Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 27 October 2015

Kipindi cha Jukwaa Langu Okt 26 2015 (FULL)


Photo Credits: dw.com/sw


Kipindi hiki hukujia kila JUMATATU, kujadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Na leo, tulizungumzia Tanzania baada ya Uchaguzi wa jana Oktoba 25, 2015

Sunday 25 October 2015

Nawatakia Jumapili Njema na Uchaguzi mwema ;Tanzania Kwanza,Burudani-Kinondoni Revival Choir Twalilia Tanzania

Wapendwa/Waungwana natumai hamajambo na Jumapili hii ya Uchaguzi Tanzania ni njema..
Mungu azadi kuibariki Tanzania na Watanzania katika yote,Uchaguzi uwe wa haki,Amani,Utulivu.
Amani,Upendo,Umoja,Mshikamano,Undugu,Hekima,Busara vikatawale...
Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika.


1Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima. 2Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli. 3Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu. 4Maana kwa kuja kwake Kristo, sheria imefikia kikomo chake, ili wote wanaoamini wafanywe waadilifu.

Neno La Leo;Warumi 10:1-21
Ukombozi kwa wote
5Kuhusu kuwa mwadilifu kwa kuitii sheria, Mose aliandika hivi: “Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya sheria ataishi.”6Lakini kuhusu kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: “Usiseme moyoni mwako: ‘Nani atapanda mpaka mbinguni?’ (yaani, kumleta Kristo chini); 7wala usiseme: ‘Nani atashuka mpaka kuzimu?’ (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu).” 8Maandiko Matakatifu yasema hivi: “Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako” nao ndio ile imani tunayoihubiri.9Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka. 10Maana mtu huamini kwa moyo akafanywa mwadilifu; na hukiri kwa kinywa akaokolewa.11Maandiko Matakatifu yasema: “Kila anayemwamini hataaibishwa.” 12Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao. 13Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.”



14Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?15Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!” 16Lakini wote hawakuipokea hiyo habari njema. Maana Isaya alisema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?” 17Hivyo basi, imani inatokana na kuusikia ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
18 Lakini nauliza: Je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:
“Sauti yao imeenea duniani kote;
maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu.”
19Tena nauliza: Je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni wa kwanza kujibu:
“Nitawafanyeni muwaonee wivu
watu ambao si taifa;
nitawafanyeni muwe na hasira
juu ya taifa la watu wapumbavu.”
20Tena Isaya anathubutu hata kusema:
“Wale ambao hawakunitafuta wamenipata;
nimejionesha kwao wasiouliza habari zangu.”
21Lakini kuhusu Israeli anasema:
“Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii.”
Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Tuesday 20 October 2015

Kipindi cha Jukwaa Langu Oct 19 2015 (Full)


Kipindi hiki hukujia kila JUMATATU, kujadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Ni kipindi cha mwisho kabla ya uchaguzi, na washiriki wengi walishiriki kutoa mchango wao kuhusu mchakato ulivyokuwa, na neno ama wosia wao kwa waTanzania wote

KARIBU

Sunday 18 October 2015

SHINE WITH SHINA ANNUAL GALA 2015 YAFANA GREENBELT, MARYLAND


Meza kuu kutoka kushoto ni Bi. Jennifer Jones ambaye ni ni mkuu wa Kamisheni ya wanawake kaunti ya Prince George, Afisa Suleiman Saleh ambaye alimwakilisha Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi. Kulia ni Dr. El Senzengakulu Zulu ambaye ndio mwanzilishi na mmiliki wa shule ya Ujamaa inayofundisha tamaduni za bara la Afrika. PICHA NA KWANZA PRODUCTION/VIJIMAMBO BLOG.
Kutoka kushoto ni Dr. John Rutayuga ambaye ni mwanzilish wa Ukwimwi Orphans akiwa meza kuu na Mr and Mrs William.
Mshereheshaji Tuma akifungua pazia ya kuashiria SHINA Gala imefunguliwa rasmi siku ya Jumamosi Octoba 17, 2015 ndani ya Hotel ya Hilton iliyopo Greenbelt, Maryland na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali Watanzania na marafiki zao wakiwemo wawakilishi wa makampuni yanayoshirikiana na SHINA kwa ajili ya kusaidia misaada mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule nchini Tanzania. 
 Kikundi cha sanaa cha Taratibu Youth Association kikifungua pazia la burudani hku wakishangilia muda wote kwa umahiri wao wa kucheza ngoma za asili kutoka Tanzania. Kundi hili hupata mialiko mabara mbalimbali kujifunza na kufanya maonesho ya ngoma za asili ambazo hua kivutia kwa watazamaji.
 Wapiga ngoma wa Taratibu Youth Association.
Mwanzilishi na mmiliki wa SHINA kwa heshima na taadhima akiwashukuru watu waliofika kwenye SHINA Gala Dinner na kusaidia kuchangisha pesa za kusaidia misaada mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule nchini Tanzania.
 Afisa Suleiman Saleh akimwakilisha Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi ambaye ndiye aliyekua awe mgeni rasmi kwenye SHINA Gala iliyofanyika siku ya Jumamosi Octoba 17, 2015 katika hoteli ya Hilton, Greenbelt, Maryland nchini Marekani.
Afisa wa Ubalozi Bwn. Suleiman Saleh akimzawadia Bi. Jessica Mushala zawadi kutoka Zanzibar ambayo baadae ilifanyiwa mnada ili fadha zisaidie kumalizia ujenzi wa shule nchini Tanzania.
Bi. Jennifer Jones Kamisheni ya wanawake kaunti ya Prince George's ambaye ndiye aliyekua msemaji mkuu huku akishangiliwa muda wote kwa ujumbe mzito aliokua akiutoa mara kwa mara kwenye hotuba yake.
Bi. Jessica Mushala akimzawadia Bi. Jennifer Jones zawadi maalum.
Bwn. Amos Mushala akimzawadia Dr. John Rutayuga zawadi maalum kutambua mchango wake katika kuendelea kupambana ikiwemo kuwasaidia waathirika wa Ukimwi nchini Tanzania.
Dr. John Rutayuga akitoa shukurani zake kwa SHINA.
Mwimbaji wa nyimbo za injili DMV Bi. Rose Kachuchuru akiimba moja ya nyimbo zake.


Mwambata wa Jeshi Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Canada Colonel Adroph Mutta katika picha na mkewe walipohudhuria SHINA Gala Dinner hiyo. 

Kwa picha zaidi bofya HAPA

Thursday 15 October 2015

Mahojiano na waasisi wa Jabali Afrika

Wawili kati ya waanzilishi wa JABALI AFRIKA, Justo Asikoye na Joseck Asikoye walipata fursa ya kutembelea Kilimanjaro Studio zilizopo Beltsville Maryland na kuzungumza na Mubelwa Bandio na Dj Luke Joe kuhusu kazi zao
Ilikuwa ni katika kipindi cha MISHUMAA YA KALE kinachosikika kila Ijumaa kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Marekani ya Mashariki
KARIBU


Tuesday 13 October 2015

Mahojiano na DC Paul Makonda Katika JUKWAA LANGU Oct 12 2015


Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015.

Katika
sehemu hii ya kipindi cha wiki hii, utasikia mahojiano yetu na Mkuu wa
Wilaya ya Kinondoni, Mhe Paul Makonda juu ya Matembezi ya Amani
yaliyoandaliwa na Ofisi yake na kufanyika wilayani humo

Pia wasikilizaji walipata fursa kumuuliza maswali na hata kutoa maoni yao juu ya kinachoendelea huko

KARIBU

Monday 5 October 2015

Ibada ya kumuombea Mama Kateng'anyenyi iliyofanyika Silver Spring MD






Broadcast live streaming video on Ustream





Broadcast live streaming video on Ustream



Padri Lehandly Kimario akiongoza ibada ya kumuombea mpendwa dada, mama na bibi yetu Bettisheba Pole Ketang'enyi iliyofanyika siku ya Jumapili Octoba 4, 2015 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.


Mtoto wa marehemu Felicia Simms akisoma wasifu wa marehemu katika ibada ya kumuombea mpendwa dada, mama, bibi Bettisheda Pole Keteng'enyi iliyofanyika siku ya Jumapili  Octoba 4, 2015 Silver Spring, Maryland nchini Marekani.

Kwa picha zaidi bofya HAPA

Sunday 4 October 2015

Muendelee vyema na Jumapili hii;Burudani-Mchanganyiko(African Praise&Worship)

Wapendwa/Waungwana;Muendelee vyema na Jumapili hii...
Baraka,Amani,Furaha,Upendo,Hekima,Busara vikatawale majumbani mwenu
Shukrani na Utukufu ni kwa MUNGU.


1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo, tunawaandikia nyinyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho, na watu wote wa Mungu kila mahali katika Akaya. 2Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.


Neno La Leo:2Wakorintho 1:1-23
Shukrani kwa Mungu
3Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye huruma na Mungu mwenye kuleta faraja yote. 4Yeye hutufariji sisi katika taabu zetu zote, ili nasi tupate kuwafariji wengine katika kila taabu kwa faraja hiyohiyo tunayopokea kutoka kwa Mungu. 5Naam, kadiri mateso ya Kristo yanavyozidi ndani yetu, ni kadiri hiyohiyo tunazidi kufarijiwa naye. 6Ikiwa tunapata taabu, basi ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu. Tukifarijika, ni kwa ajili ya kuwafariji nyinyi na kuwaunga mkono mpate nguvu ya kustahimili mateso yaleyale tunayoteseka sisi. 7Tena, matumaini tuliyo nayo kwa ajili yenu ni imara; tunajua kwamba mkishiriki mateso yetu, mtashiriki pia faraja yetu.
8Ndugu, tunataka kuwajulisheni taabu zilizotupata kule Asia; taabu hizo zilitulemea kupita kiasi, hata tukakata matumaini yote ya kuendelea kuishi. 9Naam, tulikuwa kama watu waliohukumiwa kuuawa, ili tufundishwe kumtegemea Mungu mwenye kuwafufua wafu, badala ya kutegemea nguvu zetu sisi wenyewe. 10Yeye alituokoa katika hatari kubwa ya kifo, na anaendelea kutuokoa; sisi tumemwekea tumaini letu kwamba atatuokoa tena, 11nyinyi mkiwa mnatuunga mkono kwa kutuombea. Hivyo neema tutakazokuwa tumepata kutokana na maombi ya watu wengi hivyo, ziwe sababu ya watu wengi zaidi kumshukuru Mungu kwa ajili yetu.
Badiliko katika safari ya Paulo
12Sisi tunajivunia kitu kimoja: Dhamiri yetu inatuhakikishia kwamba tumeishi ulimwenguni hapa, na hasa kati yenu, kwa unyenyekevu na unyofu tuliojaliwa na Mungu; hatukuongozwa na hekima ya kibinadamu bali na neema ya Mungu. 13Tunawaandikia nyinyi mambo mnayoweza kuyasoma na kuyaelewa. Ninatumaini kwamba mtaelewa vizuri kabisa, 14maana mpaka sasa mmenielewa kiasi fulani tu. Tunajua kwamba katika ile siku ya Bwana Yesu mtaweza kutuonea sisi fahari kama nasi tunavyowaonea nyinyi fahari.
15Nikiwa na matumaini hayo, nilikusudia kuja kwenu hapo awali ili mpate baraka maradufu. 16Nilikusudia kupita kwenu nikiwa safarini kwenda Makedonia na wakati wa kurudi pia, ili nipate msaada wenu kwa safari yangu kwenda Yudea. 17Je, mnadhani nilipopanga hivyo nimekuwa kama mtu asiye na msimamo? Je, mnadhani kwamba ninafanya uamuzi wangu kwa fikira za kibinadamu na kwamba nasema “Ndiyo” na “Siyo” papo hapo? 18Mungu ni ukweli tupu; basi, kile tulichowaambia nyinyi si jambo la “Ndiyo” na “Siyo”. 19Maana Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye mimi, Silwano na Timotheo, tulimhubiri kwenu, hakuwa mtu wa “Ndiyo” na “Siyo;” bali yeye daima ni “Ndiyo” ya Mungu.20Maana ndani yake ahadi zote za Mungu zimekuwa “Ndiyo”. Kwa sababu hiyo, “Amina” yetu husemwa kwa njia ya Kristo kwa ajili ya kumtukuza Mungu. 21Mungu mwenyewe ndiye mwenye kutuimarisha sisi na nyinyi pia katika Kristo, na ndiye anayetuweka wakfu; 22ndiye aliyetutia mhuri wa kuwa mali yake yeye na kutujalia Roho mioyoni mwetu kama dhamana ya mambo yote ambayo ametuwekea.
23Mungu ndiye shahidi wangu; yeye anajua moyo wangu! Mimi sikuja tena Korintho kwa sababu tu ya kuwahurumieni. 24Hatutaki kutumia mabavu juu ya imani yenu; nyinyi mko imara katika imani yenu. Wajibu wetu ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya furaha yenu.
Bible Society of Tanzania

"Swahili na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Friday 2 October 2015

Thursday 1 October 2015

Msiba MAREKANI na TANZANIA


Bettisheba Pole Ketang'enyi enzi ya uhai wake

Tunasikitika kutangaza kifo cha mama Betisheba Ketangenyi, mama yake Yvonne Matinyi, Felicia Simms, Fredderek Ketangenyi pia ni Dada yake na Rossie Musika, Neema Musika, Daudi Musika, Sijaona Musika kilichotekea 9/30/15 katika hospitali ya NIH Maryland mipango ya kusafiri mwili wa marehemu inaendelea kwa mdogo wa marehemu Daudi Musika
3819 Gateway terrace Burtonsville MD 20866
Unaweza kuwasiliana
Frederick Ketangenyi 267 809 5124
Felicia Simms 240 608 8686
Rossie Musika 240 408 2693
Neema Musika 571 991 9819
Specioser Musika 571332 2215
Sijaona Musika 202 487 8412