Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Michezo. Show all posts
Showing posts with label Michezo. Show all posts

Sunday 20 September 2015

Watoto wenye asili ya Tanzania wanyakua vikombe katika SETLC FALL JR. OPEN 2015 Washington, DC‏


Vijana wenye asili ya Kitanzania Briana Kagemuro na Bryan Mwombeki wameonyesha umahiri wa mchezo wa Tennis uliofanyika leo Jumamosi, September 19,2015 katika viwanja vya nyumbani kwao South East Tennis and Learning Center, South East Washington, DC.

Briana Kagemuro alikuwa katika kinyanganyiro cha Wasichana wenye umri wa miaka 12 Singles (Girls 12 singles) ambapo alimshida Isabella De Leo 6-4,6-4; Cassi Chen 7-6,6-3,10-6 na Asha verma 6-4,6-4.



Naye Bryan Mwombeki alipata kombe lake la ushindi la wavulana wenye umri wa miaka 10 (USTA) (Boy's 10 Singles) dhidi ya Jason De Silva 4-0,4-0, Arbert Vardimisky 4-3,4-1; Aarush Rajanala 4-1,4-2.


Bryan Mwombeki




Briana Kagemuro



Briana Kagemuro na Bryan Mwombeki wakiwa katika picha ya pamoja na walimu wao wa mchezo huo mapema leo siku ya Jumamosi Septemba 19, 2015 baada ya kushinda makombe yao.

Saturday 14 March 2015

PAZI REUNION HOUSTON, TEXAS LEO KUWAKA MOTO WACHEZAJI WENGI NDANI YA NYUMBA‏



 Timu ya Pazi wanaume wakipata picha ya pamoja na mashabiki wao walipokua nyumbani kwa madikodiko ambaye pia ni mmoja wa waratimu wa tamasha hili la kumbukumbu ya timu hiyo iliyowika miaka mingi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Tamasha hili lililobeba jina la Pazi Reunion litafikia tamati leo Jumamosi March 14, 2015 kwa mechi kadhaa na kuakumbuka na kuaenzi viongozi na wachezaji wa timu hiyo waliotangulia mbele ya haki.
 Pazi Queens wakiwa katika picha ya pamoja leo patakua hapatoshi.
Patrick Mwigula kutoka South Carolina na Atiki Matata kutoka Uingereza wachezaji wa Pazi waliowika miaka ya nyuma wakijadili mchezo wa leo kama walivyokutwa na kamera ya Vijimambo.
 Atiki Matata na Richard Kasesela wakipata picha ya pamoja.
Kulia ni Masawe shabiki wa Pazi wa miaka mingi si mazoezi si mechi alikua hakosekani uwanjani hapa akisalimiana na Richard Kasesela mara tu walipoonana baada ya kupoteana kwa miaka mingi.
Kutoka kushoto ni Emmanuel, Patrick na Kasesela wakikumbushana enzi zao za Pazi.
Wachezaji wa Pazi toka shoto ni Vitalis Gunda toka Maryland, Richard Kasesela toka Tanzania na Willy Crrusa toka Houston, Texas wakikumbushana enzi zao.
Kwa picha zaidi Bofya HAPA

Friday 13 March 2015

Pazi ReUnion USA. Mambo yazidi kupamba moto Houston Texas








 Watatu toka kushoto ni Richard Kasesela alipokua akiwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa George  Bush Intercontinental uliopo Houston, Texas nchini Marekani kwa ajili ya Pazi Reunion itakayofanyika siku ya Jumamosi March 14, 2015 katika uwanja wa mpira wa kikapu wa Pilgrim uliopo katika kanisa la Lutheran lililopo Houston. Wengine katika picha ni wenyeji wake waliompokea,  kutoka kushoto ni Willy Crrusa, Aika na Flora Mochiwa maarufu kama Madikodiko. Mchezaji mwingine anayekuja kwenye maadhimisho hayo ya Pazi toka nje ya Marekani ni Atiki Matata anayekuja siku ya Ijumaa March 13, 2015 akitokea Uingereza. Picha na VIJIMAMBO
 Richard Kasesela akitest uwanja wa mpira wa kikapu mara tu alipowasili uwanjani hapo mara tu baada ya kutoka uwanja wa ndege kushoto ni Davis mchezaji mwingine wa mchezo huo, Flora Mochiwa na Willy Crrusa wakiangalia kama bado wamo. Richard Kasesela richa ya kuwa mchezaji wa Pazi pia aliwahi kuwa Rais wa chama cha mpira wa kikapu Tanzania.
 Wachezaji wa mpira wa kikapu wakipata picha ya pamoja na Richard Kasesela.
 Mdau toka Columbus, Ohio akiwa tayari kushuhudia Pazi Reunion itayaofanyika siku ya Jumamosi March 14, 2015 ndani ya jiji la H-Town.
 Willy Crrusa katika picha ya pamoja na Andrew wakati wakiwa ndani ya madikodiko.
 Wageni wakipata chakula huku maongezi yakiendelea.
Andrew akipata picha ya pamoja na Richard Kasesela.

Friday 13 June 2014

Watoto Na Mitindo,Michezo;Summer Collection;[Maandalizi Ya Familly Fun Day]!!!!!!






Hamjambo Wazazi/Walezi na Watoto wangu Wapendwa?  Summer Time....Wakati wa Jua umewadia,Hiki ni kipindi kizuri sana hapa Ng'ambo kwa Michezo ya Nje,Unaweza kuvaa vizuri na si nguo nyiingi yaani makoti,Masweta na.......Pia kunakuwa na Likizo[Summer Holiday].

Maandalizi Ya  "Family Fun Day" zaidi itakuwa Michezo;Kuchora,Kuimba,Kucheza,Mitindo,Kuangalia Vipaji vya Watoto wetu,Nyama Choma na VyaKula vingine,  Kufurahi Pamoja... na Watoto.

Wengi huwa wanakwenda Likizo Afrika na sehemu nyingine kwa wale watakao kuwepo kwa mwaka huu tutafanya tukutane na kucheza pamoja.
Itakuwa baada ya mfungo wa Ramadhani ili  wote tufurahi pamoja.
  Tarehe 02/08 panapo Majaaliwa.


Kama kuna Ushauri,Msaada katika kuandaa na Mengine yote,Usisite kuwasiliana nami.
Email;rasca@hotmail.co.uk.
Simu;0750 44 100 40.


Wote Mnakaribishwa katika Yote.

kuhusu mambo ya Watoto zaidi;http://watotonajamii.blogspot.co.uk/

Swali;Kwanini watoto wetu ni waoga?

Kwanini Hawajiamini?
Kwanini wana Aibu?

Monday 9 June 2014

Kuelekea Kombe la Dunia...Mahojiano na Halifa Ramadhan kutoka Brazil‏



Photo Credits: EyesOnNews.com 
Siku chache kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia la Soka huko Brazil, mambo mengi yamekuwa yakizungumzwa kuhusu maandalizi ya michuano hiyo.
Kuna malalamiko na maandamano nchini humo ambavyo kwa hakika vinaleta taswira isiyo njema kuhusu maandalizi ya michuano hiyo
Kutaka kujua mengi, Kwanza Production imefanya mahojiano na Halifa Ramadhan.

Mtanzania mwenye maskani yake nchini Brazil ambaye amezungumzia mengi kuhusu maandalizi ya fainali za kombe la dunia na pia maisha ya nchini humo kwa ujumla.
KARIBU UUNGANE NASI
Kwa maoni ama ushauri tuandikie kupitia kwanzaproduction at gmail.com

Saturday 8 February 2014

Rekodi katika michuano ya Olimpiki Sochi‏

Michuano ya 22 ya Olimpiki ya majira ya baridi imeanza jana huko Sochi nchini Russia.
Mabadiliko mengi yametokea katika miaka sita na nusu ya maandalizi yake
Na wakati mamilioni ya watu duniani wakiwa wameelekeza macho na masikio yako huko, kujua nani atashinda nini na nani atavunja rekodi gani, tayari rekodi kubwa zaidi katika michuano hiyo imevunjwa hata kabla ya kuanza kwake.
Na tuipitie safari safari ya maandalizi ya michuano hii mpaka ilipofikia na baadhi ya vikwazo ilivyopambana navyo

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).


Hii ilikuwa ripoti ya Februari 8, 2014


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"