Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 30 September 2011

Ubatizo wa da'Arianna,Uliofanyika Tanzania!!!!!!

                             Da'Arianna na mapozzzz.
                    Siku zote uwe Nuruni.
        Shangazi akiwa sambamba na mtoto wake,Hatimaye Arianna anabatizwa.
                          Kwajina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu Amina!!
                    Mama Arianna kama anaota vile.
                         Familia pande zote 2, walikuwepo.
                       Familia sambamba na Mpendwa wao.


                 Mashangazi wa Arianna, wapo Makini.
                           Mjomba na Shangazi wakifurahi.
              Nakuaminia  MAHOZA hapo huhitaji msaada.
                 Kula mama mimi penda sana wewe Rafiki yangu.
                      Kula kwa niaba ya baba, mimi penda sana wewe ba'Mdogo.


             Asante sana mama kwa kunisababishia haya , baba yako inakuja hukohuko.
             Arianna mwanangu tumemaliza ehh, Ndiyo mama, yaani nilikuwa naogopa.


Arianna;  Ali BATIZWA katika kanisa la KIANGLIKANI  MAGOMENI,DAR-ES-SALAAM, TANZANIA.
Baadae walielekea kwenye Sherehe ya kumpongeza kwa UBATIZO na Kufika kwake TZ.


Ujumbe kutoka kwa Wazazi wa Arianna;Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa jambo hili na mengi mema aliyotutendea.Pia Tunawashukuru sana Wazazi wetu,Ndugu,Jamaa na Marafiki wote,kwa yote.
Mungu awabariki sana sana.


   :Swahili na Waswahili inakutakia maisha mema da'Arianna na Hongera sana,
    na pole sana huku kucheza kama Bongo sahau, lakini Mchanga unauzwa hata Tesco mwanangu.





Wednesday 28 September 2011

Utenzi wa Uhuru.Mpemba na Mchaga Wote ni kitu Kimoja!!!!!

KAPINGAZ Blog na JEZI ZENYE LOGO YAO,KAA MKAO WA KUVAA.!!!






KAPINGAZ Blog SIO MUDA MREFU TUTAKULETEA JEZI ZENYE LOGO YETU KAA MKAO WA KUVAA.

Mfano wa Jezi itakayokuwa na Logo yetu, karibu sana mdau.

Jezi hizi zitakuwa zikigawiwa Bure, haziuzwi. Kama utahitaji usisite kuwasiliana nasi mapema kupitia mawasiliano yetu yaliyopo kwenye Blog. Tunashauri ni vema ukatumia Email ili tuweza kuwa na kumbu kumbu nzuri badala ya simu

Mtoto Cecilia Edward Aenda India kwa Matibau!!!!!!!









Meneja wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Hamid Abdulkarim akiwa amemshika mkono Cesilia Edward (14) mwenye tatizo la moyo linalosababisha kuvimba tumbo akitoka Hospitali ya Regency jana tayari kwa safari ya New Delhi, India kwa matibabu.






CECILIA AWASHUKURU WATANZANIA
   Mtoto Cecilia Edward ambaye anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo uliopelekea kuvimba kwa tumbo amewashukuru kwa moyo mkunjufu watanzania waliojitokeza katika kumsaidia kwa hali na mali mpaka kufanikiwa kupata hela tayari kwa matibabu anayotarajia kwenda kuyapata nchini India.
   Cecilia amesafiri kuelekea katika hospitali iitwayo Fortis inayopatikana New Delhi -India kwa matibabu, jumatatu ya tarehe 26 mwezi septemba mwaka huu.
   Aidha walezi wa Sesilia familia ya mzee Kambaliko inatoa shukrani zake za dhati kwa watu wote waliojitolea kwa moyo kumsaidia binti yao kwa kutoa pesa, mavazi na hata waliowapa maneno ya faraja pamoja na wale wote wanaoikumbuka familia hiyo katika maombi.
   Kabla ya safari yake hiyo, hali ya kiafya ya sesilia ilikuwa ikiendelea vizuri, kwani alikuwa anaweza kupumua na kukaa, tofauti na awali kutokana na kupunguzwa kwa kiasi cha maji katika tumbo lake hospitalini Regency alipolazwa kwa ajili ya matayarisho kabla ya kuanza safari yake kuelekea nchini India kwa matibabu zaidi.
   Mtoto huyu aliondoka hapa nchini jumatatu ya tarehe 26 na ndege ya shirika la Quatar Airways akifuatana na daktari mmoja kutoka hospitali ya regency, pamoja  na mlezi mmoja mpaka nchini India alipotarajia kupokelewa  na madaktari tayari kwa uchunguzi wa kina na kisha kuanza matibabu yake.
   Kipindi cha Mimi na Tanzania kinapenda kuwashukuru Watanzania wote pamoja na makampuni mbalimbali yaliyojitolea katika kumsaidia Sesilia kwa ajili ya matibabu. Shukrani za pekee ziifikie hospitali ya regency hasa daktari Kanabar kwa uvumilivu na huduma nzuri kwa Sesilia. Pia kwa mchango wao wa kulipia nauli ya kwenda nchini India kwa Sesilia, mzazi na daktari ikiwa ni pamoja na matibabu ya awali anayoyapata hivi sasa.
   Watanzania, pamoja tumeweza tena. Sesilia ni mmoja tu kati ya watoto milioni moja wanaosumbuliwa na tatizo hili, hebu tujitolee kuwasaidia watoto hawa bila ya kuchoka, pia tusimsahau binti huyu kwa maombi ili upasuaji anaotarajia kufanyiwa umalizike salama na kwa mapenzi yake Mungu mtoto huyu arudie katika hali ya kawaida kama watoto wengine.
Mungu mbariki Sesilia.Amen!
        :Swahili na Waswahili tunakuombea cecilia,Mungu asimamie Matibabu yako na upone haraka.


Habari hii kutoka kwa Zainul.A.Mzinge wa www.mohammedewji.com/blog.





-

Monday 26 September 2011

Kaka Joel Atimiza Miaka 5!!!!!!!!

             Mwenyewe kaka Joel.
             Kaka Joel akiwaza juu ya miaka 5.
            Akikata keki na da'Tracey akishuhudia.
            Kaka Vin ndiye aliyetuongozea sala ya Chakula.
           da'Manjula akiwa kwenye Sala.
             Hakukuwa na Shani leo ni juisi.
         Kama kawaida ya da'Damari yupo makini kwa watoto.
            da'Damari akihakikisha kila mmoja hakosi keki.
        Mwenyekiti na msimamizi mkuu wa watoto wa Swahili Fellowship, da'Mija Mwanamke wa Shoka.
   da'Josephine ,Mdhungu Mswahili mwenye vituko alikuwepo.
    Wamama waliwakilishwa na Mke wa Mwenyekiti wa Swahili Felloship da'Edna.


Familia ya Bwana Godfrey[Mzee wa Fellowship] na bibi Mellanie wa Coventry,U.k.
Wanamshuru sana Mungu kwa kumtunza mtoto wao Joel na Mungu azidi kumsimamia katika makuzi yake,
Awe baraka kwao na kwa Jamii pia.
Shukrani za pekee ziwaendee Watoto wote wa Coventry Swahili Fellowship,Mwenyekiti da'Mija na msaidizi wake da'Damari, Bila kuwasahau Wazazi/Walezi na wote waliofanikisha sherehe ya kaka Joel.
Mungu awabariki sana na wanawapenda sana.

Familia ya Isaac na Cuthbert wa Coventry nao wanamtakia kila lililojema kaka Joel na Mungu awenawe daima,Pia wanasema asanteni sana Familia ya Godfrey kwa yoteeeee!!!Mungu awaongezee kila inapoitwa Leo.


Mengineyo; Kaka Joel anapenda sana Magari na kuyajua mnoo,Mpaka ananishinda mimi jamani, kila aonapo Gari  alipendalo atakwenda kumwambia Mjomba Isaac na Wazazi wake, kutwa anatafuta Magari kwenye Computer, kama uonavyo hapo kwenye keki alikosa Gari kapachika ka'Pikipiki.


Swali; je kupenda huku ni kwasababu ni mtoto wa kiume,akikua anaweza kufanya kazi ya Udereva au zinazohusiana na Magari au ni Utoto tuu akikuwa ataacha?.

Wewe mpendwa kunakitu ulikuwa unapenda wakati wa Utoto na mpaka Leo unakipenda/kukifanya?
Karibuni sana!!!














Saturday 24 September 2011

Mshumaa uliozimika.Leo ni BRENDA FASSIE, Sikiliza (Vul'indlela / ...!!!

Mungu wape Faraja  Yatima ,Wajane na  wote walioondokewa na wapendwa wao.

Tuesday 20 September 2011

kweli kulea Kazi!!!!!!!

Hata sijui nini anatafuta huko jamani, Mmmmhhh Tumetoka mbali sana.
Mpendwa unayakumbuka makabati ya vyombo ya Zamani yenye wavu kama wa dirisha?
mama yangu aliweka Ufuta huko,umetengenezwa kama vigorori hivi,mimi na kaka yangu tulikuwa tunautaka,
mama akasema tutapewa tukimaliza kula chakula,tumemaliza chakula mama kaondoka,lakini tunajua ulipo,mwenzangu  mimi nikaambiwa niupandie, hahahahaha kama wewe BINGWA panda,Sifa zikaniponza, nikaupandia weee nikala mweleka wa nguvu na kabati juu yangu, wenzangu wakatimua mbio,badala ya kuniokoa, Sasa na huyu naye yange mkuta yaliyonikuta jee? Kweli Kulea Kazi jamani, Wazazi /Walezi tuwe makini sana na Watoto.

Mpendwa huna kisanga kilichokukuta unachokumbuka?
Hujapitia mambo yakutaka  kuwa Bingwa/Mshindi?.

Karibuni sana.











Sunday 18 September 2011

Siku kama ya Leo dada Levina Alizaliwa!!!!!!!

Leo ni Siku muhimu kwa  da'Levina Kimwaga.
Siku kama ya Leo familia ya Bibi na Bwana Kimwaga, Walipata mtoto wa kike na Wakamwita LEVINA!!!


Tunakutakia kila la kheri,Baraka na Mafanikio kila inapoitwa Leo.


Mungu awe nawe daima.
Karibuni Waungwana Tuduwage pamoja.





Saturday 17 September 2011

Pole Zanzibar PoleTanzania!!!!!!!!

Ukatili Mbeya!!!!!!!!

VITENDO HIVI VYA KIKATILI VYA WATU KUPIGWA NONDO VITAISHA LINI MBEYA?

Bwana Elia Daudi Mwalonde mkazi wa Uyole akiwa hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya wodi namba 1 baada ya kupigwa nondo hivi karibuni.

Bwana Zefania Mwangwale mwenye umri wa miaka 31 mkazi wa Uyole akiwa katika hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya baada ya kupigwa nondo pia.

Vitendo vya watu kupigwa nondo kwa Jiji la Mbeya vimekua kama ni vitendo vya kawaida, ni jambo la kusikitisha sana kwa sababu kila mwaka lazima hivi vitendo vitokee na kupelekea watu wengi wa jiji la Mbeya kuishi katika maisha ya wasi wasi sana.
KAPINGAZ Blog inapenda kuviomba vyombo vyote vya usalama Jijini Mbeya kuona kama hivi vitendo kama ni janga kubwa kwa watu wa Mbeya.

Thursday 15 September 2011

Waswahili Wetu Leo, Mkubwa na Wanawe/Miaka50 ya Uhuru!!!!!!!!

Haya Mpedwa wewe umejiandaaje na Miaka 50 ya Uhuru?
Sikiliza hayo maneno ya Waswahili, Chura anapenda Maji lakini si ya Moto.
Watoto wa Kiswahili wanatimbwilika/kucheza.Tanzania Kiroho Safi!!!!!!
Je wewe una Amani, Uko Huru? Kila la Kheri.

Wednesday 14 September 2011

Wanaume na Mitindo,Leo tupo Igunga!!!

                       Huyu baba kavaa shanga na katupia kikoi.
                Kijana Kasuka,shanga hakukosa na katupia kikoi,anasalimia kwa mapozi kabisa.
              Hawa wamejifunika vikoi, sijui hii ya mwisho nyeusi ni kaniki au....
Haya wapendwa Leo tupo Igunga,Tanzania.Kama uonavyo wanaume wa huko na Mitindo.
Sijajua kama hii ndiyo Mitindo ya Asili au yakisasa,Maana nasikia kunamitindo ya Asili,kama ndivyo,
Hongereni kwa kuendeleza Mila ambayo wengine wanameacha.

Wapendwa sina la zaidi nawasikiliza ninyi, Vipi kuhusu mitindo hii wewe unaionaje?
Na je kama Mitindo hii niya kiasili vipi kwenye Harusi au Sherehe za Kitaifa mtu akitinga si itakuwa mwake?





Karibuni sana Waungwana.











Saturday 10 September 2011

Poleni sana Wapendwa wetu Zanzibar,Mungu awatie nguvu kwa wakati huu Mgumu!!!

MELI YA LCT SPICE ISLANDERS YAZAMA KATIKA BAHARI YA HINDI PWANI YA NUNGWI LEO USIKU.



Meli ya LCT SPICE ISLANDERS imebinuka na kuzama katika Bahari ya Hindi huko Pwani ya Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja ikielekea Pemba.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu, Issa Haji Ussi amesema tukio hilo limetokea saa 8:30 za usiku ambapo meli hiyo ilikuwa imebeba abiria 610 pamoja na mizigo.
Naibu Waziri huyo amesema meli hiyo imeondoka katika Bandari ya Malindi Unguja ikiwa katika hali ya uzima,lakini katikati ya safari ikapata hitilafu na kusababisha kubiruka na hatimaye kuzama.

Hadi sasa haijaweza kufahamika idadi kamili ya watu waliofariki,lakini vyombo vya uokozi vimefika katika eneo la tukio kutoa msaada.

Naibu Waziri Issa amesema Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya usafiri vya binafsi boti ziendazo kasi zimekwenda eneo la tukio kutoa msaada unahitajika.Jeshi la Polisi Tanzania limetuma Helkopta yake kwenye eneo la tukio

Awali, amesema Mamlaka zinazohusika zilipata taarifa za kuzama kwa meli hiyo baada ya Meli ya Mv Jitihada inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuripoti kuzama kwa meli ya Spice Islanders ambayo ililazimika kukatisha safari yake kuelekea Kisiwani Pemba na kwenda kwenye tukio.

Serikali imesema taarifa zaidi zitakuwa zikitolewa na wananchi wameombwa kuwa watulivu.

Habari kwa msaada wa Kapingaz.

Wednesday 7 September 2011

Watoto wa Shule na Tamaa!!!!!

                       Hawa wanandika kwenye ubao na chaki.
                                  Hawa wanamsikiliza mwalimu kwa tabasamu.
                                Hawa wamenyoosha mkono ili wapewe nafasi ya kujibu/kuuliza.
Baadhi ya Shule  zimeshafunguliwa hapa U.k.
watoto wa shule kila kona sasa, lakini baadhi yao walivyo jiremba mmhh,
mpaka  kugundua kama ni mwanafunzi ipo kazi.

Hili pia lipo kwa baadhi ya shule Afrika/Tanzania, hasa hizi shule za kulipia.
Sijui ndiyo kwenda na wakati auu....... Ninawaza tuu!!!!!


Mpendwa unafikiri kwa nini  baadhi ya watoto wa Shule wanakuwa na Tamaa?[1].Ni utoto tuu wakikuwa wataacha,Kutoridhika na maisha yao au...?[2.] Nivyema kwa watoto wa Shule kuvaa sare za shule au kutovaa sare kila mmoja aje na nguo zake?
[3.]Kupata chakula cha aina moja Shule au kila mtu ajitegemee.

Karibuni sana kwa Maoni,Kuelimishana katika malezi ya watoto wetu!!!!!!