Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Matangazo. Show all posts
Showing posts with label Matangazo. Show all posts

Tuesday 17 March 2015

Kipindi kipya cha Niambie Live kuanza kurushwa kesho


Hiki ni kipindi kitakachozungumzia baadhi ya mambo ambayo yametawala kwenye mitandao ya kijamii.

Kitawajia punde

USIKOSE kukifuatilia

Monday 3 February 2014

African Valentine Special,[Coventry U.K.]!!!!!!!



A special Valentine Party on 14th Feb from 10 till 6am. Come and party African way, nyama choma in the house

Entry £5, Venue Fatty Cats Night club, Foleshil

457 FOLESHILL ROAD
CV 6  5AQCOVENTRY, UK.

MORE INFO,CALL:077 72 37 95 24.

Tuesday 25 September 2012

Shindalo la Uchoraji Kwa Taasisi za Kielimu!!!!!



Image Profession ikishirikiana na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa mara nyingine inatangaza kuanza kwa muhula mpya wa pili wa Shindano ya Uchoraji maalumu kwa Taasisi za elimu.
Shindano ambalo pia linajulikana Kama: Educational Drawing Competition au Image Profession Educational Drawing Competition, lina malengo ya kuibua vipaji katika fani ya uchoraji kwa kuzingatia uwekezaji kwa watoto na vijana.
Theme/Wazo kuu la mwaka huu: ART IMITATES LIFE au SANAA HUFUATISHA MAISHA
Makundi ya ushiriki
´   Chekechea,
´   Elimu ya Msingi,
´   Elimu ya Sekondari na  
´   Elimu  ya Juu
Kwa maelezo na taratibu za Shindano tembelea Facebook Page/Group “Tanzania Drawing Competition” au wasiliana na BASATA au
DRAWING COMPETITION – IMAGE PROFESSION,
P O BOX 92 DAR ES SALAAM.
SIMU: +255 222 664 740 / +255 713 484 040
/ +255 714 676 217 / +255 716 430 084

Friday 6 July 2012

MAOMBI YA MCHANGO KUFANIKISHA MALENGO YA SHEREHE YA MIAKA 100 YA HOSPITALI TEULE YA WILAYA YA KARAGWE!!!!!


ELCT/KARAGWE DIOCESE
Kwa wadau wote wa Maendeleo
Mkoa wa Kagera
Yah: MAOMBI YA MCHANGO KUFANIKISHA MALENGO YA SHEREHE YA MIAKA 100 YA HOSPITALI TEULE YA WILAYA YA KARAGWE
- NYAKAHANGA DDH
Somo hapo juu linahusika.
Hospitali tajwa inaadhimisha miaka 100 tangu kuanza kutoa huduma za tiba na afya katika wilaya ya Karagwe. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni: Shabaha Yetu ni Huduma Bora za Afya na Tiba
Maadhimisho hayo yatafanyika tangu tarehe 27 Agosti na kilele kuwa tarehe 2 Septemba. Katika wiki hii, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kutakuwa na maonyesho yatakayoenda sambamba na utoaji wa huduma za afya bure kwa wananchi watakotembelea mabanda yaliyoandaliwa.
Uchunguzi wa afya kama vile Kisukari, moyo, shinikizo la damu, upimaji wa VVU, uchunguzi wa saratani ya matiti kwa akina mama, huduma za macho na uzazi n.k zitatolewa kwa kushirikiana na wataalam wa ndani na nje ya nchi.
Mbali na huduma hizo, malengo makubwa ya hospitali katika kuadhimisha miaka 100, ni kupambana na changamoto zilizopo wilayani na nchini kwa ujumla katika kutoa huduma bora za afya.
Baadhi ya changamoto hizo ni upungufu wa wataala wa kada mbalimbali na uchakavu wa miundo mbinu.
Kupitia sherehe hizi, hospitali ina mpango wa kuanzisha chuo cha taaluma za afya na tiba wilayani Karagwe mapema mwakani.
Chuo hicho kitatoa wataalam katika fani za Uuuguzi, Uganga, wataalam wa Maabara na Maafisa afya.
Ш Faida za Chuo hiki:
o Kusaidia kupunguza upungufu wa wataalam Mkoani Kagera na nchini kwa ujumla.
o Kusaidia vijana wanaomaliza elimu ya sekondari kupata elimu ya taaluma kwa gharama nafuu, zingatia mkoa hauna chuo cha waganga, ni gharama kubwa kwa wazazi kupeleka watoto wao nje ya mkoa kusomea taaluma hio.
o Chuo kitatoa nafasi nzuri kwa watumishi waliopo kazini kuweza kujiendeleza wakingali katika mazingira ya familia zao hivo kupunguza gharama na usumbufu wa kusomea nje.
o Chuo kitasaidia kuongeza ajira hivo kusaidia katika ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja, familia na taifa kwa ujumla.
Katika kufanikisha malengo hayo, jumla ya shilingi 1.8 billion zinahitajika. Ikiwa ni kwa ajili ya uendeshaji wa maadhimisho (utoaji wa huduma bure kwa wiki ya maadhimisho), ukarabati wa miundombinu na ujenzi wa chuo.
Kwa niaba ya menejiment ya hospitali, nakuomba ewe mpenda maendeleo uchangie kufanikisha malengo haya kwa maendeleo ya sekta ya afya.
Wote watakao changia wataorodheshwa katika kitabu maalum cha kumbukumbu.
Kwa mawasiliano zaidi piga simu kwa Mganga Mkuu: 0762 751 335 / 0712 916 800 / 0787 785 969
Shukrani
Dr. Andrew Cesari
Mganga Mkuu
Nyakahanga Hospital

Friday 25 November 2011

CITE- NA MIAKA 50 ya UHURU WA TANZANIA!!!!

Watanzania waishio Uingereza Kufanya Maombi ya Kumshukuru Mungu Kwa MIAKA 50 ya UHURU.

Waandaaji wa maombi ya ya Miaka 50 ya Uhuru chini Uingereza ”Association of Tanzanian Christians in Europe(CITE)” Wakiwa na Mwl Christopher Mwakasege wakati wa Summer Confference 2009.
Mithali 14:34 Biblia inasema Haki ya Mungu huinua Taifa na huu ndio mstari wa kusimamia katika Maombi hayo yanayowajumuisha watanzania wote waishio nchini Uingereza Hususani katika jiji la London. Kwa Mujibu Wa Mchungaji Emmanuel Chatawe ambaye ni mmoja wa waratibu wa Maombi hayo maombi hayo yatahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali.

Pamoja na Maombi hayo pia kutakuwepo na vikundi mbalimbali vya kusifu na kuabudu.Maombi hayo yameandaliwa na Umoja wa wakristo watanzania waishio bara la Ulaya(CITE).

TAREHE:10 Dec 2011

VENUE: Vision Gospel Ministry International 68 Wallis ROAD Hackney Wick London E9 5LH

TIME :13:00 – 18:00 HRS



Wakati Watumishi wa Mungu Kutoka  Tanzania  waishio nchini Uingereza wakijipanga kwa Maombi hayo, Kwa Upande wa Wakristo wa Watanzania Waishio Nchini Marekani wao wanatarajia kufanya Maombi hayo Tarehe 10 Dec 2011 .Kwa Maelezo zaidi juu ya Kusanyiko la Maombi ya Uhuru wa miaka 50 nchini Marekani Fuata LINK hapa chini.


http://hosannainc.blogspot.com/search/label/Watanzania%20Wahudumuo%20Nje


Monday 31 October 2011

COVENTRY NA EID PARTY!!!!!!!!


EID PARTY EID PARTY EID PARTY COVENTRY, U.K.!!!
KARIBUNI SANA WASWAHILI WOTE KATIKA KUSHEHEREKEA EID!!
Party hii ni ya kina MAMA na  WATOTO tuu.


Tarehe  12.11. Itakuwa jumamosi,Itaanza saa 9:00 Mchana [3:00.pm],Mpaka saa 3:00 za Usiku[9:00.pm].

Mahali ni; Moat House Leisure and Neighbourhood Centre,
                  Winston  Avenue,Coventry,Cv2 1EA.

Tiketi zimesha anza kuuzwa!!Wahi Tiketi yako Mapema!!
Bei £5 kwa Mtu mmoja.Watoto chini ya mwaka mmoja wataingia Bure!!Chakula Bure!!Kinywaji 50p.
Pia kutakuwa na michezo  ya Watoto,kama Bouncy Castle na Mingine Mingiiii!!

Kwa Maelezo zaidi na manunuzi ya Tiketi
Wasiliana na;Bi ZAYANA Kwa namba 07889257308.

UKIPATA UJUMBE HUU WAJULISHE NA WENGINE.
KARIBUNI SANA!!!!!!.

Wednesday 28 September 2011

KAPINGAZ Blog na JEZI ZENYE LOGO YAO,KAA MKAO WA KUVAA.!!!






KAPINGAZ Blog SIO MUDA MREFU TUTAKULETEA JEZI ZENYE LOGO YETU KAA MKAO WA KUVAA.

Mfano wa Jezi itakayokuwa na Logo yetu, karibu sana mdau.

Jezi hizi zitakuwa zikigawiwa Bure, haziuzwi. Kama utahitaji usisite kuwasiliana nasi mapema kupitia mawasiliano yetu yaliyopo kwenye Blog. Tunashauri ni vema ukatumia Email ili tuweza kuwa na kumbu kumbu nzuri badala ya simu