Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 31 May 2016

Kama umeguswa msaidie huyu bibi..






"Nimetumiwa na Rafiki"
~
Haya wapendwa  nataka ku share hii video na nyinyi na yoyote atakae pata imani please inbox Facebook[Nana O Al Wakuvuruga ]msaada wako. Miezi kadhaa nyuma niliwaho share hii video na baadhi ya groups ili atakae weza amsaidie huyu bibi kuna ambao wamejitolea alhamdulillah lakini kwa ufupi pesa itamtosha kwa miezi miwili mitatu kununulia kula yake halafu baada ya hapo atarudi to square one. Inawezekana mnajiuliza huyu bibi ni nani? Huyu bibi sihusiani nae na wala sijawahi kutana nae ila inshaAllah mwaka huu nitamtafuta nimjue kwa ukaribu. Mimi nilipewa video hii na mwenzangu ambae nae pia alipata kumjua mwaka jana alipoenda matembezi Tanzania. Akapewa habari ya bibi huyu ili kama anaweza amsaidie chochote. Kubwa alienipa hii taarifa kajua hawezi lifanya hili jambo peke yake ndio akanijulisha na mimi. Sasa kwa ufupi huyu bibi hakujaaliwa mtoto, amefadhiliwa na watu hicho chumba mnacho kiona kwenye video na picha nitawatumia mpate kuona vizuri mazingira anayo ishi. Hajui kula yake ataitolea wapi wala tiba, kabaki anapita akiomba ndio siku inaenda. Hicho chumba mnacho kiona kukinyesha mvua ya nguvu maji yanajaa huko chumbani kwake anashinda juu ya kitanda mpaka maji yakauke. Nahitaji watu wajitolee kwa hali na mali apate kukarabatiwa chumba chake na at least japo ajijue anapata japo mlo mmoja kwa siku. Wazee wetu kweli wana shida lakini naamini hawajafikia hali hii, kumbuka bibi huyu hakujaaliwa kuzaa kwahiyo hana matumaini zaid ya kuomba vijumbani. Please find it in your heart and inshaAllah donate whatever you can. I joke a lot this is not one of those jokes; its real for this elderly lady and ahe doesn't even know I'm doing this




"Swahili Na Waswahili"Kutoa ni Moyo.

Monday 30 May 2016

MISS TANZANIA USA PAGEANT AEESHA KAMARA TEMBELEA, KUONGEA NA KUTOA MSAADA KENTON HIGH SCHOOL


Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara akiongea na wanafunzi wa Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam siku alipotembelea shuleni hapo katika moja ya majukumu yake ya kuhudumia jumuiya. Miss Kamara anadhamini wanafunzi wawili shuleni hapo
Miss Tanzania USA Pageant Aeesha Kamara akimkabidhi msaada mwalimu mipira siku alipotembela shule ya Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania USA Aesha Kamara akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wawili anaowadhamini kwa kuwasomesha shuleni hapo.
Picha ya pamoja

TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI


TAARIFA YA MSIBA: JACQUELINE OSWALD KAPINGA WA SINZA AFARIKI

MAREHEMU JACKLINE OSWALD KAPINGA

Familia ya Marehemu Mzee Oswald Kapinga ya Sinza - Dar e salaam (karibu na  white inn) inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Jacqueline kilichotokea jana tarehe 29/05/2016 katika hospitali ya muhimbili jijini Dar es salaam. 

Familia inapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki ya kuwa, msiba utakuwa nyumbani kwa wazazi wake hapo sinza. 

Taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika, taarifa ya awali kutoka kwa familia, Marehemu wanategemea kumuhifadhi kwenye nyumba yake ya milele siku ya kesho (Jumanne) ya Tarehe 31/05/2016 katika makaburi ya sinza karibu na Ukumbi wa mwika kuanzia saa 8.00 Mchana. 

Kwa taarifa zaidi na maelekezo mbali mbali unaweza kuwasiliana na makaka wa marehemu hapo chini: 

JOSEPH O. KAPINGA (Mwananchi communication)  - 0788617654

GOSBERT O. KAPINGA - 0754286301

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, 
JINA LAKE LIHIMIDIWE
AMEN.



Sunday 29 May 2016

Natumaini Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema;Burudani-Ephraim Sekelet Uniongoze,Majaribu Ni Mtaji By Ambwene Mwasongwe,Yesu Ni Bwana by E R Mwansasu Chidumule

Wapendwa habari za Jumapili,Natumai ni njema/inaendelea vyema..
kwetu ni salama kabisa na tunaendelea vyema na leo kulikuw na jua
jumapili inaishia vizuri..

Basi tuendelee kuombeana katika yote,Uwepo wa Mungu utawale pale ulipo,
Watoto wanaondelea na shule Mungu akawaongoze vyema,wale walio kwenye mapumziko kama hapa
kwetu wakawe na wakati mzuri,
Mungu awabariki na kuwaongoza..

          

Neno La Leo;3 Yahane 1-15
Mimi mzee, nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni. 3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakashuhudia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli. 4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.

                       Uaminifu wa Gayo
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni. 6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu. 7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.



Diotrefe na Demetrio
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza. 10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuza nje ya kanisa.
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.


 
                                 
 

Salamu za mwisho
13Ninayo bado mengi ya kukuambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino. 14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana.
15Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.







"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 26 May 2016

Jikoni Leo na Bi Sheikha Agili-Achari ya Mraba





Ingredients:
2 cups sugar
1 and a half cups water
Salt
Chili powder
Red food colour 
Dried uncooked achari (slithered mangoes that have been dried in the sun)
Method:
In a pot, add everything except the achari.
Cook the mixture until it gets sticky enough and the liquid has reduced abit then add the achari and mix well while still on the stove.
You can leave the achari abit saucy(rojo) or let the liquid dry abit so they be somewhat sticky(mraba). If the syrup is done right you can even let liquid completely dry and let the achari get coated with sugar while the syrup is drying (kavu).
Once the desired stage of the achari is reached remove from the stove and let them cool.
Enjoy!!


Zaidi ingia;Sheikha Agil


"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 22 May 2016

Natumaini Jumapili ilikuwa njema/inaendelea vyema;Burudani-Natembea kidogo kidogo nikinyatanyata......Happy Birthday da'Tracey-Sarah

Wapendwa natumai Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Mungu azidi kuwabariki katika yote..


Hapa kwetu Jumapili ni njema kabisaa
Leo tunaungana na binti yetu mpendwa kwa kumbukumbu yake ya siku ya kuzaliwa
Siku kama ya leo Mungu alitubariki na kutujaalia mtoto wa kike da'Trace-Sarah
Mungu anaendelea kumtunza vyema katika yote..
Mungu yu mwema sana tunamrudishia sifa na utukufu kwakwe
Tunamwachilia binti huyu mikononi mwake Baba wa Mbinguni katika yote
Aendelee kuwa Baraka kwetu kama wazazi,walezi, Ndugu,Jammaa,Marafiki na Jamii yote
Mungu yu Mwema mnoooo
Happy Birthday da'Tracey-Sarah.

 8Mungu asema: “Nitakufunza
na kukuonesha njia unayopaswa kufuata.
Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.

Neno La Leo;Zaburi:32:8-11

9Usiwe mpumbavu kama farasi au nyumbu,
ambao lazima wafungwe lijamu na hatamu,
la sivyo hawatakukaribia.”
10Watu waovu watapata mateso mengi,
bali wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu wazungukwa na fadhili zake.
11Furahini na kushangilia kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu;
pigeni vigelegele vya shangwe enyi wanyofu wa moyo.

Bible Society of Tanzania


"Swahili Na Waswahili"Muwe na wakati mwema.

Wednesday 18 May 2016

Chaguo La Mswahili Leo:Yemi Alade - Na Gode (Swahili Version Official Video)

Chaguo La Mswahili Leo...
dada Yemi Alade ..

Sema Asanteehh hata ukikosa eehh sema Asante kweli wewe ni Mungu..........
.


"Swahili Na Waswahili"Burudika.

Tuesday 17 May 2016

Kipindi cha Jukwaa Langu May 16 2016. Ziara ya Waziri mkuu UK. Uraia pacha


Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na waTanzania waliojumuika kumsikiliza jijini London


Kipindi cha JUKWAA LANGU hukujia kila Jumatatu kikiongozwa na Mubelwa Bandio toka Beltsville Maryland, USA, kuzungumzia mambo mbalimbali yanayoihusu Tanzania ya sasa na ile tuitakayo.

Ni Tanzania kutoka jicho la DIASPORA

Na katika kipindi cha juma hili, tulizungumza na Chris Lukosi, ambaye
alitupa muhtasari wa ziara ya Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim
Majaliwa huko nchini Uingereza.

Muhtasari huo ulizua na mjadala mkali juu ya ahadi za serikali kuhusu vibali maalum kwa waTanzania waishio nje ya nchi.

Karibu

Sunday 15 May 2016

Nawatakia Jumapili njema:Burudani/Mahubiri na Mwl.Christopher Mwakasege...


wapendwa nimatumaini yangu jumapili ni njema na inaendelea vyema
Nawatakia Amani kutoka Moyoni,Imani,Baraka na Mkono wa Mungu ukawaguse
wote wenye kukata tamaa,wagonjwa,misiba,woga,kuonewa,kukataliwa/kutengwa
wagonjwa na wenye shida/tabu..
Amini Mungu yupo na ukimuita ataitika,Mungu wetu si kiziwi,kipofu...Anaweza na alitenda anatenda anaendelea kutenda....














"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Sana.

Thursday 12 May 2016

Jikoni Leo na Tupike Pamoja; Recipe of Lemon chicken

Wapendwa waungwa natumai muwazima..
hapa kwetu tupo tupo vyema kabisa na hali ya hewa ni nzuri...kijua kimetoka..
vipi huko uliko wewe?

Ni Jikoni Leo sambamba na Tupike Pamoja wametuletea toleo jipya...

nisikuchoshe na maneno meengi Karibuni..


.....twende pamoja...


zaidiingia;Tupike Pamoja



"Swahili na Waswahili"Pamoja Daima

Sunday 8 May 2016

Jumapili iendelee kuwa Njema;Burudani-Christopher Mwahangila-Mungu Ni Mungu Tu na Edson Mwasabwite - Ni Kwa Neema Na Rehema





Natuini Jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Mungu azidi kuwabariki kwa kila jambo..
wanaopitia magumu..Mungu akawaguse..
Mungu yu mwema sana...
Nawapenda wote na muwe na wakati mwema...


Umuhimu wa methali
1  Hizi ni methali za Solomoni mfalme wa Israeli, mwana wa Daudi.2Methali hizi zawapatia watu hekima na nidhamu; zawafanya waelewe maneno ya busara, 3zawafanya kuwa na nidhamu, utaratibu, uadilifu, haki na kutenda kwa usawa. 4Huwapatia wajinga werevu na vijana maarifa na hadhari. 5Mwenye hekima azisikie na kuongeza elimu yake, naye mwenye busara apate mwongozo. 6Mtu aelewe methali na mifano, maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.
7  Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa maarifa,
lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
Bible Society of Tanzania





"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.