Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 3 May 2015

Natumai Jumapili Inaendele Vyema;Burudani-Freedom-Eddie James,Worshiping You - Deluge,Phil Wickham - At Your Name...


Wapendwa;Natumaini Jumapili inaendelea vyema,Iwe yenye Imani,Tumaini,Uponyaji,Faraja,
Shukrani na Utukufu tumrudishie MUNGU....

At Your name, the mountains shake and crumble At Your name, the oceans roar and tumble At Your name, angels will bow, the earth will rejoice Your people cry out Lord of all the earth We shout Your name, shout Your name Filling up the skies With endless praise, endless praise Yahweh, Yahweh We love to shout Your name, oh Lord
1 Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima enyi viumbe vya mbinguni,
semeni Mwenyezi-Mungu ni mtukufu na mwenye nguvu.
2Semeni jina la Mwenyezi-Mungu ni tukufu.
Mwabuduni katika mahali pake patakatifu.

Neno La Leo Zaburi 29;1-11
Sauti ya Mungu katika dhoruba
(Zaburi ya Daudi)

3Sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya maji;
Mungu mtukufu angurumisha radi,
sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya bahari!
4Sauti ya Mwenyezi-Mungu ina nguvu,
sauti ya Mwenyezi-Mungu imejaa fahari.
5Sauti ya Mwenyezi-Mungu huvunja mierezi;
Mwenyezi-Mungu avunja mierezi ya Lebanoni.
6Huirusha milima ya Lebanoni kama ndama,
milima ya Sirioni kama mwananyati.
7Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutoa miali ya moto.
8Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa,
Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9Sauti ya Mwenyezi-Mungu huitikisa mivule,
hukwanyua majani ya miti msituni,
na hekaluni mwake wote wasema:
“Utukufu kwa Mungu!”

10Mwenyezi-Mungu ameketi juu ya gharika;
Mwenyezi-Mungu ni mfalme atawalaye milele.
11Mwenyezi-Mungu na awape watu wake nguvu!
Mwenyezi-Mungu na awabariki watu wake kwa amani!
            Bible Society of Tanzania








"Swahili Na Waswahili"Muwe na Wakati Mwema.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Kachiki Nadhani sijachelewa kukutakia nawe pia jpili njema pamoja na familia. N ahsante kwa neno

Rachel Siwa said...

Asante sana Kdala wa mimi, Ilikuwa njema kabisa..
Salaam hapo nyumbani.