Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 25 December 2014

Heri ya Sikukuu ya Christmas Wapendwa/Waungwana..!!!

Wapendwa/Waungwana;Nawatakia Heri,Baraka,Furaha,Amani na Upendo katika siku kuu hii ya Christmas.
Shukrani sana kwa Familia yangu,Ndugu,Jamaa,Marafiki na Wote tunaofanya/shirikiana kwa namna moja au nyingine.
kwa ujumbe/zawadi na kwa yote...

Shukrani za pekee kwa da'Rose Miriam Kinunda,[http://tasteoftanzania.com/blog/]
MiriamKinunda.commimi na familia yangu tunasema asante sana na Mungu azidi kukubariki pamoja na familia yako kila iitwapo Leo.(you surprised our famliy)
Muwe na Wakati mwema leo na siku zote.


Mathayo 2:1-23
1 Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,

2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.

3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.

4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?

5 Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

6 Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli.

7 Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota.

8 Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.

9 Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto.

10 Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.

11 Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

12 Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.




"Swahili Na Waswahili"Pamoja daima.

No comments: