Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 7 July 2012

EXTRA BONGO WAFUNIKA MBAYA KATIKA UZINDUZI WA UKUMBI WAO MPYA NEW WHITE HOUSE A.K.A BONGO RESORT KIMARA KOROGWE NDANI YA JIJI LA DAR ES SALAAM.!!!


Rais wa bendi ya Extra Bongo Ally Choki akiimba mbele ya wapenzi na washabiki wa bendi yake ndani ya ukumbi wao mpya New White House aka Bongo Resort Kimara Korogwe jana.

Rogert Hegga Katapila akiimba mbele ya washabiki wao katika ukumbi wao mpya uliopo Kimara Korogwe Dar es salaam.
Ally Choki na Henry

Mnenguaji mahiri wa Extra bongo akiwapagawisha washabiki wao ndani ya Kimara Korogwe.

Wakata nyonga wa kiume wa Extra Bongo wakiwakimbiza washabiki wao ndani ya ukumbi wao mpya Bongo Resort Kimara Korogwe.

 la Extra Bongo Banza Stone A.K.A Makaveli, Generale akipagawisha wapenzi wao ndani ya White Inn Kimara Korogwe.Jembe

Mwanamuziki wa BAIKOKO akiimba mbele ya washabiki wa Extra Bongo ndani ya Kimara Korogwe.

Tunda Man naye hakuwa nyuma katika kuwaburudisha mashabiki wa Extra Bongo.

Mwanamuzi wa Kizazi kipya Bongo Fleva Sheta akiwakimbiza washabiki wake ndani ya ukumbi mpya wa Extra Bongo katika uzinduzi wa ukumbi huo.

Extra Bongo jana walizindua ukumbi wao mpya New White House a.k.a Bongo resort uliopo kimara Korogwe. Uzinduzi huo ulisindikizwa na kundi la bendi ya taarabu Coast modern Taarab chini ya omary tego na Maua Tego, Tunda Man, Cheta na kundi maarufu la BAIKOKO ambalo linapiga muziki wenye maadhi ya utamaduni wa makabila ya watu kutoka Mkoa wa Tanga.

No comments: