Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 17 August 2017

Kikombe Cha Asubuhi;kitabu cha Hesabu..33

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah..!Mungu wetu yu mwema sana na fadhili zake zadumu milele..
Tumshukuru Mungu katika roho na kweli..

Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane. (Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.) Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya; na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria. Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu. Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana. Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.” (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.) Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu). Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekuambia: ‘Nipatie maji ninywe,’ ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yenye uhai.” Huyo mama akasema, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yenye uhai? Au, labda wewe wajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo wake walikunywa maji ya kisima hiki.” Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena. Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uhai na kumpatia uhai wa milele.” Huyo mwanamke akamwambia, “Bwana, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; na, nisije tena mpaka hapa kuteka maji.” Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.” Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume. Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.” Huyo Mwanamke akamwambia, “Bwana, naona ya kuwa wewe u nabii. Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini nyinyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudia Mungu ni kule Yerusalemu.” Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu. Nyinyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi. Lakini wakati waja, tena umekwisha wasili, ambapo wenye kuabudu wa kweli watamwabudu Baba katika roho na ukweli. Maana Baba anawataka watu wanaomwabudu namna hiyo. Mungu ni roho, na watu wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa Roho na ukweli.” Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.” Yesu akamwambia, “Mimi ninayeongea nawe, ndiye.” Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?” Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu, “Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?” Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu. Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, kula chakula.” Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua nyinyi.” Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?” Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake. Nyinyi mwasema: ‘Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika!’ Lakini mimi nawaambieni, angalieni mkaone jinsi mashamba yalivyo tayari kuvunwa. Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uhai wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna.’ Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho; wengine walifanya kazi, lakini nyinyi mnafaidika kutokana na jasho lao.” Wasamaria wengi wa kijiji kile walimwamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.” Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili. Watu wengi zaidi waliamini kwa sababu ya ujumbe wake. Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”

Asante Mungu wetu Baba yetu..
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako wakati wote..
Utukuzwe Mungu wetu,Unastahili sifa..
Uhimidiwe Baba wa mbunguni..

Tunakuja mbele zako Baba wa Mbinguni tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Muumba wetu..
Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mfalme wa Amani nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Baba wa Mbinguni utuepushe katika majaribu,Utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..
Yahweh tunaomba ututakase Miili yetu na Akili zetu  na utufunike
kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazreti..
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..
Mungu wetu tunaomba utubariki na ukabariki kazi za mikono yetu..
na  vyote tunavyoenda kufanya/kutenda tukatende kama inavyokupendeza wewe..
Baba wa Mbinguni ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo..
Jehovah nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba ukatupe kama inavyokupendeza wewe..

Maisha yetu tunayaweka mikononi mwako Mungu wetu..
Ukabariki Nyumba/Ndoa zetu,Watoto/familia zetu,Ndugu na wote wanaotuzunguka Mungu Baba ukawalinde na kuwaongoza vyema..

Roho Mtakatifu akatuongoze vyema na tukapate neema ya kuweza kusimamia Neno lako Mungu wetu,Amri na Sheria zako..
Ukatufanye chombo chema Baba wa Mbinguni nasi tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Tazama wenye shida/tabu,walio katika majaribu mbalimbali,wanaopitia magumu/majaribu Mungu wetu tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,ukawaponye kiroho na kimwili pia..
ukawape neema ya kukujua wewe na kufuata njia zako ..
Ukawakomboe na kuwarudisha wote waliopotea Baba wa Mbinguni..

Wapendwa Mungu wetu ni Mungu mwenye nguvu..
Usihangaike na kutangatanga muite Mungu wetu leo naye asikia..
Mueleze shida zako na mapito yako..
Yanini kubeba mizigo isiyo yako? Ya nini kukata tamaa?
kwanini unateseka yupo Mungu anayeweza yote..
Mpe leo maisha yako,Sema naye,Muombe,Fuata Amri na Sheria zake..
Yeye anatosha..!

“Sikiliza ewe taifa Israeli mtumishi wangu; sikiliza ewe kizazi cha Yakobo mteule wangu. Mimi, Mwenyezi-Mungu Muumba wako, niliyekufanya tangu tumboni mwa mama yako, nimekuja kukusaidia wewe. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema: Usiogope, ewe taifa la Yakobo, mtumishi wangu, naam, usiogope ewe Yeshuruni mteule wangu. “Nitaimwagilia maji nchi iliyokauka, na kutiririsha mto katika nchi kame. Nitawamiminia roho yangu wazawa wako, nitawamwagia watoto wako baraka yangu. Watachipua kama nyasi penye maji mengi, kama majani kandokando ya vijito. “Mmoja atasema: ‘Mimi ni wa Mwenyezi-Mungu’, mwingine atajiita kwa jina la Yakobo, mwingine ataandika mkononi mwake, ‘Wa Mwenyezi-Mungu’, na kujitambulisha kwa jina la Israeli.” Mwenyezi-Mungu, Mfalme na Mkombozi wa Israeli, naam, Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna Mungu mwingine ila mimi. Ni nani Mungu aliye kama mimi? Mwache atangaze na kusema wazi mbele yangu. Nani alitangaza hapo kale mambo ambayo yatatukia? Na watuambie yale ambayo bado kutokea. Enyi watu wangu, msiogope wala msiwe na hofu, Je, sikuwaambia tangu zamani mambo yatakayotokea? Nyinyi ni mashahidi wangu. Je, yuko Mungu mwingine ila mimi? Je, kuna mwenye nguvu mwingine? Huyo simjui!”
Asante Mungu wetu katika yote..
Sifa na utukufu tunakurudishia wewe..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!
Asanteni sana wapendwa/waungwana kwakunisoma..
Mungu aendelee kuwabariki katika yote yampendezayo..
Nawapenda.


Safari kutoka Misri hadi Moabu

1Vifuatavyo ni vituo ambavyo Waisraeli walipiga kambi walipotoka Misri wakiwa katika makundi ya makabila yao chini ya uongozi wa Mose na Aroni. 2Mose aliandika jina la kila mahali walipopiga kambi, kituo baada ya kituo, kwa agizo la Mwenyezi-Mungu.
3Waisraeli waliondoka mjini Ramesesi mnamo siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku moja baada ya Pasaka ya kwanza. Waliondoka kwa uhodari mkubwa mbele ya Wamisri wote, 4ambao walikuwa wanawazika wazaliwa wao wa kwanza wa kiume aliowaua Mwenyezi-Mungu; kwani Mwenyezi-Mungu alikuwa ameiadhibu hata miungu yao.
5Basi, Waisraeli waliondoka Ramesesi, wakapiga kambi yao huko Sukothi. 6Kutoka Sukothi, walipiga kambi yao huko Ethamu, ukingoni mwa jangwa. 7Kutoka Ethamu, waligeuka na kurudi hadi Pi-hahirothi, mashariki ya Baal-sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli. 8Waliondoka Pi-hahirothi, wakapita bahari ya Shamu mpaka jangwa la Ethamu; walisafiri jangwani mwendo wa siku tatu, wakapiga kambi yao Mara. 9Kutoka Mara, walisafiri hadi Elimu; huko Elimu kulikuwa na chemchemi kumi na mbili za maji na mitende sabini, wakapiga kambi yao mahali hapo. 10Walisafiri kutoka Elimu, wakapiga kambi yao karibu na bahari ya Shamu. 11Kutoka Bahari ya Shamu walipiga kambi yao katika jangwa la Sini. 12Kutoka jangwa la Sini, walipiga kambi yao Dofka. 13Kutoka Dofka walipiga kambi yao huko Alushi. 14Kutoka Alushi walipiga kambi yao huko Refidimu, ambapo hapakuwa na maji ya kunywa. 15Waliondoka Refidimu wakapiga kambi yao katika jangwa la Sinai. 16Kutoka Sinai walipiga kambi yao huko Kibroth-hataava. 17Kutoka Kibroth-hataava, walipiga kambi yao huko Haserothi. 18Kutoka Haserothi, walipiga kambi yao huko Rithma. 19Kutoka Rithma, walipiga kambi yao huko Rimon-perezi. 20Kutoka Rimon-perezi, walipiga kambi yao huko Libna. 21Kutoka Libna walipiga kambi yao Risa. 22Waliondoka Risa, wakapiga kambi yao huko Kehelatha. 23Kutoka Kehelatha, walipiga kambi yao kwenye Mlima Sheferi. 24Kutoka Mlima Sheferi walipiga kambi yao huko Harada. 25Kutoka Harada, walipiga kambi yao huko Makelothi. 26Kutoka Makelothi, walipiga kambi yao huko Tahathi. 27Kutoka Tahathi walipiga kambi yao Tera. 28Kutoka Tera walipiga kambi yao Mithka. 29Kutoka Mithka, walipiga kambi yao Hashmona. 30Kutoka Hashmona, walipiga kambi yao Moserothi. 31Kutoka Moserothi, walipiga kambi yao Bene-yaakani. 32Kutoka Bene-yaakani, walipiga kambi yao Hor-hagidgadi. 33Kutoka Hor-hagidgadi, walipiga kambi yao Yot-batha. 34Kutoka Yot-batha, walipiga kambi yao Abrona. 35Kutoka Abrona, walipiga kambi yao Esion-geberi. 36Waliondoka Esion-geberi, wakasafiri na kupiga kambi yao katika jangwa la Sini, (yaani Kadeshi). 37Kutoka Kadeshi, walipiga kambi yao mlimani Hori, mpakani mwa nchi ya Edomu.
38 Taz Hes 20:22-28; Kumb 10:6; 32:50 Kwa agizo la Mwenyezi-Mungu kuhani Aroni alipanda juu ya Mlima Hori, na huko, akafariki mnamo siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arubaini tangu Waisraeli walipotoka nchini Misri. 39Aroni alikuwa na umri wa miaka 123 alipofariki juu ya Mlima Hori.
40Mfalme wa Aradi, Mkanaani, aliyekaa Negebu katika nchi ya Kanaani, alipata habari kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja.
41Kutoka Mlima Hori, Waisraeli walipiga kambi yao Salmona. 42Kutoka Salmona, walipiga kambi yao Punoni. 43Kutoka Punoni, walipiga kambi yao Obothi. 44Kutoka Obothi, walipiga kambi yao Iye-abarimu, katika eneo la Moabu. 45Kutoka Iye-abarimu, walipiga kambi yao Dibon-gadi. 46Kutoka Dibon-gadi, walisafiri na kupiga kambi yao Almon-diblathaimu. 47Kutoka Almon-diblathaimu, walisafiri na kupiga kambi yao katika milima ya Abarimu, karibu na Mlima Nebo. 48Kutoka milima ya Abarimu, walisafiri na kupiga kambi yao katika tambarare za Moabu ngambo ya mto Yordani karibu na Yeriko. 49Walipiga kambi hiyo karibu na mto Yordani kati ya Beth-yeshimothi na bonde la Abel-shitimu kwenye tambarare za Moabu.

Maagizo kabla ya kuingia Kanaani

50Katika tambarare za Moabu, ngambo ya mto Yordani karibu na Yeriko, Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 51“Waambie Waisraeli kwamba mtakapovuka mto Yordani na kuingia katika nchi ya Kanaani, 52wafukuzeni wenyeji wote wa nchi hiyo mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zao zote za mawe na za kusubu na kupabomoa kila mahali pao pa juu pa ibada. 53Mtaichukua nchi hiyo na kukaa humo kwa sababu nimewapeni muimiliki. 54Taz Hes 26:54-56 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kura kufuata familia zenu; eneo kubwa kwa kabila kubwa na eneo dogo kwa kabila dogo. 55Lakini kama msipowafukuza wenyeji wa nchi hiyo kwanza, basi wale mtakaowaacha watakuwa kama vibanzi machoni mwenu au miiba kila upande, na watawasumbua. 56Nami nitawafanyeni nyinyi kama nilivyokusudia kuwafanya wao.”




Hesabu33;1-56



Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: