Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 4 January 2018

SALAAM ZA MWAKA MPYA;BURUDANI-SLIGHT BEARERS- INUA MACHO,POKEA SIFA,SIFA KWA BWANA..




Salaam Wapendwa/Waungwana;Heri ya Mwaka Mpya..!
Ni matumaini yangu wote mpo salama na Mungu anaendelea kuwapigania..
Tunamshukuru Mungu kwa nafasi hii tena ya kuuona mwaka huu..
Mwaka uliyopita pia natumai ulikuwa na Baraka nyingi hata kama kulikuwa na mapito/Mjaribu yoyote ni changamoto katika maisha..
Mungu wetu atabaki kuwa Mungu..
Mimi namshukuru Mungu kwa yote aliyonitendea,kuna mengi mazuri na yaliyo mema,
Baraka na palipo kuwa na ugumu/mapito ilikuwa njia ya kujifunza zaidi na kujiweka sawa
kwa yanayokuja..
Mwaka huu ukawe mwaka wenye Amani,Upendo,Furaha,Ushidi,Afya njema,Mafanikio,
Mungu akatupe neema ya kufuata njia zake,Tukasimamie Neno lake amri na sheria zake
siku zote za maisha yetu..
Mungu wetu akatubariki nasi tukapate Neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Tukapande katika wema,fadhili,Hekima,Busara na yote yanayompendeza Mungu wetu na tukavune yaliyo yake Mungu wetu..
Uwe Mwaka wa Shukrani,Shuhuda na kujitoa kwa wengine..
Tukawe salama moyoni na Mungu wetu akatuongoze katika yote..
Asanteni sana na Mungu akawatendee sawasawa na Mapenzi yake..
Nawapenda.














"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

No comments: