Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 12 October 2017

Jikoni Leo;Kahawa(Coffee)...

Habari zenu Waungwana..
Nimatumaini yangu wote hamjambo..
Siku nyingi kidogo nimepotea kwa mambo ya jikoni..
Ni muingiliano wa majukumu tuu..

Haya "Jikoni Leo" ni  Kahawa [Coffee]..
Jee wewe unapenda Kahawa? unaipikaje?unapenda kunywa kahawa wapi?
Kijiweni?kwenye migahawa au Nyumbani?
Hapo ulipo/unapoishi watu wanapenda kunywa Kahawa?
 kahawa inanywewa sana wapi
mkoa/mji gani Tanzania?kwa nini? hali ya hewa inaruhusu?Mazoea?Tamaduni? au....
Nilipokulia mimi Dar es salaam Kahawa ilikuwa kuwa inanywewa sana ..
zamani kidogo kulikuwa na vijiwe vya wazee/wanaume wanacheza karata/bao huku wakijinywea Kahawa
pia kulikuwa  na wauza Kahawa, Kashata wa kupitisha mitaani..
Sina uhakika kama utamaduni huu wa kukaa vijiweni
 kunywa Kahawa na kuongea mawili matatu kama bado upo
hata kama upo lakini umepungua sana..
Unafikiri ni kwa nini?Maendeleo?Sehemu za wazi zimepungua?ubinafsi,Hali ngumu au Vijiwe vipo vya kisasa zaidi(Migahawa]
mikubwa ya ndani imeua Vijiwe/vibaraza vya Kahawa?

Mimi hapa nilipo Kahawa inanyweka sana hasa kipindi hiki kinachokuja cha Baridi ndiyo zaidi...
Hata mimi napenda kunywa Kahawa Nyumbani huwa nakunywa hii kutoka Tanzania ,nikiwa Mtaani ni mpenzi wa Cupccino..

Karibu sana Tunywe Kahawa huku tukipeana story/kubadilishana hadithi za maisha,malezi na mengineyo..







"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.



No comments: