Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 7 November 2011

Da'Arianna Atimiza Miaka 3!!!!!!!

                     da'Arianna  kasimama tayari.
                           Kitu  cha kekiii.
              Mwenyekiti da'Mija akiandaa kekii.
                                 Arianna na mama'ke wakifurahia.
                          Mama Arianna akimsaidia kukata keki.
                              Kula mwanangu weee.
                                Dadazzzzz wakitabasamu.
               watoto wakibadilishana mawazo.
                  dada unajua mchezo huu?
                 Watoto wa Swahili Fellowship, wakisubiri kekii.
                  wametulia wenyewe.
                                    Watoto wanatabasamu naona mambo yalianza kusogea.
                       Watoto waliitikia mwaliko.
                        Mama kula eehhh,mama alikula mwishoni baada ya kuhakikisha watoto wote wamepata keki.

Familia ya bibi na bwana  Jonathan Mbwambo wa Coventry U.K.
Wanamshukuru sana Mungu kwa Mema mengi aliyo watendea, Moja  kati ya hayo ni kumlinda mtoto wao mpendwa da'Ariann mpaka leo Ametimiza miaka 3, Mungu ni Mwema sana.
Pia wanapenda kutoa Shukrani kwa Wazazi  na Watoto wa Coventry Christian Swahili Fellowship,na Wote waliojumuika nao.Shukrani za Pekee zimwendee Mwenyekiti wa Watoto da'Mija na Kamati Yake.
Mungu awabariki wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine.
Familia tunasema Asanteni sana kwa Moyo wenu na Mungu awe nanyi daima.


WENU KATIKA YOTE NA TUNAWAPENDA SANA.



         NASI SWAHILI NA WASWAHILI TUNAMTAKIA ARIANNA MAISHA MEMA YENYE AMANI NA FURAHA TELEEEEEEE.





5 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Hongera sana Arianna kwa kutimiza miaka 3. Mungu akulinde uwe na afya njema na hongera wazazi!

Goodman Manyanya Phiri said...

Wala sikupi hongera, Arianna; kwani ni umri mgumu huu. Sasa utaanza kufukuzwa mbele za wakubwa kila wakianza kuongea siri zao...!


Pole sana, mwanangu!

Mija Shija Sayi said...

Hahahahaa! kaka manyanya hiyo kali...

Hongera Arianna..

Anonymous said...

Hahahaahaha jamani yaani huyo kaka hapo juu kanichekesha mpaka basi...lakini nikweli kbs maana wanakamata maneno sana hawa watoto wa umri huu...

emu-three said...

NA sie wana Diary yangu Tunamtakia ARIANNA Maisha mema ya fanaka na baraka teleeee.