Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 24 November 2015

Kipindi cha Jukwaa Langu Nov 23 2015 (MJADALA)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk John Magufuli akizindua Bunge la 11
Kipindi hiki hukujia kila jumatatu kuanzia saa 11 jioni kwa saa za
Marekani ya Mashariki kuijadili Tanzania ya sasa na ile tuitakayo
Katika kipindi hiki tumejadili (mbali na mambo mengine) muelekeo wa serikali ya Tanzania baada ya kuzinduliwa kwa Bunge la 11.
Mjadala huu ambao ulifuata HABARI kutoka magazeti mbalimbali, umehusisha wadau toka Marekani, Canda na India
Karibu
Waweza kutusikiliza kupitia tovuti zetu www.kwanzaproduction.com na www.vijimamboradio.com

Monday 23 November 2015

MISA TAKATIFU YA KUMBUKUMBU YA NYAMITI LUSINDE BALTIMORE, MARYLAND




 Picha ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde ikiwa kanisani
siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 siku ilikofanyika misa takatifu ya
kumbukumbu na kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe.
Wilson Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae. Nyamiti
alikua mfanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani alipatwa na
mauti alipokua likizo Tanzania katika hospitali ya Kariuki alipokua
amekwenda kwa matibabu baada ya kuugua ghafla alipokua huko na baadae
kuaga Dunia Novemba 17, 2015. Picha na Vijimambo/Kwanza
Production




Father Honest Munishi akiongoza misa takatifu ya kumbukumbu ya
mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 na
kuhudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson
Masilingi akiwa ameongozana na mkewe pamoja na mwanae. 


Father Lehandry Kimario akisaidiana na Father Honest Munishi katika
kuongoza misa takatifu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde
iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland
nchini Marekani.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
nchini Marekani akiwa na mkewe Marystella Masilingi wakifuatilia misa
takatifu ya kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde
iliyofanyika siku ya Jumapili Novemba 22, 2015 Baltimore, Maryland
nchini Marekani.
Balozi Mhe. Wilson Masilingi akiongea machache jinsi alivyomjua
Nyamiti na kutoa shukurani zake kwa watu mbalimbali ikiwemo kamati
iliyowezesha kufanikisha misa hiyo na shukurani za pekee kwa Father
Honest Munishi na Father Lehandry Kimario.
Kulia ni Sima Kazaura akisoma soma la kwanza huku akiwa
amesindikizwa na Dorothy.
Kulia ni Farida Sarita akisoma soma la pili huku akiwa
amesindikizwa na Dorothy.
 Mshereheshaji Tuma akiongea jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu
Nyamiti.
 Kulia ni Rosemary Commodores akisoma wasifu wa marehemu.
 Kulia ni Afisa Ubalozi Suleiman Saleh akitoa salamu za
Ubalozi, kushoto ni mkewe.
 Dorothy akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti.
 Sima Kazaura akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu
Nyamiti
 Patrick Kajale akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu
Nyamiti
Eddah Gachuma akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti
Dj Luke akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti
Joyce akieleza jinsi alivyomfahamu mpendwa wetu Nyamiti
Pius Mtalemwa kiongozi wa kanisa la ibada ya Kiswahili DMV
akihitimisha kwa kutoa shukurani kwa wote.


Nelson Masilingi, mtoto wa Mhe. Balozi akifuatilia misa takatifu ya
kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde.


Mwambata wa Jeshi Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Canada
Col. Adolph Mutta akiwa na mkewe wakifuatilia misa takatifu ya
kumbukumbu ya mpendwa wetu Nyamiti Ivan Lusinde.


Watu mbalimbali waliohudhuria misa.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Wednesday 11 November 2015

Mahojiano na Liberatus Mwang'ombe katika kipindi cha JUKWAA LANGU


Liberatus Mwang'ombe katika moja ya mikutano yake jimboni Mbarali
Katika kipindi cha JUKWAA LANGU wiki hii tulipata fursa kuongea na aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Mbarali kupitia CHADEMA Liberatus Mwang'ombe ambaye ameeleza mengi kuhusu uchaguzi ulivyokuwa, aliyojifunza, analotaka kufanya kuhusu matokeo na hata kwa wana-diaspora wengine wenye nia ya kugombea nafasi mbalimbali Tanzania


[AUDIO]: Kipindi cha Jukwaa Langu Nov 9 2015 (Full show)


Katika kipindi cha JUKWAA LANGU tulipata fursa kumhoji
aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Mbarali kupitia CHADEMA Liberatus
Mwang'ombe.
Pia, tuliangalia (mbali na mambo mengine), mwanzo wa awamu ya tano ya utawala wa Tanzania, na matarajio ya wengine.
Tunaizungumzia TANZANIA ya sasa na ile ijayo....hasa tutakayo.

Tuambie.......
1: Je! Ni lipi unalokumbuka zaidi kuhusu uongozi wa Rais Jakaya Kikwete?
2: Unazungumziaje namna Rais Magufuli alivyoanza wiki ya kwanza ofisini?
Na nini ungependa viwe vipaumbele kwa uongozi huu??
3: Una matumaini na matarajio gani na bunge la 11 litakalosimikwa rasmi hivi karibuni?

Sunday 8 November 2015

EXIM BANK YAFANYA USAILI KWA WANA-DIASPORA NEW YORK


Exim Bank ya Tanzania siku ya Jumamosi ilifanya usaili kwa Diaspora
Watanzania wanaoishi nchini Marekani jijini New York kwa ajili ya
kuwapa kipaumbele Diaspora na hatimaye kuwapatia kazi kwenye Benki
 hiyo yenye makao makuu yake Dar es Salaam, Tanzania.

Akiongea na Vijimambo/Kwanza Production mkuu wa human resources Bwn.
Fredirick Kanga alisema sababu kubwa ya Benki hiyo kuwafanyia usaili
Diaspora ni kutambua mchango wao na mfumo wa uchapa kazi waliouzoea
ili waweze kuutumia nyumbani katika kuleta maendeleo yenye ufanisi
katika sekta mbalimbali kwenye Benki hiyo ambayo kazi kubwa ni kutoa
huduma bora kwa wateja wake.

Bwn. Fredirick Kanga akijibu swali ni kwanini wasitafute wafanyakazi
waliopo Tanzania ambao wengi wao wamemaliza masomo ya juu na hawana
kazi. Bwn. Kanga alisema sababu kubwa ya kuja Diaspora nikutokana na
kutambua mchango mkubwa wa Diaspora na ufanisi wao katika kazi na sio
kweli kwamba hatuajili Watanzania waliopo nyumbani, tunachojaribu ni
kuchanganya ujuzi wa Diaspora na nyumbani ili kufanikisha na hatimae
kutoa  huduma bora na zenye ufanisi mkubwa, huku akisema Benki ya
Exim ndio Benki yenye asilimia ndogo ya makato kwenye akaunti za
wateja wao nchini Tanzania.

Bwn. Kanga alisema tangia tuanze kuasaili Diaspora tumeisha wapatia
kazi wapatao 25 na mwaka jana pekee tuliwapatia nafasi Diapora 6 toka
Uingereza na 3 kutoka nchini Marekani. Baadhi ya Diaspora wanapenda
kurudi nyumbani lakini wanahofia jinsi gani ya kuanza maisha yao mapya
baada ya kukaa ughaibuni kwa muda mrefu. Exim Benki imeliangalia hilo
na ndio sababu kubwa inayowafanya kufanya usaili kwa WanaDiaspora
anaporudi nyumbani anauhakika na kazi yake.
 Kulia ni Paul Rupia kutoka Massachusetts akifanyiwa usaili na
Bwn. Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Ability Kakama kutoka New York akifanyiwa usaili na
Bwn. Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exam Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Pamela Mgema kutoka Texas akifanyiwa usaili na Bwn.
Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Peter Mgema kutoka Texas akifanyiwa usaili na Bwn.
Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
 Kulia ni Mariam kutoka Columbus, Ohio akifanyiwa usaili na
Bwn. Frederick Kanga na  Dinesh Arora (kulia) ambaye ni Chief
Executive Officer wa Exim Bank siku ya Jumamosi Novemba 7,
2015 katika hotel ya Hilton
katikati ya jiji la New York
Kie Mlay (kulia) kutoka Maryland akiongea jambo na Bwn, Frederick
Kanga wakati wa usaili wa kujaribu kuwaoatia Diapora nafasi za kazi
kwenye Benki ya Exim yenye makao makuu yake jijini Da es Salaam siku
ya Jumamosi Novemba 7, 2015 katika hotel ya Hilton katikati ya jiji la
New York..