Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 28 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 22...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tushuke mbele za Mungu tukishukuru na kusifu..
Mtakatifu..!!Mtakatifu..!!Mtakatifu..!! Baba wa Mbinguni,Mungu wetu na Muumba wetu, Muumba wa  Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo ni mali yako, hata sisi Baba ni Mali yako, Hatuna Mungu mwingine zaidi yako, Hakuna wa kuabudiwa kama wewe, Hakuna Mlinzi na Muamuzi katika maisha yetu zaidi yako..Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Tunakushukuru na kukusifu daima, Asante kwa ulinzi wako Usiku mzima..
Asante kwa Fadhili na wema wako Baba,Asante kwa Kibali chako na  Kutuchagua tena  kuendela kuiona siku hii..si kwanguvu zetu au ujuzi wetu Baba ni kwa Neema/Rehema zako Mfalme wa Amani..

Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..!!
Tunajiachilia mikononi mwako tukijinyenyekeza na kuomba Utamalaki na kutuatamia Yaweh... katika Nyumba zetu,watoto wetu,familia zetu na maisha yetu yapo mikononi mwako Jehovah..!


Yesu Mchungaji Mwema..!!
Basi, akasema tena, “Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo. Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyanganyi, nao kondoo hawakuwasikiliza. Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho. Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uhai – uhai kamili. “Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake. Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwamwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia, kisha mbwamwitu huwakamata na kuwatawanya. Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu. Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi, kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao. Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja. “Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena. Hakuna mtu anayeninyanganya uhai wangu; mimi nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye.” Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya. Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?” Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?”


Karibu kwenye mioyo yetu  utawale na kutuongoza katika yote,utupe macho ya rohoni Mfalme wa Amani tupate kutambua na kujitambua..Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako, tusiwe watu wa kujisifu wala kujitapa,tukawatendee wengine wema na tuwapende kama unavyotupenda sisi,tukawe na kiasi na utuokoe na kisasi Baba wa Mbinguni..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mfalme wa Amani kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua au kutojua..
Tunaomba utupe  na sisi Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Baba tunaomba ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia majaribu/magumu,wenye shida/tabu, wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao..ukawafungue walio kwenye vifungo mbali mbali Baba..wapate kupona kimwili na kiroho pia..
Yahweh..!! tunaomba ubariki kazi zetu, Biashara,Masomo,Vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri, tutembeapo hatua zetu ziwe nawe.. ututakase Miili yetu na Akili zetu na vyote tunavyoenda kugusa kutumia ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..yeye aliteseka ili sisi tupate kupona.
Tunayaweka haya mikononi mwako tukiamini na kukusifu daima..Tunashukuru na kukuabudu tukiamini wewe ni Mungu wetu Leo kesho na hata Milele..
Amina..!
Mungu awabariki sana na Asanteni sana kwa kupitia hapa
Nawapenda.



Maagizo juu ya malipo

1“Mtu akiiba ng'ombe au kondoo na kumchinja au kumwuza, atatozwa ng'ombe watano kwa kila ng'ombe, na kondoo wanne kwa kila kondoo. 2Mwizi akipatikana anavunja nyumba, akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya mauaji. 3Lakini mwizi huyo akishikwa wakati jua limechomoza na kuuawa, aliyemuua atakuwa na hatia. Huyo mwizi anapaswa kulipa. Ikiwa hana kitu cha kulipa, basi, yeye mwenyewe atauzwa ili kulipia wizi wake. 4Kama mnyama aliyeibiwa atapatikana kwa huyo mwizi akiwa hai, basi, mwizi atalipa mara mbili, awe ni ng'ombe, punda au kondoo.
5“Mtu akiwalisha wanyama wake katika shamba la mizabibu au kumwachia mnyama wake kula katika shamba la mtu mwingine, atalipa hasara hiyo kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au shamba lake la mizabibu.
6“Mtu akiwasha moto nao ukachoma miti ya miiba na kusambaa hadi kuteketeza miganda ya nafaka, au nafaka ya mtu mwingine ambayo bado haijavunwa, au shamba lote likateketea, aliyewasha moto huo lazima alipe hasara hiyo yote.
7“Mtu akimwachia mwenzake fedha au mali nyingine amtunzie, kisha ikaibiwa nyumbani mwake, mwizi akipatikana lazima alipe thamani yake mara mbili. 8Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atakaribia mbele za Mungu ili kuthibitisha kwamba hakuhusika na wizi wa mali ya mwenzake.
9“Pakiwa na ubishi juu ya ng'ombe, au punda, au kondoo, au mavazi, au kitu chochote kilichopotea ambacho kila mmoja anadai ni chake, wanaohusika wataletwa mbele za Mungu. Yule ambaye Mungu ataamua amekosa, atamlipa mwenzake mara mbili.
10“Mtu akimkabidhi mwenzake punda, ng'ombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, na mnyama huyo akafa au akaumia au akachukuliwa bila mtu yeyote kushuhudia, 11kiapo mbele ya Mwenyezi-Mungu kitaamua kati yao, kuonesha kwamba huyo aliyekabidhiwa hakuhusika na wizi wa mali ya mwenzake. Mwenye mnyama huyo atakubali hicho kiapo, na huyo mwenzake hatalipa malipo yoyote. 12Lakini kama aliibiwa kwake, ni lazima amlipe mwenyewe. 13Kama huyo mnyama aliraruliwa na wanyama wa porini, huyo mtu aliyekuwa amekabidhiwa lazima amlete kama ushahidi. Hatalipa malipo yoyote kwa ajili ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama wa porini.
14“Mtu akiazima mnyama kwa mwenzake, kisha mnyama huyo akaumia au akafa wakati mwenyewe hayuko, aliyeazima mnyama huyo ni lazima alipe kikamilifu. 15Lakini kama mwenyewe alikuwako, basi aliyemwazima hatalipa chochote. Kama alikuwa ni mnyama aliyekodishwa, mwenyewe ataikubali tu bei ya kukodisha.

Sheria za maadili

16 Taz Kumb 22:28-29 “Mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa, akalala naye, lazima atoe mahari na kumwoa msichana huyo. 17Baba wa huyo msichana akikataa katakata kumwoza binti yake, mtu huyo atalipa fedha ya mahari inayostahili msichana aliye bikira.
18“Usimwache mwanamke mchawi aishi.
19“Anayezini na mnyama lazima auawe.
20“Anayemtolea tambiko mungu mwingine badala ya Mwenyezi-Mungu pekee, lazima aangamizwe kabisa.
21“Msimdhulumu mgeni wala kumtesa, maana nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri. 22Msimtese mjane au yatima. 23Kama mkiwadhulumu hao nao wakanililia, hakika nitakisikiliza kilio chao, 24na hasira yangu itawaka, nami nitawaueni kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu yatima.
25“Ukimkopesha fedha mtu yeyote miongoni mwa watu wangu walio maskini, usiwe kwake kama mdai, wala usimtoze riba. 26Ukilichukua vazi la mwenzako kuliweka rehani, lazima umrudishie kabla ya jua kutua, 27kwa kuwa hiyo ndiyo nguo yake ya pekee; ndiyo atakayojifunika nayo. Au wadhani atalalia nini? Akinililia nitamsikiliza, maana mimi ni mwenye huruma.
28“Usimtukane Mungu, wala kumlaani mkuu wa watu wako.
29“Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mtanipa wazaliwa wenu wa kwanza wa kiume. 30Mtafanya vivyo hivyo kuhusu wazaliwa wa kwanza wa ng'ombe na kondoo wenu. Mtamwacha kila mzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba, na siku ya nane mtanitolea. 31Nyinyi mtakuwa watu waliowekwa wakfu kwangu. Kwa hiyo hamtakula nyama ya mnyama aliyeuawa na mnyama wa porini. Nyama hiyo mtawatupia mbwa.

Kutoka22;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 27 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 21...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu atosha yeye aliyetuchagua na kupatia kibali cha kuendelea kuiona leo hii.. Tunamrudishia Sifa na utukufu..
Sisi ni nani Baba wa Mbinguni, si kwamba ni wema sana hapana..Si kwamba wazuri mno hapana..si kwamba wajuaji na wenye nguvu sana ..hapana..ni kwa Neema/Rehema zako Mungu wetu umetuamsha tena na tukiwa na uwezo wa kuandika/kusoma Neno lako,Kutubu na kukutafuta wewe zaidi ya tunavyojua..

Tazama walio vitandani wakiwa wagonjwa, wengine wamekata kauli wanatamani hata kukuita Mungu kwa sauti zao lakina  wanashindwa kutubu,wengine wameshatangulia, si kwamba nao ni wabaya sana na si kwamba si wema sana..hapana,Baba wa mbinguni tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu na ukawaponye na kuwaokoe..kwakuwa uponyaji una wewe Jehovah..!!

Tunaomba Baba ukatupe macho ya Rohoni na tupate kuuona wema na fadhili zako daima, Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako,
tunakwenda kinyume  na yule mwovu na kazi zake..
Tunakuja mbele zako Mungu wetu tujinyenyekeza na kuomba na utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Yahweh..!
Nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..

Mchungaji Mwema..!!
“Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyanganyi. Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo. Mngojamlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake, na kuwaongoza nje. Akisha watoa nje huwatangulia mbele, nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake. Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake.” Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.

Tunaomba utubariki katika kazi zetu,Biashara,Masomo,Vyombo vya usafiri,Tuingiapo tutokapo,hatua zetu ziwe nawe Baba,Vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Mfalme wa Amani ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda, kutambua na kujitambua..
Ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali na walio katika vifungo mbalimbali Baba ukawafungue na kuwaponya kimwili na kiroho pia..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako tukiamini wewe ni Mungu wetu mwenye haki na Tunakushukuru na kukusifu Daima..
Amina..!!
Asanteni sana wote mnaopita hapa..Mungu aendelee kuwagusa na kuwabariki katika mahitaji yenu..
Nawapenda.


Maagizo kuhusu watumwa

(Kumb 15:12-18)

1“Haya ndiyo maagizo utakayowapa Waisraeli: 2Ukimnunua mtumwa Mwebrania, atakutumikia kwa miaka sita, lakini mwaka wa saba atakuwa huru na kuondoka, bila malipo. 3Kama alinunuliwa kabla hajaoa, ataondoka peke yake. Lakini kama alikuja na mkewe, basi, ataondoka na mkewe. 4Kama bwana wake alimwoza mke, akamzalia watoto wa kike au wa kiume, basi, huyo mwanamke na watoto wake watakuwa mali ya huyo bwana wake, na huyo mtumwa ataondoka peke yake. 5Lakini kama mtumwa huyo akisema kwamba anampenda bwana wake, mke wake na watoto wake na hataki kuondoka na kuwa huru, 6basi, bwana wake atamleta mbele ya Mungu. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingitini na kumtoboa sikio lake kwa shazia; naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
7“Mtu akimwuza binti yake kuwa mtumwa, huyo hatapata uhuru wake kama watumwa wa kiume. 8Ikiwa huyo bwana wake alimnunua awe mmoja wa wake zake, kisha asipendezwe naye, huyo bwana atamwacha baba yake huyo mtumwa amkomboe. Huyo bwana hana haki ya kumwuza kwa watu wa mataifa mengine, kwa kuwa atakuwa amekosa uaminifu. 9Kama ataamua kumwoza kwa mwanawe, atamtendea mtumwa huyo kama binti yake. 10Kama huyo bwana akioa mke mwingine, lazima aendelee kumtosheleza mkewe wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zake za ndoa. 11Iwapo huyo bwana hatamtimizia haki hizo tatu, basi, mke ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote.

Maagizo kuhusu ukatili

12 Taz Lawi 24:17 “Ampigaye mtu na kumwua, lazima auawe. 13Lakini kama hakuwa amemvizia, bali ni kwa ajali, basi, huyo mwuaji ataweza kukimbilia usalama mahali nitakapowachagulieni. 14Lakini mtu akimshambulia mwenzake makusudi na kumwua kwa ujeuri, hata kama atakimbilia kwenye madhabahu, mtamtoa huko madhabahuni pangu na kumwua.
15“Ampigaye baba yake au mama yake lazima auawe.
16“Amtekaye mtu nyara ili kumwuza au kumfanya mtumwa wake lazima auawe.
17 Taz Lawi 20:9; Mat 15:4; Marko 7:10 “Amlaaniye baba yake au mama yake lazima auawe.
18“Watu wawili wakigombana, kisha mmoja akampiga mwenzake jiwe au ngumi bila kumwua, lakini akamjeruhi kiasi cha kumfanya augue na kulala kitandani, 19iwapo huyo aliyepigwa atapata nafuu na kuweza kutembea kwa kutegemea fimbo, huyo aliyemjeruhi atasamehewa. Lakini, atamlipa fidia ya muda alioupoteza kitandani, na kuhakikisha amemwuguza mpaka apone kabisa.
20“Mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na kumwua papo hapo, ni lazima aadhibiwe. 21Lakini mtumwa huyo akibaki hai siku moja au mbili, bwana wake hataadhibiwa, kwani huyo alikuwa ni mali yake.
22“Wanaume wakipigana na kumwumiza mwanamke mjamzito, hata mimba yake ikaharibika bila madhara mengine zaidi, yule aliyemwumiza atatozwa faini kama atakavyodai mumewe mwanamke huyo na kama mahakimu watakavyoamua. 23Lakini kama yatakuwapo madhara mengine, basi, lazima amlipe uhai kwa uhai, 24Taz Lawi 24:19-20; Kumb 19:21; Mat 5:38 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu, 25kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, na pigo kwa pigo.
26 Taz Lawi 25:39-46 “Mtu akimpiga jicho mtumwa wake wa kiume au wa kike na kuliharibu jicho lake, ni lazima amwachilie aende huru bila malipo kwa ajili ya jicho lake. 27Hali kadhalika, akimpiga hata kumngoa jino mtumwa wake wa kiume au wa kike, ni lazima amwachilie huru kwa ajili ya jino lake.

Maagizo kuhusu usalama wa wengine

28“Ngombe akimpiga mtu pembe na kumwua, ng'ombe huyo atauawa kwa kupigwa mawe na nyama yake haitaliwa. Mwenye ng'ombe huyo hatakuwa na lawama. 29Lakini kama ng'ombe huyo amezoea kupiga watu pembe, na mwenyewe akaonywa lakini hakumfunga, kama ng'ombe huyo akiua mtu lazima apigwe mawe, na mwenyewe lazima auawe. 30Hata hivyo, huyo mtu akitozwa faini ili kuyaokoa maisha yake, ni lazima alipe kiasi kamili atakachotozwa. 31Ngombe akimpiga pembe mtoto wa mtu mwingine, shauri hili litaamuliwa kwa njia hiyohiyo. 32Kama ng'ombe huyo akimpiga pembe mtumwa wa kiume au wa kike, mwenye ng'ombe atamlipa bwana wa huyo mtumwa fedha zenye thamani ya shekeli thelathini, na huyo ng'ombe lazima auawe kwa kupigwa mawe.
33“Mtu akiacha shimo wazi, ama akichimba shimo kisha asilifunike, halafu ng'ombe au punda akatumbukia humo, 34huyo mwenye shimo hilo lazima atoe fidia; atamlipa mwenye mnyama huyo fedha, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
35“Ngombe wa mtu akimwumiza ng'ombe wa mtu mwingine na kumwua, basi, watu watamwuza huyo ng'ombe aliyebaki hai na kugawana bei yake; vilevile watagawana yule ng'ombe aliyekufa. 36Lakini kama huyo ng'ombe alikuwa amezoea kupiga wengine pembe na mwenyewe hakumfunga, mwenyewe atalipa ng'ombe kwa ng'ombe, na yule aliyeuawa atakuwa wake.


Kutoka21;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 26 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 20...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu kwa mambo mengi na makuu ..

Asante Baba wa Mbinguni kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine..!!
Tunaomba ukaibariki siku hii na ukatubariki katika maisha yetu..

Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Baba wa Mbinguni,Maisha yetu yapo nawe  Yahweh..!! Amani inapatikana kwako, Upendo wa kweli una wewe Jehovah..!Furaha ipo kwako..!
Tumaini letu ni wewe jehovah..!!Mungu wetu,Muumba wetu,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!!
Tunaomba ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo,Vyombo vya usafiri,Tuingiapo,tutokapo,hatua zetu ziwe nawe Jehovah..Vilaji/vinywaji,Ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo, vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na mwakozi wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..Jehovah.. ukatutakase Miili yetu na Akili zetu, tupate kutambua/kujitambua..
Roho Mtakatifu ukatuongoze kwenye kunena/kutenda na tukawe na kiasi..
Tunakwenda kinyume na yule mwovu na kazi zake zote..
Baba wa mbinguni ukatuokoe na kutufunika na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Tunakuja mbele zako Baba tunaomba utusamehe pale tulikwenda kinyume nawe,kwakuwaza,kwakutenda,kwakunena,kwakujua,kutojua..
Mfalme wa Amani tunaomba utupe na sisi Neeema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea ..
Yahweh..ukawaguse na mkono wako wenye nguvu ,ukawaponye na kuwaokoa wote waliokwenye vifungo mbalimbali,Wagonjwa,wafiwa ukawemfariji wao,wenye shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali..Baba ukawaponye kimwili na kiroho..Baba ukaonekane kwenye shida zao..
Wapendwa tuendelee kuamini na kumtumaini Mungu wetu yeye atosha..

Yesu ni ufufuo na uhai..!!


Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne. Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu, umbali upatao kilomita tatu. Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao. Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani. Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa! Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.” Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.” Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.” Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uhai. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi; na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Mimi naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”

Tunayaweka haya yote mikononi mwako Baba wa Mbinguni tukiamini na kushukuru..
Amina..!
Asante kwa wote mliopita hapa Mungu aendelee kuwabariki na kuwaongoza katika maisha yenu..
Nawapenda.

Amri kumi
(Kumb 5:1-21)

1Mwenyezi-Mungu alizungumza maneno haya yote, akasema, 2“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, niliyekutoa nchini Misri, ambako ulikuwa mtumwa.
3“Usiwe na miungu mingine ila mimi.20:3 Usiwe … mimi: Au usiwe na miungu mingine zaidi yangu.
4 Taz Kut 34:17; Lawi 19:4; 26:1; Kumb 4:15-18; 27:15 “Usijifanyie sanamu ya miungu wa uongo, au kinyago cha chochote kilicho mbinguni, katika nchi au majini chini ya dunia. 5Taz Kut 34:6-7; Hes 14:18; Kumb 7:9-10 Usiisujudie wala kuitumikia; kwa kuwa mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha hao wanichukiao. 6Lakini nawafadhili maelfu ya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
7 Taz Lawi 19:12; Kumb 18:20; Roma 13:9; Yak 2:11 “Usilitaje bure jina langu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako. Maana mimi Mwenyezi-Mungu sitaacha kumwadhibu anayetumia jina langu vibaya.
8“Usisahau kuiweka takatifu siku ya Sabato. 9Siku sita fanya kazi na tenda mambo yako yote. 10Lakini siku ya saba ni Sabato ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala watumishi wako wa kike, wala mnyama wako wa kufugwa, wala mgeni aliye nyumbani mwako. 11Maana kwa siku sita mimi Mwenyezi-Mungu niliziumba mbingu na dunia, bahari na vyote vilivyomo, kisha nikapumzika siku ya saba. Kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu niliibariki siku ya Sabato, nikaitakasa.
12“Waheshimu baba yako na mama yako, ili uishi maisha marefu katika nchi ninayokupa mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.
13“Usiue.
14“Usizini.
15 Taz Lawi 19:11; Mat 19:18; Marko 10:19; Luka 18:20; Roma 13:9 “Usiibe.
16 Taz Kut 23:1 Mat 19:18; Marko 10:19; Luka 18:20 “Usimshuhudie jirani yako uongo.
17“Usiitamani nyumba ya jirani yako, wala mke wake, wala mtumwa wake wa kiume au wa kike, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala chochote kilicho mali ya jirani yako.”
18Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kuisikia sauti ya parapanda juu ya mlima uliokuwa unafuka moshi, wote waliogopa na kutetemeka. Wote walisimama mbali, 19wakamwambia Mose, “Ongea nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza, lakini Mwenyezi-Mungu asiongee nasi, tusije tukafa.” 20Mose akawaambia, “Msiogope, maana Mungu amekuja kuwajaribu ili mpate kumcha yeye daima na msitende dhambi.”
21Watu wote walisimama mbali wakati Mose alipokaribia lile wingu zito alimokuwamo Mungu.

Sheria kuhusu madhabahu

22Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli: ‘Mmejionea nyinyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni. 23Mtaniheshimu mimi peke yangu wala msijifanyie miungu ya fedha wala ya dhahabu. 24Nyinyi mtanijengea madhabahu ya udongo ambayo juu yake mtanitambikia kondoo wenu na ng'ombe wenu kama sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Mahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, papo hapo mimi mwenyewe nitawajia na kuwabariki. 25Taz Kumb 27:5-7; Yosh 8:31 Kama mkinijengea madhabahu ya mawe, msiitengeneze kwa mawe ya kuchonga, maana mkitumia vyombo vya kuchongea mawe, mtaitia najisi. 26Wala msitengeneze madhabahu yenye ngazi za kupandia, mtu asije akauona uchi wa huyo anayepanda juu yake.’

Kutoka20;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 25 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 19...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu ni muweza wa yote..Tumshukuru na Kumsifu daima..
Yeye aliyetuumba,Yeye aliyetupa kibali  cha kuendelea na kuiona tena Leo hii,Yeye kwa Mapenzi yake, Neema/Rehema zake ametuamsha tena,

yeye aliyetuchagua sisi,Yeye ni Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba mbingu na Nchi, Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Baba yetu,Mfalme wa Amani, Muweza wa yote, Yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Hakuna kama yeye na hatokuwepo,Yeye ni Alfa na Omega..Jehovah Nissi..!! Jehovah Rapha..!! Jehovah Jireh..!! Jehovah Shammah..!!El shaddah..!!!
Unatosha Baba, Neema  zako zatutosha, hakuna wa kufanana nawe Baba..!!Sifa na utukufu ni kwako daima..!!
Tunashuka mbele zako Baba ili wewe uinuliwe Daima... Tunakuja mbele zako, tunajiachilia mikononi mwako Baba na kujinyenyekeza...
Tunaomba utuokoe na kututakasa kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana wetu  na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase miili yetu na Akili zetu. tupate kujitambua/kutambua..
Ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo , Vilaji/Vinywaji, Tuingiapo/tutokapo, Hatua zetu zikawe nawe Yahweh..!! Tazama vyote tunavyoenda kugusa/kutumia navyo tunaomba ukavitakase...
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Baba.. kwakuwaza,kwakunena, kwakutenda,kwakujua,kutojua..Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe Neema yakuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Tunakwenda kinyume na mwovu na kazi zake zote..

Baba wa Mbinguni utuokoe..
Baba wa Mbinguni tazama wenyeshida/tabu,wagonjwa,waliomagerezani pasipo na hatia,waliofungwa na mwovu Baba,wafiwa ukawe mfariji wao, Yatima na Wajane Mungu wangu na wote wanaopitia magumu/majaribu..
Tunaomba Baba ukawaponye na kuwaokoa, ukawaguse na mkono wako wenye nguvu..Uponyaji wa kweli una wewe..Ukawaweke huru Baba na wakapatekupona kimwili na kiroho.. Ukuu wako ukaonekane Baba wa Mbingu..
Asante Mungu wetu katika yote.. Maisha yetu yapo mikononi mwako..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako na Tunakushuru na kukusifu..
Tukiamini wewe ni Mungu wetu na Mlinzi wetu..kwako wewe hakuna linaloshindikana..Tunakuabu siku zote na Imani, Tumaini la kweli lipo kwako..


Utuonee huruma, ee Mungu, utubariki; utuelekezee uso wako kwa wema; dunia yote ipate kutambua njia yako, mataifa yote yajue nguvu yako ya kuokoa. Watu wote wakutukuze, ee Mungu; watu wote na wakusifu! Mataifa yote yafurahi na kuimba kwa furaha; maana wawahukumu watu kwa haki, na kuyaongoza mataifa duniani. Watu wote wakutukuze, ee Mungu; watu wote na wakusifu! Nchi imetoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, ametubariki. Mungu aendelee kutubariki. Watu wote duniani na wamche.
Amina..!!!

Asanteni wote mliopitia hapa Mungu aendelee kuwabariki katika mahitaji yenu.
Nawapenda.

Waisraeli mlimani Sinai

1Siku ya kwanza ya mwezi wa tatu tangu walipotoka nchini Misri, watu wa Israeli walifika katika jangwa la Sinai. 2Walipoondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, huko walipiga kambi mbele ya mlima Sinai. 3Basi, Mose akapanda juu mlimani kwa Mungu. Hapo Mwenyezi-Mungu akamwita Mose kutoka huko juu mlimani, akamwambia, “Hivi ndivyo utakavyowaambia wazawa wa Yakobo, hao Waisraeli, 4‘Nyinyi wenyewe mmeona nilivyowatenda Wamisri na jinsi nilivyowachukua kama tai anavyochukua watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu. 5Taz Kumb 4:20; 7:6; 14:2; 26:18; Tito 2:14 Sasa basi, kama mkiitii sauti yangu na kulishika agano langu, mtakuwa watu wangu wateule kati ya mataifa yote, maana dunia yote ni yangu. 19:5-6 Taz 1Pet 2:9 6Taz Ufu 1:6; 5:10 Mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”
7Basi, Mose akarudi, akawakusanya pamoja wazee wa Waisraeli na kuwaambia maneno hayo aliyoamriwa na Mwenyezi-Mungu. 8Watu wote wakaitikia kwa pamoja wakisema, “Mambo yote aliyoyasema Mwenyezi-Mungu, tutayafanya.” Mose akamjulisha Mwenyezi-Mungu jibu hilo la watu. 9Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Haya, mimi nitakujia katika wingu zito ili Waisraeli wapate kunisikia ninaposema nawe na kukuamini siku zote.”
Kisha Mose akamwambia Mungu jinsi watu walivyosema. 10Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Waambie wayafue mavazi yao 11wawe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Mwenyezi-Mungu nitashuka juu ya mlima Sinai mbele ya watu wote. 12Taz Ebr 12:18-20 Tena wewe utawawekea watu mpaka kuzunguka mlima. Utawakanya wajihadhari sana wasipande juu mlimani wala kuugusa mpaka wake. Yeyote atakayeugusa mlima, atauawa. 13Mtu asimguse mtu huyo; atauawa kwa kupigwa mawe au mshale awe ni mtu au ni mnyama, hataishi. Wakati mbiu itakapopigwa mfululizo, watu wote watakaribia mlimani.”
14Basi, Mose akashuka mlimani na kuwaendea watu, akawatakasa, nao wakayafua mavazi yao. 15Kisha akawaambia watu wote, “Kesho kutwa muwe tayari, na mwanamume yeyote asimkaribie mwanamke.”
16 Taz Ufu 4:5 Basi, siku ya tatu asubuhi, kukatokea ngurumo na umeme na wingu zito juu ya mlima. Ikasikika pia sauti kubwa ya mbiu ambayo iliwatetemesha watu wote kambini. 19:16-18 Taz Kumb 4:11-12 17Kisha Mose akawaongoza watu wote kutoka kambini, wakaenda kukutana na Mungu. Wote walikwenda wakajipanga chini ya mlima.
18Mlima wa Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi kwa kuwa Mwenyezi-Mungu alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi wa tanuri kubwa na mlima wote ulitetemeka kwa nguvu. 19Sauti ya mbiu ilizidi kuongezeka, na Mose akaongea na Mungu. Mungu naye akamjibu katika ngurumo.
20Mwenyezi-Mungu alishuka juu ya mlima Sinai, akamwita Mose kutoka huko juu, naye Mose akapanda mlimani. 21Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Shuka chini ukawaonye watu wote wasije kunitazama; la sivyo wengi wao wataangamia. 22Hata makuhani ambao hunikaribia wanapaswa kujitakasa; la sivyo nitawaadhibu.” 23Mose akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Watu hawa hawawezi kuupanda mlima wa Sinai kwani wewe mwenyewe ulituamuru tuweke mpaka kuuzunguka mlima.” 24Mwenyezi-Mungu akasema, “Teremka chini kisha urudi pamoja na Aroni. Lakini usiwaruhusu makuhani na watu wengine wapite mpaka na kuja kwangu, la sivyo nitawaadhibu.” 25Basi, Mose akashuka na kuwaambia Waisraeli mambo yote aliyoagizwa.

Kutoka19;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 24 April 2017

SHEREHE YA UBATIZO WA MTOTO ROSELYN HENRY KAPINGA KATIKA UKUMBI WA VIP WANYAMA HOTEL SINZA.


Cake maalum kwa ajili ya Ubatizo wa mtoto Roselyn Kapinga iliyoandaliwa na Aunt Agnes Makwati ikiwa tayari kwa kukatwa.
Aunt Eva (Doto) akiwa amembeba Roselyn kabla ya kuanza tukio la kukata Cake.
Mama wa Kiroho Aunt Esther Mbapila akitoa zawadi ya Roselyn kwa mama Roselyn
Cindy Makwati akimlisha cake Mama Roselyn kwa niaba ya Roselyn huku baba Roselyn akishuhudia tukio hilo.
Cindy akijiandaa kumlisha cake Aunt Agnes ambaye ni mama yake.
Babu Roselyn naye hakuwa nyuma katika kusherehekea Ubatizo wa mjukuu wake.




Mtoto Roselyn Henry Kapinga alipata Ubatizo siku ya Jumatatu ya Pasaka ya tarehe 17/04/2017 katika kanisa la Mt. Petro Oysterbay jijini Dar es salaam na baadae kufuatiwa na sherehe fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa ndani katika Hoteli ya Wanyama Sinza jijini Dar es salaam.

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 18...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Ni siku nyingine tena Mungu ametuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona Leo hii..Tunamshukuru Mungu katika yote,ametulinda wiki nzima na usiku umepita, tumeamka tena..Asante kwa Neema/Rehema hii..
Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..
Tunakuja mbele zako na tukijinyenyekeza, Tukishukuru na kukusifu Daima..
Tunaomba ukatulinde,ukatuponye,ukatutakase na kutufunika kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti.Maisha yetu yawe mikononi mwako Yahweh..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye Kunena/kutenda na tukawe na kiasi..
Baba ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Baba ukabariki Vilaji /vinywaji tuingiapo/tutokapo,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..

Baba tazama wenye Shida/Tabu,Wanaopitia magumu/majaribu,Wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao..Tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu na ukawaponye na kuwaokoa wapate kupona kimwili na kiroho pia..
Jehovah..Utusamehe pale tulipo kwenda kinyume nawe..kwakujua/kutojua,kwakunena/kwakutenda,kwakuwaza..
Baba tunaomba nasi ukatupe Neema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Tunakwenda kinyume na yule Mwovu na kazi zake zote..

Baba ukatuokoe na kutulinda katika safari yetu ya maisha..
tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Baba tunaiweka Nchi hii tunayoishi mikononi mwako..Ukaibariki na kutubariki wote tunaoishi humu..ukawe mlinzi mkuu na ukatawale katika yote..
Tunaiweka Tanzania na watanzania wote  mikononi mwako ukawabariki na kuwabariki watu wake popote walipo..ukaonekane juu yao.. ukawe mtalawa mkuu..
Afrika na Dunia nzima iwe mikononi mwako, ukawe mtawala mkuu na ukawaongoze wanaotuongoza wakatuongoze katika haki kweli.
Tazama watoto wetu Leo wamerudi shule Baba ukaonekane kwenye masomo yako..wapate kuelewa na kukumbuka yote wanayofundishwa..

Ukawalinde katika ujana wao na wakawe na hofu yako Mungu..
waje kuwa watu wema mbele zako na jamii pia.
Neema yako yatutosha Yahweh..Furaha na Amani vipo kwako, Upendo wa kweli una wewe..Fadhili na wema ukokwako Jehovah..Uzima wa milele unapatikana kwako Mungu wetu, Muumba wetu, Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!!
Tunayaweka haya yote mikononi mwako.. tunakuabudu na Kuamini  wewe ni Mungu wetu na hatuna Mungu mwingine Leo kesho na hata Milele..
Amina..!
Asante kwa wote mliopita hapa natumaini hamtotoka watupu..
Mungu aendelee kuwaBariki..
Nawapenda.


Yethro anamtembelea Mose
(Kumb 1:9-18)
1Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, alisikia juu ya mambo yote ambayo Mwenyezi-Mungu alimtendea Mose na Waisraeli alipowatoa katika nchi ya Misri. 2Taz Kut 2:21-22 Kwa hiyo Yethro, akiwa na Sipora, mkewe Mose, ambaye Mose alikuwa amemrudisha kwa baba yake, alimwendea Mose, 3Taz Mate 7:29 pamoja na watoto wawili wa Mose. Mtoto wa kwanza aliitwa Gershomu. Mose alimpa jina hili kwa vile alisema, “Nimekimbilia18:3 Nimekimbilia: Au nimekuwa mgeni, au mkimbizi Kiebrania: Ger. katika nchi ya kigeni.” 4Wa pili aliitwa Eliezeri,18:4 Eliezeri: Kiebrania “Eli” maana yake “Mungu wangu,” na “ezeri” maana yake “msaada.” kwa vile Mose alisema, “Mungu wa baba yangu ndiye aliyenisaidia nisiuawe na Farao.”
5Yethro, mkwewe Mose, alikuja pamoja na binti yake, yaani mkewe Mose, pamoja na watoto, akamkuta Mose jangwani alikokuwa amepiga kambi kwenye mlima wa Mungu. 6Mose alipoambiwa kuwa baba mkwe wake pamoja na mkewe na wanawe wawili wanakuja, 7alitoka kwenda kumlaki baba mkwe wake, akamwinamia na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani. 8Mose akamweleza mkwewe mambo yote Mwenyezi-Mungu aliyomtenda Farao na Wamisri kwa ajili ya Waisraeli. Alimwambia pia juu ya shida zote zilizowapata safarini na jinsi Mwenyezi-Mungu alivyowaokoa. 9Yethro akafurahishwa na yote aliyotenda Mwenyezi-Mungu kwa ajili ya Waisraeli, kwa kuwaokoa mikononi mwa Wamisri. 10Yethro akasema, “Na atukuzwe Mwenyezi-Mungu ambaye amewaokoa mikononi mwa Wamisri na kutoka utumwa wa Farao. 11Sasa najua kwamba Mwenyezi-Mungu ni mkuu kuliko miungu yote, kwani amewakomboa watu hawa mikononi mwa Wamisri ambao waliwatendea ujeuri.” 12Hapo Yethro, baba mkwe wa Mose, akamtolea Mungu sadaka za kuteketezwa na tambiko. Naye Aroni akaja pamoja na wazee wa Israeli ili kula chakula pamoja na Yethro, mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Kuteuliwa kwa waamuzi
(Kumb 1:9-18)

13Kesho yake, Mose aliketi kuamua matatizo ya Waisraeli, nao wakasimama wakiwa wamemzunguka, tangu asubuhi mpaka jioni. 14Yethro, baba mkwe wa Mose, alipoyaona mambo yote ambayo Mose aliwafanyia Waisraeli, alimwuliza, “Kwa nini unawafanyia watu mambo haya? Mbona unaketi peke yako huku watu wamekuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?” 15Mose akamjibu mkwewe, “Kwa sababu watu huja kwangu kuuliza matakwa ya Mungu. 16Wakiwa na ugomvi wowote ule wao huja kwangu nami huamua kati ya mtu na mwenzake, na kuwafunza amri za Mungu na maamuzi yake.” 17Basi, Yethro akamwambia Mose, “Unavyofanya si vizuri! 18Utajidhuru mwenyewe na hawa watu kwa uchovu, kwani hii ni kazi ngumu usiyoweza kuifanya peke yako. 19Sikiliza shauri langu kwako, na Mungu awe pamoja nawe. Wewe utawawakilisha watu mbele ya Mungu na kumletea Mungu matatizo yao. 20Hali kadhalika utawafundisha amri na maamuzi ya Mungu na kuwaonesha jinsi inavyowapasa kuishi na kufanya. 21Lakini kuhusu mambo mengine, chagua miongoni mwa watu wote, watu wanaostahili, watu wanaomcha Mungu, waaminifu na wanaochukia kuhongwa. Wape hao mamlaka, wawe na jukumu la kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, hamsini na kumikumi. 22Hao ndio watakaokuwa na vikao kila siku kutatua matatizo ya watu. Matatizo magumu watakuletea wewe, lakini yale madogomadogo watayaamua wenyewe. Kwa njia hiyo utaweza kurahisisha kazi yako kwa vile watashirikiana nawe katika jukumu hilo. 23Ukifanya hivyo, na kama ndivyo atakavyo Mungu, utaweza kustahimili na watu hawa wote wataweza kurudi makwao kwa amani.”
24Mose alilisikiliza shauri hilo la mkwewe na kufanya kama alivyoshauriwa. 25Basi, akawateua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu hamsini na watu kumikumi. 26Nao wakawa wanaamua matatizo ya watu kila wakati. Matatizo magumu walimletea Mose, lakini yale madogomadogo waliyatatua wao wenyewe. 27Baada ya kufanya hivyo, Mose na mkwewe wakaagana naye Yethro akarudi nchini kwake.
Kutoka18;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 21 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 17...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwakuwa yeye ni mwema sana..

“Muwe tayari mmejifunga mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka; muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka harusini, ili wamfungulie mara atakapobisha. Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia. Hata kama atarudi usiku wa manane au alfajiri na kuwakuta wanakesha, heri yao watumishi hao! Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe. Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
Asante Baba wa Mbinguni kwa Neema/Rehema hii kwa kutupa tena kibali cha kuendelea kuiona siku hii...
Tunaomba ikawe yenye Amani,Upendo,utuwema,Fadhili na Furaha..

Tunaomba ukaibariki katika yote,Maisha yetu tunayaweka mikononi mwako Baba wa Mbingu..
Mfalme wa Amani tunaomba ukatawale na kutamalaki katika maisha yetu..Ukatuatamie na kututakasa Miili yetu na Akili zetu..
Ukatuokoe na yule Mwovu na kazi zake zote..
Ukatufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Utusamehe Baba pale tulipokwenda kinyume nawe kwakuwaza,kunena,kutenda,kwakujua,kutojua..

Mfalme wa Aamni ukatupe neema yakuweza kuwasamehe nasi waliotukosea..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Baba wa Mbingu tunaomba ukawaponye na kuwagusa wote wanaopitia Magaumu/majaribu mbalimbali,shida/tabu,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao..
Mkono wako ukawaguse na kuwaponya wote wanaogua moyoni kwa kisasi,kutosamehe,wivu,chuki,kuumizwa,wametendwa vibaya na Imani yao imepotea,Mashaka,Hofu na kutaka kujitoa uhai..Mungu Baba ukawape uponyaji na Amani ya moyo..
Mungu Baba ukawaponye na kuwaongoza  wale ambao kila wanalolifanya halifanikiwi..Ikiwa kazi,Biashara,Masomo..
Wenye Laana,Mikosi,kukataliwa,kutengwa na kunyanyaswa kimwili na kiroho pia..
Tunaomba Baba ukaonekane nao wapate kupona na kujua wewe ni Mungu mwenye Upendo,Haki na ni Mungu wa masikini,Mtajiri na wote wanaokutegemea wewe wapo huru..
Neema yako na Fadhili zako zatutosha Baba..Hakuna kama wewe na hata kuwepo..wewe ukisema ndiyo nani aseme hapana?
Kukutegemea wewe kuna faida kubwa,Amani na Imani,Furaha na Upendo wa kweli vipo nawe Jehovah..!!

Sifa na Utukutufu ni wako Daima..Tunashukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu Leo kesho na hata Milele..
Amina..!!

3Mtumainie Mwenyezi-Mungu na kutenda mema,
upate kuishi katika nchi na kuwa salama.
4Uitafute furaha yako kwa Mwenyezi-Mungu,
naye atakujalia unayotamani moyoni.
5Mkabidhi Mwenyezi-Mungu maisha yako;
mtumainie yeye naye atafanya kitu.
6Ataufanya wema wako ungae kama mwanga,
na uadilifu wako kama jua la adhuhuri.[Zaburi 37;3-6]

Wote mliopita hapa nawatakia Amani na Asanteni sana..
Mungu aendelee kuwabariki katika yote yaliyo mema..
Nawapenda.



Maji kutoka mwambani
(Hes 20:1-13)

1Kutoka jangwa la Sini, jumuiya yote ya Waisraeli ilisafiri hatua kwa hatua kama alivyoamuru Mwenyezi-Mungu, watu wakapiga kambi huko Refidimu. Lakini huko hakukuwa na maji ya kunywa. 2Kwa hiyo watu wakamnungunikia Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akawauliza, “Mbona mnaninungunikia? Mbona mnamjaribu Mwenyezi-Mungu?” 3Lakini wote walikuwa na kiu, wakamnungunikia Mose wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri utuue kwa kiu sisi sote na watoto wetu na mifugo yetu?”
4Basi, Mose akamlilia Mwenyezi-Mungu akisema, “Nitawafanyia nini watu hawa? Wako karibu kunipiga mawe!” 5Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Pita mbele ya watu hawa ukiwachukua wazee wao kadhaa; chukua pia mkononi mwako ile fimbo uliyoipiga nayo mto Nili. 6Tazama mimi nitasimama mbele yako mwambani pale Horebu, nawe utaupiga huo mwamba na maji yatabubujika kutoka humo ili watu wote wapate kunywa.” Basi, Mose akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli. 7Mahali hapo Mose akapaita “Masa”17:7 Masa: Kiebrania maana yake: Jaribu. na “Meriba”,17:7 Meriba: Kiebrania maana yake: Kunung'unika. kwa sababu Waisraeli walimnungunikia na kumjaribu Mwenyezi-Mungu wakisema, “Je, kweli Mwenyezi-Mungu yu pamoja nasi?”

Vita na Waamaleki
8Waamaleki walikuja na kupigana na Waisraeli huko Refidimu. 9Mose akamwambia Yoshua, “Chagua wanaume uende ukapigane na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilele cha kilima, nikiishika mkononi mwangu ile fimbo ya Mungu.” 10Basi, Yoshua akafanya kama Mose alivyosema, akaenda kupigana na Waamaleki. Mose, Aroni na Huri wakapanda kilele cha kilima. 11Ikawa wakati wote Mose alipoinua mkono wake juu, Waisraeli walishinda, na alipouteremsha, Waamaleki walishinda. 12Lakini baada ya muda, mikono ya Mose ilichoka. Kwa hiyo Aroni na Huri walichukua jiwe wakaliweka karibu na Mose naye akaketi. Kisha wakaishika na kuiinua mikono yake, mmoja akauinua mkono wa kulia na mwingine mkono wa kushoto. Hivyo mikono ya Mose ikabaki imara ikiwa imeinuliwa juu hadi jua lilipotua. 13Yoshua akawakatakata Waamaleki.
14 Taz Kumb 25:17-19; 1Sam 15:2-9 Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Liandike jambo hili katika kitabu, liwe ukumbusho. Tena kariri masikioni mwa Yoshua kwamba nitawafuta kabisa Waamaleki duniani.” 15Mose akajenga madhabahu na kuiita, “Mwenyezi-Mungu ni Bendera Yangu”,17:15 Mwenyezi-Mungu … Yangu: Kiebrania “Yahweh-nisi.” 16akisema, “Inueni juu bendera ya Mwenyezi-Mungu!17:16 Inueni … ya Mwenyezi-Mungu: Makala ya Kiebrania si dhahiri. Mwenyezi-Mungu atapigana na Waamaleki kizazi hata kizazi!”
Kutoka17;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 20 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 16...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu ni mwema sana Tumshukuru kwa yote...

Ni nani aliye mkuu?
(Mat 18:1-5; Marko 9:33-37)
46Kukatokea majadiliano kati ya wale wanafunzi kuhusu nani kati yao aliyekuwa mkuu zaidi. 47Yesu aliyajua mawazo yaliyokuwa mioyoni mwao; basi akamchukua mtoto mdogo akamweka karibu naye, 48akawaambia, “Mtu yeyote anayempokea mtoto huyu mdogo kwa jina langu, ananipokea mimi; na yeyote anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma. Maana yule aliye mdogo kuliko wote kati yenu ndiye aliye mkuu kuliko wote.”[Luka 9:46-48]
Asante Baba wa mbinguni kwa Neema/Rehema yako na  kutuchagua sisi tena na kutupa Kibali cha  kuiona Leo hii, Sisi ni nani Baba..? Si kwamba ni wazuri mno,Si kwamba ni wema sana zaidi ya wengine,si kwamba tunajua sana, si kwamba tunanguvu na utashi..si kwamba hatukosei Jehovah..!! Bali ni kwa Mapenzi yako Mungu wetu...

Tunashukuru na tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kukabidhi maisha yetu mikononi mwako Yahweh..!!
Tunaomba Baba utubariki tuingiapo/tutokapo,vinywaji/vilaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!
Ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Ukatutakase miili yetu na Akili zetu,Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda,kutambua/kujitambua ..

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe..
Tunakwenda kinyume na mwovu na kazi zake zote..
Tunaomba utupe Neema ya kuweza kusameheana pia..
Utuokoe, Ututakase na kutufunika na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Baba wa Mbinguni tunawaweka  mikononi mwako wenye Shida/Tabu, wagonjwa,wanaopitia magumu/majaribu,waliovifungoni,waliokata tamaa,waliokataliwa,wenye mashaka/hofu,wasiojiweza,Yatima na wajane,Baba ukawaguse naukawaponye, kimwili na kiroho, wakauone Utukufu wako Jehovah..!

Baba usiwaache na ukawaguse na kuwapatia Mke/Mume mwema wote wanaotafuta wenza wao ili wapate kujenga familia iliyo bora na kukujua wewe..
Tazama wanaotafuta watoto pia Mungu ukawape watoto na wawe wema, wakujue wewe Mungu na wakawe baraka kwa wazazi/walezi na jamii pia..

Tazama kuna wanaohitaji kwenda shule Baba wa Mbinguni lakini kunavifungo mbalimbali , wengine wamefiwa na wanaowasomesha, wengine hali ya pesa haiko vyema, wengine hawaelewi/hawakumbuki wanayofundishwa, wengine wanapofika shuleni wanakuwa wagonjwa na mengine meengi Baba wa Mbingu hakuna mtatuzi wa haya zaidi yako Mungu wetu.. tunayaweka mikononi mwako wewe uwezaye yote hakuna litaloshindikana kwako Baba wa mbinguni..Tuna amini na kukuabudu daima..!! Wewe ukisema ndiyo hakuna wakusema siyo.. Maana wewe ni Baba wa Upendo, Baba wa Yatima, Mume wa Wajane,Mungu wetu na Muumba wetu,hakuna  na hata kuwepo wala wa kufanana nawe Jehovah..
Maisha yetu pasipo wewe ni bure kabisa..Unatosha Baba wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho..wewe ni Afla na Omega..!!
Tunayakidhi haya yote tuliyoyanena na tunayoyawaza Baba yote unayajua..Tukiamini na kushukuru..
Amina..!!
Nawapenda wote na mliopita hapa Mungu aendelee kuwabariki Asanteni sana..
Neno litasimama mambo yote yatapita lakini Neno litasimama..!!

Mana na kware

1Jumuiya yote ya Waisraeli iliondoka, ikafika jangwa la Sini kati ya Elimu na Sinai. Hii ilikuwa siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili tangu walipoondoka nchini Misri. 2Basi, jumuiya yote ya Waisraeli ikawalalamikia Mose na Aroni huko jangwani, 3“Laiti Mwenyezi-Mungu angelituua tulipokuwa nchini Misri ambako tulikaa, tukala nyama na mikate hata tukashiba. Lakini nyinyi mmetuleta huku jangwani kuiua jumuiya hii yote kwa njaa!”
4 Taz Hek 16:20-29; Yoh 6:31 Ndipo Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mimi nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Kila siku watu watatoka na kukusanya chakula cha siku hiyo. Kwa njia hii nitawajaribu nione kama watazifuata sheria zangu au hawatazifuata. 5Lakini siku ya sita, wakati watakapoandaa chakula walichokusanya, kiasi hicho kitakuwa mara mbili ya chakula cha kila siku.” 6Basi, Mose na Aroni wakawaambia watu wote wa Israeli, “Jioni, mtatambua kwamba Mwenyezi-Mungu ndiye aliyewatoa nchini Misri! 7Tena, kesho asubuhi, mtauona utukufu wa Mwenyezi-Mungu kwani ameyasikia manunguniko mliyomnungunikia. Sisi ni nani hata mtunungunikie?” 8Tena Mose akasema, “Jioni, Mwenyezi-Mungu atawapeni nyama mle, na asubuhi atawapeni mikate mle mshibe, maana yeye ameyasikia manunguniko mliyomnungunikia. Sisi ni nani hata mtunungunikie? Msitunungunikie sisi bali mnungunikieni Mwenyezi-Mungu.”
9Kisha Mose akamwambia Aroni, “Iambie jumuiya yote ya Waisraeli ikusanyike mbele ya Mwenyezi-Mungu kwani ameyasikia manunguniko yenu.” 10Wakati Aroni alipokuwa akizungumza na jumuiya ya Waisraeli, watu wote walitazama huko jangwani, na mara utukufu wa Mwenyezi-Mungu ukaonekana mawinguni. 11Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 12“Nimeyasikia manunguniko ya Waisraeli. Basi, waambie kwamba wakati wa jioni watakula nyama, na asubuhi watakula mkate. Hapo ndipo mtakapotambua kuwa mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.”
13Basi, mnamo wakati wa jioni kukaja kware wengi, wakafunika kambi ya Waisraeli. Asubuhi yake kukatokea umande, ukatanda kandokando ya kambi yao. 14Umande huo ulipotoweka, kukabaki huko nyikani kitu kama mkate mwembamba na mwepesi. 15Taz 1Kor 10:3 Waisraeli walipoona kitu hicho walishangaa, wakaulizana, “Nini hiki?”16:15 Nini hiki: Kiebrania: Man-hu. Hawakujua kilikuwa kitu gani. Basi, Mose akawaambia, “Huu ni mkate ambao Mwenyezi-Mungu amewapa mle. 16Mwenyezi-Mungu ameamuru mfanye hivi: Kila mtu na akusanye chakula kiasi anachoweza kula; ataokota kiasi cha pishi16:16 pishi: Kiebrania: Omeri; Taz Kut 16:36. moja kwa kila mtu hemani mwake.”
17Basi, Waisraeli wakafanya hivyo, na ikawa kwamba, wengine waliokota kwa wingi na wengine kidogo. 18Taz 2Kor 8:15 Lakini wote walipokipima kipimo walichookota katika pishi, waligundua kuwa aliyeokota kingi hakuwa na cha ziada, na aliyeokota kidogo, hakupungukiwa. Kila mmoja alikuwa ameokota kiasi alichoweza kula.
19Mose akawaambia watu, “Mtu yeyote asibakize chakula hicho mpaka asubuhi.”
20Lakini watu hawakumsikiliza Mose. Baadhi yao walijibakizia chakula mpaka asubuhi. Lakini asubuhi chakula hicho kikawa kimeoza na kuwa na mabuu. Mose akawakasirikia sana watu. 21Basi, kila asubuhi walikusanya chakula kila mtu kiasi alichohitaji kula. Jua lilipopanda juu na kuwa kali, kile chakula kingine kiliyeyuka.
22Katika siku ya sita, Waisraeli walikusanya chakula hicho maradufu, pishi nne kwa kila mtu. Basi, wazee wote wa jumuiya ya Waisraeli walimwendea Mose, wakamweleza jambo hilo. 23Taz Kut 20:8-11 Mose akawaambia, “Hii ndiyo amri ya Mwenyezi-Mungu. Kesho ni siku rasmi ya mapumziko; ni Sabato takatifu ya Mwenyezi-Mungu. Basi, nendeni mkapike au mkachemshe kile chakula mnachohitaji leo, na chakula kitakachosalia kiwekeni mpaka kesho.” 24Basi, wakafanya hivyo na kukiacha chakula kingine mpaka kesho yake kama Mose alivyosema. Asubuhi yake waliona kwamba hakikuharibika wala kuwa na mabuu. 25Basi, Mose akawaambia, “Kuleni chakula hicho kilichosalia kwa sababu leo ni Sabato ya Mwenyezi-Mungu. Leo hamtapata chakula huko nje. 26Kwa siku sita mtakuwa mkikusanya chakula hiki, lakini siku ya saba ambayo ni Sabato hakitakuwapo.”
27Mnamo siku ya saba watu kadhaa walitoka kwenda kutafuta chakula, lakini hawakukipata. 28Hapo Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mpaka lini mtakataa kuzitii amri na Sheria zangu? 29Fahamuni kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nimewapa siku ya Sabato, ndiyo maana nikawapa chakula cha siku mbili mnamo siku ya sita. Basi, pumzikeni kila mtu nyumbani mwake; mtu yeyote asitoke katika siku ya saba.” 30Kwa hiyo, watu walipumzika siku ya saba.
31 Taz Hes 11:7-8 Waisraeli walikiita chakula hicho “Mana.”16:31 Mana: Neno la Kiebrania lasikika kuwa na maana ya “Nini hiki?” taz. 16:15. Kilikuwa kama mbegu za mtama mweupe na ladha yake ilikuwa kama mkate mwembamba uliotiwa asali. 32Mose akawaambia, “Hili ndilo agizo la Mwenyezi-Mungu: Chukueni kiasi cha pishi moja ya mana na kuiweka kwa ajili ya wazawa wenu, ili waweze kuona chakula nilichowalisha jangwani wakati nilipowatoa nchini Misri.”
33 Taz Ebr 9:4 Mose akamwambia Aroni, “Chukua gudulia utie ndani pishi moja ya mana na kuiweka mbele ya Mwenyezi-Mungu, iwe kwa ajili ya wazawa wenu.”
34Basi, Aroni akaiweka mana mahali patakatifu mbele ya sanduku la agano ili ihifadhiwe kama vile Mwenyezi-Mungu alivyomwagiza Mose. 35Taz Yos 5:12 Waisraeli walikula mana kwa muda wa miaka arubaini, mpaka walipofika katika nchi iliyofaa kuishi, nchi iliyokuwako mpakani mwa Kanaani ambako walifanya makao yao. 36(Posho ya mana, kiasi cha pishi nne, ilikuwa sehemu ya kumi ya kipimo cha kawaida kiitwacho efa.)
Kutoka16;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 19 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 15...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru kwa yote...
Asante Baba wa Mbinguni, Baba yetu na Mungu wetu,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Asante kwa kutuchagua tena na kutupa kibali cha kuiona Leo hii..Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..!!
Tunakuja mbele zako na tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Yahweh..!!Tunaomba utubariki katika maisha yetu,Utamalaki na kutuatamia,Ulinzi upo nawe Baba,Furaha,Upendo,Tumaini,Wema na Fadhili zipo kwako Jehovah..!!
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote..
Tukawe Barua njema na tusomeke vyema Baba..
Ukatuongezee Hekima,Busara,utuwema na Kukutafuta wewe zaidi..

Tupendane sisi kwa sisi na tupende wengine..Jehovah..!!
Mwanga wa mwili
(Mat 5:15; 6:22-23)
“Hakuna mtu anayewasha taa na kuifunika kwa debe, bali huiweka juu ya kinara ili watu wanaoingia ndani wapate kuona mwanga. Jicho lako ni taa ya mwili wako; likiwa zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga. Jicho lako likiwa bovu, na mwili wako pia utakuwa katika giza. Uwe mwangalifu basi, mwanga ulio ndani yako usije ukawa giza. Basi, kama mwili wako wote una mwanga, bila kuwa na sehemu yoyote yenye giza, mwili huo utangaa kikamilifu kama vile taa inavyokuangazia kwa mwanga wake.”
Tunakwenda kinyume na Mwovu na kazi zake zote..
Tunakuja mbele zako Tunaomba Utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe..kwakuwaza,Kwakunena/kutenda,kwakujua/kutojua.Baba
Utupe Neema ya kuweza kuwasaheme nasi waliotukosea..



Mfano wa mwana mpotevu

Yesu akaendelea kusema, “Kulikuwa na mtu mmoja mwenye watoto wawili wa kiume. Yule mdogo alimwambia baba yake: ‘Baba, nipe urithi wangu.’ Naye akawagawia mali yake. Baada ya siku chache, yule mdogo aliuza urithi wake, akasafiri na fedha aliyopata, akaenda nchi ya mbali ambako aliitumia ovyo. Alipomaliza kutumia kila kitu, kukatokea njaa kali katika nchi ile, naye akaanza kuhangaika. Akaomba kazi kwa mwananchi mmoja wa huko naye akampeleka shambani mwake kulisha nguruwe. Alitamani kula maganda waliyokula wale nguruwe, ila hakuna mtu aliyempa kitu. Alipoanza kupata akili, akafikiri: ‘Mbona kuna wafanyakazi wengi wa baba yangu wanaokula na kusaza, nami ninakufa njaa? Nitarudi kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia. Sistahili hata kuitwa mwanao. Nifanye kama mmoja wa wafanyakazi wako.’ Basi, akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Alipokuwa bado yu mbali, baba yake alimwona, na kwa moyo wa huruma alimkimbilia, akamkumbatia na kumbusu. “Mwanae akamwambia: ‘Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia. Sistahili hata kuitwa mwanao.’ Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: ‘Haraka! Leteni nguo nzuri mkamvike! Mvisheni pete na viatu! Mchinjeni ndama mnono; tule na kusherehekea! Kwa sababu huyu mwanangu; alikuwa amekufa, kumbe yu hai; alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana.’ Wakaanza kufanya sherehe. “Wakati huo kaka yake alikuwa bado shambani. Alipokuwa akirudi na kukaribia nyumbani, akasikia vifijo na ngoma. Akamwita mmoja wa watumishi, akamwuliza: ‘Kuna nini?’ Huyo mtumishi akamwambia: ‘Ndugu yako amerudi nyumbani, na baba yako amemchinjia ndama mnono kwa kuwa amempata akiwa salama salimini.’ Huyo kijana mkubwa akawaka hasira hata akakataa kuingia nyumbani. Baba yake akatoka nje na kumsihi aingie. Lakini yeye akamjibu: ‘Kumbuka! Miaka yote nimekutumikia, sijavunja amri yako hata mara moja. Umenipa nini? Hujanipa hata mwanambuzi mmoja nikafanye sherehe pamoja na rafiki zangu! Lakini mtoto wako huyu aliyekula mali yako pamoja na makahaba, mara tu alipokuja umemchinjia yule ndama mnono.’ Baba yake akamjibu: ‘Mwanangu, wewe uko pamoja nami siku zote, na kila nilicho nacho ni chako. Ilitubidi kufanya sherehe na kufurahi, kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa amekufa, kumbe yu mzima; alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana.’”

Asante kwa Neema/Rehema zako zatutosha hakuna cha kulinganisha nawe Mfalme wa Amani..Tunayaweka haya yote mikononi mwako tukisifu, tukiamini na kushukuru..
Amina..!!
Mungu aendelee kuwabariki katika yote..wote mliopita hapa nawapenda na Asanteni sana..

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote...

Amina. 



Wimbo wa Mose

1 Taz Ufu 15:3 Hapo, Mose pamoja na Waisraeli wakamwimbia Mwenyezi-Mungu wimbo huu,
“Nitamwimbia Mwenyezi-Mungu kwani ameshinda kwa fahari,
farasi na mpandafarasi wake amewatosa baharini.
2 Taz Zab 118:14; Isa 12:2 Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu na uwezo,15:2 uwezo: Kiebrania: Wimbo.
yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.
Yeye ni Mungu wangu nami nitamsifu,
ni Mungu wa baba yangu nami nitamtukuza.
3Mwenyezi-Mungu ni shujaa vitani;
Mwenyezi-Mungu ndilo jina lake.
4“Magari na majeshi ya Farao ameyatumbukiza baharini,
maofisa wake wateule wamezama katika bahari ya Shamu.
5Vilindi vya maji vimewafunika,
wameporomoka baharini kama jiwe.
6“Mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu watukuka kwa nguvu;
kwa mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu wawaponda adui.
7Kwa wingi wa ukuu wako wawaangamiza wapinzani wako;
wawapulizia ghadhabu yako nayo yawateketeza kama makapi.
8Kwa pumzi ya pua yako maji yalirundikana,
mawimbi yakasimama wima kama ukuta;
vilindi katikati ya bahari vikagandamana.
9Adui alijisemea, ‘Nitawafuata na kuwakamata;
nitagawanya nyara mpaka hamu yangu iishe.
Tutaufuta upanga wetu,
tutawaangamiza kwa mkono wetu.’
10Lakini wewe uliuvumisha upepo wako,
nayo bahari ikawafunika.
Walizama majini kama risasi.
11“Ewe Mwenyezi-Mungu,
ni nani kati ya miungu anayelingana nawe?
Ni nani aliye kama wewe uliye mtakatifu mkuu,
utishaye kwa matendo matukufu,
unayetenda mambo ya ajabu?
12Uliunyosha mkono wako wa kulia,
nayo nchi ikawameza maadui zetu.
13“Kwa fadhili zako kuu umewaongoza watu uliowakomboa,
kwa nguvu yako umewaongoza kwenye makao yako matakatifu.
14Watu wa mataifa wamesikia hayo wakatetemeka;
wakazi wa Filistia wamekumbwa na kitisho.
15Wakuu wa Edomu wamefadhaishwa;
viongozi wa Moabu wamekumbwa na woga mkuu;
wakazi wote wa Kanaani wamevunjika moyo.
16Kitisho na hofu vimewavamia.
Kwa sababu ya ukuu wa nguvu zako,
wao wamenyamaza kimya kama jiwe,
mpaka watu wako ee Mwenyezi-Mungu, wapite,
naam, mpaka watu hao uliowakomboa wamewapita.
17Wewe utawaleta watu wako na kuwapanda mlimani pako;
pale ulipochagua ee Mwenyezi-Mungu pawe makao yako,
mahali patakatifu ee Mwenyezi-Mungu ulipojenga kwa mikono yako.
18Wewe, ee Mwenyezi-Mungu,
watawala milele na milele.”
19Wakati farasi wa Farao na magari yake pamoja na wapandafarasi wake walipoingia mahali pakavu baharini, Mwenyezi-Mungu aliyarudisha maji ya bahari yakawafunika. Lakini Waisraeli waliendelea kutembea pakavu katikati ya bahari.
20Basi nabii Miriamu, dada yake Aroni, akachukua kingoma mkononi, na wanawake wengine wote wakamfuata wakiwa na vingoma vyao wakicheza. 21Miriamu akawaongoza kwa kuimba,
“Mwimbieni Mwenyezi-Mungu kwani ameshinda kwa fahari,
farasi na mpandafarasi wake amewatosa baharini.”

Maji machungu

22Kisha, Mose aliwaongoza Waisraeli kutoka bahari ya Shamu, wakaenda mpaka jangwa la Shuri. Walisafiri kwa muda wa siku tatu jangwani bila kuona maji yoyote. 23Walipofika mahali panapoitwa Mara, hawakuweza kuyanywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Kwa sababu hiyo mahali hapo pakaitwa Mara.15:23 Mara: Kiebrania maana yake uchungu. 24Basi, watu wote wakamlalamikia Mose wakisema, “Sasa tutakunywa nini?” 25Taz Sira 38:5 Hapo Mose akamlilia Mwenyezi-Mungu, naye akamwonesha kipande cha mti, na Mose akakitumbukiza katika maji; maji hayo yakawa mazuri.
Huko Mungu aliwapa Waisraeli amri na agizo, ili ajue uthabiti wao, 26akawaambia, “Ikiwa mtaisikiliza kwa makini sauti yangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, na kutenda yaliyo sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na maagizo yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ndimi Mwenyezi-Mungu ninayewaponya nyinyi.”
27Kisha Waisraeli wakawasili huko Elimu ambako kulikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini. Wakapiga kambi yao huko karibu na maji.

Kutoka15;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.