Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 10 August 2017

Kikombe Cha Asubuhi;kitabu cha Hesabu..28




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Yeye aliyetupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Yeye aliye mlinzi wetu wakati wote..
Yeye aliyetuamsha salama na wenye afya..
Yeye atuongozaye katika yote..
Wema na fadhili zake ni za Ajabu mno...

Atukuzwe Mungu wetu na Baba yetu..
Asifiwe na kuabudiwa daima..
Tumshukuru Mungu wetu kwa maana anastahili sifa..
Ahimidiwe,Atukuzwe,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..

Asante Baba wa Mbinguni katika yote uliyotutendea/unayoendelea kututendea..
Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako Muumba wetu..
Muumba wa Mbingu, Nchi na vyote vilivyomo Baba ni mali yako..

Tunaomba Mungu Baba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe..
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Jehovah nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Utuepushe katika majaribu Yahweh utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..

Ukabariki kazi za mikono yetu na vyote tunavyenda kufanya/kutenda Mungu wetu tukatende sawasawa na mapenzi yako..
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu..Baba wa Mbinguni ukatupe kama itakavyokupendeza wewe..
Mfalme wa Amani ukatawale na kutuatamia katika maisha yetu..
Nyumba zetu/ndoa,watoto/familia,ndugu/jamaa na wote wanaotuzunguka..

Mungu Baba tazama wafiwa ukawe mfariji wao..Jehovah..tazama wenye Shida/tabu,wagonjwa,waliokatika vifungo mbalimbali,waliokata tamaa na waliokataliwa..Mungu wa Rehema ukawaguse na mkono wako wenye nguvu..wakapate kupona kimwili na kiroho pia..
wakapate neema ya kujua neno lako na kusimami sheria na Amri zako..
wakaijue kweli yako nayo iwaweke huru..



Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ni Kristo, huyo ni mtoto wa Mungu. Kila anayempenda mzazi humpenda pia mtoto wa huyo mzazi. Hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu: Kwa kumpenda Mungu na kuzitii amri zake; maana kumpenda Mungu ni kuzitii amri zake. Na, amri zake si ngumu, maana kila aliye mtoto wa Mungu anaweza kuushinda ulimwengu. Hivi ndivyo tunavyoushinda ulimwengu: Kwa imani yetu. Nani, basi, awezaye kuushinda ulimwengu? Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.

Asante Baba wa Upendo,Baba wa Rehema,Baba wa faraja..
Mungu wa wajane,Baba wa yatima..

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Ukatufanye chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Kazini,shuleni na kila sehemu tupitapo/tuingiapo Mungu wetu ukaonekane..
Tunenapo tukanene yaliyoyako..
Ukatupe macho ya rohoni na masikio ya kusikia kuona na kusikia sauti yako katika maisha yetu..
Ukatupe kiu ya kukutafuta wewe na kukujua zaidi..
Tukasimamie Neno lako na Sheria,Amri zako Mungu wetu..


Nawaandikieni mpate kujua kwamba mnao uhai wa milele nyinyi mnaoamini kwa jina la Mwana wa Mungu. Na sisi tuko thabiti mbele ya Mungu kwani tuna hakika kwamba tukimwomba chochote kadiri ya matakwa yake, yeye hutusikiliza. Yeye hutusikiliza kila tunapomwomba; na kwa vile tunajua kwamba yeye hutusikiliza kila tunapomwomba, twajua pia kwamba hutupatia yote tunayomwomba. Mtu akimwona ndugu yake ametenda dhambi isiyompeleka kwenye kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, naye Mungu atampatia uhai. Nasema jambo hili kuhusu wale waliotenda dhambi ambazo si za kifo. Lakini ipo dhambi yenye kumpeleka mtu kwenye kifo, nami sisemi kwamba mnapaswa kumwomba Mungu kwa ajili ya hiyo. Kila tendo lisilo adilifu ni dhambi, lakini kuna dhambi isiyompeleka mtu kwenye kifo. Tunajua kwamba kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, kwa sababu Mwana wa Mungu humlinda salama, na yule Mwovu hawezi kumdhuru. Tunajua kwamba sisi ni wake Mungu ingawa ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu. Twajua pia kwamba Mwana wa Mungu amekuja, akatupa elimu ili tumjue Mungu wa kweli; tuishi katika muungano na Mungu wa kweli – katika muungano na Mwanae, Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na huu ndio uhai wa milele. Watoto wangu, epukaneni na sanamu za miungu!

Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe Baba wa Mbinguni..
Tunayaweka haya  yote mikononi mwako Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!

Asanteni sana wapendwa/waungwana
 kwakuwanami/kunisoma
Baba wa Upendo akadumishe upendo wenu..
Msipungukiwe katika mahitaji yenu..
Mungu mwenye nguvu akawape kama itakavyompendeza yeye..
Nawapenda.

Sadaka za kila siku

(Kut 29:38-46)

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2“Waamuru Waisraeli ifuatavyo: Nyinyi mtanitolea kwa wakati wake tambiko zitakiwazo: Vyakula vya kuteketezwa kwa moto, vyenye harufu nzuri ya kupendeza. 3Waambie kwamba sadaka watakayonitolea ya kuteketezwa kwa moto, itakuwa ifuatavyo: Wanakondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari yoyote, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. 4Mwanakondoo mmoja atatolewa asubuhi na wa pili jioni; 5kila mmoja atatolewa pamoja na sadaka ya nafaka ya kilo moja ya unga uliochanganywa pamoja na lita moja ya mafuta bora yaliyopondwa. 6Hii ni sadaka ya kutolewa kila siku inayoteketezwa kabisa motoni, ambayo ilitolewa kwa mara ya kwanza mlimani Sinai kama sadaka ya chakula, harufu nzuri ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu. 7Sadaka ya kinywaji itakayotolewa na kila mwanakondoo ni lita moja ya divai. Utaimimina sadaka hii ya kinywaji kikali mahali patakatifu. 8Wakati wa jioni utamtoa yule mwanakondoo mwingine kama sadaka ya nafaka na kama sadaka ya kinywaji utaitoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, sadaka yenye harufu nzuri ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu.

Dhabihu za Sabato

9“Siku ya Sabato, mtatoa sadaka ya wanakondoo wawili wa kiume wa mwaka mmoja wasio na dosari, sadaka ya nafaka ya kilo mbili za unga laini uliochanganywa na mafuta, na sadaka yake ya kinywaji. 10Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa kila siku ya Sabato licha ya ile sadaka ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.

Sadaka za kila mwezi

11“Mwanzoni mwa kila mwezi, mtamtolea Mwenyezi-Mungu sadaka ya kuteketezwa: Fahali wadogo wawili, kondoo dume mmoja na, wanakondoo saba madume wa mwaka mmoja, wasio na dosari. 12Mtatoa sadaka ya nafaka ya unga laini kilo tatu, uliochanganywa na mafuta kwa kila fahali mmoja; mtatoa kilo mbili za unga kwa kila kondoo dume, 13na kilo moja ya unga kwa kila mwanakondoo. Sadaka hizi za kuteketezwa ni sadaka za chakula zenye harufu ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu. 14Kipimo cha sadaka ya kinywaji kinachohitajika ni lita 2 za divai kwa kila fahali; lita moja u nusu kwa kila kondoo dume, na lita moja kwa kila mwanakondoo. Hii ndiyo sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi katika mwaka mzima. 15Tena mtamtolea Mwenyezi-Mungu sadaka ya kuondoa dhambi, beberu mmoja, licha ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kila siku na sadaka yake ya kinywaji.


Sadaka ya Pasaka

(Lawi 23:5-14)

16 Taz Kut 12:1-13; Kumb 16:1-2 “Siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza ni Pasaka ya Mwenyezi-Mungu. 17Taz Kut 12:14-20; 23:15; 34:18; Kumb 16:3-8 Siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni sikukuu. Kwa muda wa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. 18Katika siku ya kwanza kutakuwa na mkutano mtakatifu. Siku hiyo hamtafanya kazi. 19Mtatoa sadaka ya kuteketezwa kama sadaka ya chakula kwa Mwenyezi-Mungu: Fahali wachanga wawili, kondoo dume mmoja, wanakondoo madume saba wa mwaka mmoja, wote wawe bila dosari. 20Sadaka ya nafaka itakayoandamana nazo itakuwa ya unga safi uliochanganywa na mafuta, kilo tatu kwa kila fahali, kilo mbili kwa kila kondoo dume, 21na kilo moja kwa kila mmoja wa wale wanakondoo saba. 22Mtatoa pia beberu mmoja kuwa sadaka ya kuondoa dhambi ili kuwafanyia upatanisho. 23Mtatoa vitu hivi licha ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kawaida inayotolewa kila siku asubuhi. 24Vivyo hivyo, kwa muda wa siku saba, mtatoa sadaka ya kuteketezwa ya kawaida ya chakula kwa kuteketezwa, ambayo ni harufu nzuri ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu. Hii mtaitoa licha ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kila siku na sadaka yake ya kinywaji. 25Katika siku ya saba mtafanya mkutano mtakatifu; msifanye kazi.

Sadaka ya sikukuu ya mavuno

(Lawi 23:15-22)

26“Mnamo siku ya kwanza ya sikukuu ya majuma wakati mnapomtolea Mwenyezi-Mungu malimbuko ya nafaka zenu, mtafanya mkutano mtakatifu; msifanye kazi. 27Mtatoa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kumpendeza Mwenyezi-Mungu: Fahali wachanga wawili, kondoo dume mmoja, na wanakondoo saba madume wa mwaka mmoja, wote hao wawe hawana dosari. 28Sadaka ya nafaka itakayoandamana nazo itakuwa ya unga safi uliochanganywa na mafuta kilo tatu kwa kila fahali, kilo mbili kwa kila kondoo dume, 29na kilo moja kwa kila mwanakondoo. 30Mtatoa pia beberu mmoja kuwa sadaka ya kuondoa dhambi ili kuwafanyia upatanisho. 31Mtatoa vitu hivi licha ya ile sadaka ya kuteketezwa ya kawaida pamoja na sadaka yake ya kinywaji.

Hesabu28;1-31


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: