Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 30 November 2014

Nawatakia Jumapili Njema;Burudani-Angela Chibalonza- Uliniumba nikuabudu na Nyingine....

Wapendwa;Natumaini jumapili ilikuwa/ inaendelea Vyema,
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

Neno La Leo;Zaburi:95;1-11
Utenzi wa kumsifu Mungu
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!
2Twende mbele zake na shukrani;
tumshangilie kwa nyimbo za sifa.
3Maana Mwenyezi-Mungu, ni Mungu mkuu;
yeye ni Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4Vilindi vyote vya dunia vimo mikononi mwake,
vilele vya milima ni vyake.
5Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya;
kwa mikono yake aliiumba nchi kavu.
6Njoni tusujudu na kumwabudu;
tumpigie magoti Mwenyezi-Mungu, Muumba wetu!
7 Maana yeye ni Mungu wetu,
nasi ni watu wa kundi lake,
ni kondoo wake anaowachunga.
Laiti leo mngesikiliza sauti yake:
8“Msiwe wakaidi kama kule Meriba,
kama walivyokuwa kule Masa jangwani,
9wazee wenu waliponijaribu na kunipima,
ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.
10Kwa miaka arubaini nilichukizwa nao,
nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka!
Hawajali kabisa njia zangu!’
11 Basi, nilikasirika, nikaapa:
‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko!’”
Bible Society of Tanzania



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Friday 28 November 2014

Jikoni Leo; Na Mswahili-Chef Issa[Issa Kapande]..

Waungwana;"Jikoni Leo"Tuangalie/Tujifunze na Mpishi wa Leo ni Mswahili, kaka yetu huyu Isaa Kapande...
Mapishi ya Viazi...Mmmhh kila mtu anaupishi wake si vibaya tukijufunza Mapishi mbalimbali.
Hata nawe kama ni mpishi/unapenda mapishi usisite kutushirikisha nasi tukajifunza kupitia mapishi yako.Tutumie kupitia Email;rasca@hotmail.co.uk
Pia usisite kuuliza pale ulipokwama/shindwa...kama wewe unajua hiki na kuna wengine wanajua kile,   Tunaweza kujifunza kupitia wengine.

Mimi natatizwa/siwezi kupika hafu keki[Half cake]..kama maandazi lakini yale yanakuwa Magumu na yamekatika katika..
Tanzania/Dar... mara nyingi yanashushiwa/kinywaji cha Tangawizi...
Msaada waungwana mwenye kuyajulia......










Shukran;Zaidi-activechef/http://activechef.blogspot.co.uk/

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 23 November 2014

Muendelee Na Jumapili hii Vyema;Burudani-Freedom (Live from Faith Christian Center) - Kenneth Reese

Wapendwa nawatakia jumapili njema,yenye Baraka,Furaha,Upendo,Amani,Shukrani,Upole kiasi......
34Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi. 35Mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu.”

Neno La LeoYohana:13:1-36.
Amri mpya
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake. 32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara. 33“Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: ‘Niendako nyinyi hamwezi kwenda!’ 34Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi. 35Mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu.”
Bible Society of Tanzania

I wanna clap a little louder than before,I wanna sing a little louder than before,
I wanna Jump higher than before,I wanna shout louder than before.........Hallelujah..!!!!




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Wednesday 19 November 2014

MISHUMAA YA KALE...Kipindi kipya kutoka VIJIMAMBO na KWANZA PRODUCTION


Photo Credits: Ye Olde Vivyl Shoppe
Baada ya pilika za wiki nzima, na mchamchaka wa maisha, sasa unakuja wakati wa kuburudika na muziki halisi wa zamani.

Katika kipindi hiki, utaweza "kuruka majoka" na "kula mangoma" kwa kusikiliza nyimbo ziliotamba miaka ya zamani, kupata historia ya wasanii na vikundi mbalimbali na pia kusikiliza mazungumzo na maDj na wasanii mbalimbali wa zamani.

Ungana na MixMaster Dj Luke Joe kwenye "one and two" na Mubelwa Bandio nyuma ya kipaza sauti kwenye kipindi kipya cha MISHUMAA YA KALE kitakachokujia kila Ijumaa kuanzia saa 11 kamili jioni mpaka saa 1 kamili usiku kwa majira ya Marekani ya Mashariki (5:00pm - 7:00pm EST)

Ungana nasi kupitia www.kwanzaproduction.com

MixMaster DJ Luke Joe. Photo Credits: IskaJojo Studios
Mubelwa Bandio



Wednesday 12 November 2014

Jikoni Leo,Wanaopenda kujifunza ya Waswahili-Jiko yetu...!!!!


Waungwana;"Jikoni Leo" Na Wanaojifunza ya Waswahili...
Mengi sina tuendelee kujifunza...[Hongera zao]



Thanks/Shukrani;Brennan Waters

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 11 November 2014

Discussion on USAID African Diaspora Marketplace III

Discussion with Jeffrey L. Jackson, Senior Private Sector Advisor, USAID.
Barbara Span, Vice President, Global Public Affairs, Western Union,
Eric-Vincent Guichard, CEO, Homestrings and Zelalem Dagne, ​
CEO, Global Tracking before the launch of the African Diaspora Marketplace III (ADM III), on October 27th 2014 at The Embassy of Tanzania in Washington, DC


Sunday 9 November 2014

Natumaini Jumapili Inaendelea Vyema;Burudani-Fanuel Sedekia - Upendo na Nyingine...


Wapendwa nawatakia Jumapilinjema...Yenye Upendo,Rehema,Baraka,Shangwe,Umoja,Sifa na Utukufu tumrudishie Mungu.....Baba,Tata,Papa...... 18Palipo na upendo hapana woga; naam, upendo kamili hufukuza woga wote. Basi, mtu mwenye woga hajakamilika bado katika upendo, kwani woga huhusikana na adhabu.


Neno La Leo;1Yohana:4:1-21
Mungu ni upendo
7Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu. 8Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo. 9Na Mungu alionesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uhai kwa njia yake. 10Hivi ndivyo upendo ulivyo: Si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu. 11Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana. 12Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana, Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu. 13Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake. 14Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu. 15Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu. 16Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi.Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye. 17Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri siku ile ya hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo. 18Palipo na upendo hapana woga; naam, upendo kamili hufukuza woga wote. Basi, mtu mwenye woga hajakamilika bado katika upendo, kwani woga huhusikana na adhabu. 19Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza. 20Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni. 21Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
[Bible Society of Tanzania]





"Swahili Na Waswahili"Baraka kwa wote.

Monday 3 November 2014

Jikoni Leo na Mitindo-Ubah Hassan

Waungwana; Jikoni Leo,Wa Afrika/Wasomali na Mitindo...
Leo tuungane da'Ubah Hassan..ni Msomali anayeishi Ng'ambo.

Si mwanamitindo tuu na jikoni pia anahusika....
basi nisikuchoshe..


Tuungane na da'Ubah...
 


Shukrani/Thanks;Andrew Day

Na kwa mambo ya mitindo zaidi nifuate;http://mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/
"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Saturday 1 November 2014

Natumaini Juma Pili ilikuwa/Inaendelea Vyema;Burudani-Kinondoni Revival Choir- Twalilia Tanzania,Imekwisha na Nyingine.....!!!!!

Wapendwa;Nawatakia Jumapili njema,Yenye Baraka,Tumaini,Imani,Upendo,Furaha,Shukrani na Utukufu tumrudishie Mungu......

18  Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
19  Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.
Neno La Leo;Zaburi 145
1  Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.
2  Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.
3  Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hautambulikani.
4  Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, Kitayatangaza matendo yako makuu.
5  Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, Na matendo yako yote ya ajabu.
6  Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.
7  Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako.
8  Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
9  Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.
10  Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
11  Wataunena utukufu wa ufalme wako, Na kuuhadithia uweza wako.
12  Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
13  Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote, Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
14  Bwana huwategemeza wote waangukao, Huwainua wote walioinama chini.
15  Macho ya watu wote yakuelekea Wewe, Nawe huwapa chakula chao wakati wake.
16  Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.
17  Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
18  Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
19  Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.
20  Bwana huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki atawaangamiza.
21  Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana; Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu milele na milele.










Shukrani;

Kinondoni Revival Choir.

    Africha Entertainment


"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.