Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Hadithi/maisha. Show all posts
Showing posts with label Hadithi/maisha. Show all posts

Thursday 10 September 2020

Miti na Misitu Thaminiwa Kiafya, Uzunguni







Mimea ni msingi wa uhai. Dunia ya nchi zilizoendelea ni kawaida leo, kwenda katika misitu midogo midogo mijini. Hapa London wakazi huingia maeneo haya yenye miti kabla baada ya kazi au shughuli za kila siku. Hii huchangia afya kwa hewa safi ya miti. Kati ya shughuli ni mbio ndogo za Jogging, kutembea na mbwa, nk.

Thursday 4 June 2015

Maisha;Hadithi Ya Kufundisha...


👌Hadithi ya kufundisha 👌
Siku moja jioni katika mji wa Washindao, kulikuwa na basi 🚍likisafiri kutoka mji huo kuelekea mji wa Wamtumainio.
Lilikuwa ni basi kubwa na limejaa abiria👫👪👬👭👫👪.
Wakati wakiendelea na safari, ghafla, mvua kubwa ☔iliyoambatana na radi⚡⚡⚡ ikaanza kunyesha.
Dereva hauogopa, wala abiria, wakaendelea na safari. Mara wakati wanaenda, radi ⚡ikaanza kufuatilia gari🚎. Kila wakienda, radi inapiga karibu na ⚡🚎⚡basi kana kwamba inalifuata basi. Likisimama, radi⚡ inapiga pembezoni mwa basi🚍⚡.
Dereva kuona hivyo, akasimamisha gari mita 5 kutoka kwenye mti 🚎............🌴. Akawaambia abiria👫👪👬👭👫👪, "Humu ndani ya basi, kuna mtu ambaye leo ni siku yake ya kufa🚷, tena kufa kwa radi⚡.
Ili tusife wote, nataka kila abiria🚶🚍💃 ashuke akaguse mti 🌴🚶💃🌴ili anayepigwa na radi, apigwe wengine wasife kwa ajili yake. "
Abiria wakitetemeka🙌🙇🙌, wakaanza kushuka🚶🚍💃 mmoja mmoja. Unaenda🌴🏃 unagusa mti , kisha unarudi 💃🚍kwenye basi. Abiria wote pamoja na dereva mmoja mmoja, wakaenda, wakagusa mti 🌴🏃na kurudi 💃🚍bila dhara lolote!
Akawa kabaki abiria mmoja tu🙇, ambaye alikuwa hajagusa mti.
Abiria wote kwa macho👀👀👀 ya hasira 😡😡😡wakamwambia akaguse mti. Akawa anaogopa 🙇🙌kufa. Akagoma. Wakamlazimisha kwa nguvu 💪sana na kumtoa nje
.🌴...... .......🚶👈🚍. Yule abiria akiwa amefumba macho😎, akaenda akagusa mti🌴🏃.
🙆Hamadi bin Vuu!
Radi kali sana⚡⚡⚡⚡⚡ ikalipiga basi🚍, abiria na wote waliokuwamo, wakafa palepale😪😔😪.
Kumbe uwepo wake ndio ulikuwa unazuia abiria wengine wasidhurike na radi.
📝MAFUNZO 📝
1. Unapofanikiwa, huwezi jua uwepo wa nani umefanikisha mafanikio hayo, usichukue sifa zote peke yako. Wapatie na wengine bila kumsahau MUNGU.
2. Unaweza kujiona huna thamani sehemu ulipo, iwe kwenye kundi la WhatsApp, darasani, kazini, kwenye basi, barabarani bila kujua kama uwepo wako ni wa muhimu sana kwa ustawi wa wengine.
3. Usimtenge wala kumnyanyasa mtu au jirani yako, huwezi jua uwepo wake unakusaidia kiasi gani.
4. Jali sana watu wako wa karibu, mchumba, mzazi, ndugu, mke, rafiki, jirani nk kwani uwepo wao ndio tunakuona unang'aa siku hadi siku.


Nimetumiwa Na Mpendwa


"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.