Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 31 August 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Makoma!!!!!!!



Waungwana;Mmmhhh Hawa ni "MAKOMA"Hili ndiyo "Chaguo La Mswahili Leo" Moooto.. Nawakubali.. Maneno Meengi sina Leo Nasikilizia kutoka Kwenu..Twende Sote  sasa -Butu Na Moyi na...Endeleaaa.







"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana

Wednesday 28 August 2013

Wanawake Na Majukumu;Vipaji/Ubunifu!!!!!









Waungwana;Wanawake Na Majukumu;Vipaji/Ubunifu/Ujuzi..

Wapo Wanawake weengi sana wanajua Vitu/Mambo Mbalimbali lakini Hawajulikani.

Unafikiri ni Kwanini?
Wewe mwenzangu unajua/Una kipaji/Ujuzi Gani /nini?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima


Sunday 25 August 2013

Tumalizie J'Pili hii kwa Amani na Upendo;Brudani-Angela Chibolonza!!!

Wapendwa;Tumalizie J'Pili hii Vyema.

Lakini,ndugu, kwa habari ya nyakati na majira,hamna haja niwaandikie..........
Neno La Leo;1:Wathesalaonike:5:1-28..
[4]Bali ninyi,ndugu, hammo gizani,hata siku ile iwapate kama mwivi[5]Kwakuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana;sisi si wa usiku, wala wa giza.[6]Basi tusilale usingizi kama wengine,bali tukeshe na kuwa na kiasi.

[16]Furahini siku zote;[17]Ombeni bila kukoma;[18]Shukuruni kwa kila jambo;maana hayo ni mapenzi ya MUNGU kwenu katika Kristo YESU.

[25]Ndugu,tuombeeni.[26]Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.[27]Nawaapisha kwa BWANA, ndugu wote wasomewe waraka huu.

[28]Neema ya BWANA wetu YESU Kristona iwe pamoja nanyi.










"Swahili Na Waswhili" Mbarikiwe Wote.

Wednesday 21 August 2013

Kisa Cha Leo na Mswahili Emu-Three;Wema Hauozi-Sehemu ya 52!!!!!



Tulitoka nje ya lile pango huku tukiwa tumekata tamaa ya kumpata huyu mtu tena,ikizingatia kuwa yeye analifahamu hilo pango lilivyo, na sisi japokuwa tupo wengi, lakini njia za kupita zilihitajia mtu mmoja mmoja,…

Bado tukiwa na matumaini ya kumpata huyo mtu akiwa hai, tuliharakisha kutoka, ili kuungana na wenzetu waliokuwa wakijibisha risasi na huyo jamaa, na baadaye kukawa kimiya, ikiashiria kuwa huenda huyo mtu alishatoka nje,

Swali likawa je kama huyo mtu kawahi kutoka nje, itakuwaje, kwani hatukukumbuka kumuacha askari zaidi ya mwanasheria, wote tulikimbilia kuingia ndani..na je hiyo amri ya kutokutumia risasi huko nje, itawezaje kuepukika, na mtu kama huyo?

Tuendelee na kisa chetu......

Tukajitahidi na sisi kutoka nje kwa haraka haraka, na tulipofika nje, tuliwaona askari wetu wamesimama huku wameelekeza silaha zao upande wa pili, kama wanawinda kitu, na mkuu ndiye aliyekuwa wa kwanza kutoka na bastola yake mkononi, akawauliza vijana wake

‘Yupo wapi’ akauliza

‘Mkuu kaingia kwenye hicho kichaka, na cha ajabu haonekani tena, lakini tuna uhakika yupo hapo, na tunahisi kuwa hayupo peek yake,…’akasema mmoja wapo, na wote wakaelekea kwenye hicho kichaka na kwa mbele wakaona watu wawili wakiwa kwenye mapigano na kila mmoja akiwa kamshika mwenzake mkono, ili kuzuia silaha yake, isielekezwe kwake.

Msaidieni mwanasheria, lakini msitumie silaha, kumbukeni tulivyoambiwa, ….’akasema mkuu, huku nay eye akielekea kule ambapo mwanasheria alikuwa akipambana na huyo mtu, na ilikuwa vigumu kuingilia kwani zile silaha walizoshika zingeliweza kufyatuka na kuleta madhara kwa yule ambaye angeliwakaribia, kwahiyo ikawa kutafuta jinsi ya kusaidia.

Mwanadada ambaye alikuwa nyuma akiwa na yule binti, alifika eneo hilo na kuona hiyo hali, na hapo akasema;.

`Mbona mumesimama, hamumsaidi mwenzenu…’akasema mwanadada, akikimbilia kule kwenye mapigano kati ya mwanasheria na huyo jamaa na alipofika tu, akasikia mlipuko wa risasi,…..oh, mwanasheria akapanua mdomo, na kudondoka chini, na yule mtu alipoona hivyo, akainuka kutaka kukimbia, lakini hakuweza hata kuinua mguu.

Risasi ililengwa bara bara, kutoka kichani, na yule mtu akatoa macho ya uwoga, na kudondoka chini, na hapo mwanadada na mkuu, wakawa wameduwaa, ina maana kazi yote imekuwa ni bure, ina maana masharti ya msituni yamevunjwa, na haijulikani ni kitu gani kitatokea.

Mkuu akamkimbilia yule mtu, na kuhakikisha hana silaha, na akamshika kuangalia kama yupo hai, na akainua kichwa kumwangalia mwanadada na kusema;

soma zaidi ingia;http://miram3.blogspot.co.uk/

Tupo pia kwenye: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate zaidi;
https://www.facebook.com/emu.three
https://twitter.com/emuthree



"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Tuesday 20 August 2013

Afya Na Jamii;TATIZO LA MIFUPA AU KUUMWA MIGUU/MAGOTI: OSTEOPOROSIS:


Tatizo hili hujulikana kwa jina la kitaalamu kama Osteoporosis. Ugonjwa huu unatokana na kupunguka kwa protini na madini kwenye mifupa (madini chokaa/calcium). Hali hii hupelekea mifupa kuwa milaini na myepesi ambapo inaweza kuvunjika kirahisi. Kipindi cha utoto hadi kufikia umri wa miaka 30, ni kipindi ambacho mifupa hujijenga zaidi. Baada ya hapo mifupa huwa ina kawaida ya kupoteza madini zaidi.
Tatizo hili linatokea sana kwa watu wazima, hasa zaidi kwaa wanawake ambao wamefikia kipindi cha kukoma hedhi (menopause), kuanzia miaka 50. Ni kipindi ambacho wanawake hupungukiwa na homoni yenye kazi ya kuilinda na kuikinga mifupa. Tatizo hili huwapata wanawake zaidi kwa kuwa wana mifupa midogo na myembamba kuliko wanaume. Miaka mitano (5) hadi aba (7) tangu mwanamke kukoma hedhi hupungukiwa na madini chokaa kwa asilimia ishirini (20%), zaidi ya wanaume. Kuanzia miaka 65 hadi 70 wanawake na wanaume hupoteza madini chokaa kwaasilimia sambamba.
NINI CHA KUFANYA
1. Mazoezi hasa kipindi ambacho umriu mepiga hatua
2. Kwa wale wenye uzito uliozidi, jitahidini kufanya utaratibu wa kupunguza
3. Jitahidi kupata madini chokaa (calcium) kwa wingi (maziwa freshi, maziwa mgando, mboga za majani)
4. Jitahidi kupata Vitamini D (mayai, maziwa, samaki, mboga za majani, pata jua)
VIRUTUBISHI
Kwa ambao tatizo limekuwa kubwa, inawapasa kujitahidi kupata virutubishi ili kuirejeshea mifupa nguvu na uimara, pia kuondokana na maumivu.
Virutubishi vifuatavyo vimewasaidia wengi wenye tatizo hili.
1. Calcium
2. Chitosan
3. Lycopen



KUKOSEKANA KWA UTE KATIKATI YA VIUNGO (JOINTS) - CARTILAGE

Kajiraba fulani ambako hujulikana kwa jina la kitaalamu kama “Cartilage” (katileji) ambako hupatikana katikati ya mifupa. Kuna kitu fulani huwa kinapatikana katikati ya mifupa miwili ya goti la mnyama (ng’ombe, mbuzi) huwa wengi wanapenda kukila kwenye baada ya kuchemshwa au kupikwa. Kama unaijua hii, basi ndio katileji yenyewe.
Katileji inasaidia kuikinga mifupa isiumie.Vilevile inafanya kazi ya kusaidia kuubeba uzito wakati wa kutembea, kuinama, kunyoosha viungo au kukimbia.
Zaidi ya asilimia 85 (85%) ya katileji ni maji, na jinsi umri unavyosonga mbele, maji hayo huwa yana kawaida ya kupungua. Na asilimia 15 niprotini.
Tatizo hili lipo zaidi kwenye sehemu ya magoti. Endapo katileji inakuwa ina tatizo, husababisha maumivu makali hasa unapotaka kusimama au kutembea, vile vile kwenye mabega, au nyonga. Pia inaweza sababisha uvimbe (goti au nyonga au bega kuvimba).
Mtu ambaye katileji yake ina tatizo aidha imelika au kutokuwepo kabisa, anatakiwa kupatiwa vitu au virutubishi ambayo vitasaidia kuirekebisha katileji au kuijaza kwa upya.
Virutubishi vifuatavyo vimesaidia wengi wenye tatizo hili:
1. Shark Cartilage
2. Calcium
3. Chitosan

OFISI ZETU ZIPO karibu na huduma zifuatazo:
1. Ofisiya TRA, au karibu na
2. Afya Dispensary, au karibu na
3. Mjasiriamali kwanza, au karibu na
4. Kanisa la Sabato au karibu na
5. Kanisa la Lutherani au karibu na
6. Uwanja wa mpira wa Mwenge.

Anaye hitaji ufafanuzi zaidi tuwasiliane: 0715 594 564 au 0756 594 564

Au tembelea website yetu www.1000ufahamu.com

Sunday 18 August 2013

J'Pili ya Leo;Tuendelee Kuwaombea Wenye Shida Na Tabu,Burudani-Upendo Nkone na Abiudi Misholi.!!!!!

Wapendwa;J'Pili hii tuendelee kuwaweka mikononi mwa BWANA wenye Shida na Tabu.
Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali,Kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua.
Neno La Leo;Matendo ya Mitume:16:16-34;






Muendelee kuwa wakati mwema Kila iitwapo Leo.

"Swahili na Waswahili" MUNGU ni mwema.

Saturday 17 August 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Mary Mary-Shackles na Nyingine!!!



Waungwana;Chaguo La Mswahili Leo...Mary Mary..[Erica na Tina]Mimi Huwa nawakubari/Nawapenda/Wananibambaaa saaana..Pia huwa nafuatilia sana vipindi vyao kwa Tv.
Je vipi wewe? 
Mengi sina,Nisikuchoshee..Pata Burudani Kitu Roho napenda......









"Swahili na Waswahili" Pamoja Daima.

Sunday 11 August 2013

Natumaini J'Pili inaendelea Vyema;Burudani-Hakuna Mungu kama Wewe na Nyingine!!!!!

Natumaini J'Pili Inaendele Vyema..
Ni neno jema kumshukuru BWANA, Na kuliimbia jina lako,Ee Uliye juu.

Neno La Leo:Zaburi:92:1-5;Ee BWANA jinsi yalivyo makuu matendo yako! Mawazo yako ni mafumbo makubwa.
Wapendwa/Waungwana; Nawatakia kila lililo Jema, Baraka,Amani na Furaha.






"Swahili NA Waswahili" Mbarikiwe Wote.

Saturday 10 August 2013

Watoto Na Malezi; Watoto wa zamani,Mnakumbuka Kipindi cha MAMA na MWANA?



Watoto wa Zamani Mpo? Mnakumbuka  MAMA na MWANA/WATOTO WETU/CHEI CHEIIII..Mhh mimi ni mmoja wa waliokuwa wapenzi  wa Kipindi cha Watoto RTD...
Enzi ya Shangazi/Mama, Debora Mwenda,Sango Kipozi,Eda Sanga na Wengine....

Mhhh Chei Chei Shangaziii..Uje tena Shangazii...


Sehemu ya Kwanza ya Hadithi ya Binti Mfalme;



Sehemu ya Pili



Kujua Mengi Kuhusiana na Watoto Nifuate Huku;http://Watotonajamii.blogspot.com Huku Utakutana na Mambo ya Watoto,Wazazi/Walezi.Hapa tutaendeleza Watoto Na Malezi kwani Swahili Na Waswahili ni Mama Leo..Lakini nimetenganisha Mambo Kidoogo..huko ndiyo Penyewe kwa Mambo ya Watoto na Jamii.

Pia kwa Mambo ya Mitindo Nifuate Huku;http://www.mitindoafrica-abroad.blogspot... Kwa Undani Zaidi..
Panapo Majaaliwa/Kwa Mapenzi ya MUNGU ipo siku yote yatakuwa kwenye Nyumba moja.
Yote Haya yapo Ndani ya SWAHILI NA WASWAHILI NA WAPENDAO YA WASWAHILI NA YASIYO YA WASWAHILI YANAYO FAA KUJUZWA WASWAHILI. 

Pamoja Daima.

Friday 9 August 2013

Tamasha kubwa la muziki wa Injili kufanyika Washington DC kesho!!!!


 Waimbaji wanaofanya vema kwenye muziki wa Injili Afrika Mashariki, Upendo Kilahiro na Christina Shusho, watatumbuiza katika Tamasha kubwa la Injili litakalofanyika Jumamosi hii jijini Washington DC

 Kama walivyoongea kwenye VIDEO HII, waimbaji hao wamekamilisha maandalizi ya tamasha hilo ambalo pia litashirikisha waimbaji wenyeji wa hapa Marekani.
 

 Tamasha hilo kubwa lililo sehemu ya Maadhimisho ya miaka mitano ya kanisa la The Way of The Cross Gospel Ministries litafanyika siku ya Jumamosi kuanzia saa kumi kamili mpaka saa tatu usiku (6:00pm - 9:00pm) na kiingilio kwenye tamasha hilo kitakuwa ni dola kumi ($10) kwa watu wazima, bure kwa watoto.

 Anwani ambapo litapofanyika tamasha hilo ni

 The Way of the Cross Gospel Ministries 

 (at University United Methodist Church) 

 3621 Campus Drive 

 College Park, MD 20740 

 Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana na

 Mch. Ferdnand Shideko +1 240 476 6718 ama

 Ms Flora Mnkande +1 240 217 6335

 Waimbaji hawa wote watatumbuiza nyimbo zao za zamani na mpya na wanawaalika watu wote kujumuika nao na waimbaji wenyeji kuweza kupata BARAKA kwa njia hii ya uimbaji

   

   
Zaidi utayapata; http://www.changamotoyetu.blogspot.com
 http://www.youtube.com/user/mutwiba

Mkono Wa EID [Eid Mubarak] Kwa Watu Wote!!!!


Nawatakia/Nawapa Mkono Wa EID [EID MUBARAK]
  Ndugu,Jamaa,Marafiki,Wa Tanzania na Watu Wote Duniani.
Muwe na Eid/Siku Kuu Njema,Yenye Amani,Upendo,Umoja,Baraka na Furaha.



Pata Burudani taratiiibu!!!!



"Swahili Na Waswahili" EID MUBARAK

Zawadi ya shilingi Milioni 10 kwa taarifa za washukiwa Zanzibar!!!!!


Kristie Trup na Katie Gee

Polisi nchini Zanzibar wameahidi kutoa zawadi ya shilingi milioni 10 za Tanzania kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazopelekea kukamatwa kwa watu waliowashambulia wasichana wawili waingereza kwa Tindikali.
Wasichana hao kutoka London, Kirstie Trup na Katie Gee, walirushiwa Tindikali kwenye nyuso zao walipokuwa wanatembea mjini Jumatano Jioni.
Taarifa zinazohusiana
afya
Serikali ya Zianzibar ndio itakayotoa zawadi hiyo.
Polisi wanasema kuwa hizo ni pesa nyingi sana kisiwani Zanzibar.
Kirstie Trup na Katie Gee, wote wenye umri wa miaka 18 kutoka London, walipelekwa hospitalini nchini Tanzania baada ya kushambuliwa Mashariki mwa kisiwa hicho.
Inaaminika kuwa walitoka Tanzania kuelekea Uingereza Alhamisi usiku.
Mama za wasichana hao, Rochelle Trup na Nicky Gee, walielezea kughadhabishwa mno na shambulizi hilo ambalo sababu yake haiwezi kujulikana na ambalo halikuchochewa kivyovyote. Walishambuliwa na wanaume wawili waliokuwa kwenye pikipiki.
Polisi walisema kuwa walirushiwa Acid kwenye nyuso zao, kifuani na kwenye mikono yao walipokuwa wanatembea mjini .
Mwandishi wa BBC anasema kuwa waliowashambulia walitoroka na polisi hawajui kwa nini wanawake hao walilengwa.
Mama za wasichana hao walisema kwenye taarifa yao kuwa walighadhabishwa mno na shambulizi hilo na hawaelewi kwa nini wasichana hao walishambuliwa ili hali walikwenda Zanzibar kwa nia njema.
''Tunashukuru kwa wale wanaotaka kujua kinachoendelea lakini tungeomba vyombo vya habari vituwache kwa sasa hadi tutakapokutana na watoto wetu,'' alisema msemaji wa familia za wasichana hao.
Wasichana hao walikuwa wamekaa Zanzibar kwa muda wa wiki mbili ingawa walitarajiwa kuwa huko kwa wiki tatu, kupitia kwa kampuni ya usafiri ya i-to-i Travel, ambayo ilisema inafanya kila iwezalo kuwarejesha nyumbani Uingereza.
Kari Korhonen, mkurugenzi mwenza wa kampuni ambayo wasichana hao walikuwa wanafanyia kazi, alisema kuwa hali yao si mbaya ikizingatiwa athari za Acid kwa mwili na visa ambavyo vimewahi kushuhudiwa vya kuchomwa kwa Tindikali
Msemaji mwingine aliongeza kuwa wasichana hao walikuwa njiani kuelekea kwa maankuli ya jioni wakati wa shambulizi hilo.

Habari zaidi;http://www.bbc.co.uk/swahili/

Thursday 8 August 2013

Shusho, Kilahiro kuhudumu Washington DC wiki hii!!!!!



 Watumishi wa Mungu Christina Shusho na Upendo Kilahiro, mwishoni mwa wiki hii watahudumu katika jiji la Washington DC na Vitongoji vyake (DMV).

 Shusho na Kilahiro ambao ni miongoni mwa waimbaji mahiri wa muziki wa Injili Afrika Mashariki, wameshawasili Washington DC tayari kwa huduma hiyo ambayo ni sehemu siku tatu za  Maadhimisho ya miaka mitano ya kanisa la The Way Of The Cross Gospel Ministries.

 Maadhimisho haya yataanza siku ya Ijumaa na kumalizika Jumapili

 Maadhimisho haya yatafanyika
The Way of the Cross Gospel Ministries
(at University United Methodist Church)
3621 Campus Drive
College Park, MD 20740


 Hii inakuwa ni mara ya pili kwa watumishi hawa kuhudumu pamoja kanisani hapo katika kipindi cha miaka miwili, ambapo mwaka 2011waliungana na Upendo Nkone kuhudumu katika Mkutano mkubwa wa Injili ulilofanyika kanisani hapo.

  Watazame na kuwasikiliza wanavyoelezea siku hizo



Mengi utayapata; http://www.changamotoyetu.blogspot.com
 http://www.youtube.com/user/mutwiba

Wednesday 7 August 2013

Jikoni Leo;da'Miriam Rose Kinunda wa Taste Of Tanzania-Q & A Book, Language and Chapati!!!

Mwenyewe da'Miriam Rose Kinunda [MIROKI]

Miriam Kinunda is answering popular questions about the book, Why using English instead of Swahili, and Chapati......


Zaidi mfuate huku;http://www.TasteofTanzania.com na A Taste of Tanzania

"Swahili na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 4 August 2013

Muwe na J'Pili Yenye Kumpendeza MUNGU;Burudani-Rose Muhando-Tembea baba na MUNGU Unashangaza!!






Wapendwa;Ni matumaini yangu J'pili Inaendelea Vyema..BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba,Watu hawa husema,Huu sio wakati utupasao kuja,huu sio wakati  wa kujenga nyumba ya BWANA.
Neno La Leo;Hagai:1:1-11;[5]Basi sasa,BWANA wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.

Muwe na J'Pili ya Kumpendeza MUNGU  na Kupendana wenyewe  Upendo wa Kweli.

"Swahili NA Waswahili" Mbarikiwe Sana.



Saturday 3 August 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Banana Zorro-Mama Yangu,Nzela na nyingine!!!!








Waungwana;"Chaguo La Mswahili Leo"  Banana Zorro.

Mama yangu wewe ni nguzo maishani mwangu Taa imulikayo mbele yangu.....Mmhhhhh...Nikisema nikulipeee itanigharimu Maisha yangu yote!!!!!!!Nikisema nikuzawadie sioni kile unachostahili... ninachoweza sema nakupenda sana mama Nakushuru kwa mema yote uliyotenda kwangu.........

Mengi sina mpenzi/mfuatiliaji.. jee hizi nyimbo zinakugusa/kuzipenda?
Zina Mafunzo/umejifunza kitu?

"Swahili NA Waswahili"

Thursday 1 August 2013

Tarehe,Mwezi,Siku kama ya Leo Alhamisi;Mimi Rachel-siwa Nilizaliwa-Asante MUNGU!!!!!!













Wapendwa/Waungwana..Tarehe kama ya Leo,Mwezi kama huu,Siku kama hii Alhamisi ..Familia ya Bibi na Bwana Kiwinga,MUNGU aliwajaalia mtoto wa kike mwenye Afya Njema.
Leo ni kumbukumbu ya Siku yangu  ya kuzaliwa, na imejirudia kama ilivyo kwa siku hii ya Alhamisi..

Na Rudisha Shukrani na Utukufu kwa MUNGU BABA MUUMBA.Yeye ananijua zaidi ya wote,Yeye amenifanya hivi nilivyo,Yeye ameniokoa na kunilinda siku zote,Yeye ni Faraja yangu katika maisha yangu,Yeye ni Dereva wangu,Yeye ni Mwalimu wangu,Yeye ni Mwamba wangu,oohh MUNGU wewe ni kila kitu Maishani mwangu,Unatoshaa BABA..Wewe ukisema ndiyo nani atasema siyo?

Shukrani; kwa Wazazi/Walezi kwa yote.Nathamini na kukumbuka meengi sana sana hasa pale ninapo kutana na Mapito/Majaribu,Furaha na Kupiga hatua mpya.Sauti zenu haziishi masikioni Mwangu,Maneno yenu/Wosia,Upendo ,Ukarimu na Faraja zenu..Sina lakusema zaidi ya Asanteni na nawaombea kila iitwapo Leo na kuwapenda Saaaana.

Shukrani; kwa Mume wangu kipenzi kwa yote,wewe ni mwanaume unaye faa kuitwa MUME/BABA,Sijilaumu wala Kujutia kamwe kuungana nawe.MUNGU asante kwa Ubavu huu wangu.

Shukrani;Watoto wangu wote,Dada zangu na Wadogo zangu,Kaka zangu wote,Mawifi,Mashemeji.

Shukrani;Ndugu,Jamaa,Marafiki,  kwenye Safari ya Maisha yangu  nimekuta na Ndugu,Watoto,Dada,Kaka .Ambao si wakuzaliwa nao katika Tumbo Moja/kutokea Ukoo mmoja,Lakini kwangu nawathamini sana sana na Nawapenda mnooo.Ni vigumu kutaja kila mmoja lakini wenyewe manajijua.

Shukrani; Blogger wote,Wapenzi/wafuatiliaji wote wa Swahili na Waswahili,Mitindo Afrika na Nga'mbo,Watoto na Jamii.Pamoja Daima.

Nichukue Fursa hii kukuomba Msamaha/Radhi kutoka moyoni ,Wewe niliyekukosea,kwa makusudi au bila ya kukusudia,Nilikukwaza,kukuletea /kukuingiza majaribuni.
Nami  nichukue Nafasi hii kwa Kuwasamehe wale wote walionikosea/kunikwaza.MUNGU BABA Na atusamehe Sote!!!!!!!

Asanteni kwa mlionitumia ujumbe,Mlionipigia simu,Mlionitumia/letea zawadi,Mlioniombe/endelea kuniombea  Sala/Dua zenu nimezipokea.

Nikisema niendelee hapa sitomaliza mpaka kunakuchaa..kwani kwa umri huu nimepitia Meengi,Ngoja niishie hapa na Mengi usome:1.Wakorintho:12:1-31.[15]Kwa maana mwili si kiungo kimoja,bali ni vingi.

Asanteni sana kwa Kunisoma na MUNGU awabariki Nyote!!!!

Ni mimi;Rachel-siwa.


"Swahili na Waswhili"Pamoja Daima.