Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 27 January 2012

Watoto wa Kiume na Wakike Wanamajukumu Sawa?


Nimatumaini yangu woote Muwazima!!!na Kama kunamgonjwa Pole sana na Mungu akuponye.
Waungwana Eti watoto wa kijijini wa Kiume na Wakike wanamajukumu sawa?Yaani si lazima wote waende kuchota maji pamoja,basi kama huyu anafagia mwingine aoshe vyombo,na ikifika saa ya kujisomea wote wanasoma,ikifika saa ya kucheza wote wanacheza.Najua kila familia inamalezi yake,Jee vipi kwa malezi ya kileo huko kijijini yameweza kubadili muonekano/Majukumu ya watoto? kama si kijiji kizima basi kuna nafuu?na kama hakuna jee tunaweza kuwasaidiaje?Sawa Mwanamke ni mwanamke, Mwanaume ni Mwanaume hilo naliheshimu pia.Jee Vipi na Watoto hawa wa Mjini?

Karibuni sana Wapendwa, kwa Mawazo,Ushauri,Kuelimishana  kwa Upendo.

Wednesday 25 January 2012

Wanawake na Urembo,Unapenda Shanga?

                                Wengine wanavaa Kiunoni.
                                     Wengine wanavaa Shingoni
                            Wengine Kichwani,Mikononi...........
Nimatumaini yangu wote muwazima!!!
Haya wapendwa leo tuangalie Urembo huu wa Shanga,Jee wewe Mama,Dada wapenda Shanga?
Nawe Baba,kaka Unapenda Mkeo,Mchumba wako ajipambe kwa Shanga?
Kuna wanaopenda kuvaa Miguuni,kuna Mikanda, Bangili,Hereni naa........,Jee wewe Unapenda/Ungependa Uvae/Avae wapi?Wengine wanapenda za Bendera ya Taifa na......Vyovyote vile ilimradi SHANGAAA!.
Kitamaduni zaidi au Vipi?

Karibuni sana Waungwa!!!!!

Tuesday 24 January 2012

Siku kama ya leo da'Nancy Alizaliwa!!!!!!

Siku kama ya Leo miaka kadhaa iliyopita,Da'Nancy Bibi ya Nyotu Alizaliwa!!!
Tunakutakia kila la kheri na baraka katika maisha yako,Mungu azidi kukubariki sana,
Upendo,Utu wema,Fadhili,Busara,Ucheshi na Mengine mengi Mungu amekujalia dada Nancy.
Wewe ni Rafiki wa nyakati zote kwa shida na Raha,Kupitia wewe nimejifunza meeengi sana sana.
Uwe na wakati mwema kila iitwapo Leo.
Familia ya Isaac Tunakupendaaa na kukuthani sanasana sana.
Mungu awe nasi Daima.




Wednesday 18 January 2012

Ulale kwa Amani da'Regia!!!!!



 Poleni sana Ndugu,Jamaa,Marafiki na Taifa pia.Bwana alitoa na Bwana Ametwaa.

Monday 16 January 2012

Utafiti;Eti kuangalia TV kwa saa Moja kunapunguza dakika22 za Maisha Yako!!!


  • Ukifuata kila linalosemwa na wanasayansi utashindwa kuishi. Leo watasema kunywa kahawa kunapunguza msongo wa mawazo. Kesho watasema kunywa kahawa  huko huko kunaongeza shinikizo la damu na uwezekano wa kupata pigo la kiharusi. Leo watasema hiki na kesho watasema kile ali mradi ni vurugu tupu. Kibaya zaidi ni ukimya wao kuhusu nini cha kufanya hasa pale tafiti zao zinapotoa matokeo yanayokinzana
  • Kwa vile nyingi ya tafiti hizi hufanyika huko Ulaya na Marekani, Waafrika inabidi kuyapokea matokeo ya tafiti hizi kwa uangalifu sana kwani huwa hayazingatii mazingira yetu na mtindo wetu wa maisha (japo sasa tunajitahidi sana kuwaiga kwa kila kitu).  
  • Utafiti uliofanywa mwaka jana na wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Queenesland unaonyesha kwamba kuangalia runinga kwa watu wenye umri wa miaka 25 na kuendelea kuna madhara makubwa kiafya na kunapunguza muda wa kuishi. Utafiti huu unaonyesha kwamba kwa kila saa moja unayoitumia ukiangalia runinga basi unajipunguzia dakika 22 katika maisha yako. Hii ni sawa na kuvuta sigara mbili. 
  • Wanasayansi hawa wanasema kwamba tatizo hasa siyo kuangalia tv bali madhara ya kukaa mahali pamoja kwa muda mrefu ambako kunasababisha magonjwa ya moyo, kisukari, kunenepeana na matatizo mengine ya kiafya yanayosababishwa na mtindo wa maisha ya kubweteka (sedentary lifestyle). Kufanya mazoezi, hata kama ni dakika 15 tu kwa siku ni jambo la muhimu na kumeonyeshwa kuwa na faida nyingi za kiafya ikiwemo kuongeza siku tatu katika maisha yako.
              Kusoma zaidi habari hii ingia kwa  Blog ya kaka Matondo[MMN]http://www.matondo.blogspot.com
                                   Ahsante kaka Matondo.

Saturday 14 January 2012

Siku kama ya leo kaka Isaac Alizaliwa!!!!!!

Siku kama ya Leo miaka kadhaa iliyopita, Kaka Isaac, babake  Sandra na Tracey,Mume ya MadameRachel-siwa,Alizaliwaaa!!!
Tunamshukuru sana Mungu kwa yote juu yako,Mungu akubariki na kukulinda kila inapoitwa Leo.
Akuongezee Miaka Mingi na Ufanikishe malengo yako.Uzidi kuwa Baraka kwetu na Kwa Watu wote.
 Tunakupenda saaana,Wako Rachel,Sandra,Tracey[ Rasca].


Friday 13 January 2012

Wanawake na Urembo!!!!!!!!






Nimatumaini yangu woote wazima,
Haya Waungwana Wanawake na Urembo! Kuna mengi kwenye hizi picha na kwa Wanawake kwa Ujumla,
Mimi leo si msemaji saana,Kazi kwenu nyie na Mitazamo yenu,kipi wewe umependa hapo/Kukuvutia na kipi hujapenda hapo,yaani kama ingekuwa wewe hapo ungeongezea nini au ungepunguza nini,Pia wewe Mwanaume kama ni Mkeo,dada,shangazi na...Ungependa nini aongeze au  apunguze nini?Na jee labda unapenda lakini hujui ufanyeje uwe/awe kama hivyo,au kunakingine unapenda hapo hakipo,Basi usisite kusema/Kutoa Mawazo,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Karibuni sana.


Tuesday 10 January 2012

Wazazi /Walezi wa sasa na Malezi!!!!!!




                        watoto kutusaidia jikoni.

kusafisha vyumba vyao.

kusaidia kusafisha na sehemu nyinngine
Wabaki na Furaha/Amani.
Ni matumaini yangu wote wazima,
Haya wapendwa,Wazazi/walezi wenzangu,vipi watoto kufanya/kusaidia kazi za nyumbani,
Hii imekaaje/wewe unaonaje?kazi kama kusafisha vyumba,kuosha vyombo,kuaanda vyakula na kazi nyingine nyingi,Jee wewe unafikiri ni Umri gani uliosahihi kwa mtoto kuanza  kumfundisha kazi ndogondogo?naje huu ni Unyanyasaji au ni malezi ya kawaida? naje Kuna kazi za watoto wa kiume na wakike?kama ndiyo jee sisi wenye watoto wa jinsia moja je?Unafikiri watoto wote wanapenda kazi? je kama hataki?.
Mimi binafsi kazi nyingine sikuwa nazipenda kufanya nilipokuwa mtoto,lakini mama alikuwa ananilazimisha, jee alikuwa ananikosea au ndiyo malezi?Jee wewe unapenda/ulipenda kazi zote ufanyazo/ulizokuwa unafanya?.
Mwana Umleavyo ndivyo akuavyo au.......

Karibuni sana Waungwana katika kusaidiana Kimawazo,Kujadili na Kuelekezana kwa Upendo!!












Thursday 5 January 2012

Waswahili na Maisha yao-Coventry Swahili Party/Mwaka Mpya[shukrani]!!!



                             Asanteni sana  Swahili dadazzzz.
                                   dada Esther Asante.
                                      Wapendwa Mungu awabariki sana.
                                       Mbarikiwe Malongazzzzz.
                                    Ahsante sana mamaKisa.
                                       Ahsante sana Dj Rik/blogger wa the network.





                   Chakula; Nyama choma na vyote,Vimepikwa kwa  da'Batuli.
Ahsanteni sana wote kwa Upendo na kutoa Muda wenu kwa kujumuika nasi ,  Mungu awabariki sana,Tunawatakia kila lililo jema.Kwaniaba ya da'Maggie ,da'Vick na Familia yangu,TUNAWAPENDA SANA.