Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 29 December 2015

[VIDEO] NesiWangu Show hosts ChildBirth Survival International

Harriet Shangarai, Stella Mpanda and Tausi Suedi
"Pregnancy is not an illness or disease" say Childbirth Survival International (CSI) Co-founders - Stella Mpanda, CNM and Tausi Suedi, MPH.

It is estimated at least 800 women die every day due to pregnancy, childbirth, and post-childbirth complications, most of which are preventable.

Mama Mpanda and Tausi Suedi have an informative discussion with Harriet Shangarai of Nesiwangu show (click here) and leave no stone unturned as they passionately talked about the challenges, gaps, achievements, opportunities, and shared personal stories.

This video will give you an in-depth picture of Childbirth Survival International, the amazing work the team is doing, and how you can partner to make a difference.

 For more information, visit www.childbirthsurvivalinternational.com

Kipindi cha JUKWAA LANGU Dec 28 2015 (FULL)


Photo Credits: govtech.com

Kipindi hiki hukujia kila JUMATATU, kujadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu Tanzania ya sasa na ile tuitakayo.
Wiki hii ni ya mwisho kwa mwaka 2015, hivyo kipindi hiki kimeangaza baadhi ya yaliyotokea katika siasa za Tanzania.
Studioni alikuwepo Dj Luke Joe, Said Mwamende na Mama Jessica Mushala.
Na kama kawaida, kwa njia ya simu tukaungana na wasikilizaji wengi ndani na nje ya Marekani
KARIBU

Monday 28 December 2015

Mahojiano na msanii Hashim Kambi Washington DC


Hashim Kambi ni msanii wa filamu nchini Tanzania.
Alikuwa mkarimu sana kupita studio zetu za Kilimanjaro hapa Beltsville Maryland na kuzungumza nasi


Friday 25 December 2015

Nawatakia Christmas Njema;Burudani-Boney M. Christmas Album FULL 1981,Baba Gaston - Kakolele Viva Christmas

Nawatakia  Christmas Njema Iwe yenye Heri,Baraka,Furaha na Aamani.

"I wish everyone a  Merry Christmas" 
 







"Swahili Na Waswahili"Muwe na Wakati mwema.

Tuesday 22 December 2015

Kipindi cha Jukwaa Langu Dec 21 2015 (FULL)


Kipindi hiki hukujia kila jumatatu kuanzia saa 11 jioni kwa saa za
Marekani ya Mashariki kuijadili Tanzania ya sasa na ile tuitakayo.

Kuna mengi tuliyogusia pamoja na wasikilizaji wetu

KARIBU

 

Tuesday 8 December 2015

Mahojiano na DC Paul Makonda katika kipindi cha JUKWAA LANGU Dec 7 2015




Kipindi cha JUKWAA LANGU hukujia kila Jumatatu kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Marekani ya Mashariki kuijadili Tanzania ya sasa na ile tuitakayo

Katika kipindi hiki, tumeungana na Mhe Paul Makonda. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni jiji Dar Es Salaam ambaye mbali na mambo mengine, ameeleza "ya moyoni" kuhusu tofauti iliyopo kati ya utendaji wa Rais wa awamu ya nne Mhe Jakaya Kikwete (aliyemteua katika wadhifa huo) na Rais wa sasa Dk John Magufuli. Kabla ya hapo aligusia namna alivyoteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya, na kwanini anaamini inastahili kuwepo namna nzuri zaidi ya kuteua watu katika nafasi kama yake.

Na kabla ya hayo yote, alizungumzia migogoro mbalimbali inayoendelea wilayani mwake kama wa kiwanda cha Urafiki, kubomolewa kwa nyumba za thamani, mgogoro wa Coco Beach nk.

Na kama ilivyo desturi, akapokea maswali na ushauri toka kwa wasikilizaji wetu

KARIBU

ASYA IDAROUS KHAMSINI ANOGESHA SIKU YA MTANZANIA SEATTLE, WASHINGTON


Walimbwende wakiwa tayari kufanya vitu vyao wakiwa na vivazi vya mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Mlimbwende akiwa kwenye kivazi kutoka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Kivazi chekundu kikiwa na riboni ya punda milia kikimfanya mlimbwende atabasamu jinsi gani alivyopendeza kivazi toka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.
Kivazi toka kwa mwanamitindo nguli Asya Idarous Khamsini kwenye siku ya Mtanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 Seattle jimbo la Washington nchini Marekani.

Sunday 6 December 2015

BALOZI WILSON MASILINGI AANZA ZIARA YA KUTEMBELEA VYAMA VYA SIASA DMV AHUDHURIA MKUTANO WA HALMASHAURI YA CCM DMV

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi leo Jumamosi Desemba 5, 2015 alihudhuria mkutano wa Halmashauri ya CCM tawi la DMV ikiwa ni moja ya ziara zake anazotarajiwa kuzifanya kutembelea matawi ya vyama vya siasa nchiMarekani yenye lengo la kudumisha mshikamano na ushirikiano wa Watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao.



Akiongea kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV Mhe. Wilson Masilingi amesema lengo kuu ni kuwa karibu na vyama vya siasa kwa lengo la kuleta umoja na mshikamano ndani ya Jumuiya za Watanzania nchini Marekani na pia kuvitambua kama sehemu na sura ya Diaspora na kutoa wito kwa Watanzania waishio Marekani kuelekeza nguvu katika kuwekeza nyumbani bila kujali ufuasi wa chama unachoamini au kushabikia, wote ni Watanzania.



Mhe. Balozi Wilson Masilingi aliiomba Halmashauri hiyo ya CCM DMV kusaidia katika maendeleo ya Tanzania kwa kupanua wigo wao pamoja na kwamba lengo lao ni siasa na siasa ni sehemu ya maisha ya jamii na maendeleo ya jamii yanategemea siasa, kwa hiyo basi mnaposikia kuna muwekezaji yupo tayari kuwekeza Tanzania msisite Ubalozi upo wazi na utafanya kila liwezekanalo kuhakikisha muwekezaji huyo hapati vikwazo vyovyote.



Mwisho Balozi Wilson Masilingi aliwashukuru Watanzania kwa kuwa mabalozi wazuri nchini Marekani na kuwaasa kuishi kwa kufuata misingi na sheria za nchi ya Marekani.



 Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea jambo na mwenyekiti wa tawi CCM DMV Bwn. George Sebo kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 mkutano uliofanyika Hampton Inn, College Park, Maryland. Picha na Kwanza Production/Vijimambo Blog
Mkutano ulianza kwa sala na kuwakumbuka wote waliotangulia mbele ya haki.


Mwenyekiti tawi la CCM DMV Bwn. George Sebo akifungua kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.


Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea machache kwenye kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.


Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea machache kwenye kikao cha Halmashauri ya CCM DMV


Picha ya pamoja.
Bwn. John Mbatta katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Given  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Catherine  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Tino Malinda  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Aunty Grace Sebo  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Grace Mlingi  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Mzee Joel  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Dr. Secelela Malecela  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Katibu wa CCM DMV Bi.Jesca Mushala  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Mwenyekiti wa CCM DMV Bwn. George Sebo  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.