Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 28 November 2011

Wanawake na Urembo!!!!!!!!

                        Huyu kapaka sijui manjano.......
                        Huyu kawa wa pinki
                        Huyu na manyonyo
                                               Huyu kakaba shingo
                                                Huyu kachora .
Haya Wapendwa Wanawake na Urembo,kila siku yanazuka mapya,Pia ya Zamani yanarudi kama si kukumbukwa.Nao zamani kulikuwa na yao mengi tuu,Zazuu,Kuchoma nywele,Kusukia Rafya[sijui kama nimepatia]na Mengine Meeeeeeengi.

Wasasa kuna wanaopenda Maziwa makubwa mpaka kuyaongeza,Kujichubua/Mkorogo,Kujichora kwa sasa si hina tuu kuna Tattoo tena mpaka kwenye Nyusi, Wananyoa na kuweka tattoo ili wasipate shida ya kupaka Wanja.Kuna wanaoongeza Kope,Kunakuweka Vidubwasha ndani ya macho  na kubadili Lenzi kuwa kama ya Wadhungu. Na Mengine meeengi labda sikuweza kuyaandika au Siyajui Yote hayo kwa SABABU YA UREMBO!
Haya sasa  Mwanamke wewe;Katika hayo yote wewe unapenda nini ili uwe Mrembo au unaweza kuongezea ambayo hayapo hapo nasi Tufunguke,Pia unachukia kipi?

Wewe Mwanaume jee unapenda Mkeo,Mchumba,Rafiki yako wa Kike atoke vipi katika hayo na Unaweza kutujuza ambayo hayapo ili awe Mrembo na Unachukia kipi?

Duuhh Lakini Urembo mwingine unataka Moyo!!
Karibuni sana Wapendwa  kwa Mawazo/Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo!!!!!




Friday 25 November 2011

CITE- NA MIAKA 50 ya UHURU WA TANZANIA!!!!

Watanzania waishio Uingereza Kufanya Maombi ya Kumshukuru Mungu Kwa MIAKA 50 ya UHURU.

Waandaaji wa maombi ya ya Miaka 50 ya Uhuru chini Uingereza ”Association of Tanzanian Christians in Europe(CITE)” Wakiwa na Mwl Christopher Mwakasege wakati wa Summer Confference 2009.
Mithali 14:34 Biblia inasema Haki ya Mungu huinua Taifa na huu ndio mstari wa kusimamia katika Maombi hayo yanayowajumuisha watanzania wote waishio nchini Uingereza Hususani katika jiji la London. Kwa Mujibu Wa Mchungaji Emmanuel Chatawe ambaye ni mmoja wa waratibu wa Maombi hayo maombi hayo yatahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali.

Pamoja na Maombi hayo pia kutakuwepo na vikundi mbalimbali vya kusifu na kuabudu.Maombi hayo yameandaliwa na Umoja wa wakristo watanzania waishio bara la Ulaya(CITE).

TAREHE:10 Dec 2011

VENUE: Vision Gospel Ministry International 68 Wallis ROAD Hackney Wick London E9 5LH

TIME :13:00 – 18:00 HRS



Wakati Watumishi wa Mungu Kutoka  Tanzania  waishio nchini Uingereza wakijipanga kwa Maombi hayo, Kwa Upande wa Wakristo wa Watanzania Waishio Nchini Marekani wao wanatarajia kufanya Maombi hayo Tarehe 10 Dec 2011 .Kwa Maelezo zaidi juu ya Kusanyiko la Maombi ya Uhuru wa miaka 50 nchini Marekani Fuata LINK hapa chini.


http://hosannainc.blogspot.com/search/label/Watanzania%20Wahudumuo%20Nje


Thursday 24 November 2011

Miaka 50 ya Uhuru - Kijitonyama Evangelical Choir!!!!!

Wanakwambia Tujibweteke aaa,Turudi Nyuma mmm,Tusonge Mbele namnamnam,
Haya wapendwa mmejiaandaje na miaka 50 ya Uhuru? Mablogger nao sijui watatoka vipi/wameandaa nini?
kwani  nimeona Vyama, Vikundi vya ngoma,Muziki,Kwaya na mengine mengi kuhusu Miaka 50 ya UHURU. Uwe Huru na mwenye Amani na kila lililo jema!!!Usisite kutujuza Nasi Umejiaandaje au Unalipi kuhusu MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA. NA VISIWANI TUUNGANE PAMOJA!!

Tuesday 22 November 2011

Siku kama ya Leo dada Akhram wa Billy Alizaliwa!!!!

Siku kama ya leo Familia ya Bibi na Bwana Billy, Walipata mtoto wa kike na wakamwita Akhram!!
dada huyu ni mtu wakucheka wakati wote mpole na mwenye heshima,Si muoengeaji sana mpaka akuzoee sana,Nakuongea kwake uwe na muda ili mmalize hayo maongezi kwani ni taratibu mnoo,Ukiona kafunga mdomo bila tabasamu ujue NJAAA Kwenye sekta ya msosi ahaaa hana Tabu kabisa!!!Usikivu,samahani na kufanya vyema darasani kwake ni maisha  ya kawaida.
Mungu awabari wazazi na awape hekima katika Malezi yenu.


Swahili na Waswahili tunakutakia kila lililo jema mwanakwetu!!!!

Thursday 17 November 2011

SHUKRANI KUTOKA KWA FAMILIA YA JUMA PENZA[JP]!!!


Marehemu JUMA PENZA enzi za uhai wake.
Familia ya Juma Penza ya Gongo la Mboto Dar es Salaam inapenda kutoa shukrani za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki walioshirikiana  nasi katika kufanikisha shughuli za msiba wa baba yetu mpendwa, aliyefariki dunia tarehe 12/10/2011 katika hospitali ya Hindu Mandal na kuzikwa tarehe 13/11/2011 katika makaburi ya Kisutu. 



Tunatoa shukrani za pekee kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. J.M. Kikwete, CCM Makao Makuu, ndugu, jamaa, majirani na marafiki kwa misaada yenu ya hali na mali na kwa namna mlivyoshiriki katika shughuli zote za mazishi.  Shukrani za pekee ziwaendee Dr. Macha Ocean Road, wauguzi na madaktari  wa Hindu Mandal.


Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru  kila mtu kipekee, tunaomba shukrani hizi  mzipokee  wote kwa mikono miwili  kutokana na jinsi mlivyohusika kwa njia moja ama nyingine katika kufanikisha  shughuli nzima ya msiba wa baba yetu mpendwa Mzee JP.


Tunawashukuru kwa jinsi mlivyokuwa karibu  nasi  kwa dua  na maombi wakati wote  hadi tulipompumzisha baba yetu kipenzi .


Vilevile  tunapenda  kuwakaribisha  katika  mkesha  wa dua  itakayofanyika  Ijumaa usiku  Novemba 18 kuamkia siku ya Jumamosi Novemba 19 ambapo khitma  itasomwa  nyumbani kwa marehemu  Gongo la Mboto Dar es es Salaam wote mnakaribishwa .


Tunawakaribisha wote kwenye Arobaini ya marehemu. Mkesha na kisomo utafanyika siku ya Ijumaa tarehe 18/11/2011 na kufuatiwa na  Khitma itakayosomwa Jumamosi tarehe 19/11/2011 kuanzia saa 5:00 asubuhi nyumbani kwa marehemu Gongo la Mboto Jijini Dar es Salaam.Inna lilah Wainna Ilaih Rajiun

Wednesday 16 November 2011

Kuna Siku za Furaha na Siku za Vilio,Yote ni MaishaTusikate Tamaa!!!

                 Siku Ndugu zangu walipokuwa na Furaha.
                                        Mshumaa ulio Zimika.
                                            Mshumaa ulioZimika

Mungu awatie Nguvu katika wakati huu Mgumu na Sikuzote,Zaidi tudumishe Upendo,Umoja,Ushirikiano na Tusikate Tamaa,Wakati kama huu ndiyo utamjua Rafiki,Ndugu wa Kweli na Mengi Mema kwa Mabaya unaweza kuyasikia.Na niwakati kwa Waliopoteza Wazazi/Wapendwa wao Kuwakumbuka na Kulia tena,Nimeamini wanaosema Kilio hakiishi Utalia kila unapokumbuka.Nilitamani niwe nanyi lakini Mungu aliye nanyi ni Zaidi yetu sisi Tuliyo mbali.Mungu awalaze Mahali Pema Peponi Nduguzangu na Rafiki zangu,Jirani zangu na Wote waliotangulia.Sina Mengi ya Kusema bali nasema Asante Mungu.Wenu MWANAPENZA.

Monday 14 November 2011

Wanawake Waswahili wa Coventry wanakutakia,Kila la kheri da'May!!!!!!!!

                                        Mwenyewe da'May.
                                           Kekiiiii
                                               Kata mwanangu kataaa Keki
             May akilishwa na dada yake Esther,dada huyu ndiyo chanzo cha shughuli hii
                       May akimlisha dada yake kwa Furaha
             Da'May baada ya kumlisha dada yake wakaangaliana,May akasema Asante dada yangu
                   May na Mswahili wa Congo
                Mama mwenye nyumbaaa alilishwa pia
                    dada akisogea kutoa Nasaha zake mambo ya Tanga hayo
                           Heheheheee da'Stellah Akitoa Nasaha zake
                   Weshuuu!! da'Tina akitoa Nasaha zake
                           Wamama wakifuatilia Nasaha mbalimbali
                        Waswahili kutoka Milton nao walikuwepo
                          Da'Edna alikuwa MC siku hiyo, Yupo sambamba na mwali
                           Da'Asha mwenye furaha akifuatilia mapango mzima wa Nasaha
                              Wamama hawa wameguswa na Nasaha
                          Da'Bai yupo makini na kamera yake,lakini sikio lipowazi Kusikiliza Nasaha
                     Da'Sarah,Mamie na Stellah,Shughuli ilikamalika
                                 Da'Tinna alikuwepo
                        Dadazzzz walikuwepo,Neema,Maggie na Vick
                           Penye Wanawake Waswahili hakukosi Mila babuu Mtu kwako yakheeee
                         Haya funga Vibwebwe jamaniiiii!!!!Twende sasa!!
                                Hahhahahha Mwali kakuaaaaaaaaaaa,Swahili na Waswahili Wapendwaaaa


                         Nyanyuka sasa Mdogo wangu ya Coventry yameisha Subiri ya Dar na  Tangaaa

                    Mpango mzima wa muziki na Ngoma ulisababishwa na da'Chikuuuu huyo wa Mwisho


Shughuli hii ndogo ya Kumtakia Ndoa Njema dada May,Iliandaliwa na da'Esther,yeye ni dada wa bi Arusi mtarajiwa, Wanawake Waswahili wa Coventry U.K,[WWCU]Walikuwa bega kwa bega na da'Esther kufanikisha jambo hili.
Wanawake Coventry mpo juu na Mungu awabariki sana!!!


Dada May anatarajia kufunga Ndoa hivi karibuni,Ndoa hiyo itakuwa Nyumbani Tanzania[Bongo].
Kwaniaba ya Wanawake wenzangu;Da'May Tunakutakia Safari njema,Ndoa njema yenye baraka na Mungu akutangulie kwa kila jambo wewe na Mume wako Mtarajiwa pamoja na Familia na Wote watakaofanikisha.
Mengi yalishasemwa  pale kwenye sherehe,Hatuna la zaidi sisi TUNAKUPENDA SANA!!!!!!!






Wednesday 9 November 2011

DR. REGINA KAPINGA AIPEPERUSHA VEMA BENDERA YA TANZANIA NDANI YA BILL AND MELINDA GATE FOUNDATION.



DR. Regina Kapinga

Mama Regina (Program Officer of Bill & Melinda Gate Foundation) ni Mtanzania wa kwanza kuchaguliwa kuwa Staff wa Bill and Melinda Gate Foundation.

kutokana na Elimu na uzoefu aliokuwa nao katika kufanya kazi kwenye Taasisi za kimataifa, Taasisi ya kimataifa inayomilikiwa na Tajiri mkubwa Duniani Bill Gate ambaye ni mmiliki wa kampuni kubwa ya technolojia ya Microsoft ikaona imtumie katika kuweza kusimamia shughuli zote zinazohusu misaada mbali mbali katika mabara maskini Duniani, yaani Afrika na Asia.

Watanzania tunakutakia afya njema ili uweze kuitangaza zaidi Nchi yetu, tunaamini kupitia wewe Taifa letu litafaidika na misaada mbali mbali kutoka kwenye Foundation hiyo.
        
Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog
Asante sana.

Monday 7 November 2011

Da'Arianna Atimiza Miaka 3!!!!!!!

                     da'Arianna  kasimama tayari.
                           Kitu  cha kekiii.
              Mwenyekiti da'Mija akiandaa kekii.
                                 Arianna na mama'ke wakifurahia.
                          Mama Arianna akimsaidia kukata keki.
                              Kula mwanangu weee.
                                Dadazzzzz wakitabasamu.
               watoto wakibadilishana mawazo.
                  dada unajua mchezo huu?
                 Watoto wa Swahili Fellowship, wakisubiri kekii.
                  wametulia wenyewe.
                                    Watoto wanatabasamu naona mambo yalianza kusogea.
                       Watoto waliitikia mwaliko.
                        Mama kula eehhh,mama alikula mwishoni baada ya kuhakikisha watoto wote wamepata keki.

Familia ya bibi na bwana  Jonathan Mbwambo wa Coventry U.K.
Wanamshukuru sana Mungu kwa Mema mengi aliyo watendea, Moja  kati ya hayo ni kumlinda mtoto wao mpendwa da'Ariann mpaka leo Ametimiza miaka 3, Mungu ni Mwema sana.
Pia wanapenda kutoa Shukrani kwa Wazazi  na Watoto wa Coventry Christian Swahili Fellowship,na Wote waliojumuika nao.Shukrani za Pekee zimwendee Mwenyekiti wa Watoto da'Mija na Kamati Yake.
Mungu awabariki wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine.
Familia tunasema Asanteni sana kwa Moyo wenu na Mungu awe nanyi daima.


WENU KATIKA YOTE NA TUNAWAPENDA SANA.



         NASI SWAHILI NA WASWAHILI TUNAMTAKIA ARIANNA MAISHA MEMA YENYE AMANI NA FURAHA TELEEEEEEE.