Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 23 August 2015

MISS TANZANIA USA: MAJAJI WAMPOKONYA USHINDI DOREEN PANGA NA KUMVIKA TAJI AEESHA KAMARA NJE YA UKUMBI


Aeesha Kamara sasa ndiye mshindi wa Miss Tanzania USA pageant
  Miss Africa 2014-15 akipata picha ya pamoja na Doreen Panga baada
ya kuvikwa taji la Miss Tanzania USA 
Miss Africa 2014-15 akipata picha ya
pamoja na Aeesha Kamara baada kuvikwa taji na maamuzi ya majaji ambao
hawakukubaliana na mshindi aliyetangazwa kwanza.

Doreen Panga kutoka New York usiku wa Aug 22, 2015, alivuliwa taji la Miss
Tanzania USA na majaji wa shindano hilo nje ya ukumbi taji alilolivaa kwa
dakika 45 na kumvika Aeesha Kamara wa Maryland kwa madai kwamba Doreen
Panga hakua chaguo lao.

Majaji hao Peter Walden, Elaine Roecklein, Tee Thompson, Bertini Huemegni,
Tina Semiti Magembe, Mayor Mlima, Uche Ibezzue wakiongozwa na Michael Lewis
McBride kwa pamoja walikataa kukubaliana na mshindi aliyetangazwa na
kufanya kikao nje ya ukumbi wakati watu wakiondoka ondoka nao
wakisikitishwa na maamuzi ya kutangazwa mshindi huku na kama majaji
wangekaa kimya basi masahabiki wa shindano hilo wangepelekea lawama kwa
majaji.Jaji Dr. Secelela Malecela japo kwamba alipingana na Doreen Panga
kutangazwa mshindi lakini hakukubaliana na majaji wenzake Doreen avuliwe
taji na apewe Aeesha Kamara aliyekua chagua la majaji wengine, yeye
alipendekeza kwa kua kosa lishafanyika waachane nalo wahakikishe mwakani
halitokei tena. Wazo lake lilipingwa na majaji wenzake pale pale.

Shindano hilo lilianza vizuri kwa nyimbo za Taifa za Marekani na Tanzania
zilizoongozwa na watoto Brian akiwa kwenye kinanda na dada yake Briana
akiwa kwenye kipza sauti,

Baadae walitambulishwa ma miss wa
kesho watoto wa DMV wenye umri wa miaka 9 na 12 na baada ya hapo waliingia
malikia wenyewe huku wakisindikizwa na wimbo wa Diamond wa mdogo mdogo na
baadae kujitambulisha kwa majaji.

Washiriki wa miss Tanzania USA
walikua Rechel Mujaya kutoka Atlanta, Joyce Mkapa toka New York, Doreen
Panga toka New York, Aeesha Kamara toka Maryland, Aziza Gama toka Maryland
na Brenda Panga toka New York. Washiriki walianza shindano kwa kujielezea
wakifuatia na shindano la vipaji na baadae kujibu maswali ya majaji.

Pia katika shindano hilo kulikua na burudani mbalimbali akiwemo Mr Tz
ambaye aliitambulisha singo ya wimbo wake mpya uliotoka mwei uliopita,
Wasanii wengine walikua kutoka Ivory Coast na Jamaica.

Baada ya hapo ndipo kulitangazwa mshindi kuwa ni Doreen Panga ushindi ambao
waliowengi hawakukubaliana nao wakiwemo majaji na mkurugenzi na mwanzilishi
wa Miss Africa USA ambao walisikika wakinong'ona huku wakiulizana imekuaje
bila kupata majibu.

Wakati majaji wakiwa nje ya ukumbi wakitafakali imekuaje tumeacha shughuli
zetu tumekuja hapa tunatoa maamuzi sasahihi halafu mtu anatuzarau maamuzi
yetu. Mashabiki walianza kuondoka baada ya shindano hilo kufikia ukingoni
na wengine wakimtupia lawama wandaaji kwa kuvurunda shindano.

Majaji walipokua wakijadiliana wafanye nini walikuja na kuazimia kwa kauli
moja  lazima wampe ukweli mwandaaji kwamba hawakufurahika na
kilichotokea ndani ya ukumbi. Mwandaaji wa Miss Tanzania USA aliitwa ndipo
majaji wakatoa dukuduku lao na mwandaaji akajitetea kwamba mshindi amesema
hataweza kushiriki mashindano hayo na ameamua kumpa taji mshindi wa pili
ambaye alikua Aziza Gama, baada ya kusikia hayo majaji walimwita Doreen
Panga na kumuuliza sababu yake ya kutaka kumvisha taji mshindi wa pili ni
nini yeye akawajibu ni kutokana na kazi zangu ninazofanya hospitali
sitaweza kupata muda wa ushiriki kwa hiyo badala yake nitampa taji mshindi
wa pili.

Majaji walishindwa kuafikiana na Doreen na kuamua kupiga kura upya ndipo
wote kwa pamoja kasolo Dr Secelea Malexela walimchagua Aeesha Kamara kwamba
ndiye aliyestahiki kuvigwa taji na ndio aliyekua chaguo lao.

Doreen Panga akavuliwa taji na kuvikwa Aeesha Kamara huku Doreen akionesha
kutokubaliana na majaji lakini wao ndio waamuzi wa mwisho na kitendo
walichokifanya ni kulinda heshima yao.

Sasa Miss Tanzania USA ni Aeesha Kamara.






No comments: