Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 5 November 2011

HATARI ILIYO MBELE KWA WAMACHINGA WANAOONGEZEKA KWA KASI KATIKA MATAA YA UBUNGO SERIKALI MNAIONA?

Trafiki Polisi akiongoza magari katika junction kubwa ya Ubungo, maarufu kama Ubungo Mataa.

Fuso ikiwa imeingia katika moja ya mtaro mkubwa ulioko bara bara ya Ubungo karibu na Ubungo mataa.

Kwa kipindi kirefu sasa eneo la Ubungo karibu na Mataa ya kuongozea magari yanayo ingia Jijini au yale yanayotoka pande mbili, mengine yakitokea Mwenge na mengine yakitoke Buguruni na kwenda sehemu mbali mbali za jiji limevamiwa na wafanya biashara ndogo ndogo maarufu kama Wamachinga.

Nimejaribu kulifuatilia kwa kipindi kirefu ili kuweza kujiridhisha kujua kama wamepewa ruhusa na nani kufanya biashara katika eneo lisilo rasmi, nilijaribu kuongea na wamachinga wachache; wa kwanza anaitwa Salum Ramadhan anauza taa za kichina katika eneo hilo, yeye alidai hawajaruhusiwa na mtu kufanya biashara hapo ila ni kutokana na ugumu wa maisha ndio umewapelekea kufanya biashara katika eneo hilo na wa pili naye Ndg. Deogratius Shirima akasema maneno hayo hayo ambayo hayapishani maana na huyu wa kwanza.

Sikuishia hapo nikataka kujua je kuna mtu yeyote ambaye anakuja kukusanya japo ushuru kutoka kwao? nao kwa pamoja wakasema kuna mtu huwa anakuja kukusanya ushuru lakini wao hawana uhakika kama ni kutoka Serikali za mitaa au la! nikawauliza swali jingine, huyu jamaa ambaye ameweka jenereta hapa na kuwapa huduma ya Umeme mnamlipa Sh. ngapi? wakasema kila taa 1 ni Sh. 1000/- nikapenda nijue sasa swali langu la msingi, wanajua HATARI iliyo mbele yao kutokana na kufanya biashara kando kando ya bara bara kubwa kama hii ambayo inapitisha magari mengi na hasa mengine yanakuwa yako kwenye mwendo wa kasi! wakasema wanaifahamu ila hawana jinsi wataenda wapi na maisha yenyewe ni magumu!
Kwa kweli nilitoka bila kuwa na jibu sahihi nini hatma yao kama gafla gari likitoka kwenye bara bara na kuwavama. 
Tatizo hili naamini serikali wanaliona ila wanalifumbia macho na pindi ajali itakapo tokea ndio wanafumbua macho na kujua sehemu sio halali, ni vema serikali ikalichukulia hatua mapema kabla halija tokea la kutokea. Tumekua tukiona sehemu mbali mbali ajali zinatokea na kuua watu wengi ambao wapo kando kando ya bara bara kwa hiyo ni vema Serikali ikachukua tahadhari mapema.

             Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog.
Asante sana.

2 comments:

ray njau said...

Hii ndiyo hali halisi ya waswahili katika mikikimikiki ya kufikia maisha na mafanikio bila ya tahadhari yoyote.

Rachel Siwa said...

ni kweli kaka yangu, sasa wanaweza hata wasifikie walitakalo naona kama Hatari imezidi zaidi ya Mafanikio.Asante kaka na karibu tena.