Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 30 August 2011

Nawatakia Eid Mubarak . Tunapo kula na kunywa, Tusisahau na Wenye Shida!!!!!

Nawatakieni kheri na Baraka  wakati huu wa Eid na Siku zote!!!
Tunapokula na Kunywa, Tusiwasahau Wenye Shida na Tabu, Wagonjwa,Wajane na Yatima, Waliomagerezani pasipokuwa na Hatia.Tugawane tulichonacho ili Tufurahi pamoja!!!!!

Mungu Atubariki Sote.

Saturday 27 August 2011

Jikoni Leo ni kwa da'Maggie!!!!!!!!!

             Chapati,Maandazi,Vitumbua.
                   Kitu cha chapati.
                                Kitu cha maandazi.
                         Kitu cha Vitumbua.


Mmmmhhh Sina lakusema zaidi nakuachia wewe Mpendwa uliye Tembelea hapa, nini unapenda hapo na unapenda kushushia na nini.
Mimi zamani nilifikiri wanaojua kupika Vitumbua ni wazee tuu, kumbe laaaa.
Pia nilikuwa najua Mama yangu tuu ndiye mpishi mzuri!!!!!


Huko Ilala kuna mama alikuwa anapika Vitumbua mpaka tukamwita mama Tatu Vitumbua.


Swali kidogo, Hivi mpishi mzuri kwenye familia anaweza kurithisha na wengine?.


Karibuni Wote.

Wednesday 24 August 2011

Mswahili Wetu Leo ni Mh; Balozi Mama Mwanaidi wa Maajar!!!!!!!




Mh; Mama Mwanaidi  Maajar; Aliongea hayo kwenye Semina ya Kina mama wa THE WAY OF THE CROSS GOSPEL MINISTRIES CHURCH.
Mpendwa baada ya kumsikiliza mama Maajar, Je  umejifunza nini?.Sikiliza kwa makini sehemu ya 1 na ya 2.

Karibuni sana kwa mawazo/maoni na kuelimishana zaidi katika kipengele hiki cha, Waswahili na Maisha yao ,Kupitia hapa Swahili naWaswahili.

Habari  kwa msaada wa DjLuke wa  Vijimambo.



Saturday 20 August 2011

Miriam Atimiza Miaka 3!!!!!!!!!

                      Da'Miriam katika poziii.

                                    Keki zote za Miriam.


                       Akijaribu kuzima huku akiogopa.
                               Miriam akisaidiwa kukata keki.
                        Nakupenda sana mama chukua hii,wapambe wakishuhudia.
                            Miriam, Nami nakupenda sana mwanangu nawe kula eehh.
                        Huyu alilishwa kwa niaba ya watoto wa kiume.
                               Na kwaniaba ya watoto wa kike naye alilishwa huyu.
   Mwenyekiti wa wanaume wa Coventry Swahili Christian Fellowship,Alihakikisha kila mtoto anapata keki.
 Mwenyekiti wa watoto wa Coventry Swahili Christian Fellowship,Akishughulika.
                       Watoto wa Kiswahili wakipata chakula.


    Mama hapo akishushia na maji ,Watoto wakifurahi kwa kumaliza vyema na walifungashiwa.
Da'Miriam na mama yake wanasema Asanteni sana kwa kuungana nao katikasiku hii Muhimu kwao.
Pia Shukrani za pekee ziwaendee wana Coventry Swahili Christian Fellowship na Wageni wote.
Anawapenda sana na Mungu awabariki.


Nasi Swahili naWaswahili,Tunakutakia maisha mema na yenye Amani siku zote!!!!!!!

Thursday 18 August 2011

Jikoni Leo ni Mihogo!!!!!!!!

        Hapa ni mihogo  iliyotiwa/kuungwa nazi ipo Jikoni .
             Hapa imepakuliwa na ipo tayari kwa kuliwa.
       Hii ni Mihogo  iliyo chemshwa/ya kuchemshwa.
    Hii ni Mihogo iliyokaangwa/yakukaangwa.



Mpendwa Leo ni Mihogo,kuna mapishi mengi katika Mihogo,wengine wanapenda Kuchemsha,Kukaanga,Kutia/Kuunga nazi.
Pia hiyo ya nazi kuna wanaochanganya na Maharage au Kunde .....n.k,Pia kuna wanaokula kwa Samaki au Mchuzi wowote.


Hiyo ya kuchemsha,kuna wanaokula kwa Kachumbari.
Kuna hii ya Kukaanga duhh hii inanikumbusha sana Shule!!Kuna wanaokula kwa Chachandu,Pilipili ya Unga,Chumvi na.....


Wewe unapenda Mihogo? Je Hupendelea ya aina gani na Kula au kuongezea na nini?.
Kinywaji gani pia unapendelea kushushia?


Karibuni sana Waungwana katika Jikoni Leo.
Nanyi  pia mnaruhusiwa kutuma/kushiriki nasi, Nini unapenda au unapika.
Tuma kupitia Rasca@hotmail.co.uk.


KARIBUNI WOTE!!!!











Monday 15 August 2011

Waswahili wa Mji wa Cork,Ireland na Futari ya Pamoja!!!!!

                         Mji wa Cork katika picha.
     Wanawake wakipika na kina baba wakijiandaa kupokea wageni.
           Waandazi/waandaaji wakiwa tayari.
              Waswahili hawa nao walikuwepo.
         Watoto wa kiswahili wametulia.
   Shekhe akisisitiza Upendo na Umoja kwa Waswahili.
     Waswahili wakisaidiana ili mambo yawe sawa.
         Kina mama na kina kaka wakiendelea na maandalizi.
 Wakiendelea na Futari.
         
  Kina mama wakishughulika.
    Lete Uji hapa!
    Vipi mko sawa!
    Baada ya kumaliza msosi.
   Wakisikiliza maongezi.
    Watu wa karibu baada ya wageni kuondaka wakijipongeza!
                                      Maalim akitoa Shukrani kwa wote waliofika na wasiofika,Mungu awabariki sana na kuwaongezea kila lililo jema na Amani.Anawatakia Funga njema na anawapenda wote.

Shughuli hii ya Futari ya pamoja iliandaliwa na Maalim picha ya chini mwenye kanzu.Kwa kumshukuru Mungu na kuunagana na familia,pia kuwashukuru Wasawhili na jamaa zake kwa kuwa naye pamoja kwa kila jambo.

Thursday 4 August 2011

Mswahili Wetu Leo ni Bi Zaituni wa Mrisho; Anaishi ILALA!!!!!!!

Bi Zaituni wa Mrisho katika Picha ndiyo Mswahili wetu wa Leo,Anaishi Ilala mtaa wa Mwanza.
Bibi huyu ana hadithi na habari nyingi sana za maisha na siasa,Leo  anaongelea kuhusu ULIMBUKENI!!
Anasema watu wanaharibikiwa sana kwa kukataa yote ya zamani na kuingia kwenye mitindio mipya tuu,kwamba si yote mapya mabaya la! bali na yazamani pia yakumbukwe hasa yale mazuri, Na tuwe tunawafundisha watoto wetu,Asema utakuta mtu kazaliwa na kukulia kwenye familia ya kiswahili lakini mwaka mmoja tuu akienda nje ya nchi,anajifanya kasahau kabisa Kiswahili, mara oohh yah oohh yes, pia hawapendi hata watoto wao wanaowazaa huko au kukulia huko kuwafundisha KISWAHILI, tena na kujisifia wakipiga simu huku nyumbani mwanangu hajui/kasahau kabisa Kiswahili,Kama baba na mama Waswahili iweje mtoto wako asiongee Kiswahili?
Mwisho anawatakia Waislam wote duniani Funga njema yenye baraka na amani.

Nami nasema Ahsante sana bi Zaituni  wa Mrisho na kaka Mtaruke[mjuukuu wa binti Mrisho] yeye ndiye aliyetuunganisha na BIBI huyu.
Haya wapendwa Waswahili neno hilo kutoka kwa bibi unalionaje? Karibuni sana kwa kuchangia,kuelimishana  na.....
Kama una lolote jema na kuelimishana , Unataka kuwaambia Waswahili wenzio karibu  sana unaweza kutumia email hii Rasca@hotmail.co.uk. katika kipengele hiki cha Waswahili na Maisha yao ndani ya Swahili na Waswahili.
Nawatakia Swaumu njema kwa Waliofunga!!

Monday 1 August 2011

Siku kama ya Leo Rachel-Siwa Alizaliwa!!!!!!!!

Siku kama ya leo, Familia ya Bibi na Bwana M.S. Kiwinga walibahatika kupata mtoto  wa kike ;Rachel-siwa.
Nawashukuru sana Wazazi wangu kwa Malezi yenu mema na  yote mliyonitendea.
Pia nakushukuru sana kaka yangu R.Kiwinga kwa kupokea ulezi na kunitunza, Tangu pale Baba alipofariki mpaka pale uliponikabidhi kwa Mume,Sina cha kukulipa bali sitoacha kukuombea.


Ahsante sana Mume wangu Issac kwa yote na kuwapamoja siku zote mpaka 27/07/11 yaani j'tano iliyopita tumetimiza miaka 15 ya ndoa yetu,Mungu atubariki sana katika maisha yetu.

Basi niwashukuru Ndugu,Jamaa,Marafiki zangu woooooteee, kwa Yote,kwani nikiandika hapa hapatatosha.


NENO LA LEO; Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika,kama sina Upendo,nimekuwa shaba iliyo na upatu uvumao.Tena nijapokuwa na unabii,na kujua siri zote na maarifa yote,nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina Upendo,si  kitu mimi.Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina Upendo, hainifaidii kitu. Upendo Hufadhili; Upendo Hauhusudu; Upendo Hautakabari; Haujivuni; Haukosi kuwa na adabu; Hautafuti mambo yake; Hauoni uchungu; Hauhesabu mabaya; Haufurahii udhalimu,bali Hufurahia pamoja na kweli.!!!


MUNGU ATUBARIKI SOTE!!!!!!!!!