Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 31 October 2012

Mpendwa Wetu da'Mamie Msuya Amefiwa na Mama Yake!!!!!


Da'Mamie Msuya Pichani.
Amefiwa na MAMA yake Mzazi Afrika.
Dada Mamie anajiandaa na safari, Ataondoka kesho kwenda Afrika.
Tuungane nae katika wakati huu mgumu kwake. Hapa U.K. Msiba upo Nyumbani kwake.
Address;3C THOMAS KING HOUSE,
WELLINGTON ST,
CV1 5SJ.
COVENTRY.
Asanteni.

Tuesday 30 October 2012

Wanawake Waswahili Wa Coventry,U.K.[WWWCU]Wamtakia Kheri na Baraka da'Maggie!!!!!!!














Watu wa Mapambo[Zay&Rachel]
Kina kaka/Baba wa Covenrty na da'Esther wakiweka sawa mambo ya Burudani.
Kina mama wa Coventry wakiandaa chakula



Wapiga picha wakiongozwa na Mwanamke wa shoka da'Mija [Mrs Manju]kutoka MI-RA COMPANY
Maombi yaliongozwa na da'Elina[Mrs Ademisoye]
Neno lilitolewa na da'Rachel-siwa [ muke ya Mubena]
kupambwa na kuhakikisha da'Maggie amefika na kuondoka yalisimamiwa na da'Lina[Wifi la Wabongo]

Mpendwa wetu da'Maggie. 
yeye ndiye aliyetukutanisha  hapo.Ndugu yangu Maggie watu wote hawa wametoa Muda,Hali na Mali kwa sababu yaMshikamano, Umoja,Utuwema, Fadhili na Upendo wa Kweli............
MUNGU  na Azidi kutuongoza.

Picha Zitaendelea usicheze mbaaali.

"Swahili na Waswhili" na "Wanawake wa Shoka"[MI-RA]
Pamoja Daima.....


Sunday 28 October 2012

Siku kama ya Leo da'Jestina George Alizaliwa!!!!!!


Siku kama ya Leo miaka kadhaa iliyopita Mpendwa wetu Da'Jestina[mamake na Imani] Alizaliwa.
Da'Jestina Tunakutakia kila lililo Jema,Baraka,Amani,Fadhili na Uishi Miaka Mingi na Utimize Malengo Yako.

MUNGU azidi kukutendea na kukulinda kila iitwapo Leo.

Ukitaka kujua mengi kuhusu dada huyu ingiahttp://www.jestina-george.com/

Tumalize J'Pili kwa Amani na Upendo;Burudani-Atta Boafo - Double Double na Nyingine Nyingii!!!!

Wapendwa; Tumalize J'Pili hii Vyema,Tuwe na Amani,Upendo,Umoja,Msamaha,Uvumilivu na Shukrani.
Neno la Leo.Mithali;29:7-9 Mambo haya mawili nimekuomba;Usininyime[matatu]kabla sijafa.Uniondelee ubatili na Uongo;Usinipe umasikini wala Utajiri;Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.............

"Swahili NA Waswahili" MUNGU Atubariki Soooote

Thursday 25 October 2012

TANZIA!!!!!



FAMILIA YA  MAREHEMU MCHUNGAJI MWAKIPUNDA WA NGAMANGA IPINDA KYELA WANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MZEE NSUBISI SAMUEL MWAKIPUNDA (MKURUGENZI WA ZAMANI WA IDARA YA MAELEZO)  KILICHOTOKEA SIKU YA JUMATANO TAREHE 24/10/2012.

MIPANGO YA MAZISHI INAFANYIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU PUGU KINYEMWEZI DAR ES SALAAM.
HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.

KWA MAWASILIANO ZAIDI
+255655994499
BWANA AMETOA BWANA, AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

AMEN

Tuesday 23 October 2012

Mswahili Wetu Leo; Arba Manillah wa Kukaye Motooooooo!!!!!!!


 Waungwana;MSwahili Wetu Leo ni  Kaka ARBA  MANILLAH.
Ni mwanamuziki anayeishi na kufanya kazi zake Nchini Ujerumani[Chemnitz, Germany].
Arba Alizaliwa na kukulia IRINGA,TANZANIA.
Bendi yake inaitwa "KUKAYE MOTO"
Kujua zaidi kuhusu kaka huyu ingiaKukaye Moto na www.kukayemoto.de Twende sote sasa....
 "WANYALUKOLO"......Kihesa,Mkimbizi,Semtema,Ruaha,Ipogolo,Kigonzile,Ilala,Lugalo.....................Dar-es-salaam,Ilala,Mabibo....

"Swahili NA Waswahili" IRINGA TO GERMANY.




Sunday 21 October 2012

Tumalizie J'Pili hii Vyema;Burudani-Wagogo mass singing

Wapendwa;Tumalizie J'Pili hii kwa Amani,Baraka,Utuwema,Upendo na Fadhili.
Nchi na vyote viijazavyo ni Mali ya BWANA,Dunia na Wote wakaao ndani yake
.
Neno La Leo;Zaburi;22:1-10.

BWANA wa Majeshi,Yeye ndiye Mfalme wa Utukufu....


MUNGU Azidi kutubariki sana


"Swahili NA Waswahili"
Pamoja Daima

Saturday 20 October 2012

Chaguo La Mswahili Leo,Mdumange,Chiwoda,Sindimba,Wamasai na Wagogo.Kiasili Zaidi!!!!!

Waungwana;"Chaguo La Mswahili "Leo kinyumbani/Kiasili Zaidi.
Haya twende sote sasa,Lakini wewe unajua kucheza Ngoma za Asili au Unajua Ndombolo tuu?
Unafikiri ipi Ngoma Nzuri zaidi ya Zote Tanzania?
Ngoma ya kwenu Inaitwaje?
Utamaduni Tanzania unaendelea au Unakufa?...

Mtu Kwao Ungana Nami........"Swahili NA Waswahili" Mkataa  Kwao Mtumwa!!!!!!

Thursday 18 October 2012

Mwakilishi Mkazi wa UNOPS Nchini Sierra Leone, Nd Omary Mjenga akutana na Balozi wa Marekani Nchini Siera Leone leo.!!!




Mwakilishi Mkazi wa UNOPS Nchini Sierra Leone, Nd Omary Mjenga, akipiga picha ya kumbukumbu Pamoja na Balozi wa Marekani Nchini Sierra Leone Bw Michael Owen, alipomtembelea leo na kufanya mazungumzo naye.

Bwana Omary Mjenga akiagana na Mh. Balozi wa Marekani Nchini Siera Leone baada ya kumaliza mazungumzo.

Balozi Michael Owen, aliwahi kuwa Naibu Balozi wa Marekani Nchini Tanzania mnamo mwaka 2001 hadi 2004.

Wednesday 17 October 2012

Wanaume na Mitindo ya Nywele!!!!!!!!




Waungwana
"Wanaume na Mitindo" Leo tuangalie Mitindo ya Nywele, ki-Leo/kisasa..haya Wewe unaionaje? Inakubamba/kuipenda au...

 Jee Wanawake mnasemaje baba watoto, Mchumba,Kaka,Mwanao na Mitindio hii, upi umeupenda zaidi?...
Wenyewe Jee kina Kaka,Baba,Mojomba mnatuambiaje?

 Mengi sina Nawasikilizawenzangu....

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima...

Kuona picha zaidi, ingia kwenye Kibaraza chetu kipya;http://mitindoafrica.blogspot.co.uk/


Sunday 14 October 2012

Nawatakia J'Pili Yenye Neema na Tumaini;Burudani-Rebecca Malope - Thank You Lord, Na nyingine nyingii!!!!

Wapendwa;Muwe na J'Pili yenye Neema,Tumaini,Amani na Upendo.
Msiwiwe na mtu cho chote,isipokuwa Kupendana;Kwa maana ampendae mwenzake ametimiza sheria.

Neno la Leo;Warumi:13:8-10 Pendo halimfanyii jirani neno baya;Basi Pendo ndilo utimilifu wa Sheria.

"Swahili NA Waswahili" MUNGU Atubariki Sooteeee.

Saturday 13 October 2012

Chaguo La Mswahili Leo;Mbilia Bel - Nadina.Mario na Franco na Nyingine Nyingiiii!!!!!


Waungwana;Chaguo La Mswahili Leo""Mambo Ya zamani Kidogo.
 Nakusikiliza wapi unakumbuka na nini kilikuwa kinavaliwa wakati huo? Scania,Mwanameka, Raizoniii,Fundi Nimwagie,Soroo, Vishati Vyembamba na Ulipiga Picha za Studio wewe? hahahah umeshika kiuno kwenye Maua!!!!

Twende Sote sasa ,Mario na Lelieeeehhh Mhhh.....

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Wednesday 10 October 2012

Wanawake na Mitindo ya Nywele!!!!





Waungwana;"Wanawake na Mitindo" Leo tuangalie Nywele, jee wewe Mama/Dada unapenda kutengeneza Nywele na unapendelea Mitindo gani? Baba/kaka jee unapenda  Mkeo,Dada na... atengeneze vipi Nywele?

Jee Nywele ndiyo Kivutio kikubwa kwa Wanawake/Kina dada?

Kuona picha zaidi ingia kwenye Kibaraza chetu kipya cha;Mitindo Africa

"Swahili NA Waswahili" Karibuni Wooote!!!!!

Tuesday 9 October 2012

Kisa cha Leo na Mswahili;Emu-Three-Uchungu wa Mwana Aujuaye Mzazi;Sehemu ya 5!!!!!


Maua alikuwa katulia kwenye chumba huku akimuomba mungu wake, mwanzoni alikuwa anashindwa hata aombe nini. Akawa anajiuliza je nimuombe Mungu  anisamehe kwa hayanmakosa niliyofanya, lakini akajiuliza kichwani makosa gani, na kama ni makosa mbona ni yeye peke yake ndiye anayeadhibiwa, mbona mwenzake waliyeshirikiana naye , hayupo, je na yeye hastahili kuadhibiwa.

Alipowaza hilo akamkumbuka mwenzake, akakumbuka jinsi walivyokuwa wakiandikiana barua, lakini ghafla akawa hamjibu barua zake tena, hasa pale alipoandika kumuelezea jinsi gani anavyojisikia,na kumwambia anaogoa isije ikawa ni mimba. Ilikuwa barua ya mwisho kumwandikia, na hakuweza kupata jibu, na hata alipoandika nyingine, na nyingine, hakiweza kupata jibu kwa mtu aliyetokea kumpenda sana.

‘Hivi huyu mtu yupo aua kapotolea nchi gani, nakumbuka mara kwa mara anakwenda Arusha kwa mjomba wake, ambaye ni tajiri mmoja wa madini,na nia na lengo lake na yeye ni kujiunga kweney biashara hiyo, lakini kwanini asimwambia, au kumjibu baraua zake,lazima nimtafute tusaidiane hili tatizo’akasema huku akiangalia nje kwa kupitia dirishani.

Akawa bado anawaza ni mambo gani kwasasa anahitajika kumuomba Mungu wake, `Au  nimuombe Munguwangu anisaidie nisiweze kuangukia kwenye mikono ya baba, baba ambaye anataka kuitoa roho yangu, bila makosa, ‘ akasema na alipofikia kuwaza hili akatikisa kichwa na akili yake ikawa anajiuliza ‘Ina maana kweli mimi sio mkosaji,hivi kweli sistahili kuadhibiwa kwa kosa hili?’akatulia na kujarabi kutafakari zaidi. Hapo akakumbuka kauli ya baba yake, ambaye kila mara wakiwa naye alipenda kumuasa nayo;

‘Binti yangu nakupenda sana, na jinsi ninavyo kupenda,  nisingelipenda ukaja kuvunja huu upendo nilio nao juu yako, nakuomba  sana usije ukaniangusha, maana kila mtu hapa kijijini anakuona kama mtoto wa mfano, na mimi huwa natamba kwao kuwa  wewe ni binti mwenye akili, binti mwenye nidhamu, binti ambaye hakuna anayeweza kumfikia kwa jinsi ulivyo hapa kijijini’ilikuwa sauti ya baba yake.

Baba yake kweli alikuwa akimpenda, lakini sio ule upndo wa kumdekeza, kwani akifanay kosa alikuwa akiadhibiwa, mpaka anawaza vibaya kuwa baba yake anataka kumuua, na sio kweli anampenda kiasi hicho. Lakini kaam hajafanay kosa, baba yake alikuwa akribu sana na yeye na kila mwaka wakifanya sherehe za shule anakwenda kushuhudia mtoto wake akipewa zawadi ya kuwa mtoto wa kwanza, na wakirudi nyumbani huchinjiwa kuku kama zawadi maalumu. Na alipofaulu kwenda sekondari, baba alimnunulia zawadi nyingi sana.

`Sasa huyu ndiye binti , binti ambaye baba alikuwa akitamba kuwa ndiye binti wa mfano..’, Maua akajikuta akifuta machozi, akaliangalia tumbo lake, ambalo bado lilikuwa halijaonyesha dalili yoyote kuwa kuna kiumbe ndani , akakunja uso na kuanza kujpiga piga tumboni huku akilaani,i hicho kiumbe kilichopo tumboni,utafikiri ndicho chenye makosa akasema;Inaendele ingia;http://miram3.blogspot.co.uk/

Diary 

Yangu

Yakeeeeeeeee!!!!!

"Swahili NA Waswahili"Pamoja Daima...