Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 20 November 2010

umepitia michezo hii?

9 comments:

Yasinta Ngonyani said...

yaani we acha tu mimi na nilivyo rafiki ndio kaka zangu kwa hiyo ilikuwa bambi kweliiiii.

Rachel Siwa said...

hahahhaa dada Yasinta nao walikuwa wanaungana nawe kuchezea watoto?

Simon Kitururu said...

Nimepitia sana tu!Hapo unaunguruma tu mwenyewe kama gari.:-)

Mija Shija Sayi said...

Kitururu umesema kweli, hapo utakuta kila gari na muungurumo wake...

Mzee wa Changamoto said...

Ouch!!!
Enzi hizo
ENZI (japo si kwa maana ya zamani) ambazo watoto walicheza pamoja, watoto walionesha ubunifu, watoto walionesha kushirikiana, watoto waliheshimu uwezo mbalimbali wa mwenzao (kama kujua kuwa "fulani" ndio mtaalamu wa mipira ya kudunda, ama nanilii anatengeneza magari ya mneso, ama mtoto wa nanilii ni mtaalamu wa zana za uwindaji)
Kuna mengi tunayapoteza katika kuondoa michezo hii
Watoto hawajui "team work" tuliyokuwa tukijifunza. Na labda hata "uzoefu wa kumiliki familia kutokana na michezo ya kibabababa" nao unaonekana sasa ambapo zaidi ya 50% ya ndoa zifungwazo zinamomonyoka.
Sasa hizi tunaheshimu na kuamini "kompyuta" hata katika kubuni "magari ya udongo"

Anyway.....kujibu swali lako nasemaaaa
NILIPITIA HILO, na nasikitika kuwa mwanangu hatapita kwani mazingira yanamfunga
BLESSINGS

Rachel Siwa said...

Aksanteni sana wapendwa kwa maoni yenu,@kaka Kitururu na da Mija vipi apite mbabe na akanyage hayo magari?

@kaka wa changamoto nimekupata pia umeeleza kwa kina na uchungu wa uwezekano wa watoto wetu kukosa
michezo hii.

Simon Kitururu said...

Mbabe akikanyaga gari si kilio hicho!Na labda kuna mpaka ``NTAKUSEMELEA KWA MAMA!´´katika tukio hilo.:-)

Anonymous said...

Rede ya wote, kombolela,kalale nacho,kujipikilisha, baba na mama,kufinyanga udongo,one touch,gombania goli, mipira ya soksi na mipira ya makaratasi ya nairon. Jamani tulifaidi!

Rachel Siwa said...

Mdau tulifaidi sana!unaonaje siku tukakumbushia?