Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 31 July 2012

Wanawake na Mitindo;Leo Mashungi/Kujitanda!!!!!!


Waungwana Leo Tuangalie Uvaaji huu Sijui kama ni Mwezi huu wa Ramadhani au Msibani/Hitimani au.....


Ukienda Rumi Fanya kama Wafanyavyo Warumi, Ukikuta Wenyeji Wanakunja Miguu nawe Kunja yako!!!!!


Kwenye Picha hizi si Woote waavaaji hivyo kila siku Waliheshimu Sehemu Husika.


Wewe unamawazo,Maoni,Ushauri Gani katika hili?


Jee nawe unapicha yako Umevaa hivi?Ruksa kushiriki Nasi, Unaweza kututumia rasca@hotmail.co.uk


Jimwage mwanakwetu!!!!" "
RAMADHANI NJEMA KWA WOOOTE"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Monday 30 July 2012

GERRY TEGETE, NGASA WASHEREHEKEA UBINGWA PAMOJA NDANI YA WHITE HOUSE KIMARA KOROGWE.!!!!!!


Mwanamuziki nguli wa Bendi ya Mashujaa Musica Chaz Baba akiimba kwa furaha kubwa ndani ya Ukumbi wa White House Kimara Korogwe usiku wa kuamkia leo.

Kutoka kulia Chaz Baba, Mrisho Ngasa Mchezaji wa Azam na Gerry Tegete Mchezaji wa Yanga wakiwa ndani ya viunga vya White House Kimara Korogwe jana baada ya kutoka kwenye Mechi kali baina ya timu zao, ya kombe la Kagame ambayo Yanga waliibuka mabingwa kwa mabao 2 kwa bila.

Kulia Gerry Tegete akishoo luv na Mchezaji mwenzake Mrisho Ngassa anayechezea club ya Azam.

Rapa maarufu wa Bendi ya Mashujaa Fagasoni akiimba ndani ya ukumbi wa White house Kimara Korogwe.


Mpiga tumba namba moja Afrika mashariki MCD akiwakimbiza washabiki wao ndani ya White house Kimara.

Mrisho Ngassa na Chaz Baba wakifurahia kwa pamoja Ushindi waYanga, Mrisho ngassa ni Mshambuliaji mahiri wa Club ya Azam.

Tegete, Henry na kulia Mrisho Ngassa ndani ya White House Kimara.

 kulikulikuwa na mechi ya fainali ya kombe la Kagame kati ya Yanga afrikani na Azam FC ndani ya uwanja wa Taifa ambapo Yanga waliibuka mabingwa

Ngassa na Tegete kwa kuonyesha mpira sio ugomvi walisherehekea pamoja ushindi wa Yanga baada ya mechi katika viwanja vya White House Kimara korogwe wakati bendi ya Mashujaa ilipokuwa inatumbuiza

Sunday 29 July 2012

Nawatakieni J'Pili Njema;Burudani- Kwaya kutoka Mbeya na Iringa!!!!!!!!!

Nawatakia J'Pili yenye Baraka, Amani,Fadhili na Shukrani.
 Mungu na Atufadhili na kutubariki,Na kutuangazia Uso wake.
Njia yake ijulike Duniani,Wokovu wake katikati ya Mataifa Yote.

Neno la Leo;Zaburi:67:1-7...

Saturday 28 July 2012

Chaguo la Mswahili Leo; Kagera Mpoo? NgojaTatuNane Wawasaidie!!!!!

Waungwana "CHAGU LA MSWAHILI LEO" ngoja niwapeleke Kagera,
 wanakwambia Mapenzi Kizunguzungu...Nshomileeeeee........

Sina Mengi leo Uwanja wako.
 Unalolote kuhusu Burudani ya Leo?
 Jimwage sasa.

mimi siimbi Natifuka tuu Twende Sote sasa............."Swahili NA Waswahili"!!!!!!! Pamoja Daima.



Tuesday 24 July 2012

Kundi la watu wanaodhaniwa majambazi wamevamia baa ya Chonya...

Kundi la watu wanaodhaniwa majambazi wamevamia baa ya Chonya eneo la River Side jijini DSM, leo asubuhi na kupora fedha..




Wakazi wa Ilala Sharifu Shamba Wamebaki wana shangaa na Kuogopa, Baada ya kusikia milio ya risasi!!!


 Poleni sana.




Shukrani; ITV.

ENGINEER WA VODACOM JOSEPH MWAPINGA APATA PIGO: AFIWA NA MKEWE.




Marehemu Belinda J. Mwapinga enzi za uhai wake.

Mwili wa Belinda ukiwa katika kanisa la roman katoliki extenal.

Baba Padre akitoa heshima yake ya mwisho kwa mwili wa Belinda. J. Mwapinga jana katika Kanisa la Katoliki Extenal Dar es salaam

Joseph Mwapinga mwenye suti nyeusi akiwa na watoto wake alio achiwa na mke wake kipenzi Belinda.


Wafanyakazi wa VODACOM Tanzania wakiwa wamebeba mwili wa Marehemu Belinda wakiufikisha katika makaburi ya Kinondoni.

Hawa ni baadhi ya waombolezaji waliohudhuria kwenye safari ya mwisho ya Belinda.


Mwili wa Marehemu Belinda ukiwa umewekwa juu ya nyumba yake ya milele katika makaburi ya Kinondoni Dar es salaam.

Mhandisi Joseph Mwapinga akiweka shada la mauwa kwenye kaburi la Mke wake.



Baba Padre akisali sala ya mwisho kwa ajili ya kumuombea Marehemu Belinda J. Mwapinga katika makaburi ya Kinondoni.
kulia kwa Padre ni Joseph Mwapinga na mwenye Tshirt nyekundu ni rafiki wa karibu wa familia, Ndugu Stephen Mapunda.

Marehemu Belinda J. Mwapinga alifariki tarehe 20/07/2012 katika Hospitali ya Muhimbili na mazishi yake kufanyika tarehe 23/07/2012 katika makaburi ya Kinondoni.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIBARIKIWE.


"Swahili NA Waswahili" Tunawapa pole wafiwa. 

Monday 23 July 2012

Jikoni Leo;Maidana-na JIKO LANGU,Mapishi-Maandazi ya Yogurt!!!!!!!!!

MAHITAJI
yogurt vijiko 2vya chakula
sukari 1/4 mug
hamira kijiko kimoja cha chai
iliki kijiko kimoja cha chai
samli kijiko kimoja cha chakula
unaweza tumia,maji/maziwa/nazi yapime katika mug uliyopimia sukari
ponda hadi unga wako uwe mlaini kiasi,katakata matonge,sukuma kata maandazi yako
yaache yaumuke yachome.
unaweza kutumia maharage,mchuzi wa nyama,maini,samaki kama kitoeo.





Waungwana Mapishi yapo Mengi haya "JIKONI LEO" ni Maandazi ya Yogurt ,Siyo Nazi kaazi kwako kama wewe Mpishi au Muonjaji!!!!


 Mpishi si Mwingine ni da'MAIDANA na "JIKO LANGU"  [LAKE].
kwa Maelezo Zaidi ingiahttp://jiko-langu.blogspot.co.uk/




"Swahili NA Waswahili" inawatakia Ramadhani Njema Waislam woote Dunia.

Sunday 22 July 2012

J'Pili ya Leo Tumsikilize;Masanja Mkandamizaji - Albam Hakuna Jipya, Zaburi ya Wani Fifte!!!!!

Masanja ndiye anayetupa Neno na Burudani J'pili ya leo.
Neno la Leo zaburi :150;1-6;Haleluya.Msifuni MUNGU katika Patakatifu pake;Msifuni katika anga la uweza wake,Endelea...

Nawatakia J'Pili yenye Baraka,Amani,Furaha,Upendo,Unyenyekevu na Fadhili!!
Na kila Mwenye pumzi na  amsifu BWANA.
HALELUYA!!!!!!!

Saturday 21 July 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Marijani Raajab - Salama,Mwajuma,Mwanameka-DDC na kitu cha-Hiba!!!

DJ Wa Swahili NA Waswahili Leo!!

Waungwana "CHAGUO LA MSWAHILI LEO"
 Turudi nyuma kidoogo Tuangalie/Tusikilize Bendi zetu , jee unaonaje Bendi hizi?
 Zinaklukumbusha nini na jee Zinakubamba/Unazipenda?
 Vipi Bendi za kileo na za zamani Tofauti iko wapi?

 Na jee zasasa wanafanya vyema zaidi kwa sababu ya usasa au wanakwenda Kinyume?

Twende sote sasa....... oohh mwajuma pesa hupatikana kwatabu...oohh mwajuma pesa hupatikana kwa shidaaaaa...Bwana Mashakaaaa wachakulalamika oohh kama amekushinda mrudishe kwaooo.......

Mhhhhh  ngoja niishie hapa na Chumvi nimeacha nisije pata Safura bure!!!!!!

"Swahili NA Waswahili" Pamoja sana.

Thursday 19 July 2012

MWANAFUNZI WA IFM AFARIKI KIFO CHA KUTATANISHA: AOKOTWA MAENEO YA KOKO BEACH AKIWA HAJITAMBUI!!!!


Marehemu Agnes B. King'unza wakati wa uhai wake.
Agnes alikuwa ni mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) akiwa mwaka wa kwanza akichukua Shahada ya Kodi (Bachelor of Taxation).

Mwili wa marehemu Agnes ukiwa kwenye jeneza ulipokuwa ukiwasili nyumbani kwao Mbezi kwa Msuguri.

Mwili wa Marehemu Agnes ukiwa kanisani tayari kwa heshima ya mwisho katika kanisa la Romani katoliki Mbezi Temboni.



Mama Mzazi wa Agnes akilia kwa uchungu baada ya kuona mwili wa Mwanae.


Aliyevaa Koti jeusi ndio baba mzazi wa Agnes Bwana Bernard King'unza.




Makamu Rais wa Serikali ya wanafunzi wa IFM akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya wanafunzi wenzake.
Baba Padre wa Parokia ya Mbezi Temboni akibariki mwili wa Agnes King'unza.


Hawa ni baadhi ya wanafunzi wenzake aliokuwa akisoma nao katika chuo cha usimamizi wa fedha IFM na kushoto mwenye shati la mistari ni mwakilishi kutoka wafanyakazi wa IFM.

Agnes aliokotwa na msamaria mmoja ambaye kwa taarifa za awali zinasema alikuwa ni mlinzi wa nyumba moja maeneo ya Koko Beach ambako ndio alikutwa ametupwa na watu wasiofahamika na kupelekwa kituo cha Polisi cha Oysterbay na baadae kukimbizwa hospitali ya Agha khan.

Marehemu Agnes B. King'unza alifariki Jioni ya tarehe 16/07/2012 katika Hospitali ya Muhimbili ambako alipelekwa baada ya Madaktari wa Hospitali ya Agha khan kushindwa kumtibu na kumrufaa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Mwili wa Marehemu Agnes King'unza umesafirishwa jana Jioni kwenda Nyumbani kwao Kalenga - Iringa kwa mazishi ambayo yatafanyika leo tarehe 19/07/2012.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.


"Swahili NA Waswahili" inawapa pole wafiwa.
Ulale kwa Amani da'Agnes

Tuesday 17 July 2012

How to make fresh coconut-milk (Tui la Nazi) - By Miriam Rose Kinunda!!!!!


Waungwana "JIKONI LEO"Si mwingine ni da'Miriam Rose  Kinunda wa "TASTE OF TANZANIA"
Leo anatuletea jinsi ya kuandaa Tui la Nazi.
Pia kaa Tayari kwa Video mpya zinakuja,Kitabu pia Kipo Njiani.
Kipende chako au........Kujua Zaidi Ingi http://tasteoftanzania.com/blog

Jamani eehh Nazi za Kopo,Box,Unga mzipumzishe haswa mliokuwa Nje ya Nyumbani.
Tena Mwezi wa Ramadhani unakuja kwa Wenzetu Wanaofunga Nazi ndiyo yenyewe au vipi?

Mimi hicho Kibao  cha Mbuzi hapa ninapoishi sijakiona,Lakini sina Hofu Jirani  yangu anaweza kuwa nacho si wanasema mpende Jirani yako? hahahhaa..
Na jee kwanini kiliitwa Kibao cha Mbuzi?

Jee wewe Unapenda Nazi? na Unapenda kuunga/kuweka kwenye Chakula Gani?

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Saaana!!!

Monday 16 July 2012

Da'Sandra-Neema Atimiza Miaka14!!!!!!!


                      Duuhh miaka 14 si mchezo!!!!!

                     da' Sandra na Rafiki yake da'Frida[Swahili ya Tz na Swahili ya Kenya] wakiwa Drayton Manor ndipo alipofanyia sherehe ndogo na Wanafunzi wenzie.
Shukrani sana kwa Wanafunzi ,Walimu wa Blue Coat

Familia ya Isaac Tunamshukuru sana MUNGU kwa Mema yoote anayotutendea.Asante sana MUNGU kwa kutujalia na kututunzia Sandra.Tunamuweka Mikononi mwako kwa kila Jambo.Wewe watosha BABA.
Asante sana kwa Woote wanaojumuika nasi kwa namna moja au nyingine katika malezi yetu.

MUNGU Azidi kukubariki sana Sandra-Neema,Uwe Baraka kwetu na kwa Watu Wote.

MUNGU Awajalie pia wanaotafuta Watoto.

MUNGU NI MWEMA!!!!!!!!

Unakata Logo/ Wapi utatengenezewa?Fuatana nami!!!!!!!

 
within three days, using the very best professional logo tools designer.

 Logo nzuri ni moja ya njia muhimu na ya pekee kujitambulisha katika soko la bidhaa zako.
 Logo ndio kielelezo cha kampuni yako, na ndio kioo cha kutambulisha bidhaa zako.
 Logo ndio Alama pekee yenye nguvu, na ndio yenye kuzungumza na wateja wako kabla ya kuwasiliana au kukutana nao.
 Basi ili uweze kuwavutia wateja wa bidhaa zako, yakupasa uwe na kielelezo kitakachosema kabla ya wewe kuzungumza.
 Kitu icho si kingine ni ile alama ya utambulisho wa kipekee, aidha ni Logo au lebo za bidhaa zako. Ili uweze kufikia malengo yako ya kibiashara, unaweza kuwasiliana na 99graphix wabunifu wa aina mbali mbali za logo (Nembo).


 99Graphix Design Email: 99graphix@gmail.com http://99graphixdesign.blogspot.com/


Ndiyo waliotengeneza hiyo "Swahili Na Waswhili" hapo juu.
        Pamoja sana.

Jikoni Leo-Mapishi ya coated chicken with chutney - Recipe of (Swahili)!!!!

Waungwana "JIKONI LEO"Si wengine ni "TUPIKE PAMOJA"
Leo wametuletea Mapishi ya Coated Chicken With Chutney.Mmmmhhhh Tamu Sanaaa!!
Hii ni Video Mpya Waungwana Usikose kupitia www.tupikepamoja.com kwa vipimo na kujua zaidi.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja saaaana!!!

EXTRA BONGO NEXT LEVEL YAWAAGA WAPENZI NA WASHABIKI WAKE KWA SHOW KALI ILIYOSINDIKIZWA NA MATONYA, Q CHIF NA CHID BENZ NDANI YA UKUMBI WAO MPYA NEW WHITE HOUSE - KIMARA KOROGWE JIJINI DAR ES SALAAM


Mkurugenzi wa Extra Bongo Ally Choki akiimba mbele ya mamia ya washabiki wake jana usiku ndani ya Ukumbi wa New White House Kimara Korogwe

Msanii wa kizazi kipya Bongo Fleva Matonya akiwarusha mashabiki wa Extra bongo usiku wa kuamkia leo ndani ya New white house Kimara Korogwe.

Q chif akiimba kwa hisia kali usiku wa kuamkia leo ndani ya ukumbi wa New white house Kimara Korogwe katika show kali ya Extra bongo ya kuwaaga mashabiki wao, usiku wa leo wanaelekea Finland kwa mwaliko rasmi wa kwenda kufanya show kadhaa huko.

Chid Benz kama kawa akiwarusha mashabiki wake.

Matonya na Q Chif

Choki na Chid Benz

Ally Choki akimsikiliza kwa umakini mdhamini mkuu wa Bendi yake Chif Kiumbe, wakati wa show ya kuwaaga washabiki na wapenzi wao iliyofanyika ndani ya ukumbi wa New white house Kimara Korogwe