Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 1 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..5.


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..


Haleluyah..!Haleluyah..!Haleluyah!!
Mungu wetu yu mwema sana na Fadhili zake za dumu milele..

Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe Baba yetu,Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo ni mali yako,Mfalme wa Amani,Muweza wa Yote,Baba wa Yatima,Mume wa Wajane,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Yahweh..,Jehovah, Eli Shaddai, Wewe Ndimi Mwenyezi- Mungu,wewe ndimi Mungu wetu..Unatosha Baba wa Mbinguni, Hakuna kama wewe..!!
Leo ni siku mpya Baba wa Mbinguni Tazama Jana imepita na kesho ni siku nyingine..!
Tazama tumemaliza vyema mwezi wa 5 na tunaanza mwezi huu mpya wa 6 Jehovah..!
Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako..

Asante kwa ulinzi wako usiku wote na siku zote umekuwa nasi ..
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa kibali cha  kuendelea kuiona tena siku hii/Mwezi huu..
Tunakuja mbele zako Baba wa Mbinguni tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako..

Tunaomba utusamehe Dhambi zetu zote Baba wa Mbinguni tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kusameheana na kuchukuliana..

Jehovah utuepushe na majaribu na utuokoe na yule mwovu na kazi zake..
Utufunike kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Roho Mtakatifu atuongoze kwenye kunena/kutenda na tukawe na kiasi..

Jehovah..Ututakase Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo yeye alikufa ili sisi tupate kupona..
Baba wa Mbinguni ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi ukatupe Neema ya kuwabariki wenye kuhitaji..
Ukatubariki tuingiapo/tutokappo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba wa mbinguni ukavitakase na kuvifunika kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..


Mfalme wa Amani tunapoanza mwezi huu Baba wa Mbinguni uwe nasi na ukatubariki na kutufungulia milango ya Neema na Baraka,Tusipungukiwe mahitaji yetu na ukatupe sawasawa na mapenzi yako..
Ukatuongoze,tupate kutambua/kujitambua,ukatupe Amani ya moyo,Furaha,Utuwema,Upendo wa kweli,Upole kiasi,Unyenyekevu,msukumo/shauku ya kujua zaidi/kujifunza zaidi Neno lako na likawe kinga,likawe mwanga,likawe nguzo,lika stawi maishani mwetu,likatufae sisi na wengine pia..
Jehovah ukaonekane kwenye maisha yetu na ukatufanye chombo kipya na tukatumike sawaswa na mapenzi yako..

Furaha ya kweli

(Luka 6:20-23)
“Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao. Heri walio na huzuni, maana watafarijiwa. Heri walio wapole, maana watairithi nchi. Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo Mungu, maana watashibishwa. Heri walio na huruma, maana watahurumiwa. Heri wenye moyo safi, maana watamwona Mungu. Heri wenye kuleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu. Heri wanaoteswa kwa sababu ya kufanya atakavyo Mungu, maana ufalme wa mbinguni ni wao. “Heri yenu nyinyi watu wakiwatukana, wakiwadhulumu na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa ajili yangu. Furahini na kushangilia maana tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Hivyo ndivyo walivyowadhulumu manabii waliokuwako kabla yenu.
Ukawaguse na mkono wako wenye nguvu na kuwaponya wote wanaopitia magumu/majaribu/mapito mbalimbali..Ukawafungue waliokatika vifungo mbalimbali na ukawaponye kiroho na kimwili pia..

Tunayaweka haya yote mikononi mwako tuliyoyanena na tusiyoyanena
Baba unajua mioyo yetu na unatujua kuliko tunavyojijua..


Tunakushukuru na kukuabudu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..

Amina..!

Asanteni sana wapendwa/waungwana..
wote mnaopitia hapa..sina Neno zuri kwenu zaidi ya kuwaombea

na Mungu aendelee kuwabariki..
Nasema..Asanteni sana sana ..
Nawapenda mno.


Sadaka nyingine za kuondoa dhambi

1“Kama mtu yeyote akitakiwa kutoa ushahidi kwenye baraza juu ya jambo aliloona au kulisikia naye akakataa kusema kitu, basi, huo ni uovu na atauwajibikia. 2Au kama mtu yeyote miongoni mwenu amekuwa najisi bila kukusudia kwa kugusa kitu chochote najisi, iwe ni mzoga wa mnyama wa porini au wa kufugwa au wadudu, atakuwa na hatia. 3Au mtu akigusa chochote kilicho najisi cha binadamu, kiwe kiwacho, ambacho humfanya mtu kuwa najisi, naye hana habari, basi, atakapojua atakuwa na hatia. 4Au, kama mtu akiapa kufanya chochote kile, chema au kibaya, kama wafanyavyo watu bila kufikiri, atakapojua atakuwa na hatia. 5Basi, mtu akiwa na hatia kuhusu mambo hayo lazima akiri dhambi yake aliyotenda 6na kumletea Mwenyezi-Mungu sadaka yake ya kuondoa hatia. Kwa ajili ya dhambi aliyotenda ataleta kondoo jike au mbuzi jike kutoka kundi lake amtoe sadaka kwa ajili ya kuondoa dhambi. Naye kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya dhambi yake.
7“Lakini kama hawezi kutoa mwanakondoo wa sadaka ya kuondoa hatia kwa ajili ya dhambi aliyotenda, basi atamletea Mwenyezi-Mungu hua wawili au makinda mawili ya njiwa: Mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi, na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. 8Atawaleta kwa kuhani, naye kuhani atamtoa mmoja awe sadaka ya kuondoa dhambi kwa kumkongonyoa shingo yake bila kukichopoa kichwa chake. 9Sehemu ya damu yake ataipaka pembeni mwa madhabahu na ile nyingine ataimimina chini kwenye tako la madhabahu. Hiyo ni sadaka ya kuondoa dhambi. 10Kisha atamtoa yule wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa kulingana na maagizo. Kuhani atamfanyia huyo mtu upatanisho kwa ajili ya dhambi yake, naye atasamehewa.
11“Ikiwa hawezi kutoa hua wawili au makinda mawili ya njiwa kama sadaka yake ya kuondoa dhambi aliyotenda, basi, ataleta unga kilo moja. Lakini hatautia mafuta wala ubani kwani ni sadaka ya kuondoa dhambi. 12Atamletea kuhani, naye atachukua unga huo konzi moja na kuuteketeza juu ya madhabahu kama sehemu ya ukumbusho, pamoja na sadaka anazotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto. Hiyo ni sadaka ya kuondoa dhambi. 13Basi, kuhani atamfanyia huyo mtu ibada ya upatanisho kwa ajili ya dhambi, naye atasamehewa. Unga unaobaki utakuwa wake kuhani kama ifanyikavyo kuhusu sadaka ya nafaka.”

Sadaka za fidia
14Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 15“Kama mtu yeyote akikosa kwa kutenda dhambi bila kujua kuhusu kutotoa vitu vitakatifu anavyotolewa Mwenyezi-Mungu, atamletea kondoo dume asiye na dosari kutoka kundi lake. Wewe utapima thamani yake kulingana na kipimo rasmi cha mahali patakatifu. Hiyo ni sadaka ya kuondoa hatia. 16Zaidi ya hayo, huyo mtu atalipa madhara yote aliyosababisha kuhusu vitu vitakatifu kwa kuongeza sehemu ya tano ya thamani yake na kumpatia kuhani yote. Basi, kuhani atamfanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya dhambi kwa huyo kondoo dume aliye sadaka ya kuondoa hatia, naye atasamehewa.
17“Mtu yeyote akitenda dhambi bila kujua, kwa kuvunja amri yoyote ya Mwenyezi-Mungu, yeye ana hatia, na atalipa adhabu ya hatia yake. 18Atamletea kuhani kondoo dume asiye na dosari kutoka kundi lake akiwa na thamani sawa na ile ya sadaka ya hatia. Na kuhani atamfanyia upatanisho kwa kosa alilofanya, naye atasamehewa. 19Hiyo ni sadaka ya hatia; yeye ana hatia mbele ya Mwenyezi-Mungu.”

Mambo Ya Walawi5;1-19


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: