Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 23 April 2011

Mshumaa wangu Uliozimika!!!!!!!!!

Saa,Siku,Wiki,Miezi.Leo Tarehe 23/04/2011  Imetimia Miaka 17.Tangu ulipotutoka Tarehe 23/04/1994.Baba yetu Mpendwa Mzee M.S.KIWINGA.Ulituacha katika Majonzi/Huzuni na kukata tamaa ya maisha.Lakini Mungu ni muweza wa yote ametusaidia na kusimama tena.Tulikupenda lakini Mungu  mwenyeezi alikupenda zaidi.Daima hatuwezi kukusahau kwa yote na mengi katika malezi yako.Utakumbukwa daima na Mke wako mpendwa,Watoto,Wajukuu,Ndugu,Jamaa,Marafiki na Majirani.
Shukurani za Dhati ziwaendee Wote walioshiriki nasi katika wakati ule mgumu.Tunaheshimu sana Michango,faraja zenu kwa wakati ule na hata sasa!Pia niwatakie kila la kheri na lililo jema kila siku.
Kwaniaba ya Familiya ya Mzee KIWINGA wa Ilala Sharifu/Shamba,Nasema asanteni sana wote na Tunawapenda.





8 comments:

mumyhery said...

Pole sana Rachel, Mlimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi, RIP Mzee Kiwinga

NAJUA WAJUA said...

Poleni sana, cha umuhimu ni kumuombea mzee wetu

Yasinta Ngonyani said...

Pole sana dada Rachel tumwombee ndio cha muhimu tupo pamoja ndugu yangu.

Simon Kitururu said...

R.I.P Mzee M.S.KIWINGA!

Mija Shija Sayi said...

Pumzika kwa amani mzee Kiwinga..

Rachel Siwa said...

Asanteni sana Wapendwa wangu kwa kuwapamoja katika kumbukumbu hii Muhimu Maishani, Nanyi Mungu awabariki na kila la kheri!.

nyahbingi worrior. said...

Amani iwe nanyi siku zote.

Never ever GIVE UP.

Rachel Siwa said...

Amina kaka Nyabingi!