joseph Mwapinga na mwenye Tshirt nyekundu ni rafiki wa karibu wa familia, Ndugu Stephen Mapunda.

Marehemu Belinda J. Mwapinga alifariki tarehe 20/07/2012 katika Hospitali ya Muhimbili na mazishi yake kufanyika tarehe 23/07/2012 katika makaburi ya Kinondoni.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIBARIKIWE.


"Swahili NA Waswahili" Tunawapa pole wafiwa. 

Thursday 19 July 2012

MWANAFUNZI WA IFM AFARIKI KIFO CHA KUTATANISHA: AOKOTWA MAENEO YA KOKO BEACH AKIWA HAJITAMBUI!!!!


Marehemu Agnes B. King'unza wakati wa uhai wake.
Agnes alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) akiwa mwaka wa kwanza akichukua Shahada ya Kodi (Bachelor of Taxation).

Mwili wa marehemu Agnes ukiwa kwenye jeneza ulipokuwa ukiwasili nyumbani kwao Mbezi kwa Msuguri.

Mwili wa Marehemu Agnes ukiwa kanisani tayari kwa heshima ya mwisho katika kanisa la Romani katoliki Mbezi Temboni.



Mama Mzazi wa Agnes akilia kwa uchungu baada ya kuona mwili wa Mwanae.


Aliyevaa Koti jeusi ndio baba mzazi wa Agnes Bwana Bernard King'unza.




Makamu Rais wa Serikali ya wanafunzi wa IFM akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya wanafunzi wenzake.
Baba Padre wa Parokia ya Mbezi Temboni akibariki mwili wa Agnes King'unza.


Hawa ni baadhi ya wanafunzi wenzake aliokuwa akisoma nao katika chuo cha usimamizi wa fedha IFM na kushoto mwenye shati la mistari ni mwakilishi kutoka wafanyakazi wa IFM.

Agnes aliokotwa na msamaria mmoja ambaye kwa taarifa za awali zinasema alikuwa ni mlinzi wa nyumba moja maeneo ya Koko Beach ambako ndio alikutwa ametupwa na watu wasiofahamika na kupelekwa kituo cha Polisi cha Oysterbay na baadae kukimbizwa hospitali ya Agha khan.

Marehemu Agnes B. King'unza alifariki Jioni ya tarehe 16/07/2012 katika Hospitali ya Muhimbili ambako alipelekwa baada ya Madaktari wa Hospitali ya Agha khan kushindwa kumtibu na kumrufaa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Mwili wa Marehemu Agnes King'unza umesafirishwa jana Jioni kwenda Nyumbani kwao Kalenga - Iringa kwa mazishi ambayo yatafanyika leo tarehe 19/07/2012.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.


"Swahili NA Waswahili" inawapa pole wafiwa.
Ulale kwa Amani da'Agnes

Tuesday 19 June 2012

TAARIFA YA MSIBA: WILLIAM FOFO MAPUNDA HATUNAYE TENA!!!!!!


Marehemu William Fofo enzi za uhai wake.

Taarifa ambazo zimetufikia hivi punde Ndugu yetu, Rafiki yetu William Fofo maarufu kwa jina la FOFO amefariki dunia usiku huu akiwa nyumbani kwake Tabata.

Taarifa kamili za sababu ya kifo chake bado hatujazipata, pindi tutakapozipata tutawajulisha, kwa sasa taratibu zote inaendelea nyumbani kwake Tabata na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Amana Ilala Dar es salaam.

Tuesday 10 April 2012

Maelfu ya watanzania wajitokeza kumzika Kanumba Jijini Dar !!..pata na [Video]


Safari ya Mwisho ya Mpendwa wetu Kanumba.Sisi Tulikupenda Lakini Mungu amekupenda zaidi.Ulale kwa Amani.
Picha kwa Masaada wa kaka LUKAZA wa http://josephatlukaza.blogspot.co.uk,Ubarikiwe.
Video kwa msaada wa[ Michuzi blog]http://issamichuzi.blogspot.co.uk.Ahsanteni Sana na   Tulie kwa Amani yeye Amekwenda..

Thursday 29 March 2012

MAZISHI YA MAREHEMU DENIS OSWALD KAPINGA


Ndg. Joseph Oswald Kapinga

Ndugu Joseph Kapinga pichani hapo juu anapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki kuwa Ratiba ya mazishi ya mpendwa mdogo wetu Denis O. Kapinga yatafanyika leo Tarehe 29/03/2012 katika makaburi ya Sinza karibu na ukumbi wa mwika.

Ratiba itakuwa kama ifuatavyo:

Mwili wa marehemu utafika Nyumbani maeneo ya Sinza karibu na New White Inn Bar bara bara ya Sinza uzuri mnamo saa 6.00 Mchana kutoka Hospitali ya Mwananyamala.

Mwili utaagwa nyumbani saa 7.00 Mchana na baadae utapelekwa kanisa la Roman Catholic Sinza kwa Ibada.

Baada ya hapo Saa 8.30 Mchana mwili wa marehemu utapelekwa Makaburi ya Sinza kwenye nyumba yake ya milele.

"BWANA ALITOA NA BWANA 

Poleni sana Familia ya Kapinga.
Swahili na Waswahili tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu kwenu.

Mungu awatie Nguvu.
Ulale kwa Amani kaka Denis.O.Kapinga.

Friday 10 February 2012

Harambee ya Msiba wa Mtanzania Mwenzetu,Washington DC.Kutoa ni Moyo!!!

Marehemu Christavina Kusaga Cryor
Familia ya Kusaga inawaomba watanzania wote walioko Marekani na hasa eneo la Washington DC na vitongoji vyake kushirikiana nao katika harambee (fundraising) ili kupata pesa ya mazishi ya mtanzania mwenzetu Christavina Kusaga Cryor aliyefariki February 7, 2012 kwa sarakani ya utumbo.

Marehemu alikuwa akiishi Landover, MD. Ameacha mume na watoto wawili- mvulana wa miaka 4 na msichana wa miaka 2. Alikuwa akisumbuliwa na cancer ya utumbo.

Tafadhali fika tushirikiane kusaidia mume wake na watoto na familia wamzike mpendwa wao. Jumla ya gharama za mazishi ni $11,000, na mpaka sasa tuna $3,000. Tunashukuru kwa waliokwisha saidia.

Harambee itakuwa Jumapili February 12, 2012, kuanzia saa 8.30 mchana (2.30pm).

Anuani ni: 3621 Campus Drive, College Park, MD 20740.

Kwa wale wa mbali au wasioweza kuhudhuria tafadhali tusaidie mchango wako kwa kutumia Capital One Bank, Account# 1351500235; Routing # 255071981. Jina la Account ni Lavorn Cryor. Tafadhali eneza habari hii kwa ndugu na marafiki wote. Asanteni sana kwa ushirikiano wenu katika wakati huu mgumu.

Kwa habari zaidi mpigie: Magoma (202.607.1976); Adelaida (240.602.3183); Matinyi (301.792.2832); Mkakile (240.938.3177); Teddy (301.254.4169); Makaya (202.460.1044); Latifah (240.603.7353); au Rebecca (202.580.4648).

M/Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amen

Friday 30 December 2011

Ulale kwa Amani Bw,John Ngahyoma!!!!!!

Shirika la utangazaji la habari BBC, limepata pengo kwa kuondokewa na Bw. John Ngahyoma.
Aliefariki dunia leo asubuhi jiji Dar es salaam.


Enzi za uhai wake Bw.John Ngahyoma aliwahi kufanya kazi katika kituo cha habari cha Radio Tanzania Dar es salaam(RTD),ITV Radio One na baadaye TVT.
Mpaka mauti inamfika Bw.Ngahyoma alikuwa anaitumikia BBC.


Msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata

Taarifa imetolewa na katibu mkuu jukwaa la wahariri BwNeville Meena.

Thursday 29 December 2011

Ulale kwa Amani da'Halima Mchuka!!!!!

DADA HALIMA WAKATI WA UHAI WAKE.

Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania, TBC – HALIMA MCHUKA amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya MUHIMBILI Jijini DSM alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa kiharusi.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa TBC CLEMENT MSHANA, HALIMA MCHUKA alikimbizwa katika hospitali ya DAR GROUP na baadae katika hospitali ya Taifa ya MUHIMBILI hapo jana baada ya kuanguka ghafla akiwa katika kituo chake cha kazi eneo la PUGU ROAD Jijini DSM.
MCHUKA alikuwa mtangazajii wa kwanza wa kike wa mpira AFRIKA MASHARIKI.

               Poleni sana Familia ya Mchuka kwa wakati huu mgumu kwenu.


                                                       R.I.P. DA'HALIMA.

Thursday 13 October 2011

Ulale kwa Amani baba Mzee Juma Penza!!!!!!!

Mzee wetu mpendwa Umetutoka tukiwa bado tunakuhitaji.
Leo sina mengi ya kusema;
Mungu akulaze mahali pema peponi Amina.

Poleni ndugu zangu wote mliopo nyumbani Tanzania na Wote tuliopo nje ya Tanzania,
Tuungane pamoja kwa wakati huu Mgumu kwetu Mgumu.

wako Rachel-Siwa[Mwanapenza].


Thursday 24 March 2011

MSIBA KWA FAMILIYA YA MZEE NGONYANI!!!!!!!!!


DADA  ASIFIWE NGONYANI HATUNAE TENA!!.









Mpendwa /Bloga wetu da Yasinta na Familiya ya Ngonyani,Wanasikitika kutangaza kifo cha Binti/dada yao mpendwa ASIFIWE NGONYANI.Kilichotokea tarehe 23/03/2011.Nyumbani Tanzania,kwa maelezo zaidi ingia www.Ruhuwiko.blogspot.com. kwa niaba yangu na familiya yangu na wapenzi/wafuatiliaji wote wa SwahilinaWaswahili, Tunaungana pamoja na Familiya ya Ngonyani katika wakati huu mgumu na kutoa pole zetu kwenu!!!SISI TULIMPENDA LAKINI MUNGU AMEMPENDA ZAIDI!!!.