Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 25 October 2011

Watoto wa Kike na Mitindo!!!!!!

                                 da'Nadia na poziiiii.
                              da'Nadia na Tabasam...
                                     da'Ester kapoziiii....
                                   da'Ester yupo makini....
                                         da'Miriam na poziiii....
                                 da'Naomi  dadalao kwa mitindo sijui Jina.....

Waungwana mnasemaje? Watoto wetu wakipendeza nasi pia roho nyeupeeeee!!!
Mpendwa wewe unapendelea watoto wakitoka vipi/wakivaa vipi?
Nini wewe ulikuwa Unapenda kutinga/kuvaa ulipokuwa mdogo?

Wengi enzi za Utoto kulikuwa na nguo maalum, yaani ya Kanisani/Jumapili, Hospitali,Siku Kuu,Yakutokea kwenda kwa ndugu na jamaaa na yaKushindia/ukiwa nyumbani au kuchezea Rede kama si mpira wa Miguuu!!!!Hahahahhha Tumetokambali mwehhhh.

Lakini Watoto wa Leo wengi wao hakuna Masharti sana kila wakati Wamependeza tuu.

Karibuni Sana Tukumbushane ya Utoto na kutoa Maoni/Mawazo yako kwani Yanathamani kwetu!!!









6 comments:

Tayanna said...

Hapa mimi pana nikuna ksanaa....yaani mtoto akipendeza naona furaha sana na pia unamjengea mazingira mazuri ya yeye mwenyewe kuwa anajijari awapo mkubwa...Bless them lord..

Yasinta Ngonyani said...

Yaani Rachel umenikumbusha mbali kwelikweli...gauni la kanisani na gauni la kushindia hizo ndizo zilikuwa nguo zangu na doti moja ya kanga..kutembea chama cha kuku...Halafu nimefurahi kweli umenikumbusha REDE...Rede redesta...eeeehh bwana weeee...

sam mbogo said...

wakati wa utoto,rede ilikuwa kipimotosha kujuwa msicha kavaa chupi gani.simnajuwa wenyewe jinsi rede inavyo chezwa,lazima kanga,gauni livutwe mpaka usawa fulani......... weweee!! tulifaidi sana,Yasinta na Rachel rede!! .kumbukumbu nzuri sana. kaka s

emuthree said...

Imekaa vyema hiyo ndugu yangu, tupo pamoja

Simon Kitururu said...

Wamependeza!

Rachel Siwa said...

Wapendwa Asanteni sana!Tayana Ameeeenn,
@ da'Yasint natumaini yameishia kwako si wanagu kina Erik na wengine,
@ Kaka wa mimi KITURURU hujakumbuka kile kikaptula chako?
@ Ndugu yangu emu-3 Pamoja sana!

@ kaka yangu SAM a.k.a kakaS kwikwikwikwi, Rede mwenzie kukudua na kukunja nguo@@@@@@wewe ndiyo wale mliokuja na vioo mtu kasimama mnaweka chini eeehhhh ili uone chhhhhuupiiiiii hahahahhha umenikumbusha mbali!!!!