Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 31 July 2013

Wazo La Leo;Kutoka Kwa da'Rose-MWANADAMU MWANADAMU MWANADAMU!!!!!!



Mwanadamu yeyote anayeweza kuongea na wewe gizani, anayekupa ujumbe fulani kwakutumia jina la kivuli,mwanadamu aliyekosa ujasiri wakujidhihirisha kwenye mwanga, nazungumza na yule mwanadamu anayekufahamu,mwanadam ambaye kama ana neno na wewe anauwezo mkubwa wakukutafuta nakukwambia, mwanadamu ambaye anakuona kwenye mwanga yawezekana kila iitwapo leo lakini hakwambii, hana uhuru na mwanga, mwanadamu ambaye hawezi kutumia silaha zake  wakati akuonapo ila ukimpa nafasi ya giza kidogo anaitumia vizuri,mwanadamu asiyekuwa na ujasiri wakukutishia ila atakutishia gizani na ngurumo nyingi zenye vishindo.......mwanadam ambaye anakuthibitishia gizani kuwa yuko kazini na anaamini utaanguka na amekaa mkao wakusubiri uanguke duuuuu!!!!!(sina jina la kumpa ila mara jingine sidhani km anastahili kuitwa mwanadam) kwa maana nyingine niASKARI WA GIZANI....... 

walio wagizani hawaoni yaliyomwangani,na waliomwangani hawaoni yalio gizani....... wa gizani hata ukimwashia taa kwa jinsi yakibinadamu ataona, lakini kwa sababu yeye ni wagizani atatumia nguvu kujibadilisha ndani yake aendelee kuona giza, japo kuwa neema ya mwanga imemfikia (kwa mana nyingine hana neema yakutambua yaliyo  kwenye nuru)....na alie kwenye mwanga hata giza limpitie bado ataona mwanga tuu japokuwa kuna misukosuko,milima,mabondo, na mikasa ya kila namna bado ataona hicho ni kipindi tu.........JARIBU NI KAWAIDA YA MWANADAMU..............)


ninachoweza kusema ni hivi...... acha vita vya rohoni viwe vya rohoni, kuna wakati huyu mwanadamu (PEPO) anaweza kukupush ubinadamu ukuingie kwa namna fulani  USIJARIBU!!!!! Huo ni mlango mkubwa wa yeye kuingia kwa sababu utafanya uwanadamu usaidie kazi za rohoni  NI MWIKO MKUBWA KUSAIDIA KAZI ZA ROHONI............. ACHA KAZI ZA ROHONI ZIFANYIKE KIROHONI(VITA TULIVYONAVYO SI VYA DAMU NA NYAMA BALI..........................),( VAENI SILAHA ZOTE ZA VITA ILI.............) 

Monday 29 July 2013

Waswahili Na Maisha Yao;Futari Ya Pamoja Marekani[DMV]!!!




Waungwana;"Waswahili na Maisha Yao",Waswahili wa Marekani DMV, wana utaratibu huu wa kukutana pamoja kila J'mosi na J'pili na Kuwa na Futari/Kufuturu pamoja.. Hii inaonyesha kuwa Waswahili hawa hawasahau baadhi ya mambo Mema/Mazuri ya kwao,Ukarimu,Umoja na Mengine meengi.

Hongereni Sana na Muwe na Funga Njema.

Shukrani;Vijimambo Blog.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Sunday 28 July 2013

Natumai J'Pili inaendelea Vyema;Mbarikiwe Wote-Burudani-Shout To The Lord, na nyingine!!


                     Ni kwa Neema ya MUNGU tuu....

Wapendwa Nawatakia J'pili yenye,Rehema,Neema,Fadhili,Shukrani,Hekima,Upendo,Furaha,Baraka,Umoja,Uvumilivu,Tumaini na Upole Kiasi.
Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika,ni heri mwanaume asimguse mwanamke.
Neno La Leo;1.Wakorintho:7:117; [10]Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza;wala hapo si mimi,ila BWANA; mke asiachane na mumewe;[11]Lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena  mume asimwache mkewe..............

"Swahili NA Waswahili" Tunawapenda Wote.








Saturday 27 July 2013

Siku kama yaLeo Tulifunga Ndoa-[Happy Anniversary]!!!!Tuliamua kufanya kazi za jamii.

Bibi Na Bwana tukielekea kuungana na Wapendwa katika kazi jamii/kujitolea



 

Mama Mchungaji na mimi Tukifurahia mambo yanavyokwenda sawa..

Tukisaidiana kuweka mambo vyema






Dada huyu yeye ni mbunifu wa vitu vya Asili,Mikufu,Bangili,Hareni na vinginevyo..
MUNGU amemjalia kazi za mikono yake..basi hutoa kwake/kurudishia yeye pia.




Kulikuwa na Michezo,Zawadi mbalimbali

Hii ndiyo Shughuli kubwa tuliyoiendea..Na pesa zote zilizopatikana..zilipelekwa huko.Wapo waliotoa Pesa,Muda,Vipaji na Mengine meengi ili tuu Jambo tulilokusudia lifanyike..na Lilifanyika kwa uwezo wake MUNGU. Kuna Mengi ya kujifunza/Tumejifunza,Kufundisha watoto wetu.


Mchungaji na Mama Mchungaji Waliwashukuru Watu wote kwa kufanikisha jambo hili


Hahahahahha maneno ya Mchungaji Rachel nimepoziii...


         Wapendwa/Waungwana Bibi na Bwana Isaac;Siku kama ya Leo tuliungana pamoja Kuwa Mwili Mmoja.
Tunamshukuru sana MUNGU kwa kutufikisha hapa.Pasipo yeye sisi si kitu.Azidi kuongoza katika safari yetu.

Shukrani Familia zetu,Ndugu,Jamaa na Marafiki katika Yote.
Shukrani Hebron Church

Kwapicha za watoto na Michezo,Tukutane;http://Watotonajamii.blogspot.com

"Swahili NA Waswahili" Tunawapenda wote.
  

Hadithi hii maana yake nini?



Mmmhh katika pitapita zangu kutafuta hadithi za Watoto wetu j'mosi, Nikakutana nahii.. kila hadithi ina mafunzo/maana ili watoto/watu wajifunze..jee nini maana ya Hadithi hii?

 Usikose kusikiliza/kuangalia Hadithi,Katuni na mengine meengi yahusiyo Watoto na Jamii.







Friday 26 July 2013

Wimbo Toka Kwa Neema Decoras Milele Nitalisifu Jina Lako!!!!



 Ndugu,

 Salamu katika Jina la Yesu Kristo,

 Ninaitwa Neema
 Decoras. Ni muimbaji wa Nyimbo za Injili toka Dar es Salaam, Tanzania.
 Nimeambatanisha wimbo wa kwanza kutoka katika albam yangu, uitwao Milele Nitalisifu Jina Lako na kuutuma kwako ili uusikilize.


 Mashairi ya wimbo huu ni haya yafuatayo:

Kibwagizo (Chorus)
 Milele, Milele, Milele eeee,
 Milele, Milele, Milele
 eeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
 Aaah,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,

 Beti 1
 Hakika Upendo wako, ooooh
 Nashindwa
 kuupima mimi,
 Ulinipenda mimi, iiiih,
 Ukatoa uhai wako,
Yote hii Bwana, aaaah
Uniepushe na mateso,
Yote hii Bwana, aaaah
Uniepushe na kuzimu,
Ukaja duniani, iiiih,
Ukapata mateso mengi,
Ulijishusha sana, aaaah,
 Ili utukomboe sisi,
 Mimi sijaona, aaaah
 Upendo kama wako tena
 Mimi sijaona, aaaah
Upendo kama wako tena
 Nasema, Milele, Milele Nitalisifu Jina Lako

 Kibwagizo
 Milele, Milele, Milele eeeee,
 Milele, Milele, Milele eeeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
  Aaah,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,

 Beti 2
 Niwapo mashakani, iiiih
 Rafiki hunikimbia,
 Niwapo ni mgonjwa, aaaah
 Watu husema pole sana,
 Lakini hawawezi, iiiih
 Kutatua shida zangu,
 Lakini hawawezi, iiiih
 Kutatua shida zangu,
 Peke yako nakuona,
 aaaah
 Waja kunifariji moyo,
 Peke yako nakuona, aaaah
 Waja kutibu afya yangu,
 Peke yako nakuona, aaaah
 Wanitendea miujiza,
 Ndio maana nasema, aaaah
 Una upendo mwingi sana,
 Ndio maana nasema, aaaah
 Una upendo mwingi sana,

 Kibwagizo
 Milele, Milele, Milele eeeee,
 Milele, Milele, Milele eeeee,

Swahili Na Waswahili;Inakutakia kila lililojema,Baraka katika Yote.Hongera Sana da'Neema Decoras.

Thursday 25 July 2013

Mtu kwao;Leo Tuangalie Jiji La Dar-es-salaam!!!!!








Waungwana ;ni Kipengele cha "Mtu Kwao" Leo Tupo/Tuangalie/Tutembelee japo kwa Macho Jiji la Dar-es-Salaam[DAR]Bandari ya Salama.

Nini kinakufurahisha katika Jiji hili na Nini kinakukera/chukiza katika Jiji hili?
zaidi ingia;Prinxali

"Swahili NA Waswahili" MTU KWAO.

Sunday 21 July 2013

Da'Sandra-Neema Atimiza Miaka 15..!!!!!!!
















 Haleluya Nampenda BWANA kwa kuwa anasikiliza Sauti yangu na dua zangu.
kwa maana amenitegea sikio lake, Kwa hiyo nitamwita siku zangu zote. Neno La Leo;Zaburi:116:1-2




Wapendwa/Waungwana; Mungu yu mwema Binti Yetu SANDRA-NEEMA. Ametimiza miaka 15.Tunamshukuru sana MUNGU katika yote,Tunamuweka binti huyu mikononi mwako BABA waMBINGUNI. Akawe baraka kwetu na Jamii pia. Asante sana MUNGU kwa zawadi hii maishani kwetu.
 Asante na Mbarikiwe sana Ndugu,Jamaa,Marafiki na watu wote mliokuwa/mnaondelea  kuwa nasi katika Maombi/Sala,Malezi kwa namna moja au Nyingine.
MUNGU akawabariki watoto woote.. pia awajaalie wanaohitaji watoto. Tuna yaweka haya yote mikononi mwa MUNGU.AMEEN!!

Familia ya Isaac inawatakia J'pili yenye Amani,Upendo,Baraka na Furaha.
  
"Swahili Na Waswahili"  Pamoja Daima.