Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Makamu wa Rais/Wa Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Makamu wa Rais/Wa Tanzania. Show all posts

Wednesday 18 April 2018

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA WATANZANIA NA WAINGEREZA ,LONDON


Picha na Habari za Freddy Macha

Ulikuwa mkutano mfupi uliokusudia kutoa shukrani kwa wafadhili na Watanzania London wanaosaidia nyumbani. Fadhila hupitia Jumuiya ya Waingereza na Watanzania (BTS) na kitengo chake cha TDT = shirika la Mfuko wa Maendeleo Tanzania. BTS ilianzishwa mwaka 1975, na mlezi wake sasa hivi ni Rais mstaafu Ali Mwinyi.

BTS ilimkaribisha Makamu wa Rais Mheshimiwa Suluhu Samia, aliyekuja London wiki hii kudhuruia mkutano wa Viongozi wa Jumuiya ya Madola.

Kawaida viongozi hutegemewa hotuba ndefu zenye maelezo yanayochosha masikio.

Mhe Suluhu alitua chuo kikuu cha lugha za Afrika na Mashariki ya Kati (SOAS) akasalimiana na kupeana mikono na wananchi wa pande zote mbili. Hiyo tu ilitosha kuonesha imani yake kwa wananchi wachapa kazi wa pande hizi mbili.

 Makamu wa Rais Mhe Suluhu Samia akizungumza na Dk Mohammed Hamza, kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Uingereza




 Balozi wetu Uingereza, Dk Asha Rose Migiro akiwa na Kaimu Balozi Uingereza Tanzania, Mhe Marc Thayre


 Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Uingereza na Tanzania – BTS. Dk Andrew Coulson aliyefungua na kufunga kikao cha Brunei Gallery, SOAS.




 Baadhi ya Watanzania waliohudhuria. Kutoka kushoto, Kiondo Wilkins, Dk Alex Paurine, Simon Mzuwanda na Joe Warioba.