Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 31 December 2014

Chaguo La Mswahili Leo-Pharrell Williams- Happy From Tanzania,DRC-Congo-Kinshasa,Goma,Burundi,Rwanda

Waungwana;Natumaini wote Mnafuraha,Amani,Upendo.....
kama wewe huna hivyo pole sana na Mungu   yu pamoja nawe!!!!!

Because I'm Happy...........!!!!!!!!
Be Happy.......!!!!!!!















"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 30 December 2014

Mwaka unakatika....Tumesonga mbele ama nyuma???


 Amani, Heshima na Upendo kwa wana-blog wote.

Kwanza namshukuru MUNGU kwa baraka ya uhai ambayo mimi nawe tunayo mpaka sasa.

Pili nikupe pole kwa harakati za maisha ambazo sote twazipitia kufanikisha yale mema tupendayo. Ni harakati kubwa sana hasa katika kusonga na maisha yetu ya kila siku na pia kuendeleza gurudumu hili la blogs

Nimekuwa nikituma makala, vipindi na kazi zangu kwenu nanyi mmekuwa wakarimu sana kuzipokea. Ushirikiano ambao umenifanya nizidi kujivunia kuwa mmoja wa bloga

Lakini pia, najivunia sana
kuwasiliana na kila mmoja wetu hivi sasa ili kuanzisha mjadala wa changamoto zilizo mbele
yetu kama JAMII YA WANA-BLOG wenye lengo la kuigusa jamii.

Ningependa tuanze kwa kujiuliza, Je! Tunasonga mbele ama nyuma katika harakati zetu.

Nashukuru
kwa blogs na tovuti mpya ambazo zinachipuka na kuendeleza nia njema ya
kuigusa jamii. Kaka Luta Kamala aliwahi kuandika akijuliza KWANINI TUNA-BLOG? (Bofya hapa) na hata Kaka Chambi Chachage aliuliza kama uwepo wa blogu zetu unakuza ama kufifisha tasnia nzima ya uandishi (Ipitie hapa)

Jibu halisi tunalo mioyoni mwetu kulingana na dhamira tulizonazo.

Lakini
kwa ujumla, haijalishi ni sababu gani ilikufanya u-blog, mwisho wa
safari sote tunajikuta na zao moja ama "mlaji" mmoja ambaye ni JAMII.

Bloga awekaye picha
anataka kuionesha jamii alichokiona.

Bloga ahabarishaye anataka kuihabarisha
jamii. Yule aandikaye Utambuzi anataka jamii ijitambue. Anayeweka
kumbukumbu ni sababu anataka jamii ije isome baadaye. Atangazaye
biashara anataka jamii ijue palipo na huduma ama biashara husika. Afunzaye mapishi, mitandao,
mavazi, mitindo nk, woote wanalenga katika kuielimisha jamii.

Kwa maana nyingine sote twaiandikia JAMII.

Na hili ni lengo jema.

Lakini swali linarejea kuwa......

Mwaka huu ambao unaomalizika wiki hii unaonekana
kuwa hatua gani kwetu?

Logo hapo juu inaonyesha hatua iliyopihgwa katika siku za mwisho za mwaka. Kuanzishwa kwa mtandao wa bloga ambao (ukitumiwa vema) utakuwa chachu ya mabadiliko ya nchi hasa kwa mwaka huu wa uchaguzi.

Ninalowaza ni hili.....

Vipi tunaweza kuweka nguvu na jitihada zetu pamoja kuweza kuitumikia vema na kwa ufasaha jamii yetu???

Mafanikio
ya bloga mmoja mmoja yanaweza kudhihirisha kuwa TUNAWEZA, lakini tunalostahili kufanya sasa, ni kushirikiana na kuwa makini katika kila jema
tutendalo.



Tunapoumaliza mwaka 2014, tuangalie nyuma na kujiuliza, mwaka unakatika....Tumesonga mbele ama nyuma??





Na jibu la swali hili, liwe CHANGAMOTO YETU sote



Baraka kwenu nyote



Heri ya Mwaka Mpya 2015

Monday 29 December 2014

NesiWangu Show...........Malaria Kit

NesiWangu Show ni kipindi kinachokusudia kuongeza mwako katika uwanja wa Afya, upatikanaji wa huduma zake na elimu-afya kwa jamii.

Katika kipindi hiki, tunazungumza na Mkurugenzi wa Jenga Tanzania Foundation, Nassor Basalama anayezungumzia kuhusu kipimo cha Malaria ambacho Jenga Tanzania Foundation inapanga kukisambaza bure kwa watu wa kipato cha chini nchini Tanzania.


Karibu uungane nasi.....

Thursday 25 December 2014

Heri ya Sikukuu ya Christmas Wapendwa/Waungwana..!!!

Wapendwa/Waungwana;Nawatakia Heri,Baraka,Furaha,Amani na Upendo katika siku kuu hii ya Christmas.
Shukrani sana kwa Familia yangu,Ndugu,Jamaa,Marafiki na Wote tunaofanya/shirikiana kwa namna moja au nyingine.
kwa ujumbe/zawadi na kwa yote...

Shukrani za pekee kwa da'Rose Miriam Kinunda,[http://tasteoftanzania.com/blog/]
MiriamKinunda.commimi na familia yangu tunasema asante sana na Mungu azidi kukubariki pamoja na familia yako kila iitwapo Leo.(you surprised our famliy)
Muwe na Wakati mwema leo na siku zote.


Mathayo 2:1-23
1 Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema,

2 Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.

3 Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye.

4 Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?

5 Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

6 Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli.

7 Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota.

8 Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.

9 Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto.

10 Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno.

11 Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

12 Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.




"Swahili Na Waswahili"Pamoja daima.

Monday 15 December 2014

Jikoni Leo;[Mkate wa Mchele]Makate or Rice Cake na Raihana Mulla...

Waungwana "Jikoni Leo" na bi'Rahiana Mulla..Mapishi ni Mkate wa Mchele[Mkate wa kumimina].
Waswahili wanasema Mchele mmoja Mapishi mbalimbali..

Haya tuendelee kujifunza......

Thanks/Shukrani;Zaidi-Raihana Mulla
"Swahili Na Waswahili"Pamoja daima.

Friday 12 December 2014

Swahili/Kiswahili Na Waswahili;ULIMI, MATAMSHI, NA KUKAA UGENINI

Watangazaji wa DW wakijadili na kujadiliana masuala kadhaa ya kilugha likiwemo lugha asilia ya mtu huathirika vipi akikaa ugenini kwa muda mrefu, yaani kwenye mazingira ambako lugha yake ya kuzawa nayo haitumiki? Jee, matamshi yake yatapotoshwa mpaka aonekane msemaji mgeni kila azungumzapo kwa lugha yake asilia? Na vipi msamiati wake, utapigwa na wakati au la?







Shukrani;John Mtembezi Inniss

Monday 8 December 2014

Tunaweza Badilika - Mzee Yusuf & Khadija Kopa


Collabo ya kihistoria kati ya Mfalme Mzee Yusuf na Malkia Khadija Kopa katika wimbo na video ya pamoja yenye malengo ya kuhamasisha jamii kupinga ukatili dhidi ya wanawake.

Video hii iliyorekodiwa mkoani Morogoro inamuonyesha Mzee Yusuf na Khadija Kopa kama mume na mke ambao wamebahatika kupata watoto wawili 'Kulwa' na 'Doto' ambao ni mapacha. Mzee Yusuf ni dereva wa daladala wakati Khadija ni mama wa nyumbani lakini pia mjasiriamali.

Pamoja na kwamba watoto wao ni mapacha ambao wanafanana na kulingana kwa karibu kila kitu ikiwemo umri lakini tofauti ya jinsi yao inaonekana kumpa haki zaidi mtoto wa kiume ambaye anaonekana kuelekea shuleni wakati pacha mwenzie anaonekana kuhangaika na shughuli za nyumbani ikiwemo kutafuta maji, kufanya usafi n.k.

Kwa upande mwingine, Mzee anaonekana kutokuijali familia yake haachi pesa ya matumizi nyumbani na hata anapoulizwa anakuwa mkali sana wakati huo huo anaonekana kuchezea mabinti wengine akiwa kazini.

Stori inabadilika kabisa pale mzee anapokutana na Mwanamabadiliko ambaye anafanikiwa kumshawishi kubadili tabia hizo kwa ajili ya manufaa ya familia yake. Kuanzia hapo Mzee anaonekana akinunua nguo za shule za mwanae wa kike na kubandika ujumbe wa mabadiliko katika gari na nyumba yake.

Baada ya hapo maisha yanaonekana kuwa ya raha mustarehe.

"Tukae na tu-starehe tule raha na maisha." Kinasema kibwagizo katika wimbo huo.



Shukrani,zaidi ingia;Tunaweza

Sunday 7 December 2014

Muendelee na Jumapili Hii Vyema;Burudani- Mchanganyiko Tusifu na Kuabudu...!!!

Wapendwa nawatakia/Muendelee na Jumapili hii Njema...
Leo sina mengi..Tusifu na Kuabu..MUNGU wetu ni mwema sana sana...
Tuwaweke kwenye maombi/sala watu wote wenye Shida/Tabu,Wanaopitia Majaribu,kukata tamaa,Wenye kuhitaji.....2Ndugu zangu, muwe na furaha mnapopatwa na majaribu mbalimbali, 


Neno la Leo;Yakobo1:1-27
Salamu;1
Imani na hekima;2-8

Umaskini na utajiri;9-11
Majaribio;12-18
Kusikia na kutenda;19-27

Bible Society of Tanzania









"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Monday 1 December 2014

Mswahili Wetu Leo;da'Louise UWACU-U&I TALK [ NUBI-KMT ] Episode 3 in Ki SWAHILI

Mswahili wetu Leo ni "da'Louise"..yeye ni mzaliwa wa Rwanda[Mnyarwanda].
da'Louise yeye anapenda kujifunza zaidi kiswahili...

Basi nisikuchoshe ungana na dada huyu wa Kinyarwanda...Hongera da'Louise.



Thanks/Shukrani;uwacuvideo

"Swahili Na Waswahili"Pamoja sana.

Sunday 30 November 2014

Nawatakia Jumapili Njema;Burudani-Angela Chibalonza- Uliniumba nikuabudu na Nyingine....

Wapendwa;Natumaini jumapili ilikuwa/ inaendelea Vyema,
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

Neno La Leo;Zaburi:95;1-11
Utenzi wa kumsifu Mungu
1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,
tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!
2Twende mbele zake na shukrani;
tumshangilie kwa nyimbo za sifa.
3Maana Mwenyezi-Mungu, ni Mungu mkuu;
yeye ni Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4Vilindi vyote vya dunia vimo mikononi mwake,
vilele vya milima ni vyake.
5Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya;
kwa mikono yake aliiumba nchi kavu.
6Njoni tusujudu na kumwabudu;
tumpigie magoti Mwenyezi-Mungu, Muumba wetu!
7 Maana yeye ni Mungu wetu,
nasi ni watu wa kundi lake,
ni kondoo wake anaowachunga.
Laiti leo mngesikiliza sauti yake:
8“Msiwe wakaidi kama kule Meriba,
kama walivyokuwa kule Masa jangwani,
9wazee wenu waliponijaribu na kunipima,
ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.
10Kwa miaka arubaini nilichukizwa nao,
nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka!
Hawajali kabisa njia zangu!’
11 Basi, nilikasirika, nikaapa:
‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko!’”
Bible Society of Tanzania



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Friday 28 November 2014

Jikoni Leo; Na Mswahili-Chef Issa[Issa Kapande]..

Waungwana;"Jikoni Leo"Tuangalie/Tujifunze na Mpishi wa Leo ni Mswahili, kaka yetu huyu Isaa Kapande...
Mapishi ya Viazi...Mmmhh kila mtu anaupishi wake si vibaya tukijufunza Mapishi mbalimbali.
Hata nawe kama ni mpishi/unapenda mapishi usisite kutushirikisha nasi tukajifunza kupitia mapishi yako.Tutumie kupitia Email;rasca@hotmail.co.uk
Pia usisite kuuliza pale ulipokwama/shindwa...kama wewe unajua hiki na kuna wengine wanajua kile,   Tunaweza kujifunza kupitia wengine.

Mimi natatizwa/siwezi kupika hafu keki[Half cake]..kama maandazi lakini yale yanakuwa Magumu na yamekatika katika..
Tanzania/Dar... mara nyingi yanashushiwa/kinywaji cha Tangawizi...
Msaada waungwana mwenye kuyajulia......










Shukran;Zaidi-activechef/http://activechef.blogspot.co.uk/

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 23 November 2014

Muendelee Na Jumapili hii Vyema;Burudani-Freedom (Live from Faith Christian Center) - Kenneth Reese

Wapendwa nawatakia jumapili njema,yenye Baraka,Furaha,Upendo,Amani,Shukrani,Upole kiasi......
34Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi. 35Mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu.”

Neno La LeoYohana:13:1-36.
Amri mpya
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake. 32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara. 33“Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: ‘Niendako nyinyi hamwezi kwenda!’ 34Nawapeni amri mpya: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi. 35Mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu.”
Bible Society of Tanzania

I wanna clap a little louder than before,I wanna sing a little louder than before,
I wanna Jump higher than before,I wanna shout louder than before.........Hallelujah..!!!!




"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Wednesday 19 November 2014

MISHUMAA YA KALE...Kipindi kipya kutoka VIJIMAMBO na KWANZA PRODUCTION


Photo Credits: Ye Olde Vivyl Shoppe
Baada ya pilika za wiki nzima, na mchamchaka wa maisha, sasa unakuja wakati wa kuburudika na muziki halisi wa zamani.

Katika kipindi hiki, utaweza "kuruka majoka" na "kula mangoma" kwa kusikiliza nyimbo ziliotamba miaka ya zamani, kupata historia ya wasanii na vikundi mbalimbali na pia kusikiliza mazungumzo na maDj na wasanii mbalimbali wa zamani.

Ungana na MixMaster Dj Luke Joe kwenye "one and two" na Mubelwa Bandio nyuma ya kipaza sauti kwenye kipindi kipya cha MISHUMAA YA KALE kitakachokujia kila Ijumaa kuanzia saa 11 kamili jioni mpaka saa 1 kamili usiku kwa majira ya Marekani ya Mashariki (5:00pm - 7:00pm EST)

Ungana nasi kupitia www.kwanzaproduction.com

MixMaster DJ Luke Joe. Photo Credits: IskaJojo Studios
Mubelwa Bandio



Wednesday 12 November 2014

Jikoni Leo,Wanaopenda kujifunza ya Waswahili-Jiko yetu...!!!!


Waungwana;"Jikoni Leo" Na Wanaojifunza ya Waswahili...
Mengi sina tuendelee kujifunza...[Hongera zao]



Thanks/Shukrani;Brennan Waters

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 11 November 2014

Discussion on USAID African Diaspora Marketplace III

Discussion with Jeffrey L. Jackson, Senior Private Sector Advisor, USAID.
Barbara Span, Vice President, Global Public Affairs, Western Union,
Eric-Vincent Guichard, CEO, Homestrings and Zelalem Dagne, ​
CEO, Global Tracking before the launch of the African Diaspora Marketplace III (ADM III), on October 27th 2014 at The Embassy of Tanzania in Washington, DC


Sunday 9 November 2014

Natumaini Jumapili Inaendelea Vyema;Burudani-Fanuel Sedekia - Upendo na Nyingine...


Wapendwa nawatakia Jumapilinjema...Yenye Upendo,Rehema,Baraka,Shangwe,Umoja,Sifa na Utukufu tumrudishie Mungu.....Baba,Tata,Papa...... 18Palipo na upendo hapana woga; naam, upendo kamili hufukuza woga wote. Basi, mtu mwenye woga hajakamilika bado katika upendo, kwani woga huhusikana na adhabu.


Neno La Leo;1Yohana:4:1-21
Mungu ni upendo
7Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu. 8Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo. 9Na Mungu alionesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uhai kwa njia yake. 10Hivi ndivyo upendo ulivyo: Si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu. 11Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana. 12Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana, Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu. 13Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake. 14Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu. 15Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu. 16Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi.Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye. 17Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri siku ile ya hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo. 18Palipo na upendo hapana woga; naam, upendo kamili hufukuza woga wote. Basi, mtu mwenye woga hajakamilika bado katika upendo, kwani woga huhusikana na adhabu. 19Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza. 20Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni. 21Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
[Bible Society of Tanzania]





"Swahili Na Waswahili"Baraka kwa wote.

Monday 3 November 2014

Jikoni Leo na Mitindo-Ubah Hassan

Waungwana; Jikoni Leo,Wa Afrika/Wasomali na Mitindo...
Leo tuungane da'Ubah Hassan..ni Msomali anayeishi Ng'ambo.

Si mwanamitindo tuu na jikoni pia anahusika....
basi nisikuchoshe..


Tuungane na da'Ubah...
 


Shukrani/Thanks;Andrew Day

Na kwa mambo ya mitindo zaidi nifuate;http://mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/
"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Saturday 1 November 2014

Natumaini Juma Pili ilikuwa/Inaendelea Vyema;Burudani-Kinondoni Revival Choir- Twalilia Tanzania,Imekwisha na Nyingine.....!!!!!

Wapendwa;Nawatakia Jumapili njema,Yenye Baraka,Tumaini,Imani,Upendo,Furaha,Shukrani na Utukufu tumrudishie Mungu......

18  Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
19  Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.
Neno La Leo;Zaburi 145
1  Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.
2  Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.
3  Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, Wala ukuu wake hautambulikani.
4  Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, Kitayatangaza matendo yako makuu.
5  Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, Na matendo yako yote ya ajabu.
6  Watu watayataja matendo yako ya kutisha, Nami nitausimulia ukuu wako.
7  Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako.
8  Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
9  Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.
10  Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
11  Wataunena utukufu wa ufalme wako, Na kuuhadithia uweza wako.
12  Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
13  Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote, Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
14  Bwana huwategemeza wote waangukao, Huwainua wote walioinama chini.
15  Macho ya watu wote yakuelekea Wewe, Nawe huwapa chakula chao wakati wake.
16  Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.
17  Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
18  Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.
19  Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.
20  Bwana huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki atawaangamiza.
21  Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana; Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu milele na milele.










Shukrani;

Kinondoni Revival Choir.

    Africha Entertainment


"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Friday 31 October 2014

Wazo La Leo; Na Mswahili-Emu-three Wa Diary Yangu.....


WAZO LA LEO: Sio kila jambo la heri laweza kirahisi tu, kuna mambo mengine huja na mitihani yake, lakini mwisho wake huwa ni neema, na furaha kama utakuwa mvumilivu na kusimamia kwenye haki.Halikadhalika mambo ya ubaya, yana mvuto wake, usipokuwa makini unaweza kuzama kwenye giza nene, na mwisho wa ubaya ni kudhalilika, na kuumbuka, na kawaida majuto huja baadaye, kama utafanikiwa kujinasua. Tujitahidi sana kuwa makini katika matendo yetu, tusivutike tu kwa tamaa, tuangalie uzuri na ubaya wake kwanza.

kwa Hadithi/Visa/Mikasa ya Maisha,Usikose pitia hapa;http://miram3.blogspot.co.uk/

Dunia Yangu ndiyo hadithi/kisa kinachoendelea sasa....[Sehemu Ya 56]

Twende Pamoja..!!!!

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Wednesday 29 October 2014

Jikoni Leo;Sheikha Agili-How to Make Swahili Biriyani..!!!!!!

Waungwana;"Jikoni Leo" na Sheikha Agili,Jinsi ya Kupika Swahili Biriyani..
Mimi nimpenzi wa mapishi ya bi Sheikha..


Nawe kama mpenzi wa Mapishi/Mpishi unaweza kutushirikisha mapishi yako...nasi tukajifunza kupitia wewe....Mlango upo wazi karibu sana.Haya tujifunze kupika biriyani....
Twende pamoja na bi'Sheikha...
.

Shukrani;Sheikha Agil

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Monday 27 October 2014

Mswahili Wetu Leo;Da'Zahabu Luciannne -Tabia Ya Bibi mbele ya Bwana[Haya Wamama wa Ng'ambo kazi kwenu]..

Waungwana; Mswahili wetu Leo...da'Zahabu Lucianne...
Haya Wamama wa Ng'ambo kwanini Hamuwaheshi ma Bwana?
 Mnasugulishaga ma Bwana masaani,Kutwa mpo kwa Facebook na Musimu......
Muache kuita ma Bwana majinaa eeh Bwana yako eehh.........


Twende pamoja na da'Zahabu...





Shukrani;Augmanify

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.